TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, September 30, 2014

Ukisikia Kigali Rwanda…. ndio hii! picha zaidi ya 20 za mitaa mbalimbali ziko hapa

21
Wataalamu wa mambo wanasema kwa jinsi mji wa Kigali unavyojengwa majengo ya kisasa wakati huu, miaka 10 baadae sifa itaongezeka maradufu kwenye list ya miji ya Afrika inayotolewa sana mifano ya kuigwa Afrika.
Pamoja na hayo, ni mji ambao ni msafi sana kimazingira, kuna usalama wa hali ya juu na ndio maana sio kitu kigeni kukutana na askari kwenye kila kona lakini pia vilevile sheria zinatekelezwa sana ambapo rushwa haina nafasi kabisa.
34
Usalama wa kutembea usiku pia ni mkubwa sana, niliwahi kuingia night club na kutoka saa tisa na nusu na barabarani kukawa kuna askari wa kutosha kila kona, nilipouliza kwanini kuna watu bado wanatembea kwa mguu pembeni mwa barabara ndio nikapewa stori mwanzo mwisho jinsi ulivyo mkali.
35
2
3
4
5
6
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
Kingine nilichojifunza ni kwamba sheria ni kali hata kwa watu wa bodaboda, yeyote anaweza kujuta sana pale atakapokamatwa hajavaa helment.
19
20
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
36
37

Hong Kong bado hali tete 

Raia wa Hong Kong wakivurumushiwa moshi
Makumi kwa mamia ya waandamanaji wa Hong Kong wanaendelea na maandamano yao kwa siku nyingine tena baada ya kudhoofisha maeneo muhimu ya jiji hilo wakati wa mchana. Waandamanaji hao sasa wanamtaka Mkuu wa utawala wa Hong Kong Leung Chun-Ying ajiuzulu..
Wakati huo huo Marekani imesema inafuatilia kwa karibu kinachoendelea Hong Kong na imeutaka utawala kuchukua hatua. Katika mkutano wa wanahabari msemaji wa Ikulu ya Marekani Josh Earnest amesema Marekani inaunga mkono matakwa ya watu wa Hong Kong.
"Duniani kote, na hii ni kweli katika Hong Kong na maeneo mengine, Marekani inaunga mkono kimataifa, uhuru, kama vile uhuru wa kukutana kwa amani na uhuru wa kujieleza. Marekani inautaka utawala wa Hong Kong kuchukua hatua, na kwa upande wa waandamanaji kutoa maoni yao kwa amani"BBC

WANACHUO WATEMBELEA KITUO CHA HALI YA HEWA UWANJA WA NDEGE DAR 


Wanachuo wa Chuo cha Ualimu Vikindu wakiwa katika Kituo cha Mamlaka ya Hali ya Hewa ndani ya Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar leo kujifunza kwa vitendo somo la utabiri wa hali ya hewa.

Mtaalam kutoka kituo cha utabiri wa hali ya hewa akianza kuwapa darasa wanachuo hao.

Mtaalam akiwafundisha kitu wanachuo hao kuhusu kipima upepo kinachofahamika kitaalam kama 'Cap Container Anemometor'.(P.T)

Mtaalam akiwaelekeza wanachuo hao juu ya kipima mvua kinachofahamika kitaalam kama 'Rain Gauge'.

Muonekano wa eneo la kituo la utabiri wa hali ya hewa ndani ya uwanja huo.


Wanachuo wakiondoka katika kituo hicho baada ya kupata somo.

