TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, April 29, 2015

Machafuko Burundi, bajeti ya TZ 2015/2016 .. Uzinduzi wa Meli za Kivita TZ..

Power ButtonNimekusogezea hizi story mtu wangu ni zile zilizopewa Headlines kwenye Magazeti ya leo April 29, Power Breakfast @CloudsFM ikafanya uchambuzi..
Wananchi wa Burundi wameonekana wakiwa wamekusanyika katika mpaka wa Tanzania kutokana na machafuko yanayoendelea kwao, Waziri wa fedha Saada Mkuya leo atawasilisha mwelekeo wa bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2015/2016, Mbunge James Mbatia ameitaka Serikali kutoa tamko kutokana na kuporomoka kwa shilingi.
Nyingine iliyosikika ni Rais Kikwete kuzindua meli mbili za kivita zitakazotumika kufanya doria Baharini, Rais mstaafu wa Marekani Bill Clinton amewasili nchini kwa mazungumzo na Rais Kikwete, Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila ametunukiwa Tuzo ya kutambua harakati zake za kutetea haki za binadamu na kuna stori yya Jeshi la Polisi kulaumiwa kwa kuwahudumia watu wenye fedha kuliko wenye kipato cha chini.
Kulikuwa na mazungumzo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Shaaban Mwinjaka ambae amezungumzia makubaliano waliyoyafanya baada ya kukutana na SUMATRA pamoja na wamiliki wa mabasi kuhusu bei mpya ya nauli iliyotangazwa.

Kingine kikubwa kwenye HEADLINES ni hii stori ya uzinduzi wa Meli kubwa 2 za kivita DAR.

16
Kutoka Dar es Salaam leo April 28  2015 kingine ambacho kimechukua nafasi kubwa kwenye HEADLINES ni hii stori ya uzinduzi wa Meli kubwa mbili za Kivita ambazo zimezinduliwa na Rais Kikwete
Meli zimekabidhiwa kwa Kikosi cha Jeshi la Maji TZ Kigamboni.. Hapa unaweza kuona pichaz kutoka kwenye uzinduzi wa Meli hizo.
15
16
15
255

Meli hizi zitakuwa zikitumiwa kwenye patrol katika eneo la Bahari.
Picha zote kutoka:  issamichuzi.blogspot.com na tanzaniangovernment.blogspot.com.

Shambulio la kigaidi Nigeria, hili limehusisha kituo cha Redio

Bomb-scare
Nigeria ni moja ya nchi ambazo zimeripotiwa kuwa na mashambulizi mengi yanayohusiana na ugaidi.. bado kuna ripoti za mashambulizi mara kwa mara, bado pia kuna ishu ya wasichana 270 abao walikamatwa na kundi la Boko Haram, mwaka mmoja umepita na bado hakuna dalili za wasichana hao kupatikana.
Leo kuna hii inayohusu watu wanne ambao wameuawa na wengine kujeruhiwa baada ya kituo cha Redio cha TA’O FM kilichopo eneo la Okene Jimbo a Kogi kulipuliwa kwa bomu jana usiku.
Bado haijafahamika sababu za kulipuliwa kwa kituo hicho na hakuna kikundi chochote cha kigaidi ambacho kimedai kuhusika na shambulio hilo mpaka sasa huku Polisi wakiendelea na uchunguzi.
Waliofariki kwenye tukio hilo ni jamaa wanne ambao walikuwa walinzi wa Kituo hicho.

Idadi ya vifo iliyoripotiwa mpaka sasa kutokana na tetemeko la ardhi Nepal… #RIP

hemaa 
Stori ambayo kwa sasa imechukua headlines kwa wingi ni ile ya tetemeko la ardhi lililotokea Nepal na kuua idadi kubwa ya watu karibu na milima ya Everest.
Idadi ya watu ambao wamethibitishwa kufariki kutokana na tetemeko hilo lililotokea siku ya jumamosi iliyopita imeongezea na mpaka sasa ni watu zaidi ya 4,500 waliofariki.
Serikali ya nchi  hiyo imesema  zaidi ya watu 10,000 wamejeruhiwa.. Hali hiyo imewaelea na Serikali imehitaji msaada kutoka mataifa mengine.
nepal
police
Waziri Mkuu wa NepalSushil Koirala amesema mahitaji ya dharura yanayohitajika yakiwa ya mahema , chakula pamoja na maji.

Hayajasahaulika ya New York, Ferguson.. Marekani bado kuna headlines za machafuko kutokana na ishu ya Ubaguzi.

