TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Thursday, January 31, 2013

JK-TUNAJUA BIASHARA YA DINI INALIPA LAKINI MSIVURUGE

Na :Patricia Kimelemeta  - Mwanachi

“Kuna baadhi ya watu wanatumia vigezo vya kidini kwa ajili ya kufanya vurugu za kuhatarisha amani, Serikali haitaweza kuwavumilia, badala yake tutatumia njia mbalimbali RAIS Jakaya Kikwete amesema kuwa mtindo wa kufanya fujo na kusababisha uvunjifu wa amani kwa visingizio vya dini nchini ni biashara inayolipa na ndiyo maana...
wakereketwa wa kufanya hivyo hawaishi.

Hata hivyo, akaonya kwamba Serikali katu haitawavumilia wanaotaka kuwavuruga Watanzania kwa kutumia dini zao.

Kikwete aliyasema hayo wakati wa kuwasilisha ripoti ya Mchakato wa Nchi za Afrika Kujitathmini zenyewe katika nyanja za Demokrasia, Utawala Bora na Uchumi (APRM) nchini Ethiopia mwishoni mwa wiki iliyopita.

Alisema ni jambo la kushangaza kuona kuwa wadau wanatumia dini kuiyumbisha nchi kwa vigezo kuwa ni miongoni mwa nchi zilizodumisha amani kwa muda mrefu.
Alisema kutokana na hali hiyo, Serikali yake haitayumba wala kusita kupambana ipasavyo na wafanya fujo hao ikiwa ni pamoja na kutumia njia za busara wakati wa kutoa uamuzi na hatua za kisheria.

“Kuna baadhi ya watu wanatumia vigezo vya kidini kwa ajili ya kufanya vurugu za kuhatarisha amani, Serikali haitaweza kuwavumilia, badala yake tutatumia njia mbalimbali ili kushughulikia matatizo hayo ikiwa ni pamoja na kutumia busara na hatua za kisheria,” alisema Kikwete.

Alisema mapendekezo yaliyotolewa na APRM ya kusimamia kwa uangalifu tofauti za kidini nchini ameyachukua kwa mikono miwili.

Alisema kitendo cha Tanzania kuwa na amani na utulivu kwa muda mrefu ni bahati iliyotokana na kutokuwapo kwa ugomvi wa kikabila, kidini ama yale ya kutokana na rangi za watu. Alisema hali hii inatokana na ukweli kuwa sera iliyopo haina ubaguzi kwa wananchi kwa misingi ya kabila, dini, rangi ama sehemu anakotoka Mtanzania, ni sera nzuri na wanaidumisha.

Kwa mujibu wa Kikwete, uzuri kuhusu dini katika Tanzania ni kwamba kila mmoja ana uhuru wa kuabudu na kwamba Serikali haina dini.

“Tunajua fika kuhusu hatari zinazoweza kusababishwa na baadhi ya wanasiasa na viongozi wa dini wenye malengo ya kuchochea fujo za kidini, hatuwezi kuyumba wala kusita kupambana ipasavyo na watu wa namna hiyo,” alibainisha.

Alisema ikiwa wataona uchochezi wa kidini unafikia kiwango cha kuhatarisha amani ya nchi ama uvunjifu wa amani na sheria na dola itachukua mkondo wake ili haki iweze kutendeka.

Wednesday, January 30, 2013

MAPOKEZI YA BALOTEL AC MILLAN
Welcome to Milan! Mario Balotelli was greeted by hundreds of AC Ultras as he went for dinner
Fireworks: AC Milan striker Mario Balotelli is mobbed by fans outside Giannino Restaurant





Shake on it: The Italian striker was greeted by Milan vice president Adriano Galliani upon his arrival
‘I started this season with City not very well and I hope to change the situation here. I felt inside me that one day I would have come.
‘I took important decisions and I hope they will be lucky for me and for Milan.’
He will have a medical at Milan and is expected to be officially unveiled later this week.

