TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Friday, January 23, 2015

Matokeo Zambia kutolewa wakati wowote


Matokeo ya kura za urais nchini Zambia sasa yameanza kukamilika katika ukumbi wa kimataifa wa Mulungushi makao makuu ya kuhesabia kura .
Matokeo yaliotolewa na tume ya uchaguzi ya Zambia Usiku wa kuamkia leo yanaonyesha kuwa Edgar Lungu mgombea wa chama tawala cha
Patriotic Front mpaka sasa bado anaongoza akiwa na kura 670397 huku mpinzani wake HakaindeHachilema wa chama cha United Party for National Development akiwa karibu sana nae kwa kura 641343.
Hivo Edgar Lungu anaongoza kwa 48.8 % na hali Hakainde Hachilema akiwa na 46,9 % na Bi Nanakwi mwanamke pekee kwenye kinyanganyiro hicho yuko nafasi ya 3 akiwa na kura 11 260 (0. 268 % )
Kwa jumla kura million 1 371 778 ndizo zimeisabiwa kutoka majimbo 111 ikiwa sasa imebakia majimbo 39 tu .CHANZO:BBC

BALOZI SEIF ASHIRIKI HARAMBEE CHUO CHA CBE 

unnamed (50)
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ally Idd akikabidhi mchango wake wa shilingi milioni 3 kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Uongozi ya Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Prof. Mathew Luhanga (katikati) kusaidia uboreshaji wa miundombinu ya chuo hicho jana usiku wakati wa harambee maalum ya ukusanyaji wa fedha iliyofanyika Hotel ya Serena jijini Dar es salamm.Kulia ni Mkuu wa Chuo hicho
unnamed (51)
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ally Idd na viongozi wa Chuo cha CBE wakitoa mkono wa shukrani kwa wadau mbalimbali waliotoa michango yao wakati wa harambee ya kuchangia maendeleo ya chuo cha CBE jana usiku jijini Dar es salaam wakati wa kilele cha maadhimisho ya miaka 50 ya chuo hicho .
unnamed (52)
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ally Idd akisoma majumuisho ya michango na ahadi zilizotolewa na wadau mbalimbali waliohudhuria harambee ya kuchangia maendeleo ya Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) jana usiku jijini Dar es salaam. Kiasi cha shilingi milioni mia tano arobaini, laki nane na elfu ishrini na tisa (540,829,000/=) zikiwa ni ahadi na fedha taslimu zilikusanywa.

WAZIRI WA FEDHA SAADA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA KARIAKOO NA MTAA WA NAMANGA


Waziri wa Fedha Saada Mkuya Salum (wa pili kulia) akiongoza na viongozi wa mkoa wa kodi wa Ilala kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) pamoja na maafisa wa Serikali alipofanya ziara ya kushtukiza leo jijini Dar es salaam katika soko la Kariakoo kujionea namna wafanyabiashara wanavyozingatia na kusimamia matumizi ya mashine za kielektroniki za EFD ambazo wanazopaswa kuzitumia mara wanapouza bidhaa zao ili kusaidia Serikali kukusanya mapato na kuboresha utoaji wa huduma za jamii nchini. Wa kwanza kulia ni Kaimu Msaidizi wa Meneja wa mkoa wa kodi wa Ilala kutoka TRA Hamidu Athmani, wa kwanza kushoto ni Kaimu Meneja wa mkoa wa kodi wa Ilala Elias Balongo na kushoto mwa Waziri ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Prof. Adolf Mkenda.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Prof. Adolf Mkenda (wa kwanza kushoto) akiteta jambo na Waziri wa Fedha Saada Mkuya Salum (wa pili kushoto) katika ziara ya kushtukiza katika soko la Kariakoo kujionea namna wafanyabiashara wanavyozingatia na kusimamia matumizi ya mashine za kielektroniki za EFD ambazo wanazopaswa kuzitumia mara wanapouza bidhaa zao ili kusaidia Serikali kukusanya mapato na kuboresha utoaji wa huduma za jamii nchini. Aliyevaa tai kulia ni wa kwanza kulia ni Kaimu Msaidizi wa Meneja wa mkoa wa kodi wa Ilala kutoka TRA Hamidu Athmani.

 Wananchi wakifuatilia ziara ya kushtukiza ya Waziri wa Fedha Saada Mkuya Salum aliyofanya leo jijini Dar es salaam katika soko la Kariakoo kujionea namna wafanyabiashara wanavyozingatia na kusimamia matumizi ya mashine za kielektroniki za EFD ambazo wanazopaswa kuzitumia mara wanapouza bidhaa zao ili kusaidia Serikali kukusanya mapato na kuboresha utoaji wa huduma za jamii nchini.

TIMU YA ARSENAL YAFANYA MAZUNGUMZO NA KAMPUNI YA TTCL

Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara wa Timu maarufu ya mpira wa miguu duniani ya Arsenal, Dam Stone (kulia) akipokea zawadi kutoka Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) iliyokabidhiwa na Meneja wa Masoko na Usambazaji wa TTCL, Robart Noel kabla ya kuanza mazungumzo ya kibiashara kati ya pande hizo mbili.
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara wa Timu maarufu ya mpira wa miguu duniani ya Arsenal, Dam Stone (kulia) akipokea zawadi kutoka Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) iliyokabidhiwa na Meneja wa Masoko na Usambazaji wa TTCL, Robart Noel kabla ya kuanza mazungumzo ya kibiashara kati ya pande hizo mbili

Thursday, January 22, 2015

Tayari hukumu ya kesi ya Rihanna na waliotumia picha yake kwenye nguo imetolewa

Rihanna Bebz 
Kuna vitu ambavyo Bongo mara nyingi watu huwa hawafuatilii lakini kumbe upande mwingine ni big deal.
Kuna siku nimekutana na tshirt zenye picha za mastaa wa Bongo zikiwa zinauzwa kwenye duka moja town, sina uhakika kama ni kweli wasanii husika wanahusishwa kwenye biashara hii!
Story kutoka Uingereza, Mahakama ya rufaa London imetoa hukumu ya kesi ya madai kati ya Rihanna na duka la Topshop Arcadia ambalo linauza nguo, Rihanna aliwashtaki kwa kuuza nguo zenye picha yake bila kuwa na makubaliano yoyote na duka hilo.
Kesi hiyo ilitolewa hukumu mwaka 2013, wenye duka wakatakiwa kulia fidia ya dola laki 5 lakini wakakata rufaa ambayo kwenye hukumu ya Mahakama ya rufaa, Rihanna kashinda tena.
bil
Hii ni moja ya Tshirt yenye picha ya Rihanna

