TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Saturday, October 10, 2015

Pichaz za kwanza nje Red Carpet mpaka ndani kwenye Fainali ya BSS 2015

Ndani ya Ukumbi wa King Solomon Hall, Kinondoni Dar es Salaam kinachoendelea sasahivi ni Fainali ya Bongo Star Search Season 8… nimeanza kukusogezea hizi pichaz za kwanza kuanzia Red Carpet mpaka ndani.
3X6A0684
Romy Jones kwenye Red Carpet.
3X6A0694 3X6A0697 3X6A0700 3X6A0706 3X6A0729 3X6A0730 3X6A0736 3X6A0753 3X6A0757 3X6A0770 3X6A0787 3X6A0801 3X6A0845 3X6A0864 3X6A0884 3X6A0890 3X6A0951 3X6A0959 3X6A0967 3X6A0969 3X6A0974 3X6A0996

Ulishawahi kuona mlo wa mchana wa Cristiano Ronaldo? basi nimekuwekea hapa mtu wangu

Michuano ya mechi za kuwania kufuzu michuano ya Euro 2016 bado inaendelea kwa michezo kadhaa kupigwa, kwa upande wa timu ya taifa ya Ureno ambao walishinda kwa goli 1-0 dhidi ya timu ya taifa ya Denmark . Baada ya ushindi huo Ijumaa ya October 9 Cristiano Ronaldo alipiga picha za mlo wake wa mchana.
Cristiano Ronaldo alipost picha ya msosi wake wa mchana aliyokula wakati ambao alikuwa anajiandaa kurudi kwao ni diet ambayo imekamilika kwa kiwango kikubwa, kwani kulikuwa na mayai, viazi, nyama, matunda, maji ya kunywa juisi. Baada ya kuweka picha hiyo katika account yake ya instagram mtandao wa dailymail.co.uk ulichambua kila aina ya chakula kilichomo katika diet hiyo.
2D3C80B500000578-0-image-a-96_1444395445042
Katika ratiba ya chakula cha mchana cha Ronaldo hakuna chakula ambacho kina asili ya sukari nyingi lengo linatajwa kuwa ni kulinda mwili wake ili kuendelea kuwa sawa kwa michuano mingine. Ureno walicheza mechi dhidi ya Denmark na kuibuka na ushindi wa goli 1-0, huu ukiwa ushindi wao wa sita katika mechi zao saba za kuwania kufuzu michuano ya Euro 2016.
2D35A11600000578-3266440-Ronaldo_right_looks_to_escape_the_attentions_of_Lars_Jacobsen_du-a-104_1444396967061

Mtazamo wa kocha wa Arsenal juu ya Liverpool kumfuta kazi Brendan Rodgers

Baada ya klabu ya Liverpool kumfukuza kazi aliyekuwa kocha wa klabu hiyo Brendan Rodgers kutokana na mwenendo mbovu wa timu yao, watu mbalimbali katika uchambuzi wa masuala ya soka wamekuwa wakizungumza mitazamo tofauti tofauti kuhusiana na maamuzi hayo.
October 9 kocha wa klabu ya Arsenal ya Uingereza Arsene Wenger amezungumzia kuhusiana na mtazamo wake juu ya uamuzi wa viongozi wa Liverpool kumfuta kazi Brendan Rodgers, Wenger ambaye timu yake ya Arsenal iliwahi kupitia katika wakati mgumu kwa miaka kadhaa ila hakufukuzwa kazi.
2D3C29B300000578-0-image-a-27_1444390674750
Wenger na Rodgers wakipeana mikono katika mechi timu zao zilipo kutana.
Wenger ana amini Rodgers angepewa zaidi ya mechi nane za kuendelea kuifundisha timu hiyo ili klabu iweze kuamua >>>”walikuwa katika nafasi nzuri ya kuwania ubingwa katika miaka miwili iliyopita lakini sasa sielewi kwa nini wamefanya hivi, sioni sababu za msingi za kufanya uamuzi wa haraka namna hii, kwangu mimi ni ngumu kuelewa”
2D2D6C4A00000578-3266324-image-a-1_1444399238639
Klabu ya Liverpool ya Uingereza haijawahi kutwaa ubingwa wa Uingereza toka mwaka 1990, lakini katika historia imetwaa taji hilo mara 18, lakini klabu hiyo ni moja kati ya vilabu vilivyotwaa taji la Ligi Kuu Uingereza mara nyingi zaidi. Hivyo kwa sasa klabu ya Liverpool imemchagua Jurgen Klopp.

