TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Thursday, December 13, 2012

ZAIDI YA DOLA MILLION MOJA KUPATIKANA KUPITIA TUKIO LA 'WINGS OF KILLIMANJARO
































ZAIDI ya dola milioni moja za Marekani zinatarajiwa kukusanywa kwa ajili ya kusaidia kazi mbalimbali katika taasisi za kijamii  kupitia  tukio la ‘Wings of Kilimanjaro’ linalotarajiwa kufanyika mwanzoni mwa Mwaka ujao.
 
Katika taarifa iliyotolewa kwa vyombo mbalimbali vya habari, imeeleza kuwa  tukio hilo hutokea mara moja sana litafanyika mwezi Januari, mwakani na linategemea kupata kiasi hicho cha fedha kutoka kwa watu zaidi ya 200 watakaohudhuria tukio hilo.
 
Aidha kutakuwa na michezo mbalimbali ikiwemo ya kupaa na parachuti na mingine mingi, na kupata fursa ya kutembea kwenye kilele cha mlima Kilimanjaro. Fedha zitakazopatikana zitasaidia taasisi za Plant With Purpose, One Foundation na World Service International ambazo zinasaidia jamii za kitanzania.
 
Meneja wa Wings of Kilimanjaro Paula Mc Rae alisema hata Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Jakaya Kikwete amefurahishwa juhudi zao za kutafuta fedha kwa ajili ya kusaidia watu wenye matatizo lakini pia kuutangaza mlima Kilimanjaro ulimwenguni kote.
 
“Katika uzinduzi wa Wings of Kilimanjaro, wataalamu wa ‘paragliding’ ikiwemo wale ambao ni maarufu duniani na abiria wao ambapo siku hiyo watakwenda mpaka eneo la Moshi ambapo watatua kwa kutumia muda wa dakika 40 tu” alisema.
 
Aidha aliongeza kuwa kati ya watu hao baadhi yao watatoka nje ya nchi kwa ajili ya tukio hilo lakini pia kushuhudia mlima mrefu kuliko yote barani Afrika mlima Kilimanjaro.

No comments:

Post a Comment