Wednesday, January 21, 2015

WAZIRI WA MAJI JUMANNE MAGHEMBE AMETOA SIKU 90, KWA MKANDARASI MEGHA ENGINEERING

unnamed (2)
Waziri wa maji Jumanne Maghembe wa kwanza kulia akizungumza na wakandarasi wanaojenga bomba la maji la Mlandizi Kimara Januari 20, 2015 mkoani Pwani wakati alipotembelea tembelea miradi ya maji inayosimamiwa na Mamlaka ya Maji Safi na maji Taka (DAWASA), kwalengo la kupata tathimini ya mradi huo ulipofikia sasa.
unnamed (4)
Waziri wa Maji Jumanne Maghembe wapili kulia akioneshwa mchoro wa mradi wa bomba la maji mlandizi kimara linalopitia makongo juu na Mhandisi wa Mradi huo, Bw Severin Mkendala jinsi mabomba mradi wa mlandizi kimara yalipopita .
unnamed (10)
Waziri wa maji Jumanne Mghembe wa pili kulia akiwa ameongozana na meneja mradi Pintu Dutta watatu kulia wakati akikagua maendeleo ya mradi wa kituo cha kusafisha maji cha ruvu juu .
unnamed (5)
Wafanyakazi wa kampuni ya WABAG Constraction wakiendela na ujenzi wa wa kituo cha kuasfisha maji cha ruvu juu .
WAZIRI wa maji Jumanne Maghembe ametoa siku 90, kwa mkandarasi Megha Engineering Infrastructure Limitedi anaesambaza bomba la maji mradi wa Mlandizi Kimara kufanikisha mradi huo na kupeleka ripoti ya maradi,mamlka ya maji safi na maji taka (Dawasco), kwalengo la kupata tathimini ya mradi.
Alitoa agizo hilo Januari 20, 2015 mkoani Pwani wakati akikagua miradi minne ya Dawasco,yakusambaza maji Ruvu juu na Ruvu Chini kufikisha Jijini Dar es Salaam.
Alisema,mpaka sasa mkandarasi alitakiwa aweamelaza kilomita 20,lakini chakushangaza mkandarasi huyo amelaza kilomita 12,tu.
Maghembe alisema utendaji kazi wa mkandarasi huyo ni mbovu na nimewaagiza wabadilike na nitakuja kuwatembelea baada ya siku 90,na kama hakutakuwa na maendeleo itabidi tuwafukuze.
"tumempatia mkandarasio huyu kiasi cha dola za kimarikani 59,ambao nisawa na bilioni 96 za kitanzani fedha hizi watanzania watazilipa hivyo ni vema mkandarasi huyu afanye kazi iliyomleta,"alisema Maghembe
Kwaupande wa maradi wa Ruvu juu wa kusafisha maji Waziri Maghembe aliridhika na utendaji kazi wa mkandarasi anayejenga mradi huo na kumtaka amalizie kufunga pampu mpya ili mgao wa maji upungue Dar es Salaam.
Aidha alimwagiza Mkurugenzi Mkuu wa DAWASA Arcado Mutalemwa kuhakikisha pampu zilizokwama bandarini zinafika leo na kufungwa siku ya Alhamisi.

TEMBO, SIMBA WASIOFUGIKA WANUSURIKA AFCON 

Doumbia-Inaction-150120SS720
MIAMBA ya soka kutoka Magharibi mwa Afrika, Ivory Coast imeanza kwa sare ya 1-1 dhidi ya Guinea katika mechi ya kundi D , michuano ya mataifa ya Afrika inayoendelea huko Guinea ya Ikweta.
Guinea walikuwa wa kwanza kufunga goli katika dakika 36' kipindi cha kwanza kupitia kwa nyota wake Mohamed Yattara, hata hivyo Ivory Coasta walisawazisha dakika ya 72' kupitia kwa Seydou Doumbia.
Nayo mechi ya pili ya kundi kund hilo baina ya Mali na Cameroon imemalizika kwa sare ya 1-1.(P.T)
Mali waliandika bao la kuongoza dakika ya 71' kupitia kwa Yambou Yatabare, lakini Simba wasiofugika, Cameroon wakasawazisha kupitia kwa Ambroise Oyongo Bitolo.
Kufuatia kumalizika kwa mechi za kwanza za kundi D, michuano hiyo leo inaendelea kwa mzunguko wa pili wa makundi.
Timu za kundi A zinaanza kutupa karata yao ya pili ambapo mechi ya kwanza itawakutanisha wenyeji Guinea ya Ikweta dhidi ya Burkinafaso ambao walipoteza mechi ya kwanza kwa mabao 2-0 dhidi ya Gabon.
Mechi ya pili inayoanza majira ya saa 4:00 usiku leo, itawakutanisha Congo na Gabon.
Chanzo:Shaffihdauda

Wanamgambo wa Kishia walivamia Ikulu ya rais

Vizuizi vya kikosi kinachotoa ulinzi wa taasisi za nchi kwenye barabara inayoelekea kwenye Ikulu ya rais katika mji wa Sanaa, Januari 20 mwaka 2015.
Vizuizi vya kikosi kinachotoa ulinzi wa taasisi za nchi kwenye barabara inayoelekea kwenye Ikulu ya rais katika mji wa Sanaa, Januari 20 mwaka 2015.
Na RFI
Kwa mujibu wa afisa wa kijeshi aliyenukuliwa na shirika la habari la Ufaransa AFP, wanamgambo wa Kishia waliokua wameizingira Ikulu ya rais, wameendesha mashambulizi na kwa sasa wanadhibiti boma la rais.
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limefanya mkutano wa dharura bila hata hivyo kutomriuhusu mtu yeyote asiyekua muhusika kushiriki mkutano huo.(P.T)
Kulingana na vyanzo viliyonukuliwa na mashirika ya habari Reuters na AFP, wanamgambo wa Kishia waliitdhibiti Ikulu ya rais.
Inaonekana kuwa kikosi kilichokua kinatoa ulinzi wa rais kilindoka katika eneo hilo kabla ya kushambuliwa na wanamgambo hao wa Kishia.
Mapigano yanaendelea karibu na boma la rais wa Yemen, bila hata hivyo kujua hatima ya rais, Abd Rabbo Mansour Hadi. Wakati huohuo, makazi ya Waziri Mkuu bado yanaendelea kuzingirwa na watu wenye silaha wakizuia barabara kuu inazoelekea kwenye makaazi hayo.
Miezi minne baada ya kuingia katika mji mkuu wa Yemen, inaonekana kuwa wanamgambo wa Ansaroullah wameamua kuongeza nguvu dhidi ya utawala uliopo sasa, huku wakiendelea kudhibiti maeneo muhimu ya mji mkuu wa Yemen. Kwa kutaka kutetea hoja yao, wanamgambo wa Kishia wanalani muswada wa Katiba, wakibaini kwamba unawakandamiza raia.
Kulingana na waangalizi wengi, wanamgambo wa Kishia, katika mashambulizi yao mapya wanaufaika na msaada kutoka moja kwa moja kwa wafuasi wa rais wa zamani wa Yemen, Ali Abdullah Saleh, ambaye alitimuliwa madarakani mwaka 2012 baada ya kuongoza Yemen kwa miongo mitatu.

