TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Thursday, February 27, 2014

The Game aweka wazi kuhusu uhusiano wake na Kim & Khloe Kardashian

game
Khloe Kardashian na The game walijiachia pamoja kwenye night club kiasi cha kuwapa watu mashaka kwamba  wawili hao wapo kwenye uhusiano wa kimapenzi hivi sasa.
Khloe alikuwa wa kwanza kukanusha uhusiano huo na kusema kwamba walikuwa wapo kwenye starehe kama marafiki.
Hivi karibuni The game amepata nafasi ya kuzungumzia kuhusu kile kilichotokea na ametoa exclusive mpya.
Akiwa kwenye radio ya BBC Radio1 Extra The game alisema asingeweza kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Khloe kwasababu alikuwa na uhusiano na dada yake Kim kipindi kilichopita.
“Watu hawajui kuhusu mimi na Khloe kwamba tumejuana miaka 12 iliyopita. Nilikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Kim Kardashian kwa muda kidogo sana. Kanye West alikuwa bado mshkaji kipindi kile na hadi sasa bado ni mshkaji wangu na najua Kim anakaribia kuwa mke wake na tayari wanafamilia. Khloe pia ni mshkaji na tuko poa pamoja kwa hiyo hizo tetesi  kati yangu na Khloe hazina ukweli”
k

Tuesday, February 25, 2014

MBEKI NA JUHUDI ZA KUSAKA AMANI SUDAN 

MBEKI_8c77f.jpg
Rais Salva Kiir,waziri mkuu wa Ethiopia Hailemariam Desalegn ba mpatanishi Thabo Mbeki
Mpatanishi mkuu wa Umoja wa Afrika kuhusu mgogoro wa Sudan,Thabo Mbeki anafanya ziara mjini Khartoum akiwa na lengo la kusaidia kutia msukumo katika juhudi za kutafuta amani kati ya serikali ya Sudan na SPLM-N.
Ziara hiyo ya Mbeki inafanyika kabla ya mazungumzo yanayotarajiwa kuanza tena mjini Ethiopia siku ya Ijumaa 28.02.2014.
Mpatanishi mkuu wa Umoja wa Afrika katika mgogoro wa Sudan Thabo Mbeki anaianza ziara yake hiyo ya mjini Khartoum ikiwa tayari serikali ya Sudan na waasi wa Kordofan Kusini wameridhia kusitisha mapigano na kuruhusu msaada kuwafikia zaidi ya watu milioni 1 kwa mujibu wa makubaliano yaliyopendekezwa kabla ya kuvunjika mazungumzo ya kusaka amani wiki iliyopita.Itakumbukwa kwamba katika mkutano huo wiki iliyopita,wajumbe wa Umoja wa Afrika waliwasilisha pendekezo hilo kwa serikali ya Khartoum na waasi hao wa kundi la SPLM-N kabla ya mazungumzo hayo ya mjini Adis Ababa kuakhirishwa kutokana na pande hizo mbili kutupiana lawama.

Mpatanishi mkuu,wiki iliyopita alisema wajumbe kutoka upande wa waasi na serikali watabidi kushauriana na kundi la wapatanishi kuhusiana na mapendekezo hayo ya Umoja wa Afrika ingawa pia hakutowa maelezo zaidi kuhusiana na suala hilo. Kimsingi sasa mazungumzo hayo yanasubiriwa kuanza tena tarehe 28 mwezi huu wa Februari. Katika kikao cha mwanzo mjini Adis mkuu wa ujumbe wa waasi Yassir Armen alisema serikali ya Sudan inataka kumaliza vita hivi bila ya kutowa suluhisho katika suala zima la hali ya kibinadamu na kisiasa.
Kwa upande wake serikali ya Khartoum inalishutumu kundi hilo la waasi wa SPLM-N kwa kuongeza masuala ambayo hayahusiani na migogoro ya Kordofan Kusini na jimbo la Blue Nile. Mgogoro na uhasama wa kikabila katika majimbo hayo mawili pamoja na uasi wa muda mrefu katika jimbo la Darfur yametokana na malalamiko ya kiuchumi pamoja na kutengwa kisiasa kwa majimbo hayo na utawala wa Khartoum unaohodhiwa na waarabu.
Ni kutokana na hali hii rais wa zamani wa Afrika Kusini ambaye sasa ni mpatanishi mkuu wa Umoja wa Afrika katika mzozo huu anataka kuzipa msukumo juhudi za kupatikana mwafaka wa amani baina ya pande hizo mbili zinazozana huku pia ukitarajiwa kufanyika mkutano wa tume ya pamoja ya Kimataifa iliyoundwa chini ya makubaliano ya amani ya mwaka 2011 kati ya Khartoum na muungano wa makundi ya waasi yaliyojitenga.Tume hiyo ilipewa jukumu la kufuatilia maendeleo ya makubaliano hayo.
Chanzo, dw.de.com/swahili. R.M
JATA WAWAPATIA ZAWADI WANAFUNZI WALIOSHINDA KUANDIKA INSHA

Wanafunzi wakiwa wamekaa tayari kwa kupokea zawadi zao

Afisa elimu mkoa wa Dar es Salaam, ambaye ndiye aliyekuwa mgeni rasmi kwa kukabidhi zawadi hizo kwa wanafunzi walioshinda




Mwanafunzi huyu ndiye aliyekuwa wa kwanza apambo alipatiwa zawadi wa Lap top


Wanafunzi watano bora ambao walishinda wakipiga picha pamoja na wadhamini wao


SHIRIKA lilisilo la kiserikali toka Nchini Japan  JICA ALUMNI ASSOCIATION OF TANZANIA (JATA)  limetumia kiasi cha Dola 800 za Kimarekani  kutoa zawadi kwa wanafunzi wa shule za sekondali nchini  walioweza  kuandika  na kuisoma  insha iliyoandaliwa na  shirika hilo.
Insha hiyo iliyoandaliwa na JATA  ilikuwa inahusu “What are the role of public secondary school in changing of social economic environment in Tanzania” ambapo jumla ya wanafunzi zaidi ya 100 walishiriki  kutoka Tanzania Bara na Visiwani.
Katibu wa Shirika hilo  nchini DK. Zacharia Mganilwa alisema JATA kwa kushirikiana na JICA wamekuwa  wakiendesha miradi mbali mbali ya maendeleo ya elimu na kwa mwaka huu wanafunzi wa shule nyingi walikuwa na mwamko wa kushiriki zoezi hilo tofauti na mwaka jana ambapo shule sita tu zilizoshiriki. 
DK. Mganila alisema  lengo la shirikia hilo kuandaa insha hiyo ni kupima uelewa wa wanafunzi kwa kuwajengea misingi ya kujiamini  na kujituma katika masomo yao .
Aidha Afisa elimu wa Mkao wa Dar es Salaam, Bw. Kiduma Mageni , kwa sasa JICA imekuwa ikitoa msaada mkubwa wa kufadhili miradi mbali mbali nchini ikiwemo ya ujenzi na upande wa elimu kwa kuwasaidia kuwapeleka baadhi ya walimu nchini Japan na kuwapatia mafunzo.
“Baadhi ya walimu huwa wanakwenda nchini Japani kwa kupata mafunzo zaidi ili wanaporudi nchini watoe mafunzo bora kwa watoto kwa kiwango kinachotakiwa, Aidha pia wajani nao wamekuwa wakijitolea katika kufundisha masomo ya hisabati na Sayansi kwenye shule za sekondari hapa nchini” alisema Bw. Mageni.
Alisema mashindano hayo pia yameleta changamoto kubwa kwa wanafunzi na kuonekana na uelewa mzuri  na kuwajenga uwezo wa kujiamini hasa kwa watoto wa kike ambao ndio wanakuwa kinara wa kuongoza na kujizolea zawadi kibao,
Alisema Mwaka jana katika shindano hilo mshindi  wa kwanza alikuwa ni mwanafunzi wa kike Faiza Khanis Ussi wa kidato cha tatu kutoka shule ya Sunni Madressa toka Zanzibar kwa  kupata alama 81  ambapo alizawadiwa Laptop moja aina HP na Certificate .
Hali kadhalika mwaka huu pia mshindi wa kwanza ni mwanafunzi wa kike kutoka mkoa wa Kilimanjaro  shule ya secondary ya Oshara  ni Zusaz Mmari  wa kidato cha nne,alipata alama 90 ambapo amepatiwa Laptop  moja aina ya HP ,Certificate  na Dictionary mbili.
Wshindi wengine waliobahatika kupata zawadi zingine mbali mbali ni Samwel Steven  ambaye alikuwa mshindi wa pili toka shule ya Kilindi iliyopo Sanya Juu, Mariaum Ramadhani toka shule ya Lumumba toka Zanzibar,  Furaha Mika toka shule ya Malangali Mbeya, ambapo jumla ya wanafunzi kumi walioshinda walipatiwa zawadi zao.

