Mchungaji Shadrack Langu (katikati), wa kanisa la KKKT Amani akiwa na baadhi ya watoto na kikundi cha VICOBA baada ya kukabidhi 
  
 
KANISA
 la KKKT-Dayosisi ya kati Usharika Amani Singida mjini, umetoa wito 
kwa madhehebu ya dini kusaidia makundi maalumu yasiyojiweza ikiwemo 
watoto wanaoishi mazingira hatarishi. 
 
Wito
 huo umetolewa na Mchungaji wa usharika huo, Shadrack Langu, wakati wa 
makabidhiano ya msaada wa chakula na vitu mbalimbali kwa kituo cha 
Malezi, Kititimo mjini Singida.
 
A u, ili kujemesema utoaji wa misaada hiyo kwa makundi yasiyojiweza, itasaidia kuijenga moyo wa upendo baina yao. 
 
Msaada
 huo wa kibinadamu uneotolewa na kikundi cha VICOBA, chini ya kanisa 
hilo, kwa ajili ya kituo hicho, chenye jumla ya watoto 40. 
 
Mchungaji
 Langu amesema moja ya majukumu ya kanisa ni kuia 
jamii, hususani makundi yasiyojiweza ili kuwajenga kimwili na kiroho 
baadaye wamudu maisha yao. 
 
“Kazi
 ya kanisa ni kuhakikisha mwanadamu anakombolewa katika maisha 
yake…ndiyo maana hata wamisionari walipokuja kwetu, walipojenga shule, 
walijenga pia zahanati na hospitali ili kusaidia jamii kimwili,”alisema 
mchungaji Langu. 
 
Mapema
 akimkaribisha mgeni rasmi, katibu wa VICOBA –KKKT Amani, Mwalimu Anna 
Abdalah aliwaasa watoto hao kuondokana na huzuni badala yake wajione 
wapo sawa na watoto wanaokula, kulala na kuishi na sehemu nzuri wakiwa 
na wazazi wao. 
 
Kwa
 upande wake mwangalizi wa kituo hicho anayetumia maisha yake kuishi na 
kuwahudumia watoto hao, Ali Makala alishukuru msaada huo na kuiomba 
jamii kuiga mfano wa akina mama wa VICOBA kutoka usharika wa Amani 
katika kusaidia kituo hicho. 
 
Msaada
 huo unaojumuisha unga wa sembe kilo 150, mchele kilo 100, mafuta ya 
kula, sabuni,  maharage, mafuta ya kupaka, dawa ya meno, kalamu, 
daftari, juisi, biskuti, miswaki na dawa ya kuulia kunguni, una thamani 
ya zaidi ya Sