TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Friday, December 12, 2014

Umeisikia ya daktari kumlazimisha mwanamke kumeza dawa za kutoa ujauzito?

Handcuffed Man
Huenda alifanya kwa kumsaidia lakini msaada wake umemgeuka na kuwa hatia, Dk. Thomas A. Pfeiffer, amefikishwa Mahakamani kutokana na kufanya kosa la kumlazimisha mwanamke mmoja kunywa dawa za kutoa ujauzito.
Dokta huyo wa New York amekutwa na hatia, anatakiwa kujibu mashtaka matatu ambayo yametokana na kumlazimisha mwanamke mmoja kunywa dawa za kutoa ujauzito, amefikishwa Mahakamani kusomewa mashtaka kisha kurudishwa jela na dhamana yake ni dola 50,000.
Daktari kaingia kwenye hatia hiyo baada ya upelelezi kubaini kwamba anahusika na kitendo hicho ambapo mwanamke aliyetumia dawa hizo alipata majeraha sehemu za kooni na mdomoni.

Baada ya kuachia Mfalme hizi ni picha za Mwana FA akiwa katika maandalizi ya video nyingine

.
Ali Kiba akiwa na Warembo katika utengenezaji wa video hiyo mpya ‘Kiboko Yangu aliyoshirikishwa na Mwana FA.
Sina Shaka na wewe mtu wa nguvu utakuwa umeshaisikiliza single mpya ya Hamisi Mwinjuma aka Mwana FA ‘Kiboko Yangu’ aliyomshirikisha Ali Kiba ambayo inaendelea kufanya vizuri katika vituo mbalimbali vya radio.
Good news ninayotaka kukupatia ni kwamba wakati single hiyo ikiendelea kufanya vizuri kwenye spika za radio yako soon inatarajiwa kuona kwenye chati za TV na hizi ndio baadhi ya picha za Behind  The Scene ambazo zikimuonesha Mwana FA na Ali Kiba wakiwa location katika uandaaji wa video hiyo mpya Kiboko Yangu.

.
.
.
.
.
.
.
Ali Kiba na Mwana FA wakiwa Location katika utengenezaji wa video mpya hiyo Kiboko Yangu.
.
Ali Kiba akiwa na Warembo katika utengenezaji wa video hiyo mpya.

Hawa ndio punda waliobebeshwa ujumbe na wanaharakati na kuachwa katikati ya Jiji

TZA-PUNDA WENYE GRAFITTI
Kenya ni moja ya nchi ambazo huwa zinakaa kwenye headlines ya kuwa na story kubwa Afrika Mashariki, ya leo inahusu punda waliobebeshwa ujumbe maalumu na kuachwa katikati ya jiji la Nairobi.
Desemba 11 katikati ya jiji la Nairobi katika moja ya barabara zenye shughuli nyingi ya Moi, lori moja lilisimama na kushusha punda wapatao 22 walio na maandishi yenye ujumbeTumechoka”.
Wanaharakati nchini Kenya wametajwa kuhusika na hii ambapo pia wamewahi kutumia njia mbalimbali ili kufikisha ujumbe wao ambapo moja ya waliyowahi kuifanya ni ile ya kuyabeba majeneza idadi sawa na Wabunge.
Taarifa zinasema kuwa huu mtindo wa kuwashirikisha wanyama kwenye maandamano ya kudai haki ilianzishwa na mwanaharakati ambaye pia ni mkurugenzi wa Pawa 254, Boniface Mwangi japo safari hii haijafahamika sababu ya kuwatumia wanyama hao kufikisha ujumbe huo.
Tumechoshwa na uongozi mbaya… ” alisikika mmoja ya wanaharakati huku akiwasukuma punda hao kutoka nje ya Lori.
Polisi wanasema wanawasaka wale waliohusika na kitendo hicho.
TZA-WANANCHI WAKISTAAJABU PUNDA WENYE GRAFITTI
TZA-UJUMBE WA PUNDA
141211133827_donkeys_7 (1)

Pale ambapo operator anajikuta akiweka picha za utupu katika bango uwanjani.

Billboard II 
Ajali popote, huyu jamaa amepata ajali kazini tena huenda katika mazingira ambayo hakuwahi kutarajia.
Kutokana na sheria kali za China, hii haikuwa makusudi lakini kwa sababu tayari kashafanya kosa anastahili hukumu.
Tumezoea kuona mabango ya kisasa katikati ya Miji kama Dar ambayo yanakuwa yanaonyesha picha kama Tv ambapo picha zinazoonekana kuwa zinabadilika badilika.
Nje ya Uwanja wa Maryland, Langzhou China jamaa anayehusika kuoperate bango moja amejikuta akiwa na hatia ya kukaa jela kwa siku 15 pamoja na na kulipa faini ya kiasi cha Yuan 3000 za China zaidi ya Dola 484 kwa kosa la kuweka picha za wasichana wakiwa tupu kwenye bango lililopo nje ya uwanja huo.
Japo walinzi waliwahi kuchomoa waya wa umeme kulizima bango hilo haikusaidia, watu walioshuhudia picha hizo zikionekana kwa  sekunde 12 walirekodi video na picha ambazo walianza kushare kupitia mitandao ya kijamii.
Mhandisi wa Kampuni inayohusika na kuweka mabango hayo naye pia amekamatwa japo hukumu yake bado haijafahamika.

