ZAIDI YA DOLA MILLION MOJA KUPATIKANA KUPITIA TUKIO LA 'WINGS OF KILLIMANJARO
ZAIDI ya dola milioni moja za Marekani zinatarajiwa kukusanywa
 kwa ajili ya kusaidia kazi mbalimbali katika taasisi za kijamii  
kupitia  tukio la ‘Wings of Kilimanjaro’ linalotarajiwa kufanyika 
mwanzoni mwa Mwaka ujao.
Katika taarifa iliyotolewa kwa 
vyombo mbalimbali vya habari, imeeleza kuwa  tukio hilo hutokea mara 
moja sana litafanyika mwezi Januari, mwakani na linategemea kupata kiasi
 hicho cha fedha kutoka kwa watu zaidi ya 200 watakaohudhuria tukio 
hilo.
Aidha kutakuwa na michezo 
mbalimbali ikiwemo ya kupaa na parachuti na mingine mingi, na kupata 
fursa ya kutembea kwenye kilele cha mlima Kilimanjaro. Fedha 
zitakazopatikana zitasaidia taasisi za Plant With Purpose, One 
Foundation na World Service International ambazo zinasaidia jamii za 
kitanzania.
Meneja wa Wings of Kilimanjaro 
Paula Mc Rae alisema hata Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk 
Jakaya Kikwete amefurahishwa juhudi zao za kutafuta fedha kwa ajili ya 
kusaidia watu wenye matatizo lakini pia kuutangaza mlima Kilimanjaro 
ulimwenguni kote.
“Katika uzinduzi wa Wings of 
Kilimanjaro, wataalamu wa ‘paragliding’ ikiwemo wale ambao ni maarufu 
duniani na abiria wao ambapo siku hiyo watakwenda mpaka eneo la Moshi 
ambapo watatua kwa kutumia muda wa dakika 40 tu” alisema.
Aidha aliongeza kuwa kati ya 
watu hao baadhi yao watatoka nje ya nchi kwa ajili ya tukio hilo lakini 
pia kushuhudia mlima mrefu kuliko yote barani Afrika mlima Kilimanjaro.

No comments:
Post a Comment