A police vehicle burns, Monday, April 27, 2015, during unrest following the funeral of Freddie Gray in Baltimore. Gray died from spinal injuries about a week after he was arrested and transported in a Baltimore Police Department van. (AP Photo/Patrick Semansky)
Machafuko mengine Marekani, waandamanaji wameingia mtaani.. wamepora vitu madukani, majengo yamechomwa moto.. bado kisa hiki kinahusishwa na ishu ya ubaguzi wa rangi kwa upande mwingine.
Kijana Freddie Gray alifariki akiwa mikononi mwa Polisi, vurugu zikaanza muda mfupi baada ya kufanyika mazishi yake.
Kifo cha Gray ambaye ni Mmarekani mweusi alifariki siku chache baada ya kulazwa Hospitali akipatiwa matibabu ya majeraha aliyopata kwenye uti wa mgongo baada ya baada ya kupigwa na Polisi.
Watu waliingia mtaani kufanya maandamano ya kupinga kitendo kilichofanywa na Polisi, baadae hali ikabadilika, majengo yakaanza kuchomwa moto na watu wengine wakaanza kuvamia maduka na kufanya uporaji.
BALTIMORE, MD - APRIL 27:  Demonstrators climb on a destroyed Baltimore Police car in the street near the corner of Pennsylvania and North avenues during violent protests following the funeral of Freddie Gray April 27, 2015 in Baltimore, Maryland. Gray, 25, who was arrested for possessing a switch blade knife April 12 outside the Gilmor Homes housing project on Baltimore's west side. According to his attorney, Gray died a week later in the hospital from a severe spinal cord injury he received while in police custody.  (Photo by Chip Somodevilla/Getty Images) ORG XMIT: 551557375
Waandamanaji hao walikuwa wakirusha mawe kuyashambulia magari ya Polisi, majengo pamoja na kufanya uharibifu mwingine huku maofisa wa Polisi 15 kujeruhiwa.
A Baltimore Metropolitan Police transport vehicle burns during clashes in Baltimore, Maryland April 27, 2015. Maryland Governor Larry Hogan declared a state of emergency and activated the National Guard to address the violence in Baltimore, his office said on Monday. Several Baltimore police officers were injured on Monday in violent clashes with young people after the funeral of a black man, Freddie Gray, who died in police custody, and local law enforcement warned of a threat by gangs. REUTERS/Shannon Stapleton - RTX1AK33
Watu 27 wamekamatwa kwa kuhusika na matukio ya uporaji katika maduka ya pombe, dawa na maduka ya kubadilishia fedha  pamoja na  kuwashambulia maafisa wa Polisi.
A man throws a brick at police Monday, April 27, 2015, following the funeral of Freddie Gray in Baltimore. (AP Photo/Patrick Semansky) ORG XMIT: MDPS130
Mmoja wa waandamanaji akirusha jiwe kwa askari.
Kifo cha Gray kilitokea April 19, hii iishu ni moja ya ambazo zimewahi kusikika zikihusishwa na suala la Polisi wa Marekani kuwaua Wamarekani weusi.. iliwahi kutokea pia Jiji la Ferguson na New York.
Kwa sasa shughuli nyingi Baltimore zimesimama, shule zimefungwa huku vikosi vya zimamoto vikiendelea na jitihada kuzima moto pamoja na Polisi kuwatawanya waandamanaji.
BALTIMORE, MD - APRIL 27:  Two cars burn in the middle of an intersection at New Shiloh Baptist Church on April 27, 2015 in Baltimore, Maryland. Riots have erupted in Baltimore following the funeral service for Freddie Gray, who died last week while in Baltimore Police custody.  (Photo by Andrew Burton/Getty Images)
27 Apr 2015, Baltimore, Maryland, USA --- April 27, 2015 - Baltimore, MD, USA - Baltimore firefighters battle a three-alarm fire at Gay and Chester Streets on Monday, April 27, 2015, in Baltimore. It was unclear whether it was related to ongoing riots. (Credit Image: © Jerry Jackson/TNS/ZUMA Wire) --- Image by © Jerry Jackson/ZUMA Press/Corbis
Firefighters battle a blaze, Monday, April 27, 2015, after rioters plunged part of Baltimore into chaos, torching a pharmacy, setting police cars ablaze and throwing bricks at officers. (AP Photo/Evan Vucci) ORG XMIT: MDEV101
A man walks past a burning police vehicle, Monday, April 27, 2015, during unrest following the funeral of Freddie Gray in Baltimore. Gray died from spinal injuries about a week after he was arrested and transported in a Baltimore Police Department van. (AP Photo/Patrick Semansky)
maxresdefault

Pacquiao atua Las Vegas na familia yake

basi 
Ukitaja majina ya mastaa hawa Manny Pacquiao na Floyd Mayweather, kila mtu anashauku ya pambano la jumamosi ambalo linasubiriwa kwa hamu na mashabiki mbalimbali duniani.
pa2
Pambano hilo ambalo linatajwa kuwa na kifahari zaidi huku viingilio vikitajwa kuwa vya gharama sana litafanyika jijini Las Vegas na litawashirikisha mabondia hao maarufu duniani.
paaa
Tayari maandalizi kwa pande zote mbili yamekamilika na kila mmoja anajiandaa kwa mara ya mwisho kabla ya kukutana ulingoni.
pa3