Thursday, February 20, 2014

Whatsapp yanunuliwa na Facebook, nini tutegemee 


Kama ulikuwa haufahamu, habari kuu katika ulimwengu wa Teknohama kwa siku ya leo ni Facebook kuinunua Whatsapp kwa bei ya dola bilioni 19.  Nunuzi hilo ni la programu pekee na siyo kampuni ingawa wafanyakazi wa whatsapp watajiunga na timu ya Facebook moja kwa moja, mission za whatsapp zitaendelea kubaki kama zilivyo, alieleza Jan Koum ambaye ni muanzilishi wa whatsapp.

Kwa wasio fahamu, whatsapp ni moja ya programu ya simu za mkononi inayokuwezesha kutuma ujumbe wa simu kupitia kwenye intaneti badala ya ujumbe mfupi (sms). Kwa kutumia whatsapp, inamaana utaepuka gharama za sms huku ikiwa imesheheni matumizi mengine mengi zaidi kama kutuma picha, sauti uliyojirekodi nk.

Hadi sasa, whatsapp ina watumiaji hai milioni 450 kila mwezi kutoka nchi nyingi duniani, huku kukiwa na watumiaji wapya zaidi ya milioni moja kila siku. Hivyo, ni dhahiri kuwa whatsapp ni programu pendwa na yenye kutumika.

Whatsapp inaweza kutumika kama njia rahisi zaidi ya mawasiliano kwa watu binafsi na hata makampuni, 

Ingawa makampuni mengi ikiwemo Facebook yamekuwa yakitegemea huduma za matangazo kama njia ya kuingeza kipato, whatsapp ni programu ambayo, huwezi kuonana na matanagazo na wamejizatiti kuwa ni wataendelea hivyohivyo bila ya matangazo. Na pia whatsapp ni bure kwa kwa mwaka wa kwanza na huchaji $1 kwa mwaka kama gharama ya kujiunga kwa miaka inayofuata. Hivyo kabla ya Facbook kuinunua whatsapp ni dhahiri walishajipanga kwenye hili, kwani, hili ndilo linaloifanya whatsapp iwe tofauti.

Akielezea sababu ya kuinunua whatsapp, mwanzilishi wa Facebook alisema, wameinunua whatsapp kwa sababu whatsapp ina thamani. Na wao wakiwa kama wafanya biashara lengo lao kubwa ni kuongeza thamani ya biashara yao illi waendelee kuwa salama. Hivyo, wanaamini nunuzi la whatsapp litakuwa na tija na manufaa kwa wote, wanunuzi na walionunuliwa. Hivyo ubora na misingi ya huduma ya whatsapp utaendelea kuwa juu kama ilivyo sasa.


Lakini, dili hili la kuinunua whatsapp halikuja ghafla, bali limekuja kwa kuangalia muelekeo na mabadiliko ya watumiaji wa mtandao. Taarifa zinaonesha kuwa, asilimia zaidi ya 52% ya watumiaji wa mtandao kwa sasa ni wale wanaotumia simu. Na pia matumizi ya email kama njia ya mawasiliano yamezidi kupunguasiku hadi siku. Na siku zinavyozidi kwenda mbele inamaanisha idadi hii itakua.

Pia, kwenye uwanja wa ujasiriamali, unatakiwa kuishi kwa kuyachunga mazingra na siyo kuomba dua mambo yasibadilike, hivyo ununuzi huu umekuja ili kuhakikisha Facebook inakuwa na udhibiti wa mazingira ya watumia intaneti na mtandao.Kitendo cha Facebook kuinunua whatsapp, kinaiwezesha kujikita zaidi kwenye kundi kubwa la watumiaji wa intaneti ambao wengi ni vijana.

Kwakuwa watumiaji wengi wa whatsapp ni wa kwenye simu, na kwakuwa yao ni moja ya programu zenye mamilioni ya watumiaji, hivyo kuimiliki whatsapp inamaanisha kumiliki hisa kubwa kwenye soko la watumiaji hao. Na hii itaiweka Facebook katika hali ya kudhitibi soko. la intaneti na mitandao jamii. Facebook pia watapata njia wa kuwafikia watumiaji hawa moja kwa moja kama ilivyokuwa kwa instagram, hivyo hii ni moja nunuzi lenye faida kwao.

Watu wengi wamekuwa wakijiuliza, je kitendo za Facebook kuinunua whatsapp kina faida yoyote kwa kampuni? na nini sisi watumiaji wa whatsapp tutegemee? Kutokna na sababu nilizozitaja juu (thamani), hivyo ni yumkini kabisa, Facebook wanaweza kufanya kati ya vifuatavyo.

1. Kuiunganisha whatsapp moja kwa moja na Facebook.
Ikumbukwe kuwa, whatsapp itaendelea kuwa whatsapp, hivyo usifikiri kwamba kesho hakutakuwa na whatsapp bali watumiaji wote watapelekwa Facebook, la , ila whatsapp itakuwa na ushirikiano wa kiutendaji na Facebook na kuzifanya ziwe imara zaidi. Ila, ili whatsapp iunganishwe na facebook, ni dhahiri kuwa whatsapp lazima ifanyiwe maboresho na kuongezewa baadhi ya matumizi ambayo yataiwezesha kuiunganisha moja kwa moja na Facebook, isiishie kwenye mawasiliano tu. Kunatakiwa kuongezwe / boreshwa zaidi zile huduma ya kijamii.


