TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, October 31, 2012

AZZAN ZUNGU MATATANI KWARUSHWA
Mwenyekiti wa Bunge katikati Bw.Mussa Azzan Zungu




























Sakata la uchaguzi wa wazazi CCM, limefanya Mwenyekiti wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Bw. Mussa Azzan Zungu pamoja na makamanda wengine wa CCM juzi walikamatwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoani Dodoma kwa tuhuma za rushwa majira ya saa 4:30 usiku wakidaiwa kujaribu kutoa rushwa ya Sh.100,000.
MAONYESHO YA WANAWAKE YAENDELEA MNAZI MMOJA

HALI YA UPATIKANAJI MAFUTA SONGEA NI TETE

Msululu wa waendesha pikipiki wakiwa wamepanga foleni katika shell ili kupatiwa huduma ya nishati ya mafuta ambayo kwa sasa imekuwa shida mkoani humo.

DKT SHEIN AFANYA UTEUZI





















NA MAELEZO ZANZIBAR 31/10/2012 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein amemteua Amina Juma Zidikheir kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Utumishi wa Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Zanzibar. Kwa mujibu wa Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Zanzibar Dkt Abdulhamid Yahya Mzee imesema kuwa uteuzi huo ameufanya kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya kifungu 8(1) (a) cha sheria ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Zanzibar namba 11 ya mwaka 2003. Amina Juma Zidikheri aliwahi kuwa Mhasibu mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kabala ya kustaafu kwake. Uteuzi huo umeanza tarehe 27 Oktoba,2012 

IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR 31/10/2012

WASANII NYOTA WA FILAMU NCHINI WAHIMIZWA KUCHANGAMKIA TUZO ZA AFRICA
Ray ,Natasha and JB

























Wasanii nyota wa filamu nchini wametakiwa kuchangamkia fursa ya kuwania tuzo za filamu za Afrika zinazoandaliwa na Africa Magic ili kujitangaza zaidi na kupata fursa ya kujiimarisha kiuchumi.
Aidha mwisho wa kuwasilisha kazi zao ni Novemba 9,2012 na washindi wa shindano hilo watatangazwa March 9,2013.

Tuesday, October 30, 2012

SERIKALI KUZIJENGEA UWEZO WIZARA KATIKA UBIA
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji), Dk. Mary Nagu (Mb) akieleza dhamira ya Serikali ya kuzijengea uwezo Wizara na Idara zake zinazohusika moja kwa moja na utekelezaji wa Sera ya Ubia baina ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP) wakati alipofungua mafunzo ya Ubia baina ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi leo Mjini, Morogoro, Wa kwanza Kulia ni Mtaalamu wa masuala ya PPP kutoka Taasisi ya IP3 nchini Marekani, Bw. Jackues Cook na wapili ni Kamishina wa PPP- Wizara ya Fedha Bw. Frank Mhilu na kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Waziri Mkuu, Bw. John Mboya.
MSANII JCB ASHIKILIWA NA POLISI KWA MAUAJI


























MSANII wa muziki wa kizazi kipya kutoka jijini Arusha, Jacob Makala a.k.a JCB a.k.a Jesus Come Back aliyetamba na wimbo wa "Ukisikia Paah (Ujue Imekukosa)", pamoja na wenzake watatu wanashikiliwa na jeshi la polisi mkoani Arusha kwa tuhuma za mauaji.


Akizungumzia tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Lebaratus Sabas alisema kuwa msanii huyo pamoja na wenzake wanashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kumpiga mwenzao hadi kufa katika ukumbi wa Viavia, sehemu ambayo walikuwa wanafanya shoo katika onyesho la Jambo Festival.


Alisema kuwa marehemu huyo ambaye alitambulika kwa jina la Alex Julius Samwel (21) mkazi wa Ilboru, alihudhuria onyesho la Jambo Festival lililokuwa likifanyika usiku wa Oktoba 25.


Kamanda Sabas alisema marehemu akiwa ukumbini na wenzake, alipigiwa simu na watu wanaodaiwa kuwa ni pamoja na JCB na wenzake wakimtaka atoke nje. Alitoka nje na aliporudi alionekana akitoka damu puani pamoja na kuwa na uvimbe sehemu za mwili.


"Watu wa karibu waliokuwa na marehemu walipomuuliza kwanini amevimba na anatoka damu ndipo alipowajibu kuwa alitoka nje na kufanyiwa fujo na msaniii huyo na wenzake huku akibainisha kuwa  mbali na kufanyiwa fujo pia walimchukulia simu yake ya kiganjani lakini alisema kuwa hajapata maumivu makubwa, ila kadri muda ulivyozidi kwenda ndivyo alivyozidi kuzidiwa na ndugu zake walimpeleka hospitali ya Father Babu na kufariki akiwa hospitalini hapo," alisema Kamanda Sabas.