Kulikuwa na mpango wa shambulio la kigaidi Jengo la Bunge Kenya?? Mfanyakazi mmoja wa Bunge katajwa

Parliament_Buildings,_Nairobi,_Kenya_-entrance-15April2010
Kuna stori mpya kila siku kuhusu ishu ya ugaidi.. Kenya ni nchi ambayo imetajwa sana kukumbwa na mashambulizi ya kigaidi, kingine kilichoripotiwa ni kuhusu mmoja ya wafanyakazi wa Bunge kutajwa kushirikiana na Kundi la Al Shabaab kupanga kufanya mashambulizi katika Jengo la Bunge la nchi hiyo.
Ali Abdul Majid amekamatwa baada ya kupatikana kwa taarifa kwamba Al Shabaab wana mpango wa kushambulia baadhi ya maeneo ikiwemo Jengo la Bunge la Senate Nairobi.
Katika taarifa hiyo Al Shabaab walipanga kushirikiana na mmoja wa wafanyakazi katika Bunge hilo ambae anasali katika Msikiti wa Pumwani Riyadh, baada ya taarifa hizo Polisi walimkamata kwa ajili ya upelelezi.

PICHA 4 za mwonekano wa Uwanja mpya wa Klabu ya AC Milan ukikamilika..

milan2
Klabu nyingi zinazochezea Ligi Kuu Ulaya, au Klabu zenye majina makubwa Duniani ni ajabu kukuta Klabu haina Uwanja wake wa nyumbani wa michezo.. Man United wana wao wa Old Trafford, Chelsea wako pale darajani Stamford Bridge.
Klabu ya AC Milan kwa sasa wanautumia San Siro Stadium kama uwanja wao wa nyumbani.. lakini good news kuhusu wao leo ni kwamba Klabu hiyo ipo katika harakati za kujenga uwanja wake mpya ambao utajengwa kisasa zaidi eneo la Portello, Jiji la Milan, Italy.
milan
Mwonekano wa Uwanja kwa juu
Uwezo wa Uwanja huu ni kuchukua mashabiki 48,000 tu kwa wakati mmoja, upo katikati ya majengo makubwa ikiwemo hoteli kadhaa pamoja na maduka ya huduma mbalimbali ambayo yamezunguka uwanja huo.
milan3 
Unaambiwa teknolojia imehusika sana hapa.. jinsi ambavyo utajengwa utawekewa soundproof ambazo zitazuia kwa kiasi kikubwa kelele za ndani ya Uwanja zisitoke nje na kukera watu wengine.
Milan Pitch
Mwonekano wa Uwanja kwa nje