Kwa mfano, tutegemee kuwa na uwezo wa kutuma visasisho(updates) ambavyo vitaonekana kwenye Facebook yako. Hii itaipe ya maisha yako hapohapo kwenye whatsapp. Hii itaipeleka whatsapp kufanana sana na moja ya mtandao unaofanya kazi zake kama whatsapp unaoitwa Wechat.Huu ni mtandao uliofanikiwa sana kwa China.

2. Kutafuta / alika marafiki wa facebook kwa kutumia namba za simu na siyo email pekee
Facebook ilipoanza, ilikuwa inategmea sana email kama njia ya kutafuta marafiki, ila kadri siku zinavyozidi kwenda, matumizi ya email kama njia ya mawasiliano ya kawaida yamekuwa yakipungua, hivyo kutegemea email kunaiweka facebook kwenye kikomo cha kutanuka. Kwakuwa whatsapp inatumia namba za simu, na kwakuwa facebook imeinunua whatsapp, basi tutegemee kuwa kutakuwa na uwezo kwa watumiaji wa Facebook kuwaalika watu wajiunge na facebook kwa njia ya ujumbe wa simu, na hii itaunganishwa vyema kwa kutumia whatsapp.

3. Kuongezwa huduma zaidi ambazo ni za kulipia.
Kwakuwa lengo la kuwekeza ni kuongeza kipato.Iwe moja kwa moja au la, ni dhahiri kuwa facebook watakuja na njia zitakazowawezesha kuongeza kipato kwa kutumia whatsapp, hivyo kutakuwa na huduma zaidi ambazo si za lazima, ila kama utazihitaji, basi utatakiwa kulipia kiasi fulani. Hii ni moja ya njia zinazotumika kipindi unaandaa bando la huduma.

Hivyo,kwa watumiaji wa Facebook na Whatsapp, tutegee mambo mengi zaidi.

RWANDA YAPONGEZA HUKUMU YA RWABUKOMBE HUKO UJERUMANI 

postsssss_91050.jpg

Mahakama moja ya Ujerumani imemhukumu meya wa zamani wa Rwanda, Onesphore Rwabukombe, kifungo cha miaka 14 gerezani kwa jukumu lake katika mauaji ya halaiki ya mwaka 1994 ya Rwanda.
Rwabukombe mwenye umri wa miaka 56 alikutwa na hatia ya kuamuru mauwaji ya mamia ya watu katika kanisa moja ambako watu walikusanyika kupata hifadhi huko Kiziguro. Amekuwa akiishi kama mkimbizi wa kisiasa nchini Ujerumani tangu mwaka 2002.
Hii ni kesi ya kwanza kufanyika Ujerumani iliyohusisha mauaji ya halaiki nchini Rwanda. Kesi hiyo iliyodumu miaka mitatu huko Frankfurt ilisikiliza ushahidi kutoka zaidi ya mashahidi 100 na wapelelezi wa jinai walipelekwa Rwanda kufanya uchunguzi.

Serikali ya Rwanda imepongeza uamuzi wa mahakama ya Frankfurt, kumhukumu Rwabukombe mshukiwa wa mauaji ya Rwanda mwaka 1994.Rwanda inasema hata kama kesi hiyo imesikilizwa nje ya nchi lakini ni ishara kwamba sheria za kimataifa zinaheshimiwa popote pale unapokimbilia.
Kesi ilisikiliza namna kati ya watu 400 hadi 1,200 walivyouwawa hapo April 11 mwaka 1994 kwenye kanisa moja huko Kiziguro, mashariki mwa Rwanda ambako Rwabukombe wakati huo alikuwa meya.
Mwendesha mashtaka mkuu Christian Ritcher alisema Ujerumani sio mahala pa hifadhi ya watenda maovu kufuatana na sheria za kimataifa anasema huo ndio ujumbe ambao umetolewa jumanne kwa sauti kubwa kufuatia hukumu hii.
Rwabukombe alikana mashtaka yote. Mawakili wake wamesema walitaka kesi ifutiliwe mbali na wamesema watakata rufaa.
Kuna baadhi ya nchi zilizowafungulia mashtaka washukiwa wa Rwanda katika nchi walizokimbilia lakini Kigali inataka washukiwa walio nje ya nchi kurudishwa nyumbani na kupatiwa hukumu kwenye nchi yao na inasisitiza washukiwa hao kurudishwa nyumbani.
Mataifa mengi yangali yanasita kuchukua hatua hiyo . Watu watano huko Uingereza wanasubiri kesi ya kusafirishwa nyumbani inayotarajiwa kuanza wiki ijayo.
Chanzo, voaswahili.com/

WATU 25 WAUWAWA UKRAINE 

ukrain_c4d8f.jpg
Licha ya kuuawa kwa watu zaidi ya 20 na wengine zaidi ya 200 kujeruhiwa usiku wa kuamkia leo mjini Kiev, waandamanaji wameapa kurudi kwenye Uwanja wa Uhuru kuendelea kushinikiza kujiuzulu.
Rais Viktor Yanukovych huku rais huyo anawalalamikia viongozi wa upinzani kutokana na vurugu hizo kati ya polisi na waandamaji na kutishia kuchukua hatua kali zaidi.
Moshi, vilio na hasira ndiyo picha ya mji mkuu wa Ukraine, Kiev, asubuhi ya leo, baada ya vurugu zilizotekea jana, ambazo zinatajwa kuwa mbaya zaidi kutokea katika maandamano ya kupinga serikali ya Kiev, ambayo yamedumu kwa karibu miezi mitatu na kukwamisha shughuli mbalimbali mjini humo. Maelfu ya polisi wa kutuliza ghasia waliokuwa na maguruneti na maji ya kuwasha waliwashambulia waandamanaji katika kambi yao mjini Kiev.
Kiongozi wa upinzani Vitali Klitschko amewataka waandamanaji kiasi cha 20,000 kwenda kuulinda uwanja wa Uhuru ambao umekuwa kitovu cha maandamano hayo, na ambao kwa sasa robo tatu inashikiliwa na polisi:
Kiongozi huyo ambae ni bingwa wa zamani wa ndondi za uzito wa juu aliwaambia waandamanaji kuwa hawataondoka katika eneo la kambi ya maandamano kwa kusema hicho ni kisiwa cha uhuru na watakilinda kwa kadiri wawezavyo.
Waandamanaji watoa kauli kali
Mapema leo wengi wa raia wameonekana kusikiliza wito wa kiongozi huyo. Mwanandamaji mmoja, Anthony Rybkovivich, mwenye umri wa miaka 32 amesikika akisema "Sitokwenda kukaa tu na kusubiri niuwawe, nakwenda kupambana."
Kiasi ya watu 10,000 wameendelea kubakia katika uwanja huo wakati moto uliowashwa kwa kutumia matairi ukiendelea kuwaka. Jengo kubwa ambalo waandamanaji wamekuwa wakilitumia kama makao makuu limewaka moto na limetelekezwa wakati wa vurugu za usiku pale ambapo polisi walipotumia kipaza sauti kutangaza wanawake na watoto waondoke katika uwanja huo kwa kile walichosema kunafanyika operesheni ya kukabiliana na magaidi.
Upinzani walaumiwa kwa vurugu
Rais Yanukovych anasema viongozi wa upinzani wamevuuka mipaka kwa kutoa wito kwa watu kubeba silaha. Katika taarifa yake, kiongozi huyo ameutaka upinzani kujitenga na makundi ya wenye itikadi kali wanachochea vitendo vya umwagikaji damu na vurugu dhidi ya vikosi vya usalama.
Aidha Yanukovych aliongeza kusema kuwa endapo hawataondoka katika uwanja wa maandamano wataonekana kama wenye kuunga mkono misimamo ya wenye itikadi kali. Na kwa hivyo ameonya kwamba mazungumzo baina yao yanaweza kubadilika muelekeo wake.
Viongozi mbalimbali wa kimataifa wamepaza sauti zao juu ya hali ya mambo nchini Ukraine. Makamu wa Rais wa Marekani, Joe Biden, ameonesha kusikitishwa kwake wakati alipozungumza na Yanukovych kwa njia ya simu. Huku sauti nyingine kutoka huko zikitoa wito wa taifa hilo kuwekewa vikwazo wazo ambalo limepingwa na Ujerumani.
Chanzo, dw.de.com

