POLISI WASTUKIA DILI LA KUMUUA JUSTIN BIEBER
  | 
| Justin Bieber | 
  | 
| Watuhumiwa wanaoshikiliwa na polisi kwa kupanga kumuua Justin Bieber, Tanner Ruane (kushoto) na Mark Staake | 
  | 
Justin
 Bieber akiwa na mama yake Pattie Malette wakati wa tamasha la 40th la 
kila mwaka tuzo za American Music Awards kwenye Ukumbi wa Nokia Theatre 
mjini Los Angeles, California Novemba 18, 2012. 
 
WAPELELEZI wamestukia mpango wa mfungwa 
wa mauaji wa kutaka kumuua na kukata maungo nyeti ya muimbaji kijana 
Justin Bieber, mtandao wa habari wa KRQE news umeripoti.
  Kwa 
mujibu wa tovuti hiyo, Dana Martin -- ambaye hivi sasa anatumikia 
vifungo viwili vya maisha mjini New Mexico kwa kumbaka na kumuua binti 
wa umri wa miaka 15 huko Vermont miaka 12 iliyopita -- alimkodi mfungwa 
mwenzake katika gereza la Las Cruces amsaidie kufanya mfululizo wa 
mauaji, mojawapo yakiwa mauaji ya muimbaji wa "Beauty and the Beat".
  Maafisa
 wa polisi wamesema mfungwa aliyoachiwa kutoka gerezani hivi karibuni 
Mark Staake na mpwa wake Tanner Ruane walikuwa wamuue nyota huyo wa pop 
wakati wa onyesho lake ambalo limeuza tiketi zote kwenye ukumbi wa 
Madison Square Garden mjini New York City mwezi Novemba. Mpango ulikuwa 
kumnyonga nyota huyo mtoto pamoja na mabodigadi wake kwa kutumia tai, na
 kisha kuwakata maungo yao ya uzazi.
  Kabla ya tukio hilo la 
kinyama kufanywa, Staake alikamatwa mjini Vermont. Hata hivyo, Martin --
 ambaye mtandao wa KRQE umesema ni mtu "anayempenda kupindukia" Bieber 
na amejichora tattoo ya muimbaji huyo kwenye mguu wake -- aliharibu 
mpango mwenyewe na kuwasimulia polisi kila walichopanga. Wapelelezi 
baadaye walirekodi simu baina ya Martin na Ruane ambazo wawili hao 
walikuwa wakijadilia mauaji hayo.
  Ruane anashikiliwa na polisi wa New York, ambao walikuta zana zote zilizopangwa kutumika katika mauaji hayo wakati akikamatwa.
  Meneja
 wa Bieber, Scooter Braun, alizungumza na gazeti la Us Weekly kuhusu 
mpango huo wa shambulizi, akisisitiza kwamba usalama wa muimbaji huyo ni
 jambo linalopewa umuhimu wa kwanza na timu yake.
  "Tunachukua kila tahadhari kumlinda na kuhakikisha usalama wa Justin na mashabiki wake," Braun aliliambia gazeti la Us. | 
  | 
  | 
 
No comments:
Post a Comment