Friday, April 24, 2015

Uchaguzi wa walimu nusura uvunjike 

Rais wa Chama cha Walimu Tanzania Gratian Mukoba.
Rais wa Chama cha Walimu Tanzania Gratian Mukoba.
UCHAGUZI wa Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) mkoa wa Simiyu uliofanyika jana, nusura uvunjike baada ya baadhi ya wagombea, kuanza kutuhumiana ndani ya ukumbi wakati wakijieleza kwa wajumbe.
Mmoja wa wagombea hao ambaye alikuwa akigombea nafasi ya Uwakilishi wa Kamati Tendaji Taifa, Chananja Buluba alipopewa nafasi ya kujieleza, alidai kuwa uchaguzi huo umegubikwa na vitendo vya rushwa.
Alidai kuna baadhi ya wajumbe walipewa Sh 50,000 hadi Sh 100,000 kutoka kwa wagombea wa nafasi za Uwakilishi wa Kamati Tendaji Taifa, Mwenyekiti na Mweka Hazina.
Akiwa anazomewa na baadhi ya wajumbe hao, mgombea huyo alieleza kuwa mbali na kupewa fedha, baadhi ya wajumbe walilipiwa sehemu za kulala kwa siku tatu pamoja na chakula.
Hali hiyo ilionekana kuwakera wajumbe wa uchaguzi huo na kumtaka athibitishe mbele yao na kuwataja watu ambao walipewa pesa, kulipiwa sehemu za kulala pamoja na chakula.
Akiwa tayari kutaka kuwataja wahusika wa vitendo hivyo, mgombea huyo alizuiliwa na Mratibu wa Uchaguzi huo ambaye ni Katibu wa CWT mkoani hapa, Fatuma Bakari kwa madai kuwa alikuwa amekiuka taratibu za uchaguzi.
Kitendo cha kuzuiliwa na katibu huyo, kilionekana kumkera mgombea huyo na kuacha kujieleza mbele za wajumbe hao, ambapo aliamua kuwaita waandishi wa habari nje ya ukumbi wa mkutano ili kuwaeleza hali hiyo.
" Nimechukia sana kitendo cha Mratibu ambaye ni Katibu CWT Mkoa kunizuia...hali ya uchaguzi huu imechafuliwa sana na rushwa, wagombea wamegawa pesa kama karanga na sijui wametoa wapi wakati wao ni walimu kama mimi," alisema Buluba.
Alibainisha kuwa pesa walizokuwa wakizitoa wagombea hao, zilikuwa na ufadhili kutoka katika vyama vikubwa vya siasa, alivyovitaja.
Alisisitiza kuwa hakuna mwalimu ambaye anaweza kumpatia mwalimu mwenzake, kiwango hicho kikubwa cha pesa. " Nina muda mrefu katika taaluma hii ya walimu...hizi pesa ni nyingi, wajumbe wote walipewa pesa hasa nafasi hizo za juu...watu wanalipiwa sehemu za kulala, chakula bure kwa siku tatu...tuligundua kuna ufadhili mkubwa wa vyama," alisema.
Hata hivyo, licha ya baadhi ya wajumbe kupewa kiasi hicho, alibainisha kuwepo kwa baadhi ya wagombea waliojitoa kugombea nafasi mbalimbali baada ya kupewa Sh 500,000. Buluba aliitaka Takukuru kuchunguza hali hiyo, kabla hajachukua maamuzi mengine, huku akitishia kuachana na chama hicho na kuanzisha chama kingine mbadala wa CWT.
" Najipanga kuanzisha mbadala wa CWT kwa sababu chama hiki ni rushwa kila sehemu kila mara.. CWT ya sasa imeshindwa kuwatetea walimu na badala yake kimegeuka kuwa chama cha kisiasa," alisema.
Katibu wa chama hicho ambaye ndiye alikuwa Mratibu wa uchaguzi huo, Fatuma Bakari alikiri kupata taarifa za kuwepo kwa vitendo hivyo, huku akidai kuwa hakuna mtu ambaye ametajwa kufanya vitendo hivyo.
" Taarifa hata sisi tumepewa kuwepo kwa vitendo hivyo, ndiyo maana kwenye uchaguzi nimemzuia mgombea huyo kuwataja wahusika kwa sababu kanuni za uchaguzi zinakataza, lakini ningeliruhusu kikao kilikuwa kinavunjika kutokana na hali niliyoiona," alisema Bakari.
Uchaguzi huo ulifanyika na Dwese Kulwa alichaguliwa kuwa Mwenyekiti kwa kura 52. Mweka Hazina ni Joyce Nkomangwa aliyepata kura 45 na Mwakilishi wa Kamati Tendaji Taifa ni Julius Mategemeo, aliyepata kura 50.CHANZO:HABARI LEO (Muro)

Ligi ya England timu 20 kushuka dimbani 


Timu ya Chelsea

Kocha wa Liverpool,Brendan Rodgers
Jumla ya timu 20 zinazoshiriki ligi ya England zinatarajiwa kushuka dimbani mwishoni mwa wiki.
Hata hivyo mechi ya Chelsea na Arsenal ,inaoonekana kuwa na mvuto zaidi kwa wengi, kufuatia matokeo ya mechi hiyo kutoa picha mbili tofauti, moja kuihakikishia Chealse ubingwa iwapo itashinda mechi hiyo,na pia Arsenal ikishinda italeta mazingira ya wazi kwa timu yoyote kati ya timu hizo mbili kutwaa ubingwa.
Kocha wa Liverpool,Brendan RodgersNaye kocha Liverpool Brendan Rodgers ameibuka na kutamba kuwa yeye ni kocha bora na hakuna kama yeye, huku akisema anamatumaini ya kuendelea kukinoa kikosi.
Pamoja na majigambo hayo Rodgers ameweka rekodi mpya ndani ya klabu hiyo kwa kuongoza misimu mitatu bila kuchukua taji lolote, tofauti na watangulizi wake tangu mwaka 1950.CHANZO:BBC (Muro)

Wahamiaji:Muungano wa Ulaya wapingwa 

Waandamanaji wakipinga vifo vya wahamiaji wanaovuka bahari ya shamu kwenda Ulaya
Makundi ya kupigania haki za kibinadamu yamesema kuwa mikakati ilioafikiwa na muungano wa ulaya kuzuia idadi kubwa ya wahamiaji wanaojaribu kuvuka hadi Ulaya kutoka Afrika sio ufumbuzi wa tatizo hilo.
Katika kikao cha dharura kilichofanyika mjini Brussels siku ya alhamisi, Viongozi wa Ulaya walikubaliana kuongeza msaada wao mara tatu ili kuimarisha usakaji na uokozi wa wahamiaji katika bahari ya shamu.
Pia waliidhinisha mikakati ya kukamata na kuharibu vyombo vinavyotumiwa kuwasafirisha wahamiaji hao.
Lakini Shirika la Human Rights Watch pamoja na lile la kuwasaidia watoto la Save the Children, yanasema kuwa EU inafaa kuongeza juhudi zake katika uokoaji badala ya kullinda mipaka yake.
Mkutano huo uliitishwa baada ya zaidi ya watu 800 kuuawa wikendi iliopita baada ya boti yao kuzama.CHANZO:BBC (Muro)

Chanjo ya Malaria,nafuu kwa Watoto


Mamilioni ya Watoto wachanga wamepoteza maisha kutokana na ugonjwa wa Malaria
Hatua za mwisho za majaribio za chanjo dhidi ya Malaria, ya kwanza kufikia hatua hii inaleta matumaini kuwa itawalinda mamilioni ya Watoto dhidi ya Malaria.
Lakini Majaribio kwa watoto 16,000 kutoka nchi saba za Afrika yameonyesha kuwa kuna mipaka katika matumizi ya dawa hizo na chanjo haifanyi kazi kwa watoto wachanga.
Baada ya Watoto kufikia umri wa miezi 5-17 walipewa dozi tatu za chanjo, Kinga ilifanya kazi mwilini kwa kiasi cha 45%.
Lakini wataalam wanasema hatua ya kuifikisha chanjo katika hatua hiyo ni kupiga hatua kubwa.
Data zilizochapishwa katika jarida moja la maswala ya kitabibu zinaonyesha mafanikio ya chanjo hiyo ni madogo mno kwa vichanga.
Wanasayansi wamekuwa wakifanyia kazi chanjo hiyo kwa zaidi ya miaka 20, lakini wachunguzi wa mambo wanaona kuwa bado kazi kubwa inahitajika.
RTS,S/AS01 ni Chanjo ya kwanza ya Malaria kufikia hatua za juu za majaribio.
kwa sasa hakuna chanjo yoyote dhidi ya Malaria iliyopatiwa kibali duniani.
Chanjo hizi zilitolewa katika nchi 11 ikiwemo Tanzania,Kenya,Burkina Faso, Gabon,Ghana,Malawi na Msumbiji.CHANZO:BBC (Muro)

SHEREHE YA UKUZAJI WA KISWAHILI YAENDELEA WASHINGTON, DC 


Rais wa CHAUKIDU Prof Lioba Moshi watatu toka kushoto akimkaribisha Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi mara tu alipowasili kama mgeni rasmi chuo kikuu cha Howard Washington, DC siku ya Alhamisi April 23, 2015 kulia ni Prof Venessa White Jackson.

Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi akimtambulisha mkewe mama Sitti Mwinyi kwa mwenyeji wao Prof Lioba Moshi pia na yeye akimtambulisha mama Sitti Mwinyi kwa Prof Venessa White Jackson kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Liberata Mulamula .

Prof Lioba Moshi Rais CHAUKIDU akielezea historia fupi ya CHAUKIDU na baadae kumkaribisha Rais mstaafu kuongea na wadau wa Kiswahili waliohudhuria sherehe ya chama hicho iliyofanyika siku ya Alhamisi April 23, 2015 katika chuo kikuu cha Howard kilichopo Washington, DC.

Ms Mamburi Lyambaya (kushoto) akimtambulisha Prof Venessa White Jackon na yeye kuwasalimia wadau wa Kiswahili waliohudhuria sherehe ya CHAUKIDU iliyofanyika katika chuo kikuu cha Howard Washington, DC.

Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi akiwa meza kuu kulia ni prof Venessa White Jackson '

Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi akitoa hotuba kwa kuwashukuru CHAUKIDU kwa kummpa mwaliko na kwa kuwa yeye ni mdau mkubwa wa lugha ya Kiswahili hakusita kukubali kuja kujumuika nao pia Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi aliwapongeza kwa kuitangaza lugha ya Kiswahili nchini Marekani.

Kutoka kushoto ni Balozi wa Umoja wa Afrika Mhe. Amina Salum Ali, Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Liberata Mulamula na mama Sitti Mwinyi wakifuatilia hotuba ya Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi.

Wanafunzi wa chuo kikuu cha Howard wakiimba nyimbo za Kiswahili kwa ustadi mkubwa kuliko wastajabisha Watanzania na wadau wengine wa Kiswahili.