DR.MIGIRO NI MKUU MPYA WA CHUO KIKUU HURIA
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Dkt. Asha Rose Migiro kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.
Taarifa iliyotolewa Dare Es Salaam na kutiwa saini leo, Jumatano, Januari 30, 2013 na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Y. Sefue imesema kuwa uteuzi huo ulianza Alhamisi ya Januari 17, mwaka huu wa 2013.
Mheshimiwa Asha Rose Migiro ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na Katibu wa NEC wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Aidha, Dkt. Migiro amepata kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN) na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Tanzania. 
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
IKULU
DAR ES SALAAM
30 Januari, 2013

KIWANDA CHA CHEMI COTEX CHATEKETEA KWA MOTO
Kiwanda cha ChemiCotex kilichopo huko Africana njia ya Tegeta jijini Dar es Salaam kinawaka moto muda huu, saa kumi na mbili jioni.

Wafanyakazi wa kiwanda hicho wakiwa nje ya jengo wakati moto ulipotokea na kuteketeza kiwanda hiccho , hata hivyo chanzo cha kutokea moto huo bado hakijajulikana.
 
LULU: SITAKI SHEREHE YA KUPONGEZWA BAADYA YA  KUTOKA MAHABUSU
Elizabeth Maiko "Lulu"

Marehemu Steven Kanumba

Na Mwandishi Wetu

STAA wa muvi aliyeachiwa huru kwa dhamana kufuatia madai ya kumuua bila kukusudia, aliyekuwa mcheza filamu mahiri wa Bongo, Steven Kanumba, Elizabeth Michael ‘Lulu’ anasemekana amegomea sherehe za kumpongeza kwa kutoka mahabusu, Risasi Mchanganyiko limekusanya data.
Lulu aliachiwa huru kwa dhamana juzi Jumatatu baada ya kusota kwenye Gereza la Segerea, Dar es Salaam kwa miezi 10 kwa kesi hiyo  ambayo imekuwa gumzo.
Kwa mujibu wa habari za kindugu, Lulu aligomea sherehe hiyo baada ya kusikia minong’ono ya kuwepo kwake kutoka kwa baadhi ya ndugu kwamba, akitoka watamuangushia bonge la pati.
Akijibu swali la paparazi wetu kuhusu sherehe hiyo, ndugu mmoja wa staa huyo (jina lipo) ambaye alikuwepo mahakamani hapo, alimkariri Lulu kwa kusema:
“Alisema sitaki sherehe kwa vile bado nina kazi kubwa mbele yangu, namwomba Mungu anisaidie katika safari ndefu ya kesi hii.”
Baada ya kumalizana na ndugu huyo, paparazi wetu alimfuata mama wa Lulu, Lucresia Karugila ambaye alikuwa katika hekaheka za kukamilisha taratibu za dhamana na kumuuliza kuhusu kuwepo kwa sherehe hiyo.
Hata hivyo, mama huyo alijibu kwa mkato: “Sina cha kuongea na nyinyi kwa sasa.”
KUTEMBELEA KABURI LA MAREHEMU KANUMBA
Wakati huohuo, habari zilizotufikia wakati tunakwenda mitamboni zinadai kwamba Lulu baada ya kuachiwa kwa dhamana ni kwenda kuzuru kaburi la marehemu Kanumba.
Inadaiwa kuwa, hilo litafanyika kwa sababu za kibinadamu zaidi kwa kuwa, marehemu na Lulu walikuwa watu waliofahamiana kikazi achilia mbali kuwepo kwa uhusiano wa kimapenzi kati yao.
Licha ya dhamana kuwa wazi, Lulu alirejeshwa gerezani mpaka jana ambapo taratibu za dhamana zilipokamilika.
MANJI ALIA NA UGUMU WA KUENDESHA TIMU
Na Khadija Mngwai
MWENYEKITI wa Yanga, Yusuf Manji (pichani), ameibuka na kusema anakumbana na ugumu mkubwa katika kuiendesha klabu hiyo tangu alipopata nafasi ya kuwa mwenyekiti, Julai mwaka jana.
 Manji amesema anakutana na changamoto nyingi likiwemo suala la ukata.
Manji ambaye anawania nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi Kuu Bara katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika Februari 24, mwaka huu, amesema klabu hiyo ina mambo mengi ya kimaendeleo inayotakiwa kufanya lakini tatizo kubwa ni ukata.
“Kwa kweli nimeona matatizo mengi yanayozikabili klabu zetu hapa nchini, hasa suala la ukata, kwani tangu nimeingia kuwa mwenyekiti ndiyo nimeona hali jinsi ilivyo na kuona ugumu unaozipata klabu zetu hapa nchini, awali nilikuwa sijui suala hilo.
“Klabu zinakumbana na ukata mkali, hasa zikiwa zinajiandaa na ligi, ndiyo maana nimeamua kuwania nafasi hii ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi, kwani klabu hazina fedha, hali inakuwa ngumu na kusababisha timu kutokuwa na viwango,” alisema Manji.
BALOTELI AAFIKI MIAKA MINNE AC MILAN
AC Milan wameafiki dili la kumsajili straika wa Manchester City, Mario Balotelli kwa mkataba wa miaka minne na nusu, mkurugenzi wa klabu hiyo ya Italia, Umberto Gandini, amethibitisha.

