Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais – Mazingira Mh. Dkt Terezya
 Huvisa akitoa hotuba wakati wa uzinduzi wa Taarifa ya Hali ya Mazingira
 ya Jiji la Dar es Salaam ambapo amesema katika Mkutano wa Tisa wa 
Mawaziri wa Mazingira wa Afrika (AMCEN) uliofanyika mjini Kampala Julai 
2002, ulibaini kuwa ukosefu wa taarifa za hali ya mazingira katika bara 
la Afrika ni moja ya sababu zinazochangia mipango duni ya usimamizi wa 
shughuli za maendeleo na utekelezaji Mikataba ya Kimataifa ya utunzaji 
mazingira.
Amesema kutokana na hali hiyo AMCEN
 iliiomba UNEP wafadhili program ya Afrika ya Mtandao wa Hali ya 
Mazingira (Africa Environmental Information Network) ili kuongeza uwezo 
wa nchi za Afrika wa kuwa na Taarifa za Hali ya Mazingira na Mtandao wa 
Habari baina ya nchi za 
Afrika.
Mh. Huvisa ameweka wazi kuwa 
taarifa hiyo imekamilika na iko tayari kwa ajili ya utekelezaji, na kuwa
 taarifa hiyo imeezea Historia ya jiji la Dar es Salaam, Jiografia na 
Fiziolojia yake, suala la uchumi Jamii, Sera, Sheria na Mfumo wa Utawala
 Kimazingira, Usimamizi wa Rasilimali ya Ardhi, Rasilimali Maji, Madini 
na Nishati, Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira, Uchafuzi wa 
Mazingira na Mabadiliko ya Tabianchi. (Picha zote na Mo Blog)

No comments:
Post a Comment