Wadau wa Kiswahili wakifuatilia sherehe ya CHAUKIDU.(Muro)

NAPE AMSHUKIA DR. WILBOARD SLAA 


KATIBU wa NEC Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye
KATIBU wa NEC Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye,amekanusha taarifa zilizopo kuwa chama hicho kinakisaidia Chama cha ACT Wazalendo akidai kuwa hawana sababu ya kufanya hivyo.
Taarifa kwa vyombo vya habari kutoka kwa Nape zinasisitiza kuwa CCM hakina sababu ya kusaidia chama kingine cha siasa hivyo uvumi huo ni uchafuzi wa kisiasa.
Akizungumzia kauli ya Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema, Dk Wilbroad Slaa,kwamba Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeanza kuandikisha Daftari la Kudumu la Wapiga Kura katika ngome ya CCM alisema huo ni upotoshaji uliokubuhu kwani tanzania nzima ni ngome ya chama hicho.
Alisema ratiba ya NEC haijapangwa kimkakati kama alivyodai Dk Slaa na kila mtanzania ataandikishwa kwa mujibu wa sheria hivyo kauli za kuwapotosha na kuwapa hofu wananchi hazina mashiko.
"Kauli hizi za Dk Slaa mzee kama yule ni uthibitisho tosha kwamba wenzetu vyama vya upinzani hasa chadema siasa zao zina lengo la kuwagawa watu kikanda,kanda wanayoiona ni kaskazini, uthibitisho wa mbegu mbaya ya chuki," alisema Nape.
Alisema CC
M wanalaani vikali siasa za namna hiyo kwani hizo sio hoja za msingi ila ni za kuwagawa wananchi na kupandikiza chuki zisizokuwa na maana na suala hilo linaonyesha jinsi wapinzani wanavyofanya siasa za kikanda.
"Tunayo taarifa kwamba Dk Slaa,Mwenyekiti wa Chadema,Freeman Mbowe pamoja na Mwenyekiti wa Nccr-Mageuzi,James Mbatia walikaa vikao wakawatenga wenzao wanaunda Umoja wa Katiba Mpya (Ukawa, ambao ni Mwenyekiti wa CUF,Profesa Ibrahim Lipumba ambaye anatokea Tabora na DK Emmanuel Makaidi ambaye anatoka Kusini, hao wote tunajua wanatoka mikoa gani,"alisema Nape
Nape alisema siasa za namna hii zinazigawa nchi na kinachoonekana ni kwamba wapinzani wanajua kuwa watashindwa na ccm ndio maana wanatafta sababu,hivyo anawatoa hofu wananchi kuwa kila mtu mwenye sifaa ataandikishwa.
"Chadema wanajua watawaangusha vibaya, hatuna mpango wa kutumia mizengwe watanzania watatuchagua, waache kuwagawa watanzania kwa kutaka madaraka, wanatakiwa kuwashawishi wananchi kujiandikisha kama CCM tunavyofanya"alisema Nape
"Wanapandikiza mbegu mbaya na chuki yenye lengo la kugawa watanzania,nchi hii ni moja ina makabila 136 na tunaishi vizuri hizi siasa chafu hazifai,, maneno ya hovyo ambayo hayastahili kusemwa na mtu mzima kama yule, watashindwa ndio maana wanasema watu wanaandikishwa kiujanja ujanja, wameanza kujenga mbinu za ajabu, wananchi wanatupenda na watazidi kutuchagua,"alisema Nape
Alivitaka vyama vya siasa kuwahamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha na waliache zoezi hilo liende kama lilivyopangwalilivyopangwa, wasiwajengee watu hofu, hii sio sawa.(Muro)

JK AONGOZA MAZISHI YA KITENGA MKOANI MOROGORO 


Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Kikwete (pichani kati) na Waziri Mkuu Mh.Mizengo Pinda (pichani shoto) wakishuhudia askari wa jeshi la Wananchi (JWTZ) wakipiga risasi hewani kama sehemu ya heshima ya kumuaga aliyekuwa mkuu wa wilaya mpya ya Kyerwa mkoani Kagera leo,Marehemu Luteni Kanali Benedict Kitenga (mstaafu) huko kwenye makaburi ya Mlima Kola Kigurunyembe mkoani Morogoro. PICHA NA IKULU.(Muro)

WAKANDARASI WAASWA KULINDA AFYA ZA WAFANYAKAZI 


Mkuu wa kitengo cha sheria wa Wakala wa usalama na afya mahali pa kazi(OSHA),Joyce Mwalubungu, akizungumza na wakandalasi waliohudhuria kwenye warsha iliyoandaliwa na Wakala wa Usalama na Afya mahala pa kazi (OSHA) iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo.

Mshauri mkuu wa ufundi wa ujasiliamali na miradi kwa vijana Jelous Chirove akizungumza na wakandarasi waliohudhuria kwenye warsha iliyoandaliwa na wakala wa Usalama na Afya mahala pa kazi (OSHA) iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo.

Mkaguzi mkuu wa Wakala wa Usalama na Afya mahala pa kazi (OSHA) akizungumza na baadhi ya wandishi wa habari katika ukumbi wa mikutano katika jengo la Kazi House jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya wakandarasi waliohudhuria kwenye warsha iliyoandaliwa na wakala wa Usalama na Afya mahala pa kazi (OSHA) iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo.(Picha zote na Avila Kakingo,Globu ya Jamii)
Na Avila Kakingo
MAKANDARASI wametakiwa kuwajibika kwa kuwahudumia wafanyakazi wao wakiwa sehemu ya kazi kwa kulinda afya na usalama wakiwa kazini.
Hayo yamesemwa na Mkaguzi Mkuu wa Wakala wa Usalama na afya Mahala Pakazi (OSHA),Akwilina Kayumba wakati wa Warsha ya Wakandarasi
iliyoandaliwa na Wakala wa Usalama na Afya sehemu ya kazi uliofanyika leo katika Ukumbi wa Shirika la Kazi Duniani, jijini Dar es salaam.
Warsha kwa hiyo imelenga kuwajengea uwezo wa Makandarasi katika kuelekea kuadhimisha siku ya usalama na Afya Mahala Pakazi Duniani ya afya Duniani itakayofanyika Aprili 28 mkoani Dodoma.
Amesema sekta ya ujenzi ina wafanyakazi wengi hivyo inatakiwa kuangaliwa kwa ukaribu katika kuepuka ajali ambazo zinaweza kutokea wakiwa kazini pamoja na magonjwa.
Kayumba amesema katika maadhimisho ya siku ya Usalama na Afya Mahala Pakazi Duniani,Wakala usalama na afya Mahala Pakazi kwa maadhimisho hayo itakuwa siku ya maombolezo,majeruhi,magonjwa na vifo vya wafanyakazi mahala pakazi.
Amesema kauali mbiu ya maadhimisho ya siku usalama na Afya Mahala Pakazi Duniani mwaka huu ikiwa na kauli mbiu 'Tushirikiane sote kudumisha usalama na afya sehemu ya kazi'.(Muro)

Kiongera kurejea uwanjani

Kiongera
Na Bertha Lumala, Dar es Salaam-shaffihdauda.com
'Simba ililazimika kuusitisha kwa muda mkataba wa Kiongera baada ya Mkenya huyo kutonesha majerahab yake ya muda mrefu ya goti na kulazimika kupelekwa India kufanyiwa upasuaji.'
Kiungo mshambuliaji wa KCB, Paul Mungai Kiongera, yuko mbioni kurejea uwanjani baada ya kuwa nje kwa muda mrefu kutokana na upasuaji wa goti aliofanyiwa mwishoni mwa mwaka 2014.
Kiongera ambaye yuko kwa mkopo KCB akitokea Simba SC ya Tanzania, bado hayuko fiti kuichezea timu hiyo ya benki msimu huu kwa kuwa bado anaendelea kutibu goti lake lililopasuliwa India mwaka jana.(P.T)
Kocha wa KCB, Elvis Ayany, ameweka wazi alipohojiwa na mtandao wa futaa.comwa Kenya leo kwamba mchezaji huyo wa kimataifa kutoka Kenya kwa sasa anafanya mazoezi mepesi na timu na huenda akarejea uwanjani katika muda wiki chache zijazo.
"Kwa sasa yuko fiti kimazoezi, amekuwa akifanya mazoezi na wachezaji wengine wa kikosi chetu, ninaamini katika wiki chache zijazo anaweza kurejea uwanjani, ni mcheza mzuri na sote tunajua ubora wake, kurejea kwake kutakuwa msaada mkubwa kwa timu ukizingatia tunaelekea kumalizika mzunguko wa kwanza wa ligi," amesema.
Timu hiyo ya benki imeyumba msimu huu wa Ligi Kuu ya Kenya; imeshinda mechi moja tu katika mechi nane za KPL.

Mikakati kupambana na wahamiaji haramu

Viongozi wa Umoja wa Ulaya wamekubaliana kuongeza zaidi fungu la fedha katika operesheni kudhibiti wahamiaji haramu, barani Ulaya.
Fedha hizo zitasaidia kusaka na kuokoa wahamiaji haramu katika bahari ya Mediterranean katika kudhibiti wimbi la wahamiaji hao wanaotaka kuingia Ulaya kutokea Afrika kaskazini.
Baada ya mazungumzo ya dharura mjini Brussels Ubelgiji viongozi hao pia wameidhinisha njia za kukamata na kuteketeza meli zinazoonekana kutumika katika biashara hiyo ya binadamu.
Nchi kadhaa za Ulaya zimeahidi kutoa meli, helikopta na nguvu kazi nyingine.
Kwa upande wake Rais wa Baraza la Ulaya Donald Tusk amesema ushirikiano mzuri unahitajika na nchi wahamiaji hao wanakotoka.BBC