Straika wa zamani wa Inter Milan, Balotelli (22) atafanyiwa vipimo vya afya mjini Milan Jumatano kabla ya kusaini mkataba wake.

Ada ya awali ya uhamisho inaaminika kuwa ni paundi milioni 19 ambayo inasemekana imeshalipwa na huenda ikaongezeka kufikia paundi milioni 22.

Tuesday, January 29, 2013

LULU KUCHEZA FILAMU MPYA ILIYOANDALIWA NA JACK WOLPER






























MSANII wa filamu Tanzania Jackline Wolper ameandaa filamu mpya atakayoshirikiana na  msanii maarufu Elizabeth Michael 'Lulu' itakayokamilika hivi karibuni baada ya msanii huyo kutoka gerezani kwa dhamana

Akizungumza na Maisha Wolpa alisema amepata faraja baada ya taaratibu na sheria kufuatwa na hatimaye Lulu kuweza kupata dhamana hivyo anatarajia kufanya naye kazi ya filamu mpya itakayoanza kurekodiwa baada ya msanii huyo kufika uraiani

Alisema kuwa anatarajia atafanya vizuri katika filamu hiyo kwani tangu awali alikuwa akifanya vizuri katika tasnia hiyo ya uwigizaji kabla ya kupatwa na matatizo

"Nimeshampokea Lulu tangu moyoni mwangu kwani kule alikokuwepo si sehemu nzuri na ukiangalia bado ni mtoto mdogo hivyo inaumiza sana" alisema Wolper

Filamu hiyo ndiyo itakayokuwa ya kwanza kuchezwa na Lulu baada ya kufika Uraiani

Wakati huo huo Rose Ndauka alisema ni wakati wa wasanii kumpokea mwenzao kwani wote ni familia moja na wanahitaji kushirikiana katika kila hali

Alisema kuwa ukiangalia umri wa msanii huyo ni mdogo hivyo ananafasi kubwa bado ya kutengeneza maisha yake na kuangalia wapi amekosea na wapi anapaswa kurekebisha

Naye msanii Single Mtambalike 'Richie Richie' alisema anashukuru kuona sheria imechukua mkondo wake na hatimaye sasa ameweza kuachiwa kwa dhamana hivyo kwa upande wao ni faraja kubwa kwani wote ni familia moja

Alisema anaamini sasa ataweza kujipanga na kufanya kazi vizuri kwani anakipaji na bado wanamuhitaji watanzania kulingana na uwezo mkubwa alionao kwenye tasnia hiyo