Wednesday, December 10, 2014

Ule ugeni kutoka Himaya ya Kifalme Uingereza umekutana na mastaa wengine Marekani, picha zipo hapa

Close-Up of Handshake 
Vyombo vikubwa vya habari Duniani pamoja na mitandao ya kijamii viliripoti kuhusu ziara ya siku tatu inayofanywa na mjukuu wa Malkia Elizabeth, Prince William na mke wake Kate Middleton huko Marekani na tukapewa taarifa siku ya jana pia kwamba ugeni huo ulipata nafasi kuingia ndani ya Ikulu ya Marekani kwa mara ya kwanza na Prince akafanya mazungumzo na Rais Obama.
Habari kubwa kwa sasa ni kuhusiana na wawili hao siku ya jana kuhudhuria mechi ya Basketball na kuushuhudia ushindi wa Cleveland Cavaliers dhidi ya Brooklyn Nets na kupata nafasi ya kukutana na staa wa Basketball LeBron James, Jay Z pamoja na Beyonce.
Walipata nafasi ya kupiga stori kidogo na mastaa hao baada ya mechi hiyo kuisha.
PW
Prince William, Kate, Jay Z na Beyonce wakisalimiana baada ya kukutana katika Ukumbi wa Barclays Centre ilipokuwa ikichezwa mechi ya Basketball kati ya Cleveland Cavaliers na Brooklyn Nets jana Desemba 09.
PW I
PW II
Waandishi wa Habari wakipiga picha wakati Prince na mkewe walipokutana na Jay Z na Beyonce.
PW III
Prince William, Kate na LeBron James.

Matokeo ya UEFA Champions League yapo hapa

article-2867609-23EC051900000578-81_636x382
Michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya imeendelea usiku huu ikiwa kwenye mzunguko wake wa mwisho wa hatua ya makundi .
Katika michezo iliyopigwa hii leo timu ya Arsenal toka England ilifanikiwa kushinda kwenye mchezo wake dhidi ya Galatasaray ya Uturuki kwa matokeo ya 2-4 katika mchezo uliopigwa huko Istanbul.
Kiungo wa Arsenal Aaron Ramsey akiifungia timu yake katika ushindi wa 2-4 dhidi ya Galatasaray.
Kiungo wa Arsenal Aaron Ramsey akiifungia timu yake katika ushindi wa 2-4 dhidi ya Galatasaray.
Arsenal ilifunga mabao yake kupitia kwa Aaron Ramsey na mshambuliaji raia wa Ujerumani Lukas Podolski ambapo kila mmoja alifunga mabao mawili .
Katika mchezo mwingine wa kundi D wawakilishi toka Ujerumani, Borrusia Dortmund walibanwa mbavu wakilazimishwa sare ya 1-1 katika mchezo dhidi ya Anderlecht ya Ubelgiji.
Matokeo haya yanamaanisha kuwa timu za Arsenal na Borrusia Dortmund zimefanikiwa kufuzu hatua ya 16 bora ambapo Dortmund wamefuzu kama washindi huku Arsenal wakishika nafasi ya pili .
Katika michezo mingine iliyochezwa usiku huu Real Madrid walifanikiwa kushinda mchezo wao wa 19 mfululizo katika mashindano yote wakiwafunga Ludogorets toka Bulgaria 4-0 .
23EB782B00000578-0-image-a-28_1418159216142
Wafungaji wa Real kwenye mchezo huo walikuwa Cristiano Ronaldo , Gareth Bale , Alvaro Arbeloa na Alvaro Medran .
Ushindi huu umewafanya Real wafuzu hatua ya 16 bora kwa kishindo wakiwa wamekusanya pointi 18 baada ya kushinda michezo yote 6 ya kundi lao .
Liverpool ambayo ilikuwa nyumbani ikicheza na Fc Basle iliambulia sare ya 1-1 matokeo ambayo yalikuwa na faida kwa wapinzani wao ambao wanaungana na Real Madrid kufuzu hatua ya kwanza ya mtoano.
Fc Basle imewatoa Liverpool kwenye michuano ya ligi ya mabingwa baada ya kuwalazimisha sare ya 1-1.
Fc Basle imewatoa Liverpool kwenye michuano ya ligi ya mabingwa baada ya kuwalazimisha sare ya 1-1.
Katika michezo mingine Juventus na Atletico Madrid walitoka sare ya bila kufungana , Olympiakos wakawafunga Malmo 4-2 , Benfica na Bayer Leverkusen nazo zikatoka sare ya 0-0 , huku As Monaco ikishinda dhidi ya Zenith St Petersburg kwa matokeo ya 2-0 .
Kwa matokeo haya timu za Juventus , Atletico Madrid , Monaco na Bayer Leverkusen zinaungana na Arsenal , Dortmund , Real Madrid na Fc Basel kufuzu hatua ya 16 bora .
sare ya 1-1 dhidi ya Atletico Madrid ilitosha kuwavusha Juventus kwenye hatua ya 16 bora.
Sare ya 1-1 dhidi ya Atletico Madrid ilitosha kuwavusha Juventus kwenye hatua ya 16 bora.

Friday, December 5, 2014

Yule mama aliyejiuzulu kwa kukosoa mavazi ya watoto wa Obama kumbe bado anafuatiliwa?

sasha-malia-2-477 
Moja ya story ambazo zilichukua uzito wa juu katika vyombo vya habari wiki iliyopita ilikuwa ni kitendo cha yule mama mfanyakazi wa Chama cha Republican Marekani, Elizabeth Lauten ambaye alikuwa kitengo cha Mawasiliano kukosoa mavazi ya watoto wa Obama bado ni story inayoendelea kuzungumziwa.
Mama huyo aliwaponda Sasha na Malia kuwa wamekosa ustaarabu kutokana na kuvalia sketi fupi katika hafla ya chakula katika Ikulu ya White House, pia alisema kuwa watoto hao ni kama hawakuwa na nyuso za furaha kuwa katika hafla hiyo, ambapo baada ya kushambuliwa na watu kwenye ukurasa wake wa Facebook aliomba radhi, na baadaye akajiuzulu.
141130152136_turkey_640x360_getty
Leo ni siku ya nne tangu amejiuzulu lakini story ni kwamba bado ameendelea kufuatiliwa na vyombo habari, huku wengine wakipiga kambi nyumbani kwa wazazi wake kuchunguza vitu mbalimbali ikiwemo rekodi ya maisha yake ya utotoni ambapo watu kwenye mitandao ya kijamii wamekosoa kwa kusema hiyo haikuwa ‘big deal’ ya kufanya vyombo vya habari kumfuatilia kiasi hicho.