Wednesday, February 19, 2014

MKUTANO MKUU WA MAAFISA WAKUU WA JESHI LA POLISI WAANZA LEO MJINI MOSHI

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Ernest Jumbe Mangu akisisitiza jambo kwenye mkutano Mkuu wa Maofisa Wakuu Waandamizi wa Jeshi la Polisi unaofanyika katika Chuo cha Taluma ya Polisi Moshi, mkoani Kilimanjaro. Mkutano huo umebebwa na kauli mbiu isemayo “Zingatia Weledi katika Kutoa Huduma Bora Kwa Jamii”.
Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi (CP) Paul Chagonja akisisitiza kwa Makamanda wa mikoa na Vikosi wa Jeshi la Polisi kufanya kazi kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu hususani katika kushughulikia migogoro, kwenye mkutano Mkuu wa Maofisa Wakuu Waandamizi wa Jeshi la Polisi unaofanyika katika Chuo cha Taaluma ya Polisi Moshi mkoani Kilimanjaro. Picha Na Hassan Mndeme-Jeshi la Polisi.
CHANZO:MTAA KWA MTAA

BARCELONA 2-0 MANCHESTER CITY, ROBO FAINALI YA LIGI MABINGWA ULAYA

Messi akishangilia baada ya kufunga bao la kwanza kwa penalti usiku huu Uwanja wa Etihad
BARCELONA imejiwekea mazingira mazuri ya kupenya Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, kufuatia ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya wenyeji Manchester City, Uwanja wa Etihad usiku huu katika mchezo wa kwanza, hatua ya 16 Bora ya michuano hiyo.
Lionel Messi alifunga bao la kwanza dakika ya 54 kwa penalti ya utata, baada ya yeye mwenyewe kuangushwa nje kidogo ya eneo la hatari na Martin Demichelis, lakini refa akatenga tuta, kabla ya beki Dani Alves kufunga la pili dakika ya 90. 

Hilo linakuwa bao la kwanza kabisa Messi anafunga dhidi ya vigogo wa Ligi Kuu ya England tangu ameanza kukutana navyo akiwa na Barca mwaka 2006 na kumaliza ukame wa kucheza saa 12 nchini humo bila kufunga.
Katika mchezo mwingine wa leo 16 Bora Ligi ya Mabingwa, Uwanja wa BayArena mjini Leverkusen, wenyeji Bayer 04 Leverkusen walichapwa mabao 4-0 na Paris Saint-Germain FC ya Ufaransa.
Mabao ya PSG yalifungwa Matuidi dakika ya tatu, pasi ya Verratti, Ibrahimovic dakika ya na 42 pasi ya Matuidi na Cabaye dakika ya 88 pasi ya Lucas.

Ndani ya eneo la hatari? Martin Demichelis akimkwatua Lionel Messi kusababisha penalti, lakini ilikuwa faulo ya ndani ya boksi? Na chini Messi akipiga penalti hiyo.


Ibrahimovic akishangilia baada ya kuifungia PSG

UKRAINE 'YATEKETEA'KATIKA MAKABILIANO

Moto mkubwa kwenye barabara za mji wa Kiev
Rais wa Ukraine, Viktor Yanukovych amewalaumu viongozi wa upinzani kutokana na vurugu zilizozuka hivi punde katika mji mkuu Kiev. Katika taarifa, bwana Yanukovych ametoa wito kwa upinzani kujiepusha na kile alichokitaja kuwa nguvu za 'misimamo mikali'.
Amesema bado kuna fursa ya kumaliza mzozo huo.
 Matamshi hayo yanakuja huku mapambano kuhusu mustakabal wa Ukraine yakizuka tena. Baadhi ya waandamanaji wanaoipinga serikali walirusha mawe na mabomu ya petroli kuwashambulia polisi waliokuwa wanawazuia kuandamana hadi makao ya bunge.
Polisi nao walijibu kwa kuwafyatulia risasi za mpira magari ya kutupa maji na maguruneti ya kuwaduwaza waandamanaji hao.
Kila upande unalaumu mwingine kwa kuanzisha mapigano hayo. Vifo vimeripotiwa miongoni mwa waandamanaji na vikosi vya usalama vile vile. Vurugu hizo zimesitisha shughuli za kawaida katika mji mkuu Kiev kwa majuma kadhaa tagu rais Victor Yanukovych akatae kutia saini mkataba mkubwa wa kibiashara kati ya Ukraine na umoja wa Ulaya na badala yake kutafuta ubia na taifa la Urusi.
Polisi pia wamejeruhiwa katika makabiliano na waandamanaji.
Vurugu za barabarani zilielekea bungeni ambapo wabunge wa ukraine walikabiliana baada ya mjadala kuhusu mswada wa kubana madaraka ya rais Victor Yanukovych ulipoahirishwa. Mmoja wa viongozi wakuu wa upinzani Vitali Klitschko amesema mazungumzo na rais Yanukovych yamegonga mwamba baada ya yeye kutaka waandamanaji kuondoka mjini Kiev bila masharti.
"Sina furaha kabisa kwa sababu hayakuwa mazungumzo na rais hataki kusikiza upinzani. Hatawataki kusikiza na njia ya kipekee ni waandamanaji wote kusitisha maandanamano amesema. Lakini kwa sasa ni muhimu kusitisha mapigano," amesema Vitali Klitschko.
Mkuu wa sera za kigeni katika umoja wa Ulaya, Catherine Ashton, amesema ana wasiwasi mkubwa kuhusiana na kukithiri kwa vurugu na kutoa wito kwa wanasiasa kushughulia maswala yaliozua tofauti zilizopo. Urusi imelaumu wanasiasa kutoka mataifa ya magaribi kwa kuchochea vurugu hizo na badala yake kukatalia mbali kile Moscow inazingatia kuwa vitendo vya kichokozi vya makundi yenye misimamo mikali miongoni mwa waandamanaji.
Ikulu ya White inasema kuwa makamu wa rais wa Marekani Joe Biden amempigia simu rais Yanukovych kumwambia kuwa ana wasiwasi mkubwa kuhusiana na vurugu hizo zinazozidi kuwa mbaya na kumtaka awaondoe wanajeshi wa serikali.