LULU ATOKA MAHABUSU KWA DHAMANA BAADA YA KUSOTA KWA MUDA MREFU
Lulu akilia wakati akitoka Mahakamani huku nyumba akifuatiwa na mama yake mzazi.
Wasanii nao wallijitokeza mahakamani hapo kumfariji Lulu, kulia ni msanii wa filamu, Muhsin Awadh 'Dk. Cheni'
 






















Baada ya jana kushindikana kwa sababu zisizo zuilika hatimaye msanii maarufu Elizbeth 'Lulu' Michael ametoka kwa dhamana baada ya kutimiza masharti yote ya dhamana yake yaliyo tolewa na mahakama kuu.

Mara baada yakutoka Lulu alieyeonekana akiwa mwenye majonizi na furaha kiasi aliomba watanzania wote wamuombee maana hii ni dhamana tu na kesi yake bado inaendela. Ali washukuru watu wote waliokuwa pamoja nae katika mkasa huuu  amabao bado unamzunguka na pia alimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuwa pamoja nae katika kipindi chote cha matatizo yanayo mkablia.

Wakili wake Ndugu Flugence Massawe amesema kwamba hii ni hatua ya kwanza kwasababu case bado inaendelea. Kwa sasa wanasubiri mahakama itoe tarehe ya Lulu kurudi mahakamani.

MAAJABU NA KWELI : MAITI YA KICHANGA YAGEUKA KUWA JOGOO MWANAYAMALA HOSPITALI

BADO tupo mwanzoni mwa mwaka lakini tukio la maiti ya kichanga kugeuka jogoo ndani ya chumba cha kuhifadhia maiti kwenye Hospitali ya Mwananyamala, jijini Dar es Salaam linaweza kuongoza mengine yote ya ajabu yanayoweza kujiri ndani ya 2013.

Mwananyama ni hospitali yenye hadhi ya mkoa kitabibu, ina rekodi za kuwa na matukio ya ajabu, ila hili siyo tu kwamba linaingia miongoni mwa hayo bali pia linaweza kutia fora.
Asubuhi ya Jumatano iliyopita, ilikuwa kizaazaa pale jokofu lililotumika kuhifadhi maiti ya kichanga cha mtoto, kukutwa kuna jogoo.


Mshangao zaidi ni kwamba ndani ya lile jokofu, pembeni ya yule jogoo, kulikuwa na hirizi pamoja na tunguri.


Habari kutoka vyanzo vyetu, zimewekwa wazi kuwa Jumanne iliyopita, saa 7 mchana, polisi walipigiwa simu, wakataarifiwa kuhusu maiti ya mtoto iliyokuwa imetelekezwa eneo la Kigogo, Mbuyuni, Dar es Salaam.


Vyanzo vyetu vimebainisha kuwa polisi baada ya kupata taarifa hizo walifika eneo la tukio na kukuta maiti hiyo ya kichanga ikiwa imefunikwa kwa kuzungushiwa sanda.



Kwa mujibu wa Moses Madilu, mkazi wa Kigogo, aliyedai kushuhudia tukio hilo, polisi walipofika eneo la tukio waliikagua maiti hiyo na kubaini kwamba ni ya kike.


Chanzo chetu kikaeleza kuwa baadhi ya mashuhuda, hususan wanawake, walitokwa na machozi kwa masikitiko kwamba itakuwa mtu alijifungua halafu akakinyonga kichanga hicho kabla ya kukitelekeza eneo hilo.


“Baada ya kujiridhisha kwa kazi yao, polisi waliichukua maiti hiyo ya kichanga, wakaipakia kwenye ‘difenda’, wakaipeleka Hospitali ya Mwananyamala,” kilieleza chanzo chetu.


HOSPITALI YA MWANANYAMALA
Ndani ya hospitali hiyo, mwandishi wetu alielezwa kuwa polisi walipofika, walishusha maiti hiyo na kumkabidhi mganga wa zamu aliyejulikana kwa jina moja la Dk. Liwa.