Alichokiandika Bill Cosby kuhusu shutuma za kubaka zinazomkabili

cosby
Mzee Bill Cosby, mchekeshaji maarufu Marekani ambaye anakabiliwa na mashtaka ya ubakaji ambapo jumla ya kesi 20 kwa mara ya kwanza amejitokeza na kuzungumzia shutuma zinazomkabili.
Watu wengi walionekana kumlaani Cosby kuhusiana na shutuma zinazomkabili lakini wapo wachache ambao walisimama upande tofauti ambapo ndiyo waliompa nguvu ya kutweet akiwashukuru kwa kuonyesha kumpa moyo.
Cosby alitweet akiwashukuru Whoopi Goldberg na Jill Scott ambao walieleza kwa nyakati tofauti namna ambavyo hawakupendezwa na kitendo cha vyombo vya habari kueneza kashfa za ubakaji juu ya Cosby.
Cosby hakuwahi kuzungumza hadharani kujibu chochote kuhusiana na shutuma hizo za ubakaji, japo shutuma zinazozungumziwa sasa zinafanya idadi ya wanawake ambao wamewahi kuripoti kuhusu kufanyiwa hivyo kufikia 20.

IPTL yazua Kizaazaa Mahakamani


Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya IPTL na PAP, Harbinder Singh Sethi
Kampuni za Pan Africa Power Solution Tanzania Limited (PAP) na Independent Power Tanzania Ltd (IPTL), zimewasilisha maombi ya kutaka Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato (TRA) akamatwe kwa kukiuka amri ya Bodi ya Rufaa za Kodi (TRAB) kwa kufuta Hati za Malipo ya Kodi za Mauzo ya Hisa (Capital Gain Certificate).
Kampuni hizo mbili, ambazo ziko kwenye mgogoro wa umiliki, ndizo zinahusika kwenye sakata la uchotwaji wa Sh306 bilioni kutoka Akaunti ya Tegeta Escrow iliyofunguliwa kuhifadhi fedha za malipo ya tozo ya kuuza umeme unaofuliwa na IPTL, kwa Shirika la Umeme (Tanesco), wakati wa kusubiri uamuzi wa mahakama katika kesi ya kupinga tozo hilo.
PAP, ambayo inadai imenunua hisa zote za IPTL, ndiyo iliyolipwa fedha zote zilizokuwa kwenye akaunti hiyo na kuamsha mjadala mkubwa bungeni ulioisha kwa Bunge kufikia uamuzi wa kuwawajibisha kisheria wote waliohusika, wakiwemo mawaziri.
Lakini uamuzi huo wa Bunge haukuwa tamati la sakata hilo baada ya kampuni hizo mbili kukata rufaa TRAB dhidi ya Kamishna wa TRA na Msajili wa Kampuni na Leseni (Brela) zikipinga kusudio la kufuta hati hizo.(P.T)
Jana kampuni hizo mbili ziliwasilisha maombi ya hati ya kutaka Kamishna Mkuu wa TRA akamatwe, zikidai kuwa amepuuza amri hiyo iliyomzuia kutekeleza azma yake ya kufuta Hati za Malipo ya Kodi ya Mauzo ya Hisa.
Katika maombi hayo walalamikaji hao wanadai kuwa licha ya TRAB kutoa zuio hilo Novemba 26, 2014, Kamishna Mkuu wa TRA, ambaye ni mlalamikiwa wa kwanza, alitoa amri ya kuziondoa hati hizo siku iliyofuata, yaani Novemba 27, 2014, bila kujali amri hiyo.
Walalamikaji hao pia wanaiomba TRAB, baada ya kumkamata Kamishna Mkuu wa TRA, itoe amri afungwe kwa kudharau amri halali iliyotolewa na bodi na pia imwamuru akidhi matakwa ya amri ya TRAB ya Novemba 26.
Pia walalamikaji hao wanaiomba TRAB imwamuru mlalamikiwa huyo, kulipa gharama za uendeshaji wa shauri hilo pamoja na amri nyingine ambazo itaona kuwa zinafaa.
Maombi hayo ya PAP na IPTL ya hati ya kumkamata na kuamuru Kamishna Mkuu wa TRA afungwe yamepangwa kusikilizwa leo na Katibu wa TRAB, Respicius Mwijage.
Hati ya kiapo inayounga mkono maombi hayo inaeleza kuwa mlalamikiwa, akiwa ni raia wa Tanzania, siyo tu kwamba alipaswa kuwa mtiifu kwa mamlaka ya bodi hiyo, bali pia alipaswa kutekeleza sheria za nchi ambazo bodi hiyo ni sehemu yake.
Hati hiyo ya kiapo ya mkurugenzi wa operesheni wa IPTL, Parthiban Chandrasakaran, inaeleza kuwa kwa kitendo hicho cha kutotii amri ya bodi hiyo, mlalamikiwa amepoteza sifa ya kuwa mtumishi wa umma katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Pia inaelea kuwa kama bodi hiyo isipotumia mamlaka yake kukubali maombi hayo ya kutoa amri inayoombwa, basi walalamikaji watapata hasara isiyoweza kufidiwa.