Saturday, September 27, 2014

RATIBA YA MICHEZO YA LEO LIGI KUU NCHINI UINGEREZA


14:45 Liverpool Vs Everton
17:00 Chelsea Vs Aston Villa
17:00 Manchester United Vs West Ham United
17:00 Crystal Palace Vs Leicester City
17:00 Hull City Vs Manchester City
17:00 Southampton Vs Queens Park Rangers
17:00 Sunderland Vs Swansea City
19:30 Arsenal Vs Tottenham Hotspur
Mechi hizo zote ni kwa saa za Afrika Mashariki (P.T)

SITTA APOKEA MESEJI ZA MATUSI 

sssita_88efd.jpg
Mwenyekiti wa Bunge la Katiba, Samuel Sitta amesema anapokea meseji za simu zaidi ya 50 kwa siku za kumtukana na kusisitiza ataendelea kupambana kuhakikisha Katiba inayopendekezwa inapatikana.
Sitta alitoa kauli hiyo bungeni mjini Dodoma jana wakati akielezea kutoridhishwa kwake na kile alichodai ni namna hukumu ya kesi iliyofunguliwa na Saed Kubenea inavyopotoshwa na wanaomchukia.
"Kuna baadhi ya vyombo vya habari wananichukia mimi binafsi. Wasichanganye chuki hizo na mchakato wa Bunge Maalumu," alisema Sitta na kuongeza;
"Mimi napokea matusi kila siku. Meseji zisizopungua 50 viongozi wa Chadema wameweka namba zangu katika tovuti nitukanwe kila siku hilo mimi niko tayari na mnaniona niko safi tu wala sihangaiki nalo."
"Lakini sasa Bunge Maalumu ni chombo cha kikatiba, kiko tofauti na mwenyekiti wake. Huwezi kuliadhibu Bunge Maalumu kwa sababu hupendi sura ya mwenyekiti wake," alisema.(P.T)
Sitta alienda mbali zaidi na kusema, "Kwa hiyo wale wanaoendeleza hayo mapambano tuendelee na tutaendelea kupambana, lakini kazi ya Bunge Maalumu itaendelea na ndugu zangu Watanzania mjue tunaandaa Katiba safi na rafiki kwa wananchi na itapatikana."
Sitta alisema baada ya kutolewa kwa hukumu hiyo ya kesi ya Kubenea dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), kumekuwa na tafsiri alizosema ni potofu.
Baada ya maelezo hayo alimpa ruksa AG, Jaji Frederick Werema kutoa ufafanuzi.
Jaji Werema alisema Mahakama Kuu, katika kutafsiri kifungu cha 25(1) (2) inakiri kwamba kuna tofauti kati ya kifungu kilichoandikwa Kiswahili na kile kilichoandikwa Kiingereza.
Alisema Mahakama Kuu katika hukumu hiyo imesema mamlaka ya kuandika Katiba Mpya ina maana ni mamlaka ya kuandika na kupitisha katiba inayopendekezwa kwa ajili ya kupelekwa kwa wananchi kwa ajili ya kupigiwa kura ya maoni.
Takukuru yalitesa Bunge
Wakati hayo yakiendelea suala la kuingizwa ama kutoingizwa kwenye katiba, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), linaonekana kulitesa Bunge la Katiba baada ya kamati 10 kati ya 12 kulirejesha tena jana.
Rasimu iliyowasilishwa bungeni na Tume ya Mabadiliko ya Katiba, ililiacha suala hilo kwa maelezo kuwa siyo moja ya mambo ya Muungano na msimamo huo ukaungwa mkono na Kamati ya Uandishi ya Bunge hilo.
Chanzo:Mwananchi

USA:Kampeni ya angani yasambaratisha IS 

Jenerali Martin Dempsey Kushoto.
Mkuu wa jeshi nchini Marekani Jenerali Martin Dempsey amesema kuwa mashambulizi ya angani dhidi ya kundi la Islamic State yameliharibu kundi hilo,lakini akaonya kuwa kampeni hiyo ya angani pekee haiwezi kuliangamiza kundi hilo.
Amewaambia waandishi habari kwamba kampeni ya nchi kavu dhidi ya kundi hilo ni muhimu nchini Iraq na Syria.
Jenerali Dempsey amesema kuwa kati ya wapiganaji elfu kumi na mbili na elfu kumi na tano kutoka kwa makundi ya upinzani nchini Syria watahitajika katika vita vya nchi kavu nchini Syria.
Idadi hiyo ni mara mbili na hata tatu kwa ukubwa ukilinganisha na idadi inayotarajiwa kupewa mafunzo ya kijeshi mbali na silaha na wanajeshi wa Marekani.BBC