Aliwataja watu wengine wanaoshikiliwa pamoja na JCB kuwa ni Robert Joseph (18) mkazi wa Sekei, Sara Ephraim (32) mkazi wa Engoshelaton pamoja na Remi Peter (22) mkazi wa Unga LTD.


Alisema kuwa mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya mkoa ya Mount Meru na watuhumiwa wote wanashikiliwa na jeshi la polisi na pindi upelelezi utakapokamilika watafikishwa mahakamani.


Katika wimbo wa "Ukisikia Paah", JCB aliwashirikisha nyota kama  Fid Q, Jay Mo na Chidi Beenz.
Kiitikio cha wimbo "Ukisikia Paah" kinasema: "Ukisikia paah ujue imekukosa, aliyelenga hana shabaha amefanya makosa."


Tuhuma dhidi ya JCB zimekuja siku chache tangu msanii mwingine wa kizazi kipya wa Arusha, Lord Eyez, kushikiliwa na polisi kwa tuhuma za kuiba vifaa vya gari la msanii mwingine Ommy Dimpoz na kujumuishwa na tuhuma za matukio mengine 30 ya wizi wa aina hiyo.


Msanii mwingine wa Arusha, Nelson Chrizostom Buchard a.k.a Father Nelly wa kundi la Xplastaz aliuawa kwa kuchomwa kisu mjini Arusha Machi 29, 2006 wakati msanii mwingine wa kizazi kipya Steve2K aliuawa 2004 kwa kudaiwa kuchomwa kisu na mtayarishaji wa muziki wake Castro Ponera. 
 

CHANZO: Gazeti la NIPASHE
MCHUNGAJI LWAKATALE ATOA UJUMBE WA AMANI
























Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Mlima wa Moto Mikocheni Mh. Dkt. Getrude Rwakatare akitoa Ujumbe kwa Watanzania waliohudhiria Ibada Maalum ya Kuliombea Taifa ambapo ametaka watu kutobaguana kwa misingi ya Dini, Ukabila wala Siasa na kusema pamoja na Utawala bora pia tunahitaji maombezi ili tuweze kufikia Malengo yaliyokusudiwa kulipeleka Taifa linapotakiwa kufikia. Dkt. Rwakatare amesema nia kubwa ya kufanya Ibada hiyo ya Maombezi ni kutaka kuweka usawa kutokana na siku za hivi karibuni kuibuka kwa Matamko mbalimbali kutoka kwa watu tofauti wakiwemo viongozi wa Kitaifa, Kidini na wa baadhi ya Makundi yanayohitilafiana na kusema tukiomba kwa jina la Mungu kila kitu kitakwenda kama tulivyomuomba ili Tanzania iendelee kuwa nchi ya Amani na Utulivu kama ilivyokuwa miaka yote ambayo ni kimbilio la watu wa Mataifa mbalimbali kwa sababu Watanzania hawajui kuchukiana na wamekuwa watu wa kushikamana kwa miaka yote
MKUTANO WA MAJAJI NA MABALOZI WAANZA JIJINI ARUSHA


























Pichani ni Waziri wa sheria na katiba Mathias Chikawe akiwa na Jaji wa mahakama ya Afrika ya haki za binadamu kwenye ufunguzi wa mkutano wa shughuli za mahakama uliowashirikisha mabalozi kutoka nchi za umoja wa Afrika (AU) unaondelea kwenye ukumbi wa hotel ya  Mount Meru jijini hapa(picha na mahmoud ahmad Arusha)