Sing'atuki ng'o:Mugabe 


Rais Robert Mugabe awalaumu baadhi ya wapinzani wake ndani ya chama cha ZANU PF kwa kupanga kumuondoa mamlakani.
Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe amelaumu baadhi ya watu ndani ya chama chake tawala cha ZANU-PF kwamba wanapanga kumng'oa madarakani.
Akizungumza katika kongamano la chama hicho, Mugabe amesema amebaini kuwepo majaribio ya kuwahonga wajumbe kumpinga kama kiongozi, lakini akasisitiza wajumbe hawawezi kupokea hongo.
Mugabe ameahidi kupambana na rushwa ndani ya chama na kukabiliana na maafisa wa chama hicho ambao kazi yao ni kutoa hongo na kupokea rushwa.BBC

Wanachama wengi wa chama hicho wangali ni wafuasi sugu wa Rais Mugabe
Hasira ya Mugabe ilionekana kufuatia madai ya njama ya kutaka kumuua yanayodaiwa kuandaliwa na naibu wake Joyce Mujuru. Hata hivyo Mujuru alikanusha madai hayo ambayo yamekuwa yakimuandamana.
Mugabe alisema kutokuwepo kwa Bi Mujuru kwenye mkutano huo wa chama kunaonyesha kuwa anaogopa.
Kadhalika Mugabe amesema Mujuru ni mwizi anayepanga kumuondoa mamlakani kwa kushirikiana na maafisa wengine wa chama.

Maelfu ya wajumbe wa chama walihudhuria kongamano hilo mjini Harare
Chama tawala cha Zimbabwe kinakumbwa na vita vya ndani kwa ndani kuhusiana na nani atarithi nafasi ya Mugabe ambaye ana miaka 91 na ambaye ameongoza tangu uhuru wa taifa hilo.
Hata hivyo amekanusha madai ya kwamba anataka kujiuzuru na kusema kuwa huo ni upuuzi.
Hivi karibuni afisa mwingine mkuu wa chama tawala, Robert Gumbo aliiambia BBC kwamba Mugabe mwenye umri wa miaka 90 amegeuza chama tawala na kukifanya kama mali yake binafsi.

Bi Joyce Mujuru amedaiwa kupanga njama ya kumuua Mugabe ili achukue mamlaka kutokla kwake.
Gumbo alisema lengo kuu la Mugabe ilikuwa kuendeleza uongozi wa chama kwa niaba ya mke wake Grace.
Bi Mujuru ambaye amekanusha madai hayo alionekana kama mtu ambaye anechukua usukani wa chama kutoka kwa Mugabe ambaye walipigania naye uhuru wa nchi hiyo kutoka mikononi mwa watwala wazungu.

Hollande ziarani Kazakhstan 

Rais wa Ufaransa, François Hollande, amejielekeza KazakhstanIjumaa Desemba 5, ili kuimarisha uchumi na biashara kati ya nchi hizo mbili.
Rais wa Ufaransa, François Hollande, amejielekeza KazakhstanIjumaa Desemba 5, ili kuimarisha uchumi na biashara kati ya nchi hizo mbili.
Na RFI
Ni ziara ya tatu ya rais wa Ufaransa nchini Kazakhstan tangu kutangazwa uhuru wa taifa hilo mwaka 1991. François Mitterrand na Nicolas Sarkozy marais wa zamani wa Ufaransa walifanya ziara ya kikazi nchi Kazakhstan kabla ya François Hollande.
Rais Hollande amewasili nchini Kazakhstan Ijumaa Desemba 5 mapema asubuhi, kwa ziara ya saa 48, ambapo lengo ni kuimarisha uchumi na biashara kati ya Ufaransa na nchi hiyo yenye nguvu katika ukanda wa Asia ya Kati.(P.T)
Kazakhstan ni nchi tajiri kutokana na rasilimali za madini hususan madini ya uranium, kwani ni ya kwanza kwa kuzalisha madini hayo ulimwenguni. Kazakhstan inazungukwa na rasilimali kama chuma, makaa ya mawe, dhahabu, fedha na kadhalika. Fedha zinazotokana na mauzo ya dhahabu nyeusi nje ya nchi inawakilisha peke yake zaidi ya nusu ya mapato ya serikaliya Kazakhstan.
Kazakhstan ni nchi jirani ya mataifa yenye nguvu ambayo ni Urusi na China. Makampuni mengi barani Ulaya yameendelea baada ya nchi zao kuanzisha bishashara na Kazakhstan.
Kwa sasa Ufaransa inachukua nafasi ya tanu katika masuala ya biashara, huku Italia ikiongoza kwa kuchukua nafasi ya kwanza.
Ufaransa inawakilishwa nchini Kazakhstan na kampuni ya mafuta Total, ambayo ni mshirika wa kampuni ya gesi ya Kashagan, aidha Areva, kampuni inayoendesha shughuli zake katika migodi ya Uranium kusini mwa nchi. Kazakhstan ni nchi ya kwanza kwa kuitolea Ufaransa kiwango kikubwa cha uranium.
Hata hivyo Ufaransa inaiuzia Kazakhstan helikopta na silaha nyingi. Ziara hiyo ya rais Hollande nchini Kazakhstan ina manufaa makubwa kwa uchumi wa Ufaransa. Rais Hollande ameshirikiana katika ziara hiyo na ujumbe mkubwa wa matajiri wa makampuni makubwa nchini Ufaransa kama EDF, GDF, Veolia, Airbus, Peugeot pamoja na Vinci.
Hayo yakijiri Kazakhstan imekua ikinyooshewa kidole na mashirika ya haki za binadamu kwa ukiukwaji wa haki za binadamu.