 “Dk. Liwa aliwaambia wale polisi wapeleke maiti hiyo mochwari.

“Polisi walifanya hivyo lakini kule mochwari walimkuta msimamizi mkuu, Omar Buyoya aliyekataa kuipokea kwa vile daktari hakuthibitisha kama kile kichanga kilikufa au kilikuwa hai.


“Polisi na Buyoya walivutana kwa muda mrefu, alitokea mhudumu mwingine wa mochwari aliyekuwa akijuana na polisi mmoja aliyebeba ile maiti, alikubali kuupokea mwili huo na kuingiza ndani kwenye jokofu la kuhifadhia maiti.”


Muuguzi huyo aliendelea kusema kuwa siku iliyofuata, Dk. Liwa alifika mochwari na alipofungua jokofu na kufunua sanda, badala ya kukuta maiti ya kichanga, alikuta jogoo, tunguri na hirizi.


“Dk.Liwa alipatwa  na mshangao mkubwa huku jasho likimtoka kutokana na uoga, aliwaita wafanyakazi ambao walijazana hapo  mochwari kushuhudia.


“Baadhi ya wafanyakazi walipigwa na butwaa huku wengine wakicheka hadi kudondoka chini na wakawa wanajiuliza kama kweli polisi wanaweza kupeleka jogoo hospitali au ni mambo ya kishirikina,” alisema muuguzi huyo.


Dk. Liwa na wafanyakazi wenzake waliondoka mochwari na kuacha hilo jogoo katika chumba cha maiti huku wakishindwa la kufanya.


KAULI YA MGANGA MKUU.....

Uwazi  ilimtafuta Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mwananyamala, Dk. Sophinias Ngonyani ambaye alikiri  kuonekana kwa jogoo badala ya maiti ya kichanga.

“Polisi walituletea kifurushi wakiamini kuwa ni maiti ya kitoto kichanga ambapo tulikipokea lakini ilipotazamwa na daktari, tulikuta jogoo, hirizi na tunguri, tuliamua kumchoma moto kwa sababu kile ni chumba cha kuhifadhi maiti siyo cha kuhifadhia mizoga ya kuku, ng’ombe au mbwa,” alisema Dk. Ngonyani.


KAULI YA POLISI ...
Naye Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, ACP Charles Kenyela alipoulizwa juu ya sakata hilo alisema kwamba wao kama jeshi la polisi walipigiwa simu na raia mwema kuwa  kuna maiti ya kichanga ambapo askari waliondoka hadi eneo la tukio na kuichukua mpaka Hospitali ya Mwananyamala.


“Polisi waliichukua hadi Hospitali ya Mwananyamala kwa wataalamu na baada ya kuikabidhi waliondoka na kuendelea na shughuli nyingine, nami nashangaa kusikia kwamba madaktari walikuta  jogoo,” alisema Kenyela.


MASWALI MATANO
Je, ni kweli polisi waliikagua maiti na kugundua ni kichanga cha kike?


Kama ndiyo, ilikuwaje kikageuka jogoo?


Kwa nini daktari hakuipima ile maiti, badala yake akaelekeza ipelekwe mochwari?


Je, au polisi walibeba mzoga wa jogoo, wakampakia kwenye difenda wakidhani ni maiti ya kichanga?


Mkweli nani, polisi wanaodai kupeleka maiti ya kichanga, au hospitali wanaosema walipelekewa mzoga wa kuku, tunguri na hirizi?


SOURCE: GPL
BUNGE LAUNDA KAMATI MAALUMU LA KWENDA MTWARA
























Spika wa Bunge bi Anne Makinda amesema Bunge limeunda Kamati Maalumu kwenda mkoani Mtwara kutafuta suluhu kuhusu suala la nishati ya gesi, iliyopatikana mkoani humo.

Spika Makinda ameyasema hayo wakati akiahirisha kikao cha Bunge kilichoanza leo Mkoani Dodoma.