 RAIS wa mahakama ya Afrika( Africa court) kutoka nchini Ghana Sophia Akuffo amefungua mkutano wa kamati ya kudumu ya umoja wa Afrika(AU) uliokutanisha majaji pamoja na mabalozi 54 kutoka nchi za Umoja wa Afrika ulionza leo Akifungua mkutono huo Raisi wa mahakama ya Afrika Sophia Akuffo amezitaka nchi za bara la Afrika kuweka muda na kutekeleza kwa vitendo na kuifahamisha jamii ya waafrika juu ya haki za binadamu na viongozi kuacha kukiuka haki hizo . Alisema kuwa katika mkutano huo washiriki wataweza kuangalia kwa undani mahusiano yaliyopo kati ya mahakama ya kutetea haki za binadamu pamoja na kamati ya wawakilishi ya umoja wa mataifa katika kuhakikisha kuwa mahakama za Afrika zinaboreshwa. Aidha alisema kuwa mkutano huo utaweza pia kuunganisha ushirikiano kati ya mahakama na mashirika mengine ya umoja wa afrika pamoja na kamati ya kudumu ya wawakilishi wa umoja huo ili kuhakikisha kuwa wanafanikiwa katika mambo mbali mbali . “mkutano huu ni muhimu sana kwani majaji na mbalozi wataweza kujadili mambo mazuri ambayo yayawezesha hata mahakama kuondokana na baadhi ya changamoto zinazowakabili”alisema Uwanone Aliongeza kuwa katika mkutano huo wataweza kuweka mkakati juu ya Mahakama na kuweza kubuni njia mbali mbali ambazo zitaweza kulinda haki za binadamu ndani ya afrika. Alieleza kuwa kamati ya wawakilishi ya kudumu ya umoja wa mataifa itaweza kuweka umakini mkubwa kwenye mahakama za Afrka kwa kuwa hiyo ni moja ya sera zilizoko ndani ya umoja wa mataifa. Hata hivyo mkutano huo umehudhuriwa na wadau mbali mbali wa mahakama ya haki za binadamu akiwemo makamu wa rais wa mahakama hiyo ,mwenyekiti wa kamati ya wawakilishi wa umoja wa mataifa pamoja na muwakilishi wa kamati hiyo.

Monday, October 29, 2012

MATOKEO YA UCHAGUZI WA MADIWANI CCM NA CHADEMA 
















CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimeendelea kukipa wakati mgumu Chama cha Mapinduzi (CCM) katika siasa, ambapo kwenye matokeo ya udiwani katika uchaguzi uliofanyika leo, chama hicho kimefanikiwa kutetea kata zake na kunyakua nyingine za CCM.
Hata hivyo uchaguzi huo ambao ulifanyika kwenye kata 29 katika halmashauri mbalimbali nchini, umemalizika huku vurugu kubwa zikitawala na kusababisha wafuasi wa vyama hivyo kuumizana.
Hadi sasa matokeo ya kata 14 yanaonyesha kuwa CCM ilikuwa imefanikiwa kurejesha kata zake saba, huku CHADEMA ikinyakua kata sita, ambapo mbili zilikuwa za kwao na nne imewanyang’anya CCM na CUF ikiwa na kata moja.
matokeo ya udiwani katika baadhi ya kata yalikuwa yakiendelea kutolewa huku CHADEMA ikiendelea kuikaba CCM kwa kuzitwaa baadhi ya zilizokuwa kata zake.

Jijini Arusha katika Kata ya Daraja Mbili, CCM ilipoteza kata hiyo kwa CHADEMA iliyozoa kura 2192 dhidi ya 1315 za chama tawala.
CHADEMA wameweza kuzirejesha kata zao mbili za Nangerea jimboni Rombo, ambapo mgombea wao Frank Sarakana alijizolea kura 2370 dhidi ya 1134 za Dysmas Silayo wa CCM pamoja na ile ya Mtibwa, mkoani Morogoro.
Wilayani Sikonge katika kata ya Ipole, CCM walipoteza kata hiyo kwa CHADEMA iliyopata kura 577 dhidi ya 372 za washindani wao, na vilevile kuitwaa kata nyingine ya Lengali wilayani Ludewa iliyokuwa ya CCM.
CHADEMA pia ilikuwa ikiongoza katika kata ya Mpwapwa, mkoani Dodoma, hadi tunakwenda mitamboni usiku.
Nayo CCM ilifurukuta kwa kuzirejesha kata zake za Msalato ya mkoani Dodoma, Bang’ata ya Arumeru Magharibi kwa kuwa 1177 dhidi ya 881 za CHADEMA, Mletele ya Songea CCM ilishinda kwa kura 950 na CHADEMA ilipata 295.
Pia CCM iliweza kutetea kata zake za Mwawaza mjini Shinyanga, Lwenzela mkoani Geita, Bungala wialayni Kahama na Bagamoyo mkoani Pwani kwa kuibwaga CHADEMA wakati Chama cha Wananchi (CUF) kilishinda kata ya Newala.

JK AWASILI SAME KWA ZIARA






















Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na viongozi mbalimbali na wananchi baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro leo Oktoba 28, 2012 tayari kuanza ziara ya siku nne ya Mkoa wa Kilimanjaro akianzia Wilaya ya Same.

VIONGOZI WAPYA WA UVCCM WAPOKELEWA KWA MAPIGANO DAR
Mmmoja wa mwanachama wa CCM akipatiwa msaada baada ya kujeruhiwa katika vurugu zilizotokea wakati wanachama hapo walipokuwa wakiwapokea viongozi wao wapya Jijini Dar es Salaam wakitokea Dodoma.