WAKATI SSERENKUMA AKITUA, SIMBA KUSAINI BEKI WA KATI KUSUKA SIMBA MPYA  

23
Na Baraka Mbolembole,
Wakati kiungo raia wa Uganda, Danny Sserenkuma akitaraji kutua nchini Jumatano hii kujiunga na Simba SC, Suleimani Matola ambaye ni kocha msaidizi wa mabingwa hao mara 19 wa kihistoria wa Tanzania Bara amesema kuwa timu yake ilimuhitaji zaidi kiungo Mkenya, Paul Kiongera lakini kutokuwa na uhakika wa urejeo wake uwanjani wanalazimika kuweka mbinu zao kwa Sserenkuma wakati huu wakihitaji kurudisha ubingwa wa ligi ambao mara ya mwisho waliutwaa msimu wa 2011/12.
Matola amesema kuwa Simba inatakiwa kumsajili mlinzi wa kati licha ya kumpandisha kutoka kikosi pili kijana,, Hassan . Simba ilihitaji kiungo-mbunifu katika eneo lake la mbele, Sserenkuma mwenye kasi, chenga, mpigaji hodari wa mipira iliyokufa, mfungaji makini, ni mchezaji mwenye maarifa mengi binafsi ambaye wakati mwingine anaweza kuibeba timu nzima katika mabega yake na kuipatia matokeo.(P.T)
Usajili wa dirisha kubwa ulifanywa kwa pupa, haukukidhi mahitaji muhimu ya nafasi lakini hilo linaweza ‘ kusahihishwa’ vizuri na usajili huu mdogo, na Matola amekiri wazi kuwa Sserenkuma ni chaguo ambalo Simba walilitaka. Uwepo wa Emmanuel Okwi, Amis Tambwe na Sserenkuma unaileta ‘ Simba Mpya katika msimu uleule’. Ushindi mara moja katika michezo saba ya mwanzo msimu huu ni matokeo mabaya.
Lakini faida kubwa kwa Simba ni kwamba timu za juu nazo hazikuwa na matokeo bora kuliko. Simba wapo nyuma kwa pointi tano dhidi ya viongozi Mtibwa Sugar. Kufunga mabao ilikuwa tatizo, lakini pia safu ya ulinzi ilikuwa na ‘ matobo’ ambayo yameruhusu mabao sita. Ni mechi mbili tu ambazo Simba haijaruhusu bao ( Yanga SC 0-0 Simba SC, Simba 1-0 Ruvu Shooting), wamefunga mabao saba katika michezo saba, ila hawajafunga katika mchezo mmoja tu.
Hii ni dalili na ubora wa timu, lakini katika ligi yenye mabadiliko ya kimbinu na ufundi, wachezaji kama Sserenkuma ni wa lazima kwa timu yenye malengo makubwa. Kuelekea mchezo wa hisani ‘ Nani Mtani Jembe-2′ kati ya Simba na Yanga wiki ijayo, Simba hawatajali sana matokeo, ila hawatapenda kufungwa na mahasimu wao, watatazama vizuri uwiano wa kiuchezaji kati ya idara na idara, kiucheza
TAMBWE, OKWI, SSERENKUMA,
Ni mfumo gani ambao utawapanga ‘ nyota watatu wa kimataifa’ katika safu ya mashambulizi?. Nani ambaye atafurahi kuona Tambwe akizungukwa na Okwi akitokea upande wa kushoto, Sserenkuma akitokea upande wa kulia na guu lake la kushoto?. Wakati wa kilele cha mafanikio ya FC Barcelona barani Ulaya, David Villa, Pedro Rodriguez na Leo Messi walitengeneza utatu wa hatari katika safu ya mashambulizi, hii ndiyo safu ya mashambulizi iliyomtetemesha, Sir Alex Ferguson pale Wembley, Mei, 2011 katika fainali ya mabingwa ulaya.
22
Katikati ya uwanja walikuwa na ‘ pass-masters, Xavi Hernandez, Andres Iniesta ambao walisaidiwa katika ukabaji na kijana mahiri katika upokonyaji wa mipira na kuanzisha pasi sahihi kwa wenzake, Sergio Busquets. Kila mtu wa soka anakumbuka kuhusu ubora wa ‘ Barca ya Pep Guardiola’ katika mfumo wa 4-3-3. Je, Patrick Phiri anaweza ku-copy na ku-paste na kuifanya Simba kucheza huru na kupata matokeo katika mfumo ambao ulimpatia mafanikio makubwa Pep?.
Phiri anaweza sababu alishafanikiwa kwa matumizi Ya mfumo huo. Ujanja wa Okwi katika ufungaji na utengenezaji wa nafasi za mabao kwa wenzake. Okwi amefunga mabao matatu msimu huu, Tambwe amefunga bao moja, wakati Danny anatua akiwa na tuzo ya ufungaji bora kutoka KPL. Itashangaza kama Simba wataendelea kufunga kwa ku-bahatisha mara baada ya ujio wa Sserenkuma.
ndiyo kwenye soka, majina makubwa si kigezo cha ushindi, lakini mafanikio binafsi ya Tambwe, Okwi na Sserenkuma yanawatambulisha kama wachezaji bora kutoka nje ya nchi ambao wapo katika ligi kuu ya Tanzania Bara. Utulivu, uvumilivu, u-tayari, uwajibikaji ni baadhi ya mambo muhimu ambayo wachezaji wanatakiwa kuwa nayo, ata mashabiki, wanachama na viongozi wa klabu.
Kilicho muhimu zaidi ni mbinu za mwalimu na namna wachezaji wake watakavyoweza kuchukua mafunzo kutoka katika viwanja vya mazoezi na kwenda nayo katika michezo rasmi huku wakiwafanya kwa kiwango kisichopungua asilimia 70-65.
Chanzo:http://shaffihdauda.co.tz/

