BODI YA CHUO CHA HABARI ZANZIBAR YAZINDULIWA
Picha ya pamoja ya wajumbe wapya wa Bodi hiyo wakiwa na Waziri wa Habari Utamaduni,Utalii na Michezo Saidi Ali Mbarouk.(Picha na Makame Mshenga)
Na: Khadija Khamis – Maelezo Zanzibar
 Waziri wa Habari Utalii Utamaduni
 na Michezo Said Ali Mbarouk amesema kuwa juhudi na utendaji kazi mzuri 
wa wajumbe wa Baraza la Chuo cha Uwandishi wa habari Zanzibar ndizo 
zitakazokipa sifa nzuri na ubora wa hali ya juu Chuo hicho.
 Ameyasema hayo jana huko katika 
ukumbi wa Chuo cha Habari Vuga mjini Zanzibar wakati akizindua Bodi mpya
 ya Baraza la Chuo hicho.
 Waziri Mbarouk amesema ubora wa 
taaluma inayopatikana Chuoni hapo inatokana na juhudi za makusudi ambazo
 zinapaswa kufanywa na Wajumbe wa Bodi hiyo mpya ambao wana wajibu wa 
kushauri na kuelekeza namna bora ya kukiendeleza Chuo.
 Amesema kushindwa kuwajibika kwa 
Bodi hiyo kutakifanya chuo kushindwa kutimiza malengo yake na kuwafanya 
wahitimu wake kuhitimu bila ya vigezo vinavyokubalika hasa katika 
kipindi hiki cha ushindani.
 “ Ili twende na wakati uliopo 
hivi sasa lazima Chuo kitoe wataalamu waliobobea katika fani za habari 
za kisasa na wenye vipaji vya kuweza kukabiliana na soko la ajira kwa 
faida yao na Taifa kwa ujumla” Alisema Waziri.
 Waziri huyo aliwataka wajumbe wa 
bodi hiyo kukikuza na kukiendeleza chuo hicho kwa ufanisi mkubwa ili 
kuwa mfano wa kuigwa katika vyuo vingine.
 Alisema kuwa Serikali ya 
Mapinduzi ya Zanzibar ina matumani makubwa na Bodi hiyo mpya na kwamba 
itaweza kukabiliana na changamoto ambazo zinaweza kujitokeza katika 
kipindi chote cha uwepo wa Bodi hiyo.
 Alizigusia
 baadhi ya Changamoto zinazokikabili Chuo hicho kuwa ni pamoja na Uhaba 
wa Madarasa na Ofisi na kuwataka Wajumbe wa Bodi hiyo kufikiria na 
kupanga namna bora kukukabiliana na jambo hilo.
 Kwa
 upande wake Mwenyekiti wa Bodi hiyo Chande Omar aliishukuru Serikali 
kwa kuteuliwa na kuahidi kuwa watatekeleza kazi zao ipasavyo kwa mujibu 
wa sheria zinavyoelekeza.
 Amesema kuwa watajitahidi kufanya kazi kwa mashirikiano ya hali yajuu ili kutimiza malengo ya Chuo kama yalivyopangwa.
 Bodi
 hiyo iliyoteuliwa ina jumla ya Wajumbe saba ambao ni Saleh Yusuf 
Mnemo,Salim Said Salim, Ali Nasor Sultan, Najma Khalfani Juma,Yussuf 
Omar Chunda na Asha Bakari Makame na Mwenyekiti wao Chande Omar Omar.

No comments:
Post a Comment