Rais Obama ataka mgao sawa wa rasilimali

Rais wa Marekani Barak Obama, amesema Marekani inafanya mabadiliko ya kiuchumi na kijamii baada ya miaka mingi ya kujirudia kwa mdororo wa uchumi na vita, huku uchumi ukiongeza ajira kwa kasi kubwa kuliko wakati wowote tangu mwaka 1999.
Pia amesema Wamarekani wengi zaidi wana bima za afya kuliko wakati wowote kabla ya hapo.
Akihutubia taifa kupitia baraza la Congress lenye wajumbe wengi kutoka chama cha Republican, Rais Obama ametumia hotuba hiyo kutangaza mpango wa kujenga uchumi wa kati kwa wananchi wote wa Marekani, ambapo wananchi wa kipato cha chini watapata huduma za afya na elimu kwa gharama nafuu.
Rais Obama ametangaza hatua za kusaidia familia za wafanyakazi kunufaika kutokana na kukua kwa uchumi.Mkakati wa Bwana Obama anaouelezea kama uchumi wa daraja la kati, unahusisha kupandisha kodi kwa matajiri.
Hotuba ya Rais Obama ilibeba mapendekezo kuhusu kodi, vyuo vya jamii, huduma za internet, usalama katika mtandao wa komputa na likizo ya ugonjwa.
Bwana Obama amesema hali ya kutoka katika mdororo wa uchumi imetoa fursa ya kuongezeka kwa kipato na fursa kwa kila mtu.
Amesema uchumi wa daraja la kati ni wazo kwamba nchi hiyo inafanya vizuri kabisa wakati kila mtu anapata haki katika mapato na kila mtu anatendewa haki kama ilivyoanishwa katika sheria za nchi hiyo.
Mpango wake wa kuongeza kodi kufikia dola bilioni 320 katika kipindi cha zaidi ya miaka kumi ni pamoja na kuziba mianya ya kukwepa kodi kwa wenye vipato vikubwa, ambapo matajiri wakubwa watalipa kodi ya kukua kwa mtaji kutoka asilimia 23.8% hadi asilimia 28%.

Tuesday, January 20, 2015

Kuhusu ile ishu ya Wanafunzi kupigwa mabomu ya machozi Kenya, iko hapa kauli ya Rais Kenyatta

uhunye
Waziri wa usalama nchini Kenya, Joseph Nkaissery amewaomba radhi  wanafunzi wa shule ya msingi ya Lang’ata baada ya  kupigwa mabomu ya machozi jana walipoandamana kupinga kunyang’anywa kipande cha ardhi ambacho kilikuwa uwanja wao wa kuchezea.
Jana hata hawataki tusherehekee, tukicheza wanatupiga na rungu wanatuletea madogi”– Mwanafunzi.
0
Waziri wa usalama Kenya, Joseph Nkaissery.
Rais Uhuru Kenyatta amelaani tukio hilo na  kumtaka Waziri wa Ardhi,  Charity Ngilu na Mwenyekiti wa Tume ya Ardhi,  Mohammed Swazuri kuwajibika na kueleza kwanini walizembea, huku Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo pia kalaumiwa kwa kusindwa kuzuia watoto hao kujihusisha na vurugu.
Bado haijafahamika ni nani aliyehusika na ujenzi huo.

Wampinga Kabila kuwania urais nchini DRC

Rais wa Drc Congo Joseph Kabila
Polisi nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo wamewafyatulia risasi waandamanaji kwenye mji mkuu Kinshasa walio na hasira katika kile kinachoonekana kama jitihada za kutaka kuongoza uongozi wa rais Joseph Kabila.
Watu kadha walitolewa eneo la kati kati mwa mji wakiwa na majeraha ya risasi ambapo pia kulitoka makabiliano kwenye chuo kikuu cha mji huo.
Milio ya risasi iliripotiwa katika maandamano mengine katika mji ulio mashariki wa Goma.
Watu kadhaa walipatikana na majeruhi ya risasi katikati mwa mji huo huku ghasia zengine zikiripotiwa katika katika chuo kimoja kikuu.
Viongozi wa upinzani waliitisha maandamano hayo baada ya bunge dogo kuidhinisha sheria siku ya jumamosi inayoagiza kufanyika kwa hesabu ya idadi ya watu kabla ya uchaguzi wa urais utakaofanyika mwaka ujao.
Wabunge hao wa upinzani wamesema kuwa mpango huo utachelewesha uchaguzi huo ambao umekuwa ukingojwa kwa hamu kwa miaka kadhaa.
Rais Joseph Kabila ambaye amekuwa mamlakani kwa miaka 15 amehudumu miula miwili na hawezi kuwania tena urais kulingana na katiba.
Bunge kuu linatarajiwa kuungazia mswada huo wa uchaguzi hii leo.

Nimekuletea taarifa hii ya matumaini kwa watu wa Mali kuhusu Ugonjwa wa Ebola

ebola_3022684b 
Mwaka 2014 haukuwa mwaka wenye story nzuri kutoka nchi za Afrika Magharibi kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola watu zaidi ya elfu kumi walifariki na wengine zaidi ya elfu tano wakiripotiwa kuugua ugonjwa huo.
Umoja ya Mataifa na Serikali ya Mali wametangaza kuwa nchi hiyo haina tena ugonjwa hatari  wa Ebola baada ya kutoripotiwa taarifa za mgonjwa yeyote wa Ebola kwa muda wa siku kipindi cha siku 42 zilizopita.
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kupambana na Ebola ulioandikwa katika ukurasa wa Twitter unawashukuru wafanyakazi wa Afya waliojitolea kupambana na Ebola nchini Mali kwa kuhakikisha ugonjwa huo umedhibitiwa.
Mbali na Mali kuonekana kuathiriwa na ugonjwa huo, Guinea, Sierra leone na Liberia ni mataifa ambayo yamepata athari kubwa kutokana na ugonjwa huo.
Waziri wa Afya wa Mali amewasifu wahudumu wa Afya  na washirika wa Kimataifa kwa msaada wao.

Pale ambapo Askari walitumia mabomu machozi kuwatawanya watoto walioandamana Kenya

watoto1 
Askari Polisi wa Kenya katika mji mkuu Nairobi leo wamewafyatulia mabomu ya machozi wanafunzi wa shule ya msingi Lang’ata waliokuwa wakiandamana kupinga kunyang’anywa ardhi ambayo ilikuwa kiwanja chao cha michezo.
watoto2
Polisi hao wakiwa na mbwa waliwatawanya wanafunzi ambao wengi wao inasemekana kuwa watoto wenye umri wa miaka sita baada ya kuangusha ukuta mpya uliojengwa katika eneo la shule.
watoto3
Baadhi yao walipelekewa hospitalini baada ya kupata majeraha madogo madogo huku polisi mmoja akiumizwa baada ya kupigwa jiwe usoni na wanafunzi.
Hii imetokea leo January 19, siku ambayo wanafunzi hao walifika shule kwa mara ya kwanza baada ya mgomo wa walimu uliokuwepo kwa wiki mbili kutokana na madai yao ya mishahara.