Urusi lazima ijitegemee:Putin 

Rais Vladimir Putin amewaonya wananchi wa Urusi kuwa watakabiliwa na wakati mgumu siku za usoni na kuwataka kujitegemea, amesema katika hotuba yake kwa taifa akilihutubia bunge.
Urusi imeathirika kwa kiasi kikubwa kiuchumi kutokana na kushuka kwa bei za mafuta na vikwazo kutoka nchi za magharibi vilivyowekwa dhidi ya Urusi kwa kujiingiza katika mgogoro wa nchi jirani ya Ukraine.
Sarafu ya Urusi ya rouble, ikiwa ishara ya utulivu chini ya utawala wa Bwana Putin, ilipata anguko kubwa la siku moja, Jumatatu kuwahi kushuhudiwa tangu mwaka 1998.
Serikali imeonya kuwa Urusi itaingia katika kipindi cha mtuamo mwaka ujao.
Akizungumza na mabaraza yote mawili ya bunge la Kremlin, Bwana Putin pia amezishutumu serikali za magharibi kutaka kuiwekea Urusi vikwazo vipya.
Ameeleza kuwa hajutii kulitwaa jimbo la Ukraine la Crimea, akisema eneo hilo lina maana kubwa kwa Urusi.
Amesisitiza kuwa mkasa huo kusini mashariki mwa Ukraine umethibitisha sera ya Urusikuwa ilikuwa sahihi lakini amesema Urusi itaheshimu jirani yake Ukraine kama nchi ndugu.
Akizungumza mjini Basel Uswisi, waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry amesema nchi za magharibi hazitaki vita na Urusi.
"Hakuna anayenufaika na mvutano huu... Si mtindo wetu au matamanio yetu kuona Urusi ikitengwa kutokana na vitendo vyake yenyewe," amesema Bwana Kerry.
Urusi itaweza kujenga upya imani, amesema, kwa kuondoa misaada kwa waasi wanaotaka kujitenga mashariki mwa.CHANZO:BBC

Ndege ya KDF yaanguka Somalia


Ndege ya jeshi la KDF nchini Kenya imeanguka katika eneo la Kismayu nchini Somali.
Ndege hiyo ilianguka siku ya Alhamisi mwendo wa saa tisa na robo ilipokuwa ikirudi Kenya baada ya kutekeleza mashambulizi katika eneo la Jamaame kusini mwa Somalia.
Kulingana na msemaji wa Jeshi kanali david Obonyo: ''Ndege ya KDF iliokuwa ikirudi nchini Kenya baada ya kufanya mashambulizi katika eneo la Jamaame kusini mwa Somali,ilikumbwa na matatizo ya kiufundi na kuanguka katika eneo la Kismayu .
Kanali Obonyo hata hivyo hakusema iwapo kulikuwa na majeruhi yoyote.
Jeshi la Kenya limesema kuwa ndege hiyo ilianguka kutokana na hitilafu za kimitambo baada ya kufanya oparesheni katika eneo la Jamaane Kusini mwa Somalia.
Hata hivyo baadhi ya mitandaoa iliyohusishwa na kundi la AL shabaab imechapisha habari kuwa AL shabaab wamedai kuwa ndio waliodungua ndege hiyo mwendo wa saa tisa Alasiri, Afrika Mashariki.
Msemaji wa kiksoi cha kivita cha Al shabaab Sheikh Abdi Azizi Abu Musab amenukuliwa akisema kuwa walishambulia ndege hiyo kwa kombora baada ya kulipua kijiji cha Bulaguduud.
Kwa mujibu wa mwandishi wa BBC wa idhaa ya kisomali, ni vigumu kwa Al Shabaab kufanya shambulio kama hilo katika mji wa Kismayu kwa kuwa eneo hilo zima limefurika vikosi vya usalama vya AMISOM.
Mnamo mwaka wa 2012, majeshi ya Kenya yaliuteka mji wa bandari wa Kismayu, unaotazamiwa kuwa mji muhimu sana wa kiuchumi katika eneo zima la Somalia kutoka kwa wanamgombo hao wa Al shabaab.CHANZO:BBC

Wednesday, December 3, 2014

Kama ulisikia kuhusu yale mauaji ya Wanawake Dar es salaam, kuna hii taarifa mpya.

Dar yetu
Picha kutoka #DARYETU @Daryetu on Instagram
Kama ulisikia kuhusu mauji ya Wanawake mbalimbali kwenye jiji la Dar es salaam utakua ulitamani kujua wanaohusika manake stori zilikua zinaripotiwa tu na taarifa zinazoambatana nazo ni kwamba uchunguzi unaendelea.
Sasa mpaka sasa unaambiwa ni zaidi ya Wanawake 11 wameuawa Dar es Salaam katika kipindi cha miaka miwili na kutupwa barabarani au mitaroni huku miili yao ikiwa imefanyiwa vitendo vya unyama na udhalilishaji.
Kutokana na mauaji kuendelea, Polisi wamefanikiwa kuwakamata watu wawili akiwemo ABOUBAKAR KASSANGA Mkazi wa Mwenge na EZEKIEL ASENEGALA mkazi wa Tandika Dar es Salaam ambao wamekiri kuhusika na vitendo hivyo ndani ya kipindi cha miaka miwili.
Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam SULEIMAN KOVA amesema baada ya kuwahoji watuhumiwa hao ambao pia wamekiri kuwauwa wasichana wawili hivi karibuni waliotajwa kwa majina ya WANZE MAKONGORO na JACKLIN MASSANJA wamesema wamekuwa wakiwalaghai wasichana kimapenzi na badae kuwaua.
Katika hatua nyingine Kamishna KOVA ametoa tahadhari kwa wasichana kuacha tabia ya kuwa na uhusiano wa kimapenzi wa ghafla na watu wasiowafahamu ambapo tukio la mauaji ya wasichana hao wawili lilitokea Novemba 19 mwaka huu ambapo baadhi ya vitu vinavyosadikiwa kuwa vya wasichana hao vimekutwa mahala wanapoishi watuhumiwa hao.
Kamishna KOVA amesema upelelezi bado unaendelea ili kuunasa mtandao mzima wa uhalifu huo.