TUZO ZA KILI ZAZINDULIWA RASMI

kili_bf22f.jpg
Dar es Salaam. Tuzo za Muziki, maarufu 'Kilimanjaro Music Award' zimezinduliwa rasmi jana na zitafikia kilele chake Mei 3 kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
Tuzo hizo zinaratibiwa na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) kwa kushirikiana na TBL kupitia kinywaji chao cha Kilimanjaro.
Mratibu wa Tuzo hizo kwa upande wa Basata, Kurwijira Ng'oko alisema mwaka huu wameboresha zaidi tuzo hizo, ambapo hivi sasa wanataka muziki uwe ni ajira rasmi kwa hiyo msanii ambaye atapendekezwa katika vipengele vya tuzo hizo kama hajasajiliwa Basata hataruhusiwa kushiriki.
Ng'oko alisema pia tuzo ya mtayarishaji chipukizi wa mwaka haitakuwapo kwa vile watayarishaji ni wale wale kila mwaka na hivyo kufanya tuzo kujirudia.
Naye meneja wa bia ya Kilimanjaro ambao ni wadhamini wa tuzo hizo, George Kavishe alisema kuwa Watanzania ndio watakaoteua msanii atakayeingia kwenye mchakato wa kinyang'anyiro cha tuzo hizo kwa kutoa mapendekezo yao kwa njia ya simu au mitandao ya kijamii. chanzo, mwananchi

Monday, February 17, 2014

HALI MBAYA YA HEWA MAREKANI 

hh_105f4.jpg
Gari la kuondoa theluji likiwa kazini huko Atlanta, Georgia
Dhoruba kali ya majira ya baridi kali imesababisha zaidi ya watu 300,000 eneo la kusini mashariki mwa Marekani kukosa umeme wakati dhoruba hiyo ikielekea eneo la kati ya Atlantic na sehemu za kaskazini mashariki mwa taifa hili.
Dhoruba imesababisha kunyesha kwa darzeni ya sentimeta za theluji kote katika eneo la Washington DC hapo Alhamis. Wakati katika baadhi ya maeneo ya Washington imeripotiwa kuwepo mpaka sentimeta 46 za theluji.
Serikali kuu imefungwa pamoja na darzeni ya serikali za mji na mashule. Huko North na South Carolina, dhoruba imesababisha barabara ndogo na barabara kuu hazipitiki na kulazimisha madereva kuacha magari yao.
Watabiri wa hali ya hewa wamesema Carolina zote mbili zilitarajiwa kupata zaidi ya sentimeta 20 za barafu na theluji hadi Alhamis asubuhi baada ya kupata mchanganyiko wa theluji na mvua hapo Jumatano.
Hali ya hewa imesababisha maelfu ya safari za ndege kufutwa kwa muda, abiria kukwama kwenye viwanja vya ndege. Darzeni ya vifo vimeripotiwa kusababishwa na dhoruba ikiwemo watu watatu kufariki wakati gari la kubeba wagonjwa lilipoteleza kwenye barabara zilizokuwa na barafu huko Texas.
CHANZO:VOA

DODOMA YAFURIKA , WAJUMBE WAWASILI VYUMBA VYAADIMIKA 

dodomapix_64492.png
Na Elizabeth Edward na Hebel Chidawali, Mwananchi
Dar es Salaam/Dodoma.Wakati Wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba wakiwasili mjini Dodoma, Ofisi ya Bunge imetangaza kuandaa utaratibu wa malazi kwa wajumbe hao katika hoteli mbalimbali mjini humo.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Katibu wa Bunge na Katibu wa Baraza la Wawakilishi, jumla ya hoteli 27 zimeainishwa kuwapokea wajumbe hao 640 ambao wanatarajiwa kuwapo mjini Dodoma kwa muda wa miezi mitatu.
Pamoja na utaratibu wa malazi, taarifa hiyo pia iliagiza wajumbe hao kuwasili wakiwa na nakala halisi za vitambulisho vitakavyotumika kwa ajili ya usajili.
Taarifa hiyo ilieleza kuwa usajili utafanyika leo na kesho kwenye Ofisi za Bunge, ambapo zoezi hilo litajumuisha ujazaji wa fomu, upigaji picha za vitambulisho sambamba na kukabidhiwa vitendea kazi.
Baada ya zoezi hilo Katibu wa Bunge na Katibu wa Baraza la Wawakilishi watakutana na wajumbe kwa ajili ya kutoa maelekezo ya awali yanayohusiana na utaratibu wa ukaaji, jiografia ya viwanja vya Bunge na huduma za utawala.
Kikao cha kwanza cha mkutano huo kitafanyika Jumanne ijayo, ambapo pamoja na masuala mengine kitahusisha uchaguzi wa mwenyekiti wa muda atakayesimamia upitishwaji wa kanuni na uchaguzi wa Mwenyekiti wa Bunge hilo.
Wiki iliyopita Ikulu ilitangaza majina ya wajumbe 201, yaliyoteuliwa na Rais Jakaya Kikwete kushiriki katika uchambuzi wa Rasimu ya Pili ya Katiba na kutengeneza Katiba Mpya.
Mbali ya wajumbe wa Bunge la Katiba, pia wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) wako Dodoma wakiendelea na vikao vyao.
Mji wafurika wageni
Kutokana na kuwapo kwa ugeni huo, Mji wa Dodoma umefurika wageni wakiwamo wajumbe wa Bunge la Katiba na Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) huku, maeneo mengi yakionekana kufanyiwa usafi.
Hata hivyo, wageni wengi walionekana kuingia jana na baadhi ya watumishi wa hoteli hizo walikiri kuwasajili baadhi ya wageni, ambao wapo katika orodha hiyo.
Gazeti hili jana lilishuhudia kukiwa na maandalizi ya mwisho kwa ajili ya mapokezi hayo, huku baadhi ya maeneo yakiendelea kukarabatiwa ikiwamo kupaka rangi.
Moja kati ya maeneo ambayo wageni wengi wamepangwa kufikia ni Hoteli ya New Dodoma ambayo imepangiwa vyumba 87.
Katika eneo la hoteli hiyo, jana kulikuwa kukifanyika usafi wa hali ya juu ikiwemo kupata rangi, kusafisha maji kwenye bwawa la kuogelea, kupulizia dawa baadhi ya maeneo na katika bustani ikiwamo kufagia paa la juu upande wa vibanda.
Hoteli nyingine ambayo kulikuwa na usafi katika kumbi zake pamoja na mandhari ya nje ni Fifty Six

