TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, December 18, 2012

WAZIRI HUVIZA ATOA TAARIFA YA HALI YA MAZINGIRA






















Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais – Mazingira Mh. Dkt Terezya Huvisa akitoa hotuba wakati wa uzinduzi wa Taarifa ya Hali ya Mazingira ya Jiji la Dar es Salaam ambapo amesema katika Mkutano wa Tisa wa Mawaziri wa Mazingira wa Afrika (AMCEN) uliofanyika mjini Kampala Julai 2002, ulibaini kuwa ukosefu wa taarifa za hali ya mazingira katika bara la Afrika ni moja ya sababu zinazochangia mipango duni ya usimamizi wa shughuli za maendeleo na utekelezaji Mikataba ya Kimataifa ya utunzaji mazingira.
Amesema kutokana na hali hiyo AMCEN iliiomba UNEP wafadhili program ya Afrika ya Mtandao wa Hali ya Mazingira (Africa Environmental Information Network) ili kuongeza uwezo wa nchi za Afrika wa kuwa na Taarifa za Hali ya Mazingira na Mtandao wa Habari baina ya nchi za Afrika.
Mh. Huvisa ameweka wazi kuwa taarifa hiyo imekamilika na iko tayari kwa ajili ya utekelezaji, na kuwa taarifa hiyo imeezea Historia ya jiji la Dar es Salaam, Jiografia na Fiziolojia yake, suala la uchumi Jamii, Sera, Sheria na Mfumo wa Utawala Kimazingira, Usimamizi wa Rasilimali ya Ardhi, Rasilimali Maji, Madini na Nishati, Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira, Uchafuzi wa Mazingira na Mabadiliko ya Tabianchi. (Picha zote na Mo Blog)

No comments:

Post a Comment