CHARLES BONIFACE MKWASA ‘MASTER’ AULA TFF

mkwasa_52ea7.jpg
Charles Boniface Mkwasa
Na Prince Akbar, DAR ES SALAAM
ALIYEKUWA kocha wa Yanga SC, Charles Boniface Mkwasa ameteuliwa kuwa Ofisa Mtaalamu wa Elimu ya Mafunzo wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Katibu wa TFF, Selestine Mwesigwa ameithibitishia BIN ZUBEIRY kwamba Mkwasa amepewa nafasi hiyo baada ya kurejea kutoka Uarabuni, alipokwenda kufundisha klabu.
Kwa upande wake, Mkwasa, maarufu kama Master kwa jina la utani tangu enzi zake anacheza nafasi ya kiungo Yanga SC na Taifa Stars, amesema kwamba amekwishaanza kazi yake hiyo mpya TFF na anatarajia kuifanya kwa ufanisi kwa sababu ana utaalamu nayo.(P.T)
Kuhusu Mkataba wake na Yanga SC, Mkwasa alisema kwamba wakati anakwenda Uarabuni alipewa likizo ya mwaka mmoja, lakini kwa sababu amerudi kabla ya muda huo ameona bora kukubali kazi hiyo ya TFF kuliko kukaa bure.
"Kama Yanga SC watanihitaji kurudi kazini kabla ya muda huo, ni suala la kuzungumzika tu, kwa sababu TFF ipo kwa ajili ya maendeleo ya soka hapa nchini na Yanga ni klabu ya Tanzania,"amesema mume huyo wa Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Dodoma, Betty Mkwasa, mtangazaji maarufu wa zamani wa Redio na Televisheni.
Mkwasa alijiunga na Yanga SC Desemba mwaka jana akitokea Ruvu Shooting ya Pwani, lakini baada ya msimu Mei mwaka huu akaondoka pamoja na aliyekuwa kocha Mkuu wa klabu hiyo, Mholanzi Hans va der Pluijm kwenda Uarabuni.
Hata hivyo, baada ya muda mfupi wa kufanya kazi huko, Pluijm aliyemchukua Mkwasa kwenda naye huko- akatofautiana na uongozi wa timu na kusitishiwa mikataba.
Wakati Pluijm alirejea Ghana anakoishi, Mkwasa alirudi nyumbani Tanzania na sasa anaibukia TFF..
Chanzo:bongostaz

Friday, September 26, 2014

Mchinjaji wa IS atambuliwa

Mkurugenzi wa FBI James Comey
Mkurugenzi mkuu wa FBI James Comey amesema kitengo chake kimemtambua mtu ambaye huficha sura yake ambaye ni muuaji,ambaye pia huoneshwa wakati akiwachinja mateka watatu kwenye video inayo nadi wanamgambo wa dola ya kiislam IS.
Pamoja na hayo Bwana Comey amegoma kuutaja uraia wa mtu huyo ama hata kutaja jina lake,ingawa imeshajulikana lafudhi ya mtu huyo kuwa ni mwenye asili ya mji wa London, na Comey amesema kwamba utambuzi wa mtu huyo umefanikishwa kwa msaada mkubwa wa marafiki wa kimataifa.
Muuaji huyo wa waandishi James Foley na Steven Sotloff pamoja na mfanyakazi wa kujitolea David Haines walipigwa picha ya video na kuwekwa kwenye mitandao na wanamgambo hao wa dola ya kiislam na kusaidia kufanya maamuzi juu ya mipango ya wapiganaji wa jihad.BBC