Na Heka Wanna na Shakila Galus,MAELEZO
  20/12/2012
MATUKIO ya uhalifu nchini imepungua kutokana na ushirikiano mzuri baina ya wananchi kwa kutoa taarifa za uhalifu  kwa jeshi la polisi. 
Akiongea na waandishi wa habari jana jijini Dar es salaam  Naibu Kamishna wa Polisi (DCP), Isaya  Mnguru
 alisema kuwa kwa kipindi cha kuanzia Januari hadi Novemba, 2012 
ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka 2011 takwimu zinaonesha hali 
ya uhalifu imepungua.
Aidha kumejitokeza na matukio kadhaa ya 
makosa dhidi ya kuania mali,makosa dhidi ya binadamu, makosa dhidi ya 
maadili na makosa dhidi ya usalama barabarani.
DCP
 Mnguru alisema kuwa hali ya mwenendo wa uhalifu kwa mwaka 2012 makosa 
makubwa ya jinai yaliyotolewa taarifa katika vituo vya polisi ni 66,255 
ikilinganishwa na makosa 69,678 yaliyo ripotiwa kwa kipindi cha mwaka 
2011 ni upungufu wa makosa 3,423 ambao ni sawa na 4.9%.
Aliendelea
 kuwa takwimu zinaonesha matukio makubwa ya usalama barabarani 
yaliyoripotiwa ni 21,531 ikilinganishwa na matukio 22,208 yaliyoripotiwa
 mwaka jana ambapo ni upungufu wa matukio 677 ambao ni sawa na 3%.
Mnguru alisema kuwa matishio ya usalama nayo yamepungua kwani mpaka sasa hivi hakuna tishio la dhahiri   hapa nchini kuhusiana na  tishio la ugaidi.
Alisema  hali hiyo  imetokana
 na hatua zilizochukuliwa katika kuimarisha ulinzi kwenye mipaka na 
maeneo nyeti sambamba na kuwatahadharisha wananchi kuwa waangalifu na 
kutoa taarifa za nyendo za watu au vikundi wanavyovitilia mashaka.
Aliongeza kuwa  jeshi
 la polisi linaendelea kubuni na kutekeleza kikamilifu mikakati ya 
kukabiliana na uhalifu ikiwemo kushirikiana na wadau wote wa ulinzi na 
usalama katika kubadilishana taarifa za kiintelijensia pamoja na uzoefu 
wa kuzuia uhalifu kwa kuibua mifumo mipya na kuboresha ya zamani.
Alisema  namba za simu za makamanda wa polisi  zimesambazwa
 nchini kote wananchi wasisite kuzitumia wapoona viashiria vya uhalifu. 
aliwaonya wale wote wasiopenda kutii sheria kwa hiari yao kuacha tabia 
hiyo wakiemo madereva wa mabasi ya abiria kutotii sheria za barabarani 
pamoja na waendesha pikipiki maarufu kama bodaboda kutovaa kofia ngumu 
na kupakia abiria zaidi ya mmoja.
No comments:
Post a Comment