Huu ndio unyama alioufanya mama kwa mtoto wake ndani ya saa 24 baada ya kujifungua

new j
Mwanamke nchini Marekani anashikiliwa kwa tuhuma za mauaji baada ya kuamua kumweka mtoto wake aliyetoka kujifungua katikati ya barabara kisha kumchoma moto.
Mwendesha mashtaka aliyekua akisimamia kesi hiyo alisema mwanamke huyo Hyphernkemberly Dorvilier anashtakiwa kwa kosa la kuua kwa kukusudia.
Polisi walipofika eneo la tukio walimkuta mtoto huyo akiteketea kwa moto katikati ya barabara ya makazi ya watu ambayo ni maili 30 kutoka jiji la Mashariki mwa mji wa Philadelpia na kumkimbiza katika hospitali ya St. Christopher lakini alifariki masaa mawili baada ya tukio hilo.
Mashahidi walisema walimwona mama huyo akichoma kitu lakini hawakujua ni nini na walipomuuliza alisema alikuwa akichoma uchafu.

Mwaka mmoja umepita tangu afariki mtangazaji Komla Dumor, BBC imeandaa kumbukumbu hii.

W1_MH_896 
Mwaka mmoja umepita tangu afariki Komla Dumor, mmoja ya watangazaji maarufu sana wa kituo cha BBC, alikuwa akiendesha kipindi cha Focus on Africa.
Shirika la habari la BBC limetangaza kuandaa Tuzo kwa heshima ya mtangazaji huyo mwaka mmoja baada ya kifo chake kilichotokea January 18, 2014 London na kuzikwa January 22 nyumbani kwao Accra, Ghana.
Dumor alikuwa mwandishi na mtangazaji mwenye kipaji cha kipekee kutoka Ghana, huku akisifika Afrika na duniani kote kwa kufanya kazi kwa kujitolea ambapo alikuwa akitoa taswira tofauti kuhusu Afrika kwa dunia nzima.
Shirika la BBC limejitolea kuendeleza kazi ya Komla kwa kutangaza tuzo ya uandishi wa habari kwa heshima kama mwandishi mahiri, Tuzo  itakayokuwa ikitolewa kwa waandishi wenye kipaji cha hali ya juu.
Hizi ni picha za kumbukumbu ya mwaka mmoja iliyofanyika  January 18 nyumbani kwao, Accra Ghana.
1.1959116-620x330
1.1959111

Monday, January 19, 2015

JAJI MUTUNGI AVIONYA VYAMA VYA SIASA VINAVYOENDEKEZA MIGOGORO 



Hivi Karibuni kumekuwa na wimbi kubwa la Migogoro ndani ya vyama vya Siasa. Jambo hili linaleta Taswira mbaya kwa jamii, hasa kipindi hiki ukielekea katika uchaguzi Mkuu wa nchi.
Athari za migogoro hii ni nyingi, ikiwemo chama cha kushindwa kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria ya vyama vya siasa, kupoteza mvuto kwa jamii na wanachama wake, ukosefu wa amani na utulivu ndani ya chama na kupoteza sifa za usajili.
Hivi sasa mfumo wa demokrasi ya vyama vingi vya siasa una takribani miaka 23 tangu urejee tena mwaka 1992. Hivyo jamii inategemea kuwa mwanasiasa na vyama vya siasa kuonyesha ukomavu na busara katika kuokuongoza na kushiriki shughuli za chama.
Mojawapo ya ukomavu na ustarabu huo ni kuweka mifumo, kuongoza na kushiriki shughuli za chama katika namna ambayo itaepusha migogoro.
Mojawapo ya Mambo ya kuzingatia ni chama kudhibiti tofauti za wanachama na baina ya viongozi kwa njia ya kidemokasia na utawala bora katika kuongoza na kushiriki shughuli za chama na kuheshimu na kufuata sheria, katiba na kanuni za chama.
Hivyo natumia nafasi hii kama ninavyotambulika na jamii kuwa ni mlezi wa vyama vya siasa, kuvisihivyama vyote vya siasa, kutekeleza wajibu wao kwa mujibu wa sheria, katiba na kanuni zake. Pia kuwa mfano mzuri kwa jamii kwa kudumisha amani na utulivu ndani ya vyama vya siasa.

MESSI AFIKISHA HAT TRICK YA 42 BARCA IKIUA 4-0 LA LIGA


BARCELONA imejibu mapigo ya Real Madrid iliyoichapa 3-0 Getafe. Barca imepata ushindi mnono wa mabao 4-0 dhidi ya Deportivo La Coruna katika La Liga usiku huu Uwanja wa Riazor. 
Lionel Messi alifunga bao la kwanza kwa Barcelona kwa kichwa maridadi dakika ya 10, kisha akafunga la pili zuri, akiwalamba chenga mabeki kabla ya kumtungua kipa dakika ya 33. 
Mwanasoka huyo wa kimataifa wa Argentina akafikisha hat-trick yake ya 22 katika La Liga kwa bao la dakika ya 62, kabla ya beki wa Deportivo, Sidnei kujifunga dakika ya 83 kukamilisha pointi tatu dhidi ya timu ya Luis Enrique.  
Kikosi cha Deportivo La Coruna kilikuwa; Juanfran, Sidnei, Lopo, Luisinho; Bergantinos, Dominguez, Medunjanin (Lucas 79); Cuenca, Cavaleiro (Rodriguez 46), Riera (Toche 63)
Barcelona; Bravo; Jordi Alba, Alves, Pique, Mascherano, Rakitic, Busquets/Bartra dk66, Iniesta/Rafinha dk66, Suarez, Messi na Neymar/Pedro dk70.