Tuesday, December 2, 2014

Maamuzi ya Rais Kenyatta kwa Mawaziri wake kufuatia kuendelea kwa mashambulizi ya kigaidi Kenya

Quit job key in place of enter key
Baada ya nchi hiyo kuelemewa na mashambulizi mara kwa mara na shinikizo la wananchi Rais Uhuru Kenyatta amemwachisha kazi  Waziri wa Usalama Joseph Ole Lenku na kumteua Waziri mpya wa Usalama Joseph Nkaiseri, kuchukua nafasi hiyo huku  Inspekta Jenerali wa Polisi David Kimaiyo akilazimishwa kuachia ngazi.
Baada ya lile shambulio la siku kumi zilizopita ambapo kundi la Al Shabaab liliwaua abiria 28 waliokuwa wanasafiri kwa basi kutoka Mjini Mandera karibu na mpaka wa Somalia, Kimaiyo na Ole Lenku wamekuwa wakikabiliwa na shinikizo za kujiuzulu kufuatia kukithiri kwa mashambulizi ya kigaidi na kuhatarisha  usalama, ambapo jana Novemba 02 wachimba kokoto 36 wameuawa na kikundi cha Al Shaabab katika kaunti ya Mandera.
… Hapa ni mahali tukemekaa kama mimi mwenyewe nimekaa miaka tisa ile mambo nashuhudia saa hii sijawahi jionea na macho yangu watu kuuliwa sijawahi ona, by the way maisha yetu iko hatarini…
“...Nakimbilia usalama wangu juu nahofia pale kwa nyumba hujui watavamia lini  watakuja lini, saa ndio natoka kwangu kwa nyumba nakaa nakuja kukaa hapa kulingana na ile mazingira tunayo  nakaa hapa kupata ulinzi wa Serikali inakuwa ni ngumu sana, sisi ndio tunafanya msituni tulio eneo la hapa Mandera Town wavamivi wanavyokuja wanapita njia za misituni sasa Polisi kujua ni ngumu…
Rais Kenyatta amesema kuwa baada ya mazungumzo na Kimaiyo alikubali kustaafu mapema kwa sababu zake binafsi.

Monday, December 1, 2014

Kuhusu mkataba wa Gerard , stori hii hapa.

Football - FA Premier League - Liverpool FC v Tottenham Hotspur FC
Baada ya kuwepo kwa uvumi kuhusiana na mustakabali wa muda mrefu wa nahodha wa klabu ya Liverpool hatimaye uongozi wa klabu hiyo umeibuka na kumpa ofa ya kumuongezea star huyo mkataba .
Gerard kimsingi anamaliza mkataba wake na klabu hiyo na ndani ya siku 31 zijazo atakuwa huru kuanza mazungumzo na klabu nyingine pasipo hata kuomba ruhusa toka kwa Liverpool kama ilivyo utaratibu wa mikataba .
Liverpool imepeleka ofa ya kwanza ya kumuongezea Gerard mkataba huku ikikanusha kuwa haijawahi kuzungumzia suala la kumpa mkataba ambao una thamani ya nusu ya maslahi anayoyapata kwa sasa .
stevie g
Taarifa za Gerard kuongezewa kupewa ofa ya mkataba mpya ilifichuliwa na kocha wa klabu hiyo Brendan Rogers ambaye amesema kuwa Liverpool inafahamu mchango wa mchezaji huyo kwenye historia yake na haiwezi kumkosea heshima kwa kumpa ofa ambayo iko chini ya kile anachopata kwa sasa .
Kocha huyo wa Liverpool pia alikanusha habari za kuwepo kwa uhusiano mbaya kati yake na Gerard baada ya kuvuma kwa habari kuwa nahodha huyo alikerwa na kitendo cha kuwekwa benchi kwneye mchezo dhidi ya Real Madrid huko Santiago Bernabeu na kwenye mchezo wa jumamosi iliyopita ambao Liverpool ilishinda 1-0 dhidi ya Stoke City .
Gerrard-1-1024x768
Rogers amefafanua kuwa anafahamu kwamba Gerard ni mchezaji muhimu lakini hawezi kucheza mechi zote au dakika zote  90 kwenye kila mechi hivyo ni muhimu kupumzika kutokana na umri wake kuwa mkubwa .
Hata hivyo bado Gerard mwenyewe hajathibitisha kuwa atasaini mkataba mpya au la japo ishara zote zinaelekea nahodha huyo kusaini mkataba huo kutokana na mapenzi makubwa aliyo nayo kwa Liverpool ambayo ndio klabu pekee aliyoichezea tangu mwanzo wa maisha yake kama mchezaji na inatarajiwa kuwa atastaafu akiwa na klabu hiyo .
_The_player_of_Liverpool_Steven_with_another_trophy_048859_