Kocha wa Liverpool kamkejeli Jose Mourinho? hili ni jina analotaka kuitwa, zipo pia pichaz za utambulisho wake

Jioni ya October 7 klabu ya Liverpool ya Uingereza ilitangaza rasmi kuingia mkataba wa miaka mitatu na kocha Jurgen Klopp na kujiunga na klabu hiyo, taarifa zilizotoka  Ijumaa ya October 8 ni kuwa atatambulishwa mbele ya waandishi wa habari pamoja na kufanya mahojiano na waandishi wa habari.
2D3BB6EF00000578-3266211-image-a-31_1444388005147
Jurgen Klopp aliwahi kuwa kocha wa Borussia Dortmund ya Ujerumani kabla ya mwishoni mwa msimu uliyomalizika kuacha kazi na kukaa bila timu kwa kipindi fulani. Jurgen Klopp ametambulishwa Ijumaa ya October 9 hii ikiwa ni siku moja imepita toka asaini mkataba wa miaka 3 wenye kipengele cha kuongezewa mwaka mmoja zaidi, kocha huyo amesaini mkataba wenye thamani ya pound milioni 21.
2D3A48B900000578-3266211-There_was_time_for_Klopp_Werner_and_Ayre_to_share_a_joke_at_the_-a-29_1444387955704
Jurgen Klopp ambaye alianza kazi ya ukocha katika klabu ya Mainz 05 mwaka 2001 – 2008 ambapo alihamia katika klabu ya Borussia Dortmund. Moja kati ya kauli zinazovutia wengi alizozungumza katika mkutano na waandishi wa habari ni kuwa yeye ni kocha wa kawaida kauli ambayo ilihusishwa kama kijembe kwa Jose Mourinho ambaye anajiita ‘the special one’.
2D3A78AB00000578-0-image-a-25_1444384875520
” Ni heshima kubwa kuwa kocha katika moja kati ya klabu kubwa duniani, hii ni fursa kwangu ya kujaribu na kuisaidia klabu, haukuwa muda sahii kwa mimi kujiunga lakini naweza sema ni wakati mzuri kwangu. Sitajiita jina lolote sabau mimi ni  mtu wa kawaida na mama yangu anatazama huu mkutano kupitia Tv akiwa nyumbani, ila kama utapenda kuniita jina itakuwa vizuri ukiniita ‘the normal one’ ” >>> Jurgen Klopp
2D3AB05200000578-0-image-a-28_1444384887414
2D39944F00000578-0-image-a-30_1444384909995

Mambo ni moto mtu wangu !! Hili ndio chimbo tutakaposhuhudia Mshindi wa BSS 2015 leo.. (Pichaz)

Zimebaki saa chache kushuhudia Fainali za Mashindano ya Bongo Star Search 2015… umepata ticket yako??? Kama jibu ni YES basi good news ikufikie kwamba kila kitu kimekamilika tayari, nimegusa nje mpaka ndani nikaona hii sio ya kunipita wala sio ya kukupita mtu wa nguvu unaependa Burudani.
Usiku wa leo tunakutana Ukumbi wa King Solomon Hall NAMANGA, Dar es Salaam… October 09 2015 mambo yako tayari kwa ajili ya Mshiriki mmoja kuibuka na Ushindi na kutangazwa mshindi anayefunga Historia ya headlines za BSS 2015.
Hizi hapa pichaz mtu wangu, nje mpaka ndani mambo ni motomoto !!
3X6A0584
Kuhusu Red Carpet je? YES, hapo kitu kinamaliziwa sasahivi..!!
3X6A0579 3X6A0582 3X6A0587 3X6A0588 3X6A0589 3X6A0590 3X6A0591 3X6A0596 3X6A0597 3X6A0599 3X6A0600 3X6A0602 3X6A0603 3X6A0609 3X6A0615