GHASIA ZAONGEZEKA JAMHURI YA AFRIKA YA KATI

pp_a07cb.jpg
Mama huyu alia baada ya dadake kuuawa katika ghasia mjini Bangui
Takriban wanajeshi 1,600 wa Ufaransa na 6,000 wa Umoja wa Afrika wamo nchini humo kujaribu kulinda raia wakati ghasia zenye maafa zikiendelea kati ya Wakristo na Waislam
Waziri wa ulinzi wa Ufaransa anasema lazima tahadhari zichukuliwe ili Jamhuri ya Afrika ya Kati isigawanyike. Onyo hilo limetolewa huku makundi ya kutetea haki za binadamu yakionya kuwa mauaji ya kikabila yanaendelea katika taifa hilo lililokumbwa na mgogoro wa kisiasa.
Waziri huyo Jean Yves Le Drian alifanya mazungumzo mjini Bangui na maafisa wa ngazi ya juu ya jeshi la Ufaransa pamoja na kaimu rais wa Jamhuri ya Afrika ya Kati Catherine Samba- Panza aliyeungana naye wakati wa ziara yake kusini magharibi mwa nchi.
Hii ni mara ya tatu kwa waziri Le Drian katika Jamhuri ya Afrika ya Kati, tangu Ufaransa ilipozindua operesheni ya kijeshi mwishoni mwa mwaka jana. Onyo lake limetolewa huku makundi mawili ya kutetea haki za binadamu Amnesty International na Human Rights Watch yakionya juu ya mauaji ya kikabila katika baadhi ya maeneo ya nchi yanayolenga waislam walio wachache.
Akizungumza na kituo cha televisheni ya Ufansa France 24, kamishina wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya wakimbizi Antonio Guterres alisema hali katika Jamhuri ya Afrika ya Kati ni janga la kibinadamu. Alitoa mwito kwa jamii ya kimataifa kuongeza idadi ya walinda amani haraka ili kurejesha uthabiti nchini humo.
Takriban wanajeshi 1,600 wa Ufaransa na 6,000 wa Umoja wa Afrika wamo nchini humo kujaribu kulinda raia wakati ghasia zenye maafa zikiendelea kati ya Wakristo na Waislam. Jumuiya ya Ulaya inategemewa kupeleka wanajeshi 500 katika mji mkuu Bangui mapema mwezi Machi.
Jumanne, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon alisema ameomba Ufaransa kupeleka wanajeshi zaidi nchini humo kuzuia ghasia hizo kuendelea. Takriban watu 1,000 wameuawa na maelfu kutoroshwa makazi yao.

Tuesday, February 11, 2014

A PROPOSED CHURCH BUILDING FOR GOOD NEWS INTERDENOMINATIONAL PROPHETIC FIRE MINISTRIES ( JENGO LINALO TARAJIWA KUJENGWA LA HUDUMA YA HABARI NJEMA)

 A MAN OF GOD, PROPHET STARFFORD GODSON JACOB, INVITES ALL THOSE MEN AND WOMEN OF GOD, TO CONTRIBUTE IN THIS SPECIAL ACTIVITY OF BUILDING THE CHURCH. IF YO FEEL BLESSED TO DO SO, PLEASE YOU MAY SEND YOUR CONTRIBUTION THROUGH THE FOLLOWING: EQUITY BANK AC 3001111174678 QUALITY CENTER BRANCH ( 2 Samuel 7: 5).
 for more details please contact the Prophet through +255757208288 / + 255713055459 
                   or 
E - M ail; gadsonstar@yahoo.com



  MTU WA MUNGU NABII STARFFORD GODSON JACOB, ANAWAKARIBISHA WATU WOTE WA MUNGU WA KIKE NA WA KIUME, KUCHANGIA KATIKA UJENZI WA KANISA. KILA ANAYEJISIKIA KUMTOLEA MUNGU ANAWEZA KUCHANGIA KUPITIA AKAUNTI NAMBA: 3001111174678 EQUITY BANK TAWI LA QUALITY CENTER NYERERE ROAD ( 2 samweli 7:5).
kwa mawasiliano zaidi piga simu +255757208288 / + 255713055459 
        au 
kwa barua pepe: gadsonstar@yahoo.com

MTU WA MUNGU NABII STARFFORD GODSON JACOB AKIOMBA KABLA YA KUANZA KUHUBIRI ( A MAN OF GOD, PROPHET STARFFORD GODSON JACOB PRAYING BEFORE START DELIVERING THE MASSAGE)


Wednesday, February 5, 2014

ZITTO AIBUKA NA DVD

Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe.
WAKATI Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, akijipanga kuanza ziara katika mikoa kadhaa nchini kujibu mapigo ya tuhuma dhidi yake zilizotolewa na baadhi ya viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwenye ziara ya Operesheni M4C Pamoja Daima, mbunge huyo ameibuka na DVD inayowananga viongozi wa CHADEMA.
Vyanzo vyetu vya habari vilisema kuwa DVD hizo zitasambazwa kwenye mikoa na maeneo yote atakayofanya mikutano ya hadhara mbunge huyo, kama moja ya harakati na mikakati ya kujisafisha na tuhuma za usaliti zinazomkabili ndani ya chama.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini kuwa DVD hizo zinatengenezwa kwenye kampuni moja iliyopo eneo la Kariakoo ambayo imepewa tenda ya kuchapa nakala 10,000 na kampuni nyingine zaidi ya tatu, nazo zimepewa tenda ya kuchapa DVD hizo kwa idadi tofauti.
Hata hivyo jambo la kushangaza ni kwamba katika jaradio la DVD hizo kuna rangi ya njano, nyeupe, bluu nyepesi, bluu nzito pamoja na bendera ya taifa.
Rangi zilizotumika kwenye jaradio hilo hazina uhusiano na rangi za bendera ya CHADEMA wala chama chochote cha siasa nchini.
Mbali ya jaradio hilo kupambwa na rangi hizo, pia limepambwa na picha kadhaa za mikutano aliyopata kuifanya mwanasiasa huyo katika maeneo mbalimbali na nyakati tofauti nchini, huku picha kubwa ikimwonyesha Zitto akiwa amevalia suti huku akitabasamu.
Jaradio hilo pia limezungukwa na maandishi mbalimbali ambayo yanasomeka:
‘Uadilifu, Uzalendo na Uwajibikaji, ndio silaha yetu katika kutetea wanyonge na maskini wote wa Tanzania, tuungane kwa pamoja.’  ‘Tanzania Kwanza’
Maandishi mengine makubwa yanamtambulisha mbunge huyo ambayo  nayo yanasomeka:
‘Zitto Zuberi Kabwe, Mtetezi wa Wanyonge, Tumaini la Maskini wa Tanzania”
Jaradio hilo pia limeweka mawasiliano ya mbunge huyo ya simu ya mkononi, barua pepe, Facebook na Twitter.
Hakuna maelezo yanayoonyesha kama DVD hizo zinauzwa au zinatolewa bure.
Ndani ya DVD
DVD hizo ambazo nakala tunayo, zinaonyesha picha ya mikutano ya hadhara ya mbunge huyo aliyoifanya mkoani Kigoma mara baada ya Kamati Kuu (CC) ya CHADEMA kumvua nyadhifa zake na Mahakama Kuu kushikilia hatima ya uanachama wake baada ya kukabiliwa na tishio la kuvuliwa uanachama.

Kwa mujibu wa DVD hizo, katika moja ya mikutano ya mkoani Kigoma, Zitto anasikika akiuambia umati wa wafuasi wake waliofurika kumsikiliza akieleza chanzo cha mgogoro wake na CHADEMA ni msimamo wake wa kuhoji hesabu za fedha za vyama vya siasa, kikiwemo CHADEMA na kumuagiza Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kufanya uhakiki.

Kama ambavyo amepata kukaririwa mara kwa mara, Zitto ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) anasema CHADEMA ilimtaka awajulishe kwanza kabla ya kumuagiza CAG kufanya ukaguzi ili kutoa fursa ya kuweka hesabu zao vizuri.