Spika amesema matokeo ya Kamati hiyo Maalumu yatawasilishwa kujadiliwa Bungeni.

Iddi Maalim wa TBC anaripoti katika taarifa iliyosomwa saa saba mchana ifuatavyo:
Bunge sasa linaunda Kamati ambayo itakwenda Mtwara, kuwasikiliza Wananchi halafu ndani ya kikao hiki –mkutano huu unaofanyika– Kamati ya Bunge itakuwa imekwenda Mtwara, itawasikiliza Wananchi, italeta masuala ambayo yanazungumzwa kule Mtwara kisha yatajadiliwa.

Hili alikuwa analizungumza baada ya kusema kuwa amepokea vikaratasi na maombi mengi kwamba Bunge lijadili suala la Mtwara, gesi kama suala ambalo ni la dharura.

Lakini akasema kwamba, ile hoja si ya dharura na akaeleza pia ukweli kwamba Wabunge ambao wanasema lijadiliwe kama suala la dharura wengi wao hawalifahamu kwa undani, kwa hiyo badala ya kujadili jambo ambalo hawalifahamu kwa undani, ni afadhali ataunda kamati ambayo itakwenda Mtwara ikirudi itakuja na majibu, na mapendekezo ya Wananchi na ndipo Bunge litajadili ndani ya Mkutano huu wa kumi.
CHADEMA WAMALIZA KIKAO CHA BARAZA KUU
VIONGOZI WAKUU WA CHADEMA

WAFUASI WA CHADEMA


Monday, January 28, 2013

TASWA YAANZA MCHAKATO WA TUZO ZA MWANAMICHEZO BORA WA MWAKA

CHAMA cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), kimeanza mchakato wa Tuzo kwa Wanamichezo Bora wa Tanzania mwaka 2012.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wa TASWA, Amir Mhando, Kamati ya Utendaji ya TASWA imeamua kama ilivyokuwa mwaka uliopita kwamba suala la mchakato wa kuwapata wanamichezo hao lifanywe na kamati maalum nje ya Kamati ya Utendaji ya TASWA lengo ikiwa ni kupanua wigo na kuwashirikisha wadau wengi zaidi katika jambo hili nyeti.

Jukumu la Kamati ya Utendaji ya TASWA itakuwa ni kuhangaika na mambo ya wadhamini na masuala mengine yahusuyo sherehe hizo ambazo tunataka ziwe za aina yake.

Kutokana na hali hiyo Kamati ya Utendaji ya TASWA iliyokutana wiki iliyopita iliteua kamati maalum ya watu 11 kusimamia mchakato wa kuwapata wanamichezo hao, ambapo kamati hiyo inayotarajia kuanza vikao vyake Jumatano Januari 30, 2013 itakuwa chini ya uenyekiti wa mwanachama wa TASWA, Haji Manara.
"Kamati ya Utendaji imemkabidhi jukumu Manara baada ya kujiridhisha pasi na shaka uzoefu wake katika masuala ya michezo na pia uzoefu wake katika mambo mbalimbali ya kiutawala, hivyo kuwa na imani kwamba ataendesha vizuri mchakato kama walivyofanya watangulizi wake," ilisema taarifa hiyo.

Wajumbe saba wa kamati hiyo wanatoka nje ya Kamati ya Utendaji ya TASWA ambao ni Jane John, Dina Ismail, Jabir Idrissa, Tullo Chambo, Abdallah Mweri na ofisa mmoja ambaye ataombwa kutoka Baraza la Michezo la Taifa (BMT), wakati wajumbe wanne wanatoka Kamati ya Utendaji ya TASWA ambao ni Grace Hoka, Zena Chande, Alfred Lucas na Amir Mhando.