Tuesday, April 21, 2015

Ethiopia yaanza siku 3 za maombolezi 

Islamic State wakienda kuwaua raia wa Ethiopia.
Ethiopia imeanza siku tatu za maombolezi ya kitaifa kwa heshima za raia wake waliouawa na wanamgambo wa kundi la Islamic State nchini Libya.
Bendera zitapepea nusu mlingoti wakati nalo bunge la nchi hiyo likikutana kujadili hatua ambazo litachukua kufuatia mauaji hayo ya raia wake zaidi ya ishirini.
Msemaji wa serikali Redwan Hussein, alisema kuwa waathiriwa hao wanaaminika kuwa wahamiaji waliojaribu kusafiri kwenda barani ulaya.
Mungano wa Afrika ambao una makao yake makuu nchini Ethiopia ulilaani mauaji hayo na kusema kuwa utafanya mikakati ya kuhakikisha kuwepo usalama nchini Libya.
Wanamgambo wa Islamic State walitoa kanda ya video ambayo inakisiwa kuonyesha mauaji hayo yanayoonyesha watu hao wakipigwa risasi na kukatwa vichwa.CHANZO:BBC(V.S)

Mwanafunzi darasa la nne ajinyonga chumbani 

MWANAFUNZI wa darasa la nne katika Shule ya Msingi Pugu jijini Dar es Salaam, Festo Filbert (11) amekutwa chumbani kwake akiwa amejinyonga hadi kufa kwa kutumia mkanda wa kuvalia nguo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Ilala, Mary Nzuki alisema tukio hilo lilitokea jana katika eneo la Majohe kwa Ngozoma.
Alisema sababu za kujinyonga mwanafunzi huyo bado hazijafahamika kwani hakuacha ujumbe wowote.
"Mtoto huyu alikutwa chumbani kwake anakolala akiwa peke yake, hakuna aliyejua sababu za kifo chake," alisema.
Alisema maiti ya mwanafunzi huyo, imehifadhiwa Hospitali ya Amana na polisi wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.CHANZO:MTANZANIA (Muro)

Majimbo yapasua kichwa wana-Ukawa

Mwenyekiti wa Ukawa, Profesa Ibrahim Lipumba.
Mwenyekiti wa Ukawa, Profesa Ibrahim Libumba.
HATIMA ya kuachiana kwa majimbo ya uchaguzi kwa vyama vya siasa vya upinzani vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), inatarajiwa kujulikana wiki ijayo.
Itajulikana baada ya mkutano baina vyama washirika, uliolenga kutaka kufikiwa kwa mwafaka wa ugawanaji wa majimbo katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu.
Hayo yamethibitishwa na mmoja wa viongozi wa Ukawa, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba.
Vyama vingine vinavyounda umoja huo ni Chadema inayoongozwa na Freeman Mbowe, NCCRMageuzi ya James Mbatia na NLD ya Dk Emmanuel Makaidi.
Alikuwa akizungumza na gazeti hili juzi mjini hapa juu ya mchakato wa makubaliano ya majimbo, ambayo baadhi yamezua mvutano ndani ya Ukawa. Kwa Lipumba, suala hilo limepangwa kumalizwa Aprili 28, mwaka huu jijini Dar es Salaam, ambapo viongozi vinavyounda umoja huo vitatu watakutana.
Aliwataja viongozi kutoka vyama hivyo, watakaohusika katika majadiliano ya kina ni pamoja na wenyeviti wa vyama, makamu wenyeviti, makatibu na wajumbe wa sekretarieti kutoka ndani ya vyama hivyo watakuja kufikia makubaliano ya mwisho.
Ukawa ulianzishwa Februari mwaka jana wakati wa Bunge Maalumu la Katiba baada ya kushikamana katika kulipinga bunge hilo la kihistoria na baadaye kususa, kabla ya kusaini makubaliano kwa ajili ya kusimamisha mgombea mmoja katika nafasi zote kuanzia udiwani, ubunge na urais.
Hata hivyo, Lipumba alisema baada ya majadiliano ya muda mrefu ya viongozi wa Ukawa kuhusu Umoja wao, kulijitokeza mvutano wa kuachiana majimbo kadhaa, ambapo kila chama kilidai kinakubalika kwenye maeneo hayo na hivyo suala hilo kuachwa kulifanyiwa kazi kwa kina zaidi.
"Majimbo yote bado kufikiwa mwafaka wa pamoja na sasa tumepanga kukutana Aprili 28, mwaka huu Dar es Salaam kuweza kuweka wazi juu ya majimbo haya," alisema Profesa Lipumba.
Alisema kwa Jimbo la Morogoro Mjini pia bado maafikiano yanaendelea na kwamba moja ya sifa ni kuweka mgombea anayekubalika na wananchi wote.
Katika taarifa yake kwa umma hivi karibuni, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano,Tumaini Makene alisema Chadema na washirika wenzake wa UKAWA, bado wanaendelea na mazungumzo ya kusimamisha mgombea mmoja kwa nafasi za udiwani, uwakilishi, ubunge na urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mazungumzo bado yanaendelea vizuri, hayajafikia tamati na yakikamilika na makubaliano kufikiwa, viongozi wakuu wa UKAWA watatoa taarifa rasmi kwa umma wa Watanzania. CHANZO: HABARI LEO (Muro)