DVD hiyo pia inamuonyesha Zitto akisema sababu nyingine ya ugomvi wake na CHADEMA ni dhamira yake ya kutaka kuwania uenyekiti wa CHADEMA, nafasi ambayo kwa sasa inashikiliwa na Freeman Mbowe, Mbunge wa Hai na Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.

Huku akishangiliwa na maelfu ya wafuasi wake, baadhi wakiwa na mabango ya kumsifia, Zitto anasema hajawahi kupewa fedha na CCM kuisaliti CHADEMA na kuongeza kwamba atakuwa wa mwisho kutoka ndani ya chama hicho alichojiunga nacho akiwa na umri wa miaka 16.

Dk. Kitila Mkumbo naye yumo

DVD hiyo pia inamuonyesha aliyekuwa Mjumbe wa Kamati Kuu na Baraza Kuu la CHADEMA, Dk. Kitila Mkumbo, akieleza sababu za yeye kutaka kujiuzulu kabla ya Kamati Kuu kuamua kumvua uanachama.

Dk. Kitila pia anaonekana  kwenye DVD hiyo akielezea waraka ulioandikwa na Samson Mwigamba ambao ulinaswa ukielezea mikakati ya kutaka kuung’oa uongozi wa Mbowe kwenye nafasi ya uenyekiti.

Kwa kifupi maelezo ya Dk. Kitila ni  yale aliyopata kuyatoa siku yeye na Zitto walipofanya mkutano na vyombo vya habari katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam wakitetea waraka huo kwamba haukuwa wa uasi kama ilivyotafsiriwa na CHADEMA.

Wiki iliyopita gazeti hili liliibua mkakati  unaodaiwa kufadhiliwa na  Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa kutaka kumtumia Zitto kupambana na CHADEMA waziwazi.

Katika mkakati huo CCM inadaiwa kutaka kukodisha helikopta ya kumpeleka Zitto katika mikoa minne kwa gharama ya sh milioni 50, mara tu baada ya CHADEMA kuhitimisha Operesheni yao ya M4C Pamoja Daima.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka vyanzo vilivyo karibu na Zitto na CCM, yeye na chama hicho sasa wana adui mmoja – CHADEMA; na wameamua kujibu mapigo baada ya kuridhika kwamba kwa vyovyote Zitto amekwisha kupoteza uanachama wake katika CHADEMA.

Nia yao ni kumtumia Zitto kuleta mpasuko katika CHADEMA, na kufunika mjadala wa mgogoro wa CCM, kero za wananchi na mchakato wa Katiba mpya.

Zitto ambaye alivuliwa nyadhifa zake zote ndani ya CHADEMA – Naibu Katibu Mkuu Bara, Mjumbe wa Kamati Kuu, Mjumbe wa Baraza Kuu na Naibu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni – anatarajia kutumia helikopta yenye uwezo wa kubeba watu wanne, ambayo inadaiwa kukodishwa na wapinzani wa CHADEMA.

Kwa mujibu wa habari hizo, lengo la ziara ya Zitto ni kujibu mapigo ya CHADEMA, hasa katika maeneo ambayo baadhi ya makada na viongozi wa chama hicho wamepita na kuzungumzia hatima yake kisiasa, hasa walipojibu maswali ya wananchi kuhusu sakata lake kuvuliwa uongozi kwa tuhuma za usaliti, na hatimaye Zitto kwenda mahakamani kuzuia chama kujadili uanachama wake.

Katika kesi ya msingi, Zitto aliyewahi kuwa maarufu akiwa kiongozi wa CHADEMA, anaomba arudishiwe nyadhifa zake zote, na apatiwe nakala za uamuzi wa Kamati Kuu (CC) ili aweze kukata rufaa Baraza Kuu.
CHANZO NI TANZANIA DAIMA

WHO YAONYA KUHUSU WIMBI LA SARATANI

999_928f6.jpg
Uraibu wa pombe na sigara husababisha saratani
Shirika la Afya duniani WHO limeonya kuhusu kuibuka kwa wimbi baya la maambukizi ya ugonjwa hatari wa saratani kote duniani.
Shirika hilo limesema nusu ya ugonnjwa wa Saratani yanaweza kuzuiwa na kwamba juhudi mpya zinastahili kufanyika ili kukabiliana na tatizo la kunenepa kupita kiasi, ulevi na uvutaji sigara.
Watu milioni kumi na nne wanajulishwa kuwa wanaugua saratani kila mwaka, lakini idadi hiyo inatarajiwa kuongezeka na kufikia milioni ishirini na nne katika kipindi cha miongo miwili ijayo.
Taasisi ya utafiti wa kimataifa kuhusu ugonjwa wa Saratani katika shirika la WHO lilionya kuwa gharama ya matimabu inaongezeka kwa kiwango ambacho ni vigumu kumudu.
Taasisi hiyo imesema serikali zinahitajika kutekeleza sheria kali zaidi kuhusu matumizi ya pombe na sukari kama vile kuongeza bei na marufuku ya matangazo ya kibiashara ya bidhaa hizo.
CHANZO:BBC

NINI HATMA YA KESI YA KENYATTA ICC? 

KESNYATA_185c0.jpg
Pande zinazohusika katika kesi inayomkabili Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta kwenye mahakama ya kimataifa ya ICC Mjini The Hague zimekuwa na kikao cha kujadili mstakabali wa kesi hiyo.
Kiongozi wa mashtaka wa ICC Fatou Bensouda amekiri kuwa bado hana ushahidi wa kutosha kuwezesha kesi hiyo kuendelea.
Mawakili wanaomwakilisha Rais Kenyatta wanataka kesi hiyo kuhusiana na ghasia za baada ya uchaguzi wa Kenya mwaka 2007 itupiliwe mbali.
Bensouda amesema kuwa bado kuna maswala yanayozua utata na ambayo yanahitaji uchunguzi wa kina. Viongozi wa mashitaka wanasema kuwa mashahidi wengi wamehongwa au kutishwa kiasi cha kujiondoa katika kesi hiyo.
Viongozi wa mashitaka ICC wanasema kuwa Kenyatta aliongoza ghasia hizo lakini kesi dhidi yake imefanywa dhaifu kutokana na baadhi ya mashahidi kujiondoa katika kesi hiyo.
Mawakili wa Kenyatta wanatuhumu upande wa mashitaka kwa kusisitiza kutaka taarifa kuhusu akaunti ya benki ya Rais Kenyatta kuona ikiwa kuna pesa zozote zilizotolewa kwa lengo la kutumika wakati wa ghasia za baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007/08
Wakili wa waathiriwa wa ghasia za baada ya uchaguzi amesisitizia mahakama kuwa kutupiliwa mbali kwa kesi kutawakosesha waathiriwa haki. Mahakama inatarajiwa kutoa uamuzi katika siku chache zijazo.
Rais Kenyatta alifikishwa ICC kutokana na tuhuma kuwa alikuwa mmoja wa washukiwa wakuu wa ghasia za baada ya uchaguzi mkuu nchini Kenya mwaka 2007/2008. Anakabiliwa na makosa ya mauaji na uhalifu mwingine dhidi ya binadamu.
Kadhalika Kenyatta alishitakiwa pamoja na makamu wake William Ruto kwa tuhuma sawa. Kesi dhidi ya Ruto inaendelea katika mahakama hiyo.
Watu 1,200 walipoteza maisha yao katika ghasia za uchaguzi mkuu mwaka 2007/08 huku maelfu wakilazimika kutoroka makwao. Wote wamekanusha mashitaka.
Kesi yenyewe ilitarajiwa kuanza Jumatano, lakini ikaahirishwa kwa mara ya nne mwezi jana wakati ambapo wendesha mashitaka waliposema kuwa shahidi mwingine alijiondoa kwenye kesi huku wakiomba mahakama kuwapa muda zaidi kutafuta ushahidi. CHANZO BBC SWAHILI