DROGBA KWENYE MIKONO YA GALATASARAY
Taarifa hii nimeipokea kwamba club ya soka ya Galatasaray imekubali dili la kumsaini mchezaji Didier Drogba kwa miezi la 18 hivyo kumchukua kutoka kwenye club yake ya Shanghai Shenhua.
Mchezaji huyu ambae aliondoka Chelsea last summer imeelezwa kwamba atasaini hilo dili baada ya kumalizika kwa mechi za Ivory coast kwenye AFCON ambapo game yao ijayo inachezwa jumapili ijayo.
Kusaini kwa Drogba na Galatasaray itakua dili kubwa la pili la club hiyo huku la kwanza likiwa ni kumchukua mchezaji Wesley Sneijder kupitia dirisha la usajili wiki iliyopita.
LULU AMEACHIWA HURU KWA DHAMANA
Habari zilizotufikia hivi punde zinadai kuwa Mahakama kuu ya Tanzania imemwachia kwa dhamana msanii wa filamu nchini Tanzania, Elizabeth Michael aka Lulu aliyekuwa mahabusu katika gereza la Segerea jijini Dar es Salaam.

Lulu alifikishwa mahakamani akituhumiwa kumuua msanii mwenzake, Steven Kanumba, ambaye hata hivyo baadaye alibadilishiwa kesi na kushitakiwa kwa kuua bila kukusudia.

Msanii huyo ameachiwa huku akipewa masharti ya kuacha Hati ya Kusafiria Mahakamani, kuripoti Mahakamani kila tarehe mosi, pamoja na wadhamini wawili waliotoa milioni 20 mmoja.

Kwa wiki kadhaa sasa, baadhi ya watu wamekuwa wakisikika wakiomba dua njema kwa msanii huyo ili aweze kuachiwa kwa dhamana na kufuatilia kesi yake akiwa nje na familia yake.

Lulu aliwasilisha mahakamani hapo maombi ya dhamana, kupitia kwa jopo la mawakili wake, linaloongozwa na Wakili Kennedy Fungamtama, Peter Kibatala, Fulgence Masawe wa Kituo cha Msaada wa Sheria na Haki za Binadamu (LHRC).


Awali, maombi hayo ya dhamana yaliwasilishwa mahakamani hapo kwa hati ya dharura na kusikilizwa na jaji Zainabu Muruke.

Mara baada ya tukio la mauaji ya Kanumba kutokea, kesi ya msanii huyo ilifunguliwa katika Mahakama ya Kisutu ili kukamilisha hatua za awali, hasa masuala yote ya kisheria, upelelezi na kushtakiwa kwa mauaji ya kuua bila kukusudia kwa kupitia Kifungi cha 196.

Kesi ya Lulu yenye namba 125, jalada lake lilifungwa na kuhamishiwa Mahakama Kuu kwa kuwa ndiyo yenye uwezo wa kusikiliza kesi za mauaji.

Mara baada ya kufika mahakamani hapa leo asubuhi, dalili njema za kuachiwa kwa msanii zilianza kujitokeza hasa baada ya dhamana yake kuwa wazi, ikiwa ni kutokana na hoja zilizokuwa zinajadiliwa mahakamani hapo.

Katika mitandao ya kijamii, ikiwamo facebook, baadhi ya watu walionekana wakipost habari na picha mbalimbali za msanii huyo zikionyesha dhahiri kumuombea mema ili atoke na kuendelea na maisha yake wakati kesi hiyo inaendelea.

Lulu ni miongoni mwa wasanii wa kike wenye mvuto mkubwa katika jamii, huku uwezo wake na umahiri wake wa uigizaji ukiacha watu midomo wazi.

Umaarufu wa Lulu ulitokea tangu mdogo akiigiza katika kundi la Kaole Sanaa Group, akicheza kama mt0to hadi kufikia kuwa msichana na mwenye mvuto miongoni mwa mabinti wa filamu Tanzania.

