TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Thursday, December 20, 2012

MKUU WA MKOA WA ARUSHA AMZAWADIA TUZO MWANDISHI WA NEW HABARI

ARUSHA


MKUU wa Mkoa wa Arusha amemzawadia   tuzo ya uandishi bora  wa habari za jamii na maendeleo Meru , mwandishi wa habari  Mary Mwita   wa magazeti ya Mtanzania na Rai ya  Kampuni ya New habari (2006) LTD.
 Mkuu wa Mkoa huyo ametoa  tuzo hiyo ,ikiwa ni ahadi yake ,na agizo alilotoa kwa uongozi wa Halmashauri hiyo kupeleka jina la Mwandishi wa habari aliyeandika habari bila kupotosha jamii katika Halmashauri hiyo ,na kuweza kumpata Mwandishi huyo .
 Mkuu alitoa Tshs 500,000 ikiwa ni tuzo  na kiasi cha fedha zilizokabidhiwa kwa wadau wengine mwaka huu waliobainika kuchangia maendeleo ya Meru.
 Mkuu huyo alisema kuwa  huwezi kutaja maendeleo bila kuhusisha vyombo vya habari na waandishi wa habari ,na kuwa kila Halmashauri inatakiwa kutambua  mchango wa maendeleo ya wadau  ikiwa ni pamoja na waandishi wa habari .
 Akimpongeza Mwandishi  Mary Mwita ,alisema wakati umefika wa waandishi wa habari kuandika habari za kweli  bila kupotosha umma ,ikiwa ni kuwawezesha wananchi kujifunza na kupata ujuzi kupitia habari hiyo ,badala ya kuandika habari za uongo .
 Mlongo alisema kuwa ni wazi kuwa kila mtu katika jamii akisimama katika nafsi yake kulingana na karama aliyopewa Maendeleo ya haraka yatafikiwa na kuwawezesha wananchi kupunguza kasi ya umaskini katika jamii .
 Katika hatua nyingine alipongeza uongozi wa Halmashauri ya Meru kwa kutambua mchango wa maendeleo ya wadau  na kutaka Halmashauri nyingine kuiga mfano huo wa kutunikia zawadi wadau waliosaidia maendeleo ya Halmashauri.
 Kwa upande wake  Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Meru Trisas Kagenzi alisema kuwa  zoezi la kuwazawadia wadau ni endelevu ,na kuwa wataendelea kutambua mchango wao kwa kuwa bila ushirikiano na wadau  wa maendeleo ,maendeleo yanaweza kuchelewa .
 Kagenzi alisema kuwa Mwandishi Mary Mwita ,amekuwa akiandika habari bila kupotosha umma  kwa kujituma na kutaka waandishi wengine kuiga mfano wake.

No comments:

Post a Comment