MLEMAVU AFAIDI MKONO WA KIELECTONIKI

mkono_18778.jpg
Mfumo wa mkono wa kieletroniki
Mlemavu mmoja kutoka Denmark Dennis Aabo amekuwa binadamu wa kwanza kupewa mkono wa kieletroniki wenye hisia kama ule wa binadamu.
Italia
Katika tukio linalopigiwa upatu kuimarisha hali ya walemavu katika siku za usoni, madaktari huko Italia wameuunganisha mkono huo wa kielektroniki na neva za mabaki ya mkono wa Dennis uliokatwa baada ya ajali mbaya ya fataki na hivyo kumwezesha kuhisi kupitia kwa vidole vya mkono huo wa kielektroniki .
mkono2_de0a9.jpg
Silvestro Micera aliyeongoza upasuaji huo alifurahishwa mno na uwezo wa mgonjwa wake kuutumia mkono huo bandia .
'' tumeshangazwa sana na urahisi wa mgonjwa wetu kuwasiliana mara moja na mkono huu bandia wa kielektroniki kuekelea majukumu ya kushika na kuhisi vitu tofauti .
Hata ikiwa upasuaji huu utakuwa wa muda tu, ninahakika Denis ameotambua mwenyewe kuwa utakuwa wenye manufaa makubwa kwake katika siku za usoni''
Dennis hakuficha furaha yake alisema mkono huo umebadilisha kabisa hali yake.
''hisia zangu za mkono zimeimarika maradufu maanake ninawezajua ugumu na mfumo wa kitu chochote ni kama mkono wa kawaida''

KOMBE LA DUNIA MWAKA 2014, CHANGAMOTO, FURSA KWA BIDHAA

Na Shaffih Dauda
Mwaka 2014 umetawaliwa na tukio kubwa zaidi la kimichezo nalo ni kombe la dunia. Ni wakati wa makampuni yenye misuli mikubwa na hata washirika na wadhamini kujipanga kwa ajili ya kwenda sawa na kipyenga kitakachopulizwa rasmi jijini Sao Paulo nchini Brazil. Chapa kama Adidas, Coca-Cola, Visa, Continental na McDonald zimewekeza paundi bilioni 5.5, kwa ajili tu ya kushiriki kupata haki ya kufanya biashara kwenye michuano hiyo, inayoandaliwa kila baada ya miaka minne na shirikisho la mpira wa miguu duniani FIFA.
Ni wakati wa kujiuliza sasa ni zipi changamoto na fursa zitakazozikumba chapa hizi nchini Brazil? Kombe la dunia ni nafasi kwa bidhaa mpya pia washirika wa kibiashara kupata nafasi ya kuwasiliana na asilimia 50 ya watu wote duniani, kwani mashabiki zaidi ya bilioni 4 watawasha televisheni zao kuangalia michuano hiyo, pia ulimwengu wa digitali pamoja na mitandao ya kijamii, hivyo ni nafasi kwa bidhaa kupata umaarufu ingawa kutakuwa na ushindani kwenye kupata nafasi. Nani atawika? Hilo ni swali muhimu sana kwetu.
Brazil ni nchi ambayo itatawaliwa na rangi za kila aina kutoka kila kona ya dunia, pamoja na ushabiki uliotukuka wa mchezo wa soka nchini humo, na ni muda pia wa bidhaa kufikia malengo ya kibiashara kwa kuwa huo ni muda wa thamani.
Adidas kwenye ubora wametumia njia zote kukabiliana na wapinzani wao NIKE, ambayo ni bidhaa maarufu katika bara la Amerika kusini. Mnamo mwezi Disemba Adidas walizindua mpira maalum utakaotumika kwenye kombe la dunia uliopewa jina la BRAZUCA, ambapo kampuni hiyo kubwa kwa kuzalisha vifaa vya michezo yenye makazi yake nchini Ujerumani, ilifanya utafiti kwa kuwahoji wakazi zaidi ya milioni moja nchini Brazil, ili kufahamu namna walivyoupokea huo mpira, lakini pia kampuni hiyo ya Adidas iligawa mpira mmoja mmoja kwa kila mtoto aliyezaliwa ile siku ya uzinduzi. mmmhh mambo hayo! Wananchi wa Brazil ni moja ya wateja lakini kwa upande mwingine watatumika kama njia ya kutangaza bidhaa, na makampuni mengi yanategemea kufaidika na michuano hiyo kwa kuitumia kama ngazi kwa kuwa karibu na wananchi kupitia mitandao ya kijamii pia na biashara za kutembeza mitaani. Mitandao ya kijamii ni njia nzuri na bora kwa mashabiki kufuatilia michezo kwa kubadilishana uzoefu kupitia Twitter, Facebook and YouTube. Coca-Cola kama wadhamini wa michuano ya kombe la dunia, wameshaanza kutumia nafasi ya kufanyika kipindi cha kiangazi kwa kutumia ziara ya kombe la dunia wakijihusisha na mashabiki moja kwa moja kwenye mitandao ya kijamii kama Instagram jambo ambalo linamvuto kwa mashabiki wa soka.
Pamoja na kufanya mitandao ya kijamii ni vyema kwa mameneja bidhaa kutumia fursa kama ilivyokuwa kwa (Super Bowl 2013 ) na Adidas (2012 kwenye michuano ya Olympic ) kufanikisha kuwatumia walaji kama mabalozi kupitia idadi zao kwenye mitandao ya kijamii.. Walaji watakuwa na uwezo wa kuangalia video kwa mahitaji ya Brazil, na kutokana na mazingira kumetoa fursa kwa technolojia kuweza kumsaidia mlaji kupata fursa ya kushuhudia matukio . Wadhamini wengine wa Kombe la dunia la FIFA 2014 ni kampuni ya VISA, wameikuza technolojia yao ya digitali kwa walaji kupitia bidhaa yao ‘Go World’ inayofanana na ile ya kampeni ya michuano ya Olympic 2012.
VISA ni maarufu kwenye mtandao wa YouTube, kwa maudhui maalum ya video zinazoonyesha maisha halisi ya watu, pia mashindano ya mbio kuendana na matakwa ya walaji. Sasa katika hili itasaidia sana kujenga imani ya watu juu ya VISA. Moja ya changamoto kwa bidhaa ni wananchi kukosa imani na bidhaa husika kutokana na umaarufu wao, kwenye kujikita katika tasnia ya michezo. Changamoto ya kombe la dunia la Fifa 2014 kwa washirika wa kibiashara, ni kutafuta nafasi ya kujikita kwenye nyoyo za watu ili kupata nafasi ya kuzungumza kutakakopelekea kupata uhuru wa kujitawala kibiashara kwa muda mrefu, na bidhaa kupata fursa mpaka siku ya fainali