Mawaziri wa escrow hawatuhusu-Hoseah

Dar es Salaam. Wakati wananchi wakisubiri vigogo wa serikalini na mawaziri wanaotuhumiwa kuhusika kwenye kashfa ya uchotaji fedha kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow kufikishwa mbele ya vyombo vya umma, ni watumishi watano tu wa umma waliofikishwa mahakamani, lakini Mkurugenzi wa Takukuru, Dk Edward Hoseah ana jibu la suala hilo; kazi yao ni kufikisha mahakamani 'vidagaa'.
Katika kashfa hiyo ya Sh306 bilioni, mawaziri wa sasa na zamani pamoja na makatibu wakuu wa wizara, wanatuhumiwa kwa njia moja au nyingine kuhusika kwenye kufanikisha kwa makusudi au uzembe uchotwaji wa fedha hizo, kuikosesha mapato Serikali na kupokea mgawo wa fedha hizo, lakini hadi sasa ni watumishi wa Mamlaka ya Mapato (TRA), Wizara ya Nishati na Madini, Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Tanesco na Benki Kuu (BoT) pekee waliofikishwa mahakamani.
Wote watano, ambao ni vigogo kwenye taasisi zao, wameshtakiwa kwa kosa la kuomba na kupokea rushwa ili kufanikisha mkakati huo ulioibuliwa na gazeti la The Citizen na baadaye Bunge kulidaka na kufikia maazimio ya kutaka wahusika wote wawajibishwe na mamlaka zinazowahusu.
Juzi, mkurugenzi huyo wa Takukuru aliliambia gazeti hili kuwa taasisi yake itaendelea kuchunguza watu wote waliohusika katika kashfa ya escrow bila ya ubaguzi, lakini akabainisha kuwa kazi ya kuwapeleka mahakamani mawaziri na vigogo inatakiwa ifanywe na Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP).
Dk Hoseah, ambaye aliwahi kuingia kwenye mzozo wa DPP wa zamani kutokana na madai yake kuwa mafaili mengi ya kesi za rushwa hayafanyiwi kazi, alisema sheria haiwaruhusu kuwapeleka mahakamani mawaziri iwapo watabainika kuhusika kwenye vitendo vya rushwa.
Kwa mujibu wa kifungu cha 57 cha Sheria Namba 11 ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ya Mwaka 2007, endapo vigogo na mawaziri watabainika kuhusishwa na vitendo vya rushwa, jalada la uchunguzi wao litakabidhiwa kwa DPP ili achukue hatua ya kuwapeleka mahakamani.
Dk Hoseah alisema kwa sasa Takukuru inaendelea na uchunguzi wake mpaka itakapojihakikishia ushahidi wa kutosha dhidi ya vigogo hao.
"Bunge lilitoa maazimio yake na likaagiza kuchukuliwa hatua...Takukuru tulishaanza na tunaendelea na uchunguzi. Taratibu zote zikishakamilika kisha ushahidi ukapatikana kwa vielelezo vyote, basi watafikishwa mahakamani wala hakuna tatizo lolote," alisema.
"Lakini watafikishwa mahakamani baada ya sisi kuwasilisha jalada letu la uchunguzi kwa DPP ambaye ndiye mamlaka ya kuwafikisha mahakamani kama sheria inavyotuagiza."
Udhaifu huo wa sheria pia ulizungumziwa na Bunge wakati wa kujadili kashfa ya escrow na kuazimia kuwa sheria inayounda Takukuru ifanyiwe kazi ili iwe na mamlaka hayo ya kufikisha mahakamani vigogo wa rushwa kubwa.
Waliohusishwa na rushwa
Mawaziri waliotajwa kwenye sakata hilo ni Profesa Anna Tibaijuka, ambaye alikuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na ambaye aliingiziwa Sh1.6 bilioni na mwanahisa wa zamani wa Kampuni ya IPTL, James Rugemarila. Tibaijuka alivuliwa wadhifa huo kutokana na sakata hilo.Wengine ni Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, ambaye Rais Jakaya Kikwete alisema amemuweka kiporo baada ya Bunge kumuona kuwa hakushughulikia vizuri suala hilo na kuisababishia Serikali kukosa mapato.
Wengine ni mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Bajeti na ambaye alikuwa Mwanasheria Mkuu, Andrew Chenge, ambaye aliingiziwa pia Sh1.6 bilioni kwenye akaunti yake na Rugemarila; waziri wa zamani wa Nishati na Madini, William Ngeleja, aliyeingiziwa Sh40.4 milioni; aliyewahi kuwa Waziri wa Nishati na Madini, Daniel Yona (Sh40.4 milioni), mbunge wa zamani wa Sumbawanga (CCM), Paul Kimiti (Sh40.4 milioni) na aliyekuwa mjumbe wa Bodi ya Tanesco, Dk Enos Bukuku (Sh161.7 milioni).
Vigogo waliotajwa kwenye sakata hilo ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliackim Maswi, ambaye amesimamishwa, Fredrick Werema, ambaye alijiuzulu kwa maelezo kuwa ushauri wake kuhusu suala la kodi kwenye fedha hizo haukueleweka na ulisababisha tafrani.
Awali, Dk Hoseah aliliambia gazeti dada la The Citizen kwamba katika uchunguzi wake, hakuna kiongozi wala kigogo yeyote ambaye atapona.
"Yeyote yule ambaye atabainika katika uchunguzi wetu, lazima afikishwe mbele ya sheria, hakuna kigogo wala kiongozi yeyote ataweza kukwepa endapo ushahidi utaonekana wazi," alisema.
Alipoulizwa kama uchunguzi huo unamjumuisha Profesa Tibaijuka, mkurugenzi huyo alisema hawezi kutaja jina la mtu kwa kuwa ni kinyume cha sheria kutaja jina au taarifa ambazo ziko kwenye uchunguzi."
Waliofikishwa mahakama ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu hadi sasa ni Mhandisi Mkuu wa Mradi wa Umeme Vijijini (Rea), Theophillo Bwakea na Mkurugenzi wa Huduma za Kisheria wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Rugonzibwa Mujunangoma, ambao kwa pamoja wanadaiwa kupokea rushwa ya Sh485.1 milioni.
Wengine ni Meneja Misamaha ya Kodi wa TRA, Kyabukoba Leonard Mutabingwa, Mwanasheria Mwandamizi wa Tanesco, Steven Roman Urassa na Mkurugenzi wa Fedha BoT, Julius Rutta Angello wanaokabiliwa na mashtaka ya kuomba na kupokea rushwa ya jumla ya Sh1.923 bilioni.
Maoni ya wasomi
Akizungumzia suala hilo, Profesa Gaudence Mpangalla kutoka Chuo Kikuu cha Ruaha alihoji sababu za Serikali kushindwa kuchukua hatua za haraka kuijengea uwezo Takukuru ili iweze kuwafikisha mahakamani watuhumiwa wa aina hiyo.
"Kama tunavyoona hivi sasa inawapandisha kizimbani watumishi wengine, sasa kuna tofauti gani na waziri atakayebainika kukutwa na kosa kama hilo? Sioni tofauti yoyote kwa wakosaji hao," alisema.
"Udhaifu huo unaweza kujenga imani kwamba Serikali inawabeba mafisadi kwa mgongo wa ofisi ya DPP kwa sababu mashtaka mengi hayafanyiwi kazi katika ofisi hiyo."Mara kadhaa Dk Hoseah amekuwa akitoa kauli zinazoonyesha kuwa ameshawasilisha majalada mengi ofisi ya DPP, lakini amekuwa akiyakalia au kuyarudisha kutaka uchunguzi ukamilike.
Hata hivyo, Profesa Chris Maina wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), anaona hilo halitafanyika kwa hivi sasa.
"Kwa jinsi sakata hilo lilivyoibuliwa na ushahidi kuwekwa wazi na Rais akaonyesha hisia zake, lazima DPP ajaribu kuwa makini sana na mawaziri au vigogo watakaofikishwa mbele yake," alisema.
"Inamlazimu achukue hatua za haraka. Hili suala siyo sawa na mashtaka mengine... lakini tusubiri kwa sababu ni kiongozi mpya aliyeingia ofisi hiyo hatujui itakuwaje."
CHANZO:MWANANCHI