Saturday, October 27, 2012

MTOTO WA KIBRAZIL ASIYEKUWA NA MAKANYAGIO ATIMIZA NDOTO YAKE YA KUKUTANA NA MESSI.
Mtoto Gabriel akicheza mpira na nyota wake Lionel Messi wakati alipopata mwaliko wa kutembelea kambi ya Barcelona

Gabriel akipiga danadana mbele ya shujaa wake Messi ambaye hayupo pichani kumdhihirishia kuwa naweza kufanya vitu vikubwa japo sina makanyagio

Lionel Messi akisaini jezi ya mtoto huyo kwa furaha baada ya kushangazwa na kipaji chake cha uchezaji wa mpira

Wachezaji wa Barcelona wakipiga picha na Gabriel kutoka kushoto ni Victor Valdes,Beki Adrioan na Dani Alves























GABRIEL Muniz ni mtoto wa Kibrazil mwenye umri wa miaka 11 ambaye alikuwa na ndoto za kukutana na Lionel Messi siku moja. Na ndoto yake hatimaye imetimia, hasa baada ya habari yake kuwa maarufu na kuwagusa wengi mioyoni huku pia ikiwapa changamoto ya kutokata tamaa ya maisha.

Gabriel hana makanyagio. Alizaliwa hivyo hivyo. Ingawa familia yake ilidhani kwamba angekuwa na matatizo makubwa katika maisha yake ya kawaida, alianza kutembea kabla hajatimiza umri wa mwaka mmoja. Ilimchukua muda mrefu kuweza kuruka kutoka kutembea hadi kucheza mpira, lakini aliweza yote hayo. Na, hakika, hakuna anachopenda zaidi ya kucheza soka.

Anacheza bila ya viatu, na hutumia vifaa maalum kuvaa chini inaponyesha mvua ili kumuepushia kuteleza. Ukimuangalia anavyocheza mpira utashangaa. Ana kasi na "maujuzi" – anaki paji sana na anafanya kila awezalo kumuiga shujaa wake, Leo Messi.

Gabriel alikuwa na bahati sana kualikwa katika wakati wa mazoezi ya Barcelona, na mwishoni mwa mazoezi akapata fursa ya kukutana na wachezaji, na kuzungumza nao hasa Wabrazil wenzake Dani Alves na Adriano.

Lakini tukio lake kubwa zaidi lilikuwa halijawadia. Pale kocha Tito Vilanova alipomuuliza kama amepata fursa ya kukutana na wachezaji wote, Gabriel alijibu: "Sijaonana na Messi bado".

Hatimaye 'mchawi' huyo wa Kiargentina akatokea. Wote wakaanza kuuchezwea mpira na Messi akapigwa na butwaa pale alipoona ufundi wa kuchezea mpira alionao Mbrazil huyo mdogo.

Ilionekana kama ni jambo lisilowezekana kwa mtoto asiye na makanyagio kukimbia na kukokota mpira, achilia mbali kupiga 'vibaiskeli', matobo na tikitaka, lakini yeye anaweza.

Friday, October 26, 2012

MAJINA YA WALIOHUSIKA KUMUUA KAMANDA BARLOW YATAJWA























wandishi wa habari Albert G Sengo kutoka Mwanza ameripoti kwamba majina ya watu watano  wanaotuhumiwa kuhusika moja kwa moja na kifo cha aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Leberatus Barlow yametajwa na Polisi.
Akitaja hayo majina mbele ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Said Mwema, Mkurugenzi wa upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba  amesema simu iliyoporwa ya mwanamama ambaye alikuwa akisindikizwa nyumbani na marehemu ndiyo imesaidia kukamilisha upelelezi huo na wahusika kukamatwa.
Waliotajwa kuhusika na hayo mauaji ni Muganyizi Michael Peter (36) ambaye ametajwa kwamba ndiye aliyemuua Barlow, Chacha Waitare Mwita (50), Magige Mwita Marwa (48),  Buganzi Edward Kusuta pamoja na Bhoke Marwa Mwita (42) ambao wote wamekatwa wakiwa Dar es Saalam walipokimbilia baada ya mauaji.
lisema Kikosi kazi cha upelelezi kilichokuwa chini yake  Manumba kilijigawa kwenye makundi matatu moja ni lile la Ukamataji, Mahojiano na jingine la intelijensia huku wakitumia njia ya sanyansi kufatilia kupitia mitandao ya simu.
 