Picha za gari ya David Beckham baada ya ajali 

becks 2
Moja kati ya story zilizoshtua wapenda michezo nchini England mwishoni mwa wiki hii ni ajali ambayo aliipata nyota wa zamani wa Manchester United na Real Madrid pamoja na timu ya taifa ya England David Beckham .
Becks alipata mkasa huo wakati akiwa anatoka kumchukua mwanae anayefahamika kwa jina la Brooklyn toka kwenye mazoezi ya kila siku ya timu yake ya Arsenal .
Gari la David Beckham aina ya Audi likiwa limeharibika vibaya baada ya ajali aliyoipata mwishoni mwa wiki iliyopita .
Gari la David Beckham aina ya Audi likiwa limeharibika vibaya baada ya ajali aliyoipata mwishoni mwa wiki iliyopita .
Gari ya Beckham aina ya Audi iligongana na gari nyingine ndogo na star huyo alipata jeraha kwenye bega lake japo halikuwa jeraha kubwa sana .
Picha inayoonyesha magari mawili likiwemo la David Beckham lililopo upande wa kulia baada ya ajali aliyoipata star huyo.
Picha inayoonyesha magari mawili likiwemo la David Beckham lililopo upande wa kulia baada ya ajali aliyoipata star huyo.
Mtoto wa star huyo Brooklyn amabye ni mchezaji wa timu ya Vijana ya Arsenal hakuumia kwenye ajali hiyo ambayo magari yote yaliyohusika yaliharibika vibaya .
Picha inayoonyesha familia nzima ya Beckham akiwa na mkewe Victoria Beckham na wanae wa kiume Brooklyn , Romeo na Cruz.
Picha inayoonyesha familia nzima ya Beckham akiwa na mkewe Victoria Beckham na wanae wa kiume Brooklyn , Romeo na Cruz.

Thierry Henry kurudi Arsenal?

titi enzi hizo
Nyota wa zamani wa Arsenal Thierry Henry ameiaga timu yake ya New York Red Bulls aliyokuwa anaichezea baada ya mkataba wake kuisha .
Henry ameichezea Red Bulls kwa muda wa miaka minne na nusu na inadhaniwa kuwa huenda akatangaza kustaafu soka baada ya kuwa kwenye mchezo huo kwa karibu miaka 20 .
Henry ambaye katika ubora wake aliwahi kuzichezea timu za As Monaco , Juventus , Arsenal na Fc Barcelona ukiachilia mbali timu ya taifa ya Ufaransa alinukuliwa akisema kuwa angependa kurejea kwenye klabu yake ya zamani ya Arsenal ambako inaaminika kuwa atajiunga na benchi la ufundi chini ya kocha wake wa zamani Arsene Wenger .
henry
Moja ya ishara zilizowapa watu sababu ya kuamini kuwa huenda kuna mpango wa nyota huyo kurejea Arsenal ni kitendo chake cha kubadili picha ya ukurasa wake rasmi wa mtandao wa kijamii wa Facebook ambapo alitoa picha inayomuonyesha akwia amevalia jezi ya New York Red Bulls na kuweka picha ya uwanja wa nyumbani wa Arsenal The Emirates Stadium .
Timeline ya ukurasa rasmi wa facebook wa Thiery Henry ikionyesha uwanja wa Emirates unaotumiwa na Arsenal .
Timeline ya ukurasa rasmi wa facebook wa Thiery Henry ikionyesha uwanja wa Emirates unaotumiwa na Arsenal .
Henry hadi leo anashika nafasi ya nne kwenye orodha ya wafungaji bora wa ligi kuu ya England katika historia ya ligi hiyo na amewahi kutwaa mataji karibu yote kluanzia kombe la dunia na kombe la ulaya akiwa na timu ya taifa ya Ufaransa , Ligi za England na Hispania pamoja na ligi ya mabingwa barani ulaya .
Kocha wa klabu ya Girondins Bordeaux Willy Sagnol ambaye aliwahi kucheza na Henry kwenye timu ya taifa ya Ufaransa amemkaribisha nyota huyo kujiunga naye kwenye benchi la ufundi la klabu hiyo inayoshiriki ligi ya Ufaransa ofa ambayo Henry bado hajakubali au kutoa tamko la kuikataa .
titi
Henry alijiunga na New York Red Bulls wakati mkataba wake na Fc Barcelona ulipomalizika na amekuwa moja kati ya wachezaji walisaidia kupandisha umaarufu kwenye ligi ya Marekani maarufu kama MLS .

Mchezaji bora wa Afrika huyu hapa 

FBL-WC-2014-MATCH54-GER-ALG
Kituo cha habari cha Uingereza  BBC kimemtaja nyota wa timu ya taifa ya Algeria Yacine Brahimi kuwa mchezaji bora wa Afrika kwa mwaka 2014.
Brahimi ambaye anachezea klabu ya Ureno ya Fc Porto anakuwa raia wa kwanza wa Algeria kutwaa tuzo hiyo ambayo hutolewa na BBC kila mwaka .
Yacine Brahimi ametwaa tuzo ya BBC ya mchezaji bora wa Afrika .
Yacine Brahimi ametwaa tuzo ya BBC ya mchezaji bora wa Afrika .
Brahimi ametwaa tuzo hii kufuatia uwezo aliouonyesha kwa mwa huu akiwa na timu yake ya taifa hasa kwenye michuano ya kombe la dunia ambako Algeria walifanikiwa kufika hatua ya 16 bora .
BBC imekuwa na utaratibu wa kuandaa tuzo hizi kila mwaka ambapo kwa miaka miwili iliyopita kiungo wa Ivory Coast Yaya Toure amekuwa akitawala .
yacine