Bila shaka habari za kuachiwa kwa dhamana kwa msanii huyo zitakuwa njema kwa siku ya leo kwa mashabiki na wadau wote wa filamu Tanzania.
UGOMVI WA VIONGOZI WASABABISHA KANISA KUFUNGWA

Katika hali isiyo ya kawaida jeshi la polisi mkoa wa Ilala jijini Dar es salaam limelazimika kupiga kambi katika eneo lililopo kanisa la Morovian Tanzania jimbo la mashariki usharika wa Tabata, kutokana na uwepo wa mgogoro wa uongozi wa kanisa hilo jambo lililowafanya waamini wa kanisa hilo kushindwa kufanya ibada kama ilivyo ada baada ya upande mmoja wa uongozi kufunga milango ya Kanisa hilo na kuondoka na funguo.

Sunday, January 27, 2013

WAZIRI MKUU MSTAAFU EDUWARD LOWASA ANUSURIKA KUFA KATIKA AJALI

 Gari la  Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli na Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje Ulinzi na Usalama Edward Lowassa likiwa limebonyea kwa ubavuni baada ya kupata ajali iliyotokea jana asubuhi.
-- 
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli na Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje Ulinzi na Usalama Edward Lowassa Mh. Edward Lowassa amenusurika kifo,baada ya gari lake alilokuwa akisafiria kupata ajali eneo la Bwawani mkoani Morogoro.

Gari hilo la Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli na Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje Ulinzi na Usalama Edward Lowassa liligongwa na basi la Morobest, wakati basi hilo lilipolipita basi jingine kwenye daraja na kukutana uso kwa uso na gari lakini dereva wa  Mh. Lowasa kwa ustadi mkubwa alilikwepesha gari lisigonge upande alipokuwa amekaa  mzee na kuligonga ubavuni nyuma kwa upande wa dereva na hakuna aliyejeruhiwa.

Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli na Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje Ulinzi na Usalama Edward Lowassa na msafara wake aliendelea na safari hadi morogoro ambako ameshiriki katika harambee ya ujenzi wa kanisa la KKKT Kilakala ambapo yeye na Marafiki Zake Wamechangia Shilingi Milioni 18

VURUGU ZILIZOTOKEA MTWARA KATIKA MGOGORO WA GESI  MHE. PINDA AZUNGUMZA NA WANANCHI 
Moja ya nyumba ikiteketea wakati wa vurugu mkoani Mtwara ambapo magari 18, pikipiki 7 viliteketezwa kwa moto  vyote vikiwa ni mali za halmashauri ya Masasi na baadhi ni vya watumishi wa halmashauri hiyo.
Gari la wagonjwa likiteketea kwa moto.

Sehemu ya magari yakiendelea kuteketea kwa moto.
Jengo la Mahakama lililochomwa moto.
Nyumba inayosemekani ni nyumba ya waziri ikiwa imeharibiwa vibaya.
 
Nyumba inayosemekana ni ya Mwenyekiti wa CCM baada ya kuharibiwa.

Baadhi ya Viongozi wa Vyama vya siasa  na viongozi wa ASAs mbalimbali wakionyosha mikono kuomba idhini ya kuchangia  katika mkutano kati yao na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kuusu mgogoro wa gesi kwenye ukumbi wa VETA mjini Mtwara Januari 27, 2013. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Thursday, January 24, 2013

 HAFLA YA WALEMAVU ILIYOANDALIWA NA MWENYEKITI WA MAKAMPUNI YA IPP MEDIA DK. MENGI

Wageni waalikwa waliohudhuria hafla hiyo


Wanahabari wakiwa kazini
Wanahabari wakiwa bize na kuchukua matukio wakati Waziri Mkuu Mizengopita Pamoja na Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP MEDIA walipokuwa wakiingia ukumbini.
Steve na Francisca
Mahafudha,Jackson na Avity wakiwa wamepozi
 

Mwanamziki nguli wa kizazi kipya Profesa J
 
IPP MEDIA TEAM
Aisha na Fatma
 

DJ wetu wa siku hiyo toka EASTV RADIO
 

 

Mama Dayana Kinduli
Hawa walikuwa MC waetu siku hiyo Gondwe, Zembela