Kukamatwa kwa watuhumiwa hao wa Dar na wale wa Mwanza kunafanya jumla yao kuwa 10 na bado jeshi linasaka wengine  Lakini chanzo cha hao wauaji kufanya hivyo bado hakijatajwa.
Liberatus Barlow aliuawa Oktoba 13 mwaka huu, saa 8 usiku kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana katika eneo la Minazi mitatu huko Kitangiri wakati alipopita kumsindikiza Mwalimu Dorothy Moses nyumbani kwake kutoka katika kikao cha harusi kilichofanyika Mtaa wa Rufiji.
WANAFUNZI VYUO VIKUU IRINGA WAPINGA RIPOTI YA WAZIRI KUHUSU KIFO CHA DAUDI MWANGOSI


























Wanafunzi hao jana waliandamana hadi garden na kuongea na waandishi kupinga ripoti ya waziri na kulaani kifo cha mwandishi Mwangosi
UJENZI WA BARABARA ZA RELI WASHIKA KASI DAR


















































Ujenzi wa baraba za reli zimeshika kasi kama unavyoona hapo juu watu wakiwa bize na kazi

Wednesday, October 24, 2012

HATIMAYE H.BABA AMVISHA PETE YA UCHUMBA FROLA MVUNGI
























ULE uchumba uliodumu kwa muda mrefu kati ya mastaa filamu na muziki wa Bongo Fleva nchini, Hamis Baba ‘H. Baba’ na Flora Mvungi umefikia pazuri baada ya H – Baba kumtolea mahari na kumvalisha pete ya uchumba. H-Baba akimvisha pete ya uchumba, Flora Mvungi. Tukio hilo lililokuwa na mvuto wa aina yake lilichukua nafasi juzi Jumamosi, katika Ukumbi wa The Atriums Hotel, Sinza – Afrika Sana, Dar na kuhudhuriwa na ndugu wa pande zote mbili. Kinyume na ilivyozoeleka, zoezi la kutoa mahari kufanyika nyumbani, kwa wawili hawa ilikuwa tofauti kwani kila kitu kilimalizikia ukumbini humo. 
Kila la heri tunawatikia ili muweze kutimiza ndoto yenu.
TAARIFA KAMILI KUHUSU BOBAN NA NYOSSO KUSIMAMISHWA KUCHEZA SIMBA























Club ya Simba imeleza kuhusu kuwasimamisha wachezaji wake wawili ambapo wa kwanza ni Haruna Moshi Shaaban (Boban aliesimamishwa kuichezea timu ya wakubwa kutokana na vitendo vya utovu wa nidhamu na kutokuwa na heshima kwa mwajiri (timu) ambapo klabu imempa muda wa siku 21 kutoa maelezo kuhusu makosa yake lakini akishindwa kutoa maelezo ya kuridhisha, klabu inaweza kumchukulia hatua zaidi.
Katika kipindi hicho (siku 21 kuanzia jana), Boban atapokea nusu ya mshahara wake wa kila mwezi na hatopata marupurupu yoyote yanayohusiana na timu ya wakubwa
Kwa upande wa Nyoso, uongozi umemwagiza afanye mazoezi na kikosi cha timu ya pili (Simba B) hadi atakapoimarisha kiwango chake cha uchezaji, hii imetokana na ripoti ya benchi la ufundi iliyoonyesha kwamba mchezaji huyo amekuwa akifanya makosa mengi ya kiuchezaji yanayoigharimu klabu yake japo amekuwa akipewa maelekezo na walimu lakini bado amekuwa akirudia makosa yaleyale.
Kutokana na hilo, Nyoso atafanya mazoezi na wachezaji wa kikosi cha pili hadi walimu watakaporidhika kwamba amejirekebisha na yuko tayari kutumikia kikosi cha wakubwa ambapo kwa muda wake wote huo akifanya mazoezi na timu B, Nyoso atakuwa akipata mshahara wake wa kila mwezi kama kawaida na pia atapata marupurupu wanayopata wachezaji wa Simba B.
MKATABA WA UJENZI WA DARAJA LA KILOMBERO WASAINIWA























 Mtendaji Mkuu wa Tan roads Mhandisi Patrick Mfugale (kushoto) na  Mtendaji Mkuu kutoka kampuni ya ujenzi ya China Railway 15 Bureau group Corporation (CR15G) Zhang Tonggang (kulia) wakiweka saini mkataba wa ujenzi wa daraja la  Kilombero lenye urefu wa  meta 384 na ujenzi wa barabara zake za miingilio za lami( kilometa 9.142)  zoezi hilo litagharimu shilingi bilioni 53.2

Hafla hiyo imefanyika Jijini Dar es Salaam na kushuhudiwa na Waziri wa Ujenzi, Dkt, John Magufuli ,katibu Mkuu wa Wizara hiyo Balozi Herbert Mrango  Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Tanroads  Bi. Hawa Mmanga , Mbunge wa  Mikumi Abdul Salim Ameir na Mbunge kutoka Morogoro Kusini Innocent Kalgeris .
Ujenzi wa daraja hilo utaziunganisha Wilaya za Mahenge na Ulanga pamoja na kuboresha Usafiri wa mikoa ya kusini  na kuleta kichocheo cha ukuaji wa shughuli za kiuchumi. (Picha na Mwanakombo Jumaa-Maelezo)  
 

REDDS MISS TANZANIA KUPATA SH. MILIONI 8 NA GARI... WA MWISHO KUONDOKA NA SH. 700,000

MSHINDI wa taji la urembo la Redd's Miss Tanzania 2012 ataondoka na Sh. milioni 8 pamoja na gari, waandaaji kampuni ya Lino Agency wametangaza leo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, mkurugenzi wa kampuni ya Lino Agency, Hashim Lundenga alisema warembo 30 kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania watachuana katika fainali za shindano hilo litakalofanyika Novemba 3, 2012 kwenye ukumbi wa Blue Pearl Hotel (Ubungo Plaza) jijini Dar es Salaam.

Alisema mshindi wa pili atapata zawadi ya pesa taslimu Sh. milioni 6.2, wa tatu Sh. milioni 4, wa nne Sh. milioni 3, wa tano Sh. milioni  2.4 na kwamba mshindi wa sita hadi wa 15 kila mmoja atapata Sh. milioni 1.2.

Aliongeza kuwa washiriki wengine wote waliobaki yaani wa 16-30 kila mmoja apata Sh. 700,000.

Alisema katika shindano hilo ambalo ndani yake kuna mashindano mengine madogo, tayari washiriki watatu wameshajipatia tiketi ya kuingia katika Top 15, ambao ni Lucy Stephano aliyeshinda taji la Miss Photogenic, Magdalena Roy aliyetwaa taji la Top Model na Mary Chizi (Top Sport Woman).

Lundenga alisema shindano dogo jingine la kumtafuta mrembo wenye kipaji, Miss Talent, lifanyika Ijumaa Oktoba 26, 2012.

Aliongeza kuwa mshindi wa shindano dogo la Miss Personality atapatikana Oktoba 28, 2012.

Naye meneja wa kinywaji cha Redds Original, Victoria Kimaro amesema huu ni wakati mwafaka wa kumpata mshindi bomba mwenye vigezo sahihi na hivyo akawataka wapenzi wote wa fani ya urembo na wapenda maendeleo kote nchini kujiandaa kupata tiketi za kushuhudia fainali hiyo mapema ili kupata fursa ya kupata burudani mbalimbali.

"Kwa kweli tunatarajia shindano la mwaka huu litafana sana hasa kwa kuzingatia kuwa maandalizi yote yameshakamilika kwa kiwango kikubwa. Na sisi kama wadhamini wakuu tunahakikisha kuwa mwaka huu kila atakayefika kwenye ukumbi wa Ubungo Plaza atakuwa na jambo la kusimulia kwa sababu ni shindano la kipekee," alisema Vicky.

Shindano la Redds Miss Tanzania 2012 linadhaminiwa na
Kampuni ya TBL kupitia kinywaji chake cha Redds Original, Star TV na Giraffe Hotel

Mshindi wa mwaka jana alikuwa ni Salha Israel, ambaye alizawadiwa gari aina ya Jeep Patriot lenye thamani ya Sh. milioni 72 pamoja na fedha taslimu Sh. milioni 8.
LIGI DARAJA LA KWANZA KUANZA KESHO

MICHUANO ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) inaanza kutimua vumbi kesho (Oktoba 24 mwaka huu) kwenye viwanja mbalimbali nchini.

Kundi A kutakuwa na mechi tatu ambapo Burkina Faso itacheza na Mbeya City kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro wakati JKT Mlale itakuwa mwenyeji wa Small Kids kwenye Uwanja wa Majimaji, Songea.

Nayo Kurugenzi itaumana na Majimaji katika Uwanja wa Wambi ulioko Mufindi mkoani Iringa. Kundi hilo litamaliza raundi ya kwanza keshokutwa (Oktoba 25 mwaka huu) kwa mchezo kati ya Mkamba Rangers na Polisi Iringa utakaofanyika Uwanja wa Jamhuri, Morogoro.

Mechi za kundi B kwa kesho ni Ndanda dhidi ya Transit Camp katika Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara na Villa Squad itakipiga na Moro United kwenye Uwanja wa Mabatini mjini Mlandizi. Oktoba 25 mwaka huu ni Green Warriors v Tessema (Mabatini, Mlandizi) na Polisi Dar v Ashanti United (Uwanja wa Chamazi).

Kundi C kesho (Oktoba 24 mwaka huu) ni Kanembwa FC v Polisi Dodoma (Uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma), Mwadui v Morani (Kambarage, Shinyanga), Pamba vs Polisi Mara (Kirumba, Mwanza) na Rhino Rangers vs Polisi Tabora (Ali Hassan Mwinyi, Tabora).

MECHI YA MTIBWA SUGAR, JKT RUVU YAPELEKWA MBELE

MECHI namba 79 ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Mtibwa Sugar na JKT Ruvu iliyopangwa kuchezwa Novemba 3 mwaka huu Uwanja wa Manungu mkoani Morogoro, sasa itafanyika Novemba 7 mwaka huu.

Mabadiliko hayo yamefanyika kwa vile Novemba 4 mwaka huu, Mtibwa Sugar itacheza mechi namba 30 dhidi ya Simba kwenye Uwanja wa Jamhuri, mjini Morogoro. Mechi hiyo awali ilikuwa ichezwe Oktoba 3 mwaka huu lakini ikabadilishwa ili kutoa fursa kwa mechi za Super Week zilizooneshwa moja kwa moja na kituo cha televisheni cha Super Sport cha Afrika Kusini.
WANACHUO WACHAMBUA SERA MBOVU ZA SERIKALI UN






















Mtaalam wa Mazingira wa UNDP Bw. Amani Ngusaro akitaja baadhi ya vikwazo vinavyo kwamisha uboreshaji wa Mazingira katika maeneo ya makazi ikiwemo uhaba wa maji na kutaka vikwazo hivyo viangaliwe upya na kuboreshwa sambamba na kutolewa kwa elimu ya Mazingira na uhamasishaji katika ngazi zote
 Wanafunzi kutoka vyuo vikuu mbalimbali jijini wakitoa maoni yao katika mjadala wa wazi uliofanyika katika ukumbi wa Karimjee ambapo wamelalamikia baadhi ya Sera za Serikali zisizotekelezeka wakati wa maadhimisho ya wiki ya Umoja wa Mataifa kusheherekea miaka 67.
Aidha Afisa Misitu Mkuu katika Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Freddy Manyika alitoa nasaha zake kwa kusema kuwa sisi wananchi ndio tunatakiwa kuwa wa kwanza kufanya mabadiliko na sio kuilaumu serikali kwani ndio tunaozungukwa na mazingira. Aidha pia ametumia nafasi hiyo kutangaza kuwa suala la mabadiliko ya hali ya hewa sio jambo la mzaha hivyo serikali inatakiwa kuwa na sera madhubuti zitakazo wawezesha wananchi kukabiliana na madhara yatokanayo na janga hilo ili kujitahidi kuirejesha ardhi na mazingira yetu kwa ujumla katika hali bora
UVCCM WAPATA VIONGOZI WAO BAADA YA MSUGUANO MKALI






















 MWENYEKITI UVCCM TAIFA NI Mhe.JUMA SADIFA-2012-2017
MAKAMU MWENYEKITI UVCCM TAIFA NI Mhe.MBONI MHITA

WAJUMBE NEC

Jery Slaa
Deo Ndegembi
Anthony Mavunde
Jonas Nkya
Kutokea JF

Tuesday, October 23, 2012

DODOMA HAPATOSHI : UCHAGUZI WA UVCCM LEO






















Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM, Martine Shigela akizungumza na waandishi wa habari jana mjini Dodoma kuhusu maandalizi ya Mkutano Mkuu wa UVCCM. Kulia ni Cosmas Hinju, Mwenyekiti wa Kamati ya habari na mapambo wa maandalizi ya Mkutano huo, 
Kivumbi cha uchaguzi ndani ya umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi unafanyika leo mjini Dodoma na wagombea wote huku wakiwa matumbo moto kutokana na mpambano mkali uliopo wa uchaguzi huo.
ALEX FERGUSON NA RIO WAMALIZA MZOZO


















Kocha wa Manchester United Sir Alex Ferguson amesema ameshayamaliza na mchezaji wake Rio Ferdinand ambae weekend iliyopita kwenye game na Stoke City aligoma kuvaa t-shirt ya kampeni ya kupinga ubaguzi wa rangi kwenye soka ambapo ndio alikua mchezaji pekee ambae hakuvaa t shirt ya hiyo kampeni.
Fergie amesema aliaibika kutokana na hicho kitendo cha Rio lakini baadae aligundua ilitokana na tatizo la mawasiliano ila kwa sasa tayari ameshafanya nae mazungumzo hivyo sio ishu kubwa tena manake wameyamaliza ambapo Fergie amesema pia kwamba Rio ataongezewa mkataba wa mwaka mmoja baada ya huu wa sasa kuisha.
Ukiachia Rio Ferdinand ambae mdogo wake Anthony Ferdinand wa QPR alikua na ishu ya ubaguzi kutoka kwa John Terry hivi juzi, zaidi ya wachezaji 30 kwenye Premier League wamepinga hiyo kampeni.
SAKATA LA DAWA FEKI ZA ARV  TAARIFA ZAIDI ZATOLEWA
Waziri wa Afya Dk. Hussein Mwinyi

 Kiwanda cha kutengeneza dawa cha Tanzania Pharmacetical Industrial (TPI) kimesema Serikali inabidi iharakishe uchunguzi kuhusu mtu aliyeingiza nchini dawa bandia ya kupunguza makali ya virusi vya ukimwi iitwayo TT-VR 30 ili kuondoa wasiwasi ulioenea kwa watumiaji.
Mkurugenzi mtendaji wa TPI Ramadhani Madabida amesema uchunguzi wa awali unaonyesha serikali inamfahamu mtu alieingiza hizo dawa Tanzania, zilipotoka na tarehe ya kuingizw hivyo kuharakishwa kwa mchakato huo kutakomesha mizengwe ya baadhi ya wawekezaji kutoka nje kutaka kuchafua ubora wa bidhaa zinazotengenezwa Tanzania.
Tayari serikali imewasimamisha kazi Mkurugenzi mkuu wa bohari ya dawa nchini MSD Joseph Mgaya pamoja na mkuu wa kitengo cha udhibiti ubora na afisa udhibiti ubora wa MSD kutokana na kuidhinisha matumizi ya dawa hiyo bandia ya kupunguza makali ya virusi vya ukimwi.

Sunday, October 21, 2012

WANAHARAKATI WAPATIWA MAFUNZO YA KUJILINDA NA KUTUNUKIWA VYETI























Wanaharakati wakiwa na vyeti vyao baada ya kumaliza mafunzo yao ya ulinzi kwa wanaharakati wa haki za binadamu yaliyotolewa na kituo cha Haki za Binadamu Tanzania(THRD).
DK. BILAL KUFUNGUA MKUTANO WA WAFANYABIASHARA WANAWAKE























Makamu wa Rais wa Tanzania Dk. Mohamed Gharib Bilal anatarajiwa kuwa Mgeni rasmi katika ufunguzi wa Mkutano wa Saba wa Kimataifa wa Wanawake wafanyabiashara wa Nchi za Mashariki mwa Afrika unaonza kesho jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuimarisha mtandao wao. 

Kauli hiyo imetolewa leo na Mwenyekiti wa Tanzania Women Chamber of Commerce (TWCC) Fatma Riyami wakati akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake. 

Amesema kuwa mkutano huo ambao ni wa saba (7) unafanyika nchini Tanzania kwa mara ya kwanza tangu walipoanzisha ushirikiano huo wa wanawake wafanyabiashara kwa nchi za Afrika Mashariki. 

Mwenyekiti huyo amesema kuwa wajumbe wa mkutano huo wanatarajiwa kutoka katika nchi za Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Ethiopia, Sudan Kusini na mwenyeji Tanzania. 

Amesema kuwa mkutano huo utakuwa fursa nzuri kwa wajumbe kutoka nchi zote saba kubadilishana uzoefu katika kazi ya kuwainua kiuchumi akinamama na kuimarisha Mtandao wa Wafanyabiashara Wanawake katika Nchi za Afrika Mashariki. 

Ameongeza kuwa hatua hiyo itasaidia kufanya soko la wafanyabiasha wanawake wa Afrika Mashariki kuwa kubwa na hivyo kuwainua kiuchumi akinamama. 

Aidha, Riyami amesema kuwa TWCC imeanzisha matawi katika Mikoa ya Kagera, Mwanza, Pwani, Dodoma, Mbeya, Dar es Salaam na Arusha ikiwa na lengo la kutaka kuwa karibu na wafanyabiashara wanawake kwa nia ya kuimarisha umoja wao. 

Wakati huo huo, mwenyekiti huyo amewasisitiza wajumbe wa mkutano huo kufika katika Hoteli hiyo ifikapo saa 1.30 Asubuhi. Mgeni rasmi atafungua mkutano huo saa 2.00

Saturday, October 20, 2012

SEND OFF YA ROMANA MALYA AMENG'ARAJE SASA !



























Sina maneno mengi najua umejionea mwenyewe watu walivyopendeza.
HARUSINI : SALMARH NA SAID WANG'ARA