NYALANDU AZIMA MARUFUKU MAGARI YA TANZANIA JKIA


WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, amesema serikali ya Kenya imekubali kuyaruhusu magari ya abiria na watalii kutoka Tanzania, kuingia ndani ya Uwanja wa Ndege wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi.
Awali, Serikali ya Kenya iliyazuia magari hayo kuingia uwanjani hapo huku ukiyatoza ushuru kwa yale yanayoingia, jambo ambalo lililalamikiwa na wafanyabiashara wa Tanzania.
Marufuku hiyo ya Kenya kwa magari ya Tanzania, ilidumu kwa zaidi ya wiki mbili, ambapo katika kusaka suluhu hiyo Nyalandu alikutana na wafanyabiashara hao jijini Arusha kisha kukutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Biashara na Utalii wa Kenya, Phyllis Kandie.
Katika mazungumzo yake na Kandie, Nyalandu alisema kwa sasa magari ya Tanzania yataendelea kuingia uwanjani hapo wakati ufumbuzi wa kudumu ukitafutwa.
Alisema kutakuwa na vikao vya kazi baaina ya Wizara ya Utalii ya Kenya na wizara yake, ambapo vitaanzia ngazi ya watandaji, watalaamu, makatibu wakuu na mawaziri.
Alisema katika mikutano hiyo masuala mbalimbali kuhusiana na biashara ya utalii yatazungumzwa baina ya nchi hizo mbili.
Hata hivyo, alisema katika vikao hivyo suala la mpaka wa Bolongoja halitajaliwa wala kuwepo kwenye ajenda.
"Kwa sasa wafanyabiashara wetu wataingia Jomo Kenyatta kama ilivyokuwa awali. Tumezungumza na kupanga kuwa na vikao kujadili na kuzipatia ufumbuzi changamoto zote kuhusiana na sekta ya utalii.
"Niwahakikishie tu katika vikao hivyo maslahi ya pande zote yatazingatiwa, lakini suala la mpaka wa Bolongoja halitajadiliwa wala kuwemo kwenye ajenda za vikao vyetu.
"Wataalamu na watendaji wa wizara yangu watakutana na wenzao jijini Arusha na maofisa wa Jumuia ya Afrika Mashariki watashiriki ili kutafuta ufumbuzi wa kudumu," alisema Nyalandu.
Kupatiwa ufumbuzi kwa tatizo hilo kumekuwa faraja kubwa kwa wafanyabiashara na wadau wa utalii katika mikoa ya Arusha na Kilimanjaro, ambapo walipongeza jitihada za haraka zilizofanywa na Nyalandu.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana, wadau hao wa utalii walisema Nyalandu ameonyesha utendaji kazi kwa vitendo na kwamba, hilo linapaswa kuwa mfano kwa viongozi wengine.
Walisema waziri huyo baada ya kupata taarifa za wafanyabiashara wa Tanzania kuzuiwa kuingiza magari Jomo Kenyatta, aliwafuata kwenye maeneo yao na kuwasikiliza kero zinazowakabili kisha kufunga safari kukutana na waziri Kandie jijini Nairobi.
"Hawa ndio aina ya viongozi ambao Tanzania ya sasa na inayokuja inawahitaji, wanaposikia wananchi wana kero na wananyimwa haki ama kunyanyaswa wanakwenda kuwasikiliza na kutafuta ufumbuzi wa haraka. "Kwa hili Waziri Nyalandu anastahili pongezi na viongozi wengine waige mfano huu, wangekuwa wengine wangeanza kuleta siasa na tatizo kuchukua muda mrefu kupata ufumbuzi," alisema John Mlay, ambaye ni mmoja wa wafanyakazi kwenye kampuni za usafirishaji watalii.

AFCON:KUNDI B LASHINDWA KUTOA MBABE


Kundi B katika michuano ya kombe la mataifa ya Afrika lenye timu za Zambia, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, Tunisia na Cape Verde limeshindwa kuibua mbabe baada ya timu zote kutoka sare ya kufungana bao 1-1.
Katika mchezo wa kwanza wa kundi hilo Zambia iliumana na majirani zake Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, ambapo Zambia iliweza kujipatia bao la mapema ikiwa ni katika dakika ya pili lililofungwa na Given Singuluma na kudumu hadi mapumziko. Hata hivyo Yannick Bolasie aliweza kuisawazishia timu yake ya DR Congo katika dakika ya 66. Hadi kipenga cha mwisho kinapulizwa timu zote zilikuwa zimeambulia goli moja na pointi moja.
Timu ya Tunisia ilivaana na Cape Verde katika mchezo wa pili wa kundi B. Walikuwa ni Tunisia walioanza kujipatia bao katika dakika ya 70 likifungwa na Ali Moncer. Lakini dakika saba baadaye Cape Verde ilisawazisha kupitia mkwaju wa penalti uliofungwa na Almeida Ramos. Mchezo huu nao ulimalizika kwa sare ya 1-1, hivyo kutokuwepo mbabe wa kundi.
Leo ni mechi za kundi C ambapo Ghana itaonyeshana kazi na Senegal, zikifuatiwa na mchezo kati ya Algeria na Afrika Kusini.
Kundi A linaongozwa na timu ya Gabon ambayo iliirarua Burkina Faso 2-0 katika mchezo wa Jumamosi, huku wenyeji Equatorial Guinea wakitoka sare ya 1-1 na Congo.
CHANZO:BBC

CAMERON :NI SAWA NA MAGAZETI KUKERA

David Cameron na Rais Obama mjini Washington juma hili
Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron, amepinga matamshi ya Papa ya juma lilopita aliposema kuwa siyo sawa kufanya mzaha juu ya imani ya watu wengine.
Akijibu kuhusu mashambulio yaliyofanywa na wapiganaji Waislamu dhidi ya gazeti la Ufaransa la Charlie Hebdo, Papa alisema iwapo mtu atamtusi mama ake, ataraji ngumi.
Bwana Cameron hata hivyo alisema katika nchi huru kuna haki ya kukera kuhusu dini ya mtu mwengine.
Aliliambia shirika la habari la CBS la Marekani, kwamba vyombo vya habari vinafaa kuweza kuchapisha vitu ambavyo vinawakera baadhi ya watu - ikiwa siyo kinyume na sheria.
CHANZO:BBC

Thursday, January 15, 2015

TAKWIMU SAHIHI NA ZA WAKATI ZITASAIDIA KULETA MAENDELEO KWA HARAKA BARANI AFRIKA.


NA: VERONICA KAZIMOTO
14 JANUARI, 2015
KAMPALA.
WITO umetolewa kwa washiriki wote wa Mkutano wa Kumi wa Maendeleo ya Takwimu Afrika kuelendelea kutoa takwimu sahihi na kwa wakati ili kuleta maendeleo yanayokusudiwa ya kiuchumi na kijamii barani Afrika.
Wito huo umetolewa jana na Waziri Mkuu wa Uganda Mhe. Dkt. Ruhakana Rugunda wakati akifungua Mkutano wa Kumi wa Maendeleo ya Takwimu Afrika uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Speke Munyoyo Kampala, Uganda.
Dkt. Rugunda amesema kuwa, ili kupata maendeleo kwa haraka, ni lazima takwimu zitolewe kwa wakati na ziwe sahihi kwa ajili ya kusaidia kupanga mipango mbalimbali ya maendeleo.
"Ili Bara la Afrika liweze kuendelea kwa haraka, linahitaji takwimu sahihi na zinazotolewa kwa wakati ili takwimu hizo zisaidie katika kupanga mipango mbalimbali ya maendeleo", amesema Waziri Mkuu Rugunda.
Dkt. Rugunda ameongeza kuwa ili kuweza kufanikisha hilo, kuna umuhimu kwa nchi za Afrika kusaidia program mbalimbali za uzalishaji wa takwimu na matumizi yake kwa ajili ya kupanga mipango ya maendeleo.
Kwa upande wa Waziri wa Fedha wa Uganda Matia Kasaija amesema kuwa, ili kuweza kulinganisha takwimu za nchi mbalimbali, ni vyema takwimu zinazozalishwa zikafuata mbinu bora za uzalishaji wa takwimu.
Matia Kasaija amesema mbinu bora za uzalishaji wa takwimu ni zile zinazofuata viwango vinavyopendekezwa na Umoja wa Kimataifa - Kitengo cha Takwimu.
Mkutano wa Kumi wa Maendeleo ya Takwimu Afrika umewakutanisha washiriki takribani 400 kutoka nchi mbalimbali za Afrika ikiwemo Tanzania. Mkutano huu ni wa siku tatu na unatarajia kumalizika kesho tarehe 15 Januari, 2015.

HASHIM KAMBI KUONGOZA NYOTA BONGO KATIKA FILAMU YA CPU


MSANII mkongwe katika tasnia ya filamu Swahilihood Hashim Kambi 'Ramsey' ni moja kati ya wasanii wakubwa Bongo ambaye atawaongoza wasanii nyota na wakongwe katika filamu kubwa ya CPU inayotarajiwa kuingizwa katika Dvd baada ya kuonyeshwa katika majumba ya sinema ndani na nje ya Bongo.
Filamu ya CPU ni kazi kubwa sana kutengenezwa na watayarishaji wa ndani na kushirikisha wasanii zaidi ya mia mbili ndio filamu kubwa yenye ubora wa kipekee awali ilionyeshwa katika ukumbi wa sinema Century Cinemax Mlimani City kwa siku kumi mfululizo na kuacha gumzo kwa wapenzi wa sinema.
Kwa mara ya kwanza itauzwa katika Dvd ili kwa wale wapenzi wa filamu walioshindwa kuingia katika majumba ya sinema ilipoonyeshwa waweze kushuhudia teknolojia ya juu kutumika Bongo na kuwavutia wengi mtaani kwetu ambako ndio soko la filamu za kibongo lipo.
CPU inawakutanisha wasanii nyota na wakongwe ka aKulwa Kikumba 'Kulwa Kikumba ' Dude', Richard Mshanga 'Masinde', Dotnata, na nyota wengine kibao ambao wanafanya vizuri katika tasnia ya filamu wakiongozwa na Hashim Kambi 'Ramsey' msanii aliyejijengea mashabiki wengi.

NYALANDU AKARIBISHA WAFANYABIASHARA WA SAUDI ARABIA KUWEKEZA SEKTA YA UTALII NCHINI 

 


Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu (wa pili kushoto) akimsikiliza kwa makini Mwenyekiti wa Chemba ya Biashara ya Saudi Arabia Dk. Abdulrahman Al-Zamil (wa tatu kushoto) jijini Riyadh, Saudi Arabia. Wengine katika picha kutoka kulia ni Mshauri wa Ushirikiano wa Kimataifa wa Mamlaka ya Wanyamapori ya Saudia Mohammad Sulayem; Katibu Mkuu wa Maliasili na Utalii Dk. Adelhelm Meru na Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia Prof. Abdillah Omari.

Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu (kushoto) katika mazungumzo na Mwenyekiti wa Chemba ya Biashara ya Saudi Arabia Dk. Abdulrahman Al-Zamil jijini Riyadh, Saudi Arabia.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira Mhe. James Lembeli (kushoto) akikaribishwa na Mwenyekiti wa Chemba ya Biashara ya Saudia Dk. Abdulrahman Al-Zamil jijini Riyadh, Saudi Arabia.

Waziri Kivuli wa Maliasili na Utalii Mhe. Peter Msigwa (kushoto) akikaribishwa na Mwenyekiti wa Chemba ya Biashara ya Saudia Dk. Abdulrahman Al-Zamil jijini Riyadh, Saudi Arabia.

Ujumbe wa Serikali ya Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu (wa tano kushoto) ukiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa Chemba ya Biashara ya Saudia Dk. Abdulrahman Al- Zamil (wa sita kushoto) mara baada ya kumalizika kwa mazungumzo baina ya pande mbili jijini Riyadh, Saudi Arabia. Wengine pichani kutoka kushoto ni pamoja na Mkurugenzi wa Wanyamapori Herman Keraryo; Mkurugenzi Mkuu TANAPA Allan Kijazi; Mhe James Lembeli; Mhe Peter Msigwa; Katibu Mkuu Maliasili na Utalii Dk. Adelhelm Meru pamoja na maafisa kutoka Chemba ya Biashara ya Saudia.
Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu amewakaribisha wafanyabiashara kutoka Saudi Arabia kuwekeza katika sekta ya utalii nchini ambayo ina fursa nyingi za uwekezaji. Nyalandu alitoa wito huo kufuatia mazungumzo yake na Mwenyekiti wa Chemba ya Wafanyabiashara ya Saudi Arabia Dk. Abdulrahman Al-Zamil yaliyofanyika Riyadh, Saudi Arabia jana.
Waziri Nyalandu ambaye anaongoza ujumbe wa Wizara ya Maliasili na Utalii nchini Saudia alibainisha kuwa mazingira ya uwekezaji nchini yanavutia na kutaja maeneo hayo kuwa ni pamoja na ujenzi wa hoteli na loji za kisasa zitakazoweza kuvutia watalii wengi zaidi katika maeneo ya mijini pamoja na ndani ya maeneo ya uhifadhi.
Alisema kuwa utalii wa Tanzania unakua kwa kasi nzuri kutokana jitihada zinazofanywa na serikali pamoja na wadau mbalimbali katika kutangaza vivutio vya utalii na kuwa juhudi hizo lazima ziende sambamba na upatikanaji wa huduma bora za malazi. "Upatikanaji wa huduma nzuri za malazi ya bei nafuu utasaidia kuvutia watalii wengi zaidi nchini na kwa maana hiyo tunawakaribisha kuja kuzitumia fursa zilizopo ili kuweza kukuza uchumi wa nchi yetu", alisema Nyalandu.
Waziri Nyalandu ambaye anaongoza ujumbe wa Wizara ya Maliasili na Utalii nchini Saudia, alisema kuwa Tanzania ni ya pili ulimwenguni baada ya Brazil kwa kuwa na vivutio vizuri vya asili vya utalii na kuwa rasilimali hizi zinapaswa sasa kutumiwa vema ili kuinua uchumi na njia pekee ni pamoja na kuvutia wawekezaji na mitaji kutoka Saudia ili kufikia azma hiyo.
Kwa upande wake Dk. Al-Zamil aliahidi kuwashirikisha wafanyabiashara wenzake kutikia wito huo na kwa kuanzia timu ya wafanyabiashara pamoja na mawakala wa utalii watafika nchini katika siku chache zijazo ili kuona namna gani wataweza kuzitumia fursa zilizopo kikamilifu. Aidha, katika eneo la utalii Al- Zamil alisema kuwa Chemba yake itafanya kila liwezekanalo kubadilisha mtazamo wa Wasaudia wanaotembelea kwa wingi maeneo mbalimbali ya utalii duniani ili waweze kuitembelea Tanzania na kujionea vivutio mbalimbali vya utalii vinavyopatikana nchini.
Aidha, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Dk. Adelhelm Meru alisema kuwa serikali itaandaa Kongamano Maalum la Uwekezaji nchini Saudi Arabia ili kuweza kutangaza fursa mbalimbali zzilizopo nchini ambazo zikitumika vema zinaweza kuinua uchumi wa taifa.
Hivi sasa Tanzania inategemea idadi kubwa ya watalii kutoka Mataifa ya Ulaya na Amerika na kwamba japokuwa idadi ya watalii kutoka nchi za kiarabu haizidi 15,000 kwa mwaka, bado jitihada za utangazaji na uwekezaji zikifanywa vizuri idadi ya watalii kutoka mataifa ya kiarabu itaweza kuongezeka nchini.
Ujumbe wa Tanzania unajumuisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Dk. Adelhelm Meru; Balozi wa Tanzania Saudi Arabia Prof. Abdillah Omari; Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira Mhe. James Lembeli, Waziri kivuli wa Maliasili na Utalii Mhe. Mchingaji Peter Msigwa; Mkurugenzi Mkuu wa Hifadhi za Taifa Allan Kijazi pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori Herman Keraryo.

Wednesday, January 14, 2015

SERIKALI YASAINI MAKUBALIANO YA UTEKELEZAJI WA MRADI.

unnamed
Katibu Mkuu Wizara ya Maji Mhandisi Mbogo Futakamba akiwa na Rais wa Kampuni ya China Railway International Group Co. Ltd Dkt. Lu Bo wakisaini makubaliano ya utekelezaji wa mradi wa kutoa maji kutoka mto Ruvuma hadi Mtwara. Makubaliano hayo yalifanyika Beijing, China tarehe 10 Januari 2015. nyuma ya Katibu Mkuu (aliyesimama) ni Waziri wa Maji Mheshimiwa Prof. Jumanne Abdallah Maghembe (Mb).
unnamed2
Katibu Mkuu Wizara ya Maji Mhandisi Mbogo Futakamba akipeana mikono na Rais wa Kampuni ya China Railway International Group Co. Ltd Dkt. Lu Bo baada ya makubaliano ya utekelezaji wa mradi wa kutoa maji kutoka mto Ruvuma hadi Mtwara. Makubaliano hayo yalifanyika Beijing, China tarehe 10 Januari 2015.
unnamed3
Mheshimiwa Waziri wa Maji, Prof. Jumanne Abdallah Maghembe (Mb) akipeana mikono na Rais wa Kampuni ya China Railway International Group Co. Ltd Dkt. Lu Bo baada ya saini makubaliano ya utekelezaji wa mradi wa wa kutoa maji kutoka mto Ruvuma hadi Mtwara. Makubaliano hayo yalifanyika Beijing, China tarehe 10 Januari 2015. Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Mhandisi Mbogo Futakamba.

PROF. MARK MWANDOSYA AFANYA ZIARA YA KIKAZI NCHINI SUDANI 

New Picture (1)
Mhe. Prof. Mark Mwandosya akifafanua jambo wakati wa mkutano wa pamoja na Waziri wa Maji na Umeme wa Sudan Mhe Mutaz Moussa Abdallah Salim. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Bwana Felix Ngamlagosi ambaye ameongozana pamoja na maafisa wengine na Waziri Prof. Mwandosya
New Picture (2)
Mhe. Prof. Mark Mwandosya akitoa maelezo katika mkutano wa pamoja na Waziri wa Maji na Umeme wa Sudan Mhe Mutaz Moussa Abdallah Salim.
New Picture (3)
Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Mhe. Prof. Mark Mwandosya katika mkutano wa pamoja na ujumbe wa Sudan ulioongozwa na Waziri wa Maji na Umeme wa Sudan Mhe Mutaz Moussa Abdallah Salim.
New Picture
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Kazi Maalum), Mhe. Prof. Mark Mwandosya akikaribishwa na mwenyeji wake Waziri wa Maji na Umeme wa Sudan Mhe. Mutaz Moussa Abdallah Salim mara alipowasili katika Ofisi za Wizara hiyo Jijini Khartoum.
12 – 17 JANUARI 2015
Mheshimiwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Kazi Maalum), Prof. Mark Mwandosya yuko ziarani nchini Sudan ambako atatembelea miradi mbalimbali ya maendeleo nchini humo ikiwemo miradi mikubwa ya mabwawa yaliyojengwa katika bonde la Mto Nile pamoja na kubadilishana uzoefu na taasisi za Sudan zinazojihusisha na udhibiti wa huduma katika sekta za maji, nishati, mawasiliano na usafirishaji.
Ujumbe wa Mhe. Prof. Mwandosya umejumuisha wataalamu kutoka Wizara ya Maji, Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA), Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA) na Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA).
Mhe. Prof. Mwandosya alianza ziara yake Jumatatu ya tarehe 12 Januari, 2015 kwa kutembelea Wizara ya Rasilimali za Maji na Nishati ya Umeme ya Jamhuri ya Sudan.
Katika ziara hiyo Mhe. Prof. Mwandosya alieleza kuwa pamoja na shughuli zingine, ameandamana na taasisi za udhibiti kutoka Tanzania ili kujifunza na kubalishana uzoefu katika shughuli za udhibiti kutoka kwa taasisi kama hizo katika nchi ya Sudan. Waziri alieleza kuwa shughuli za udhibiti Tanzania zimekuwa zikifanyika kwa kipindi cha takribani miaka 10 sasa. Waziri alieleza kuwa pamoja na mafanikio yaliyopatika katika kutekeleza majukumu yao, Mamlaka za Udhibiti bado zina changamoto nyingi ambazo inabidi kukabiliana nazo kwa kujifunza na kubadilisha uzoefu na taasisi kama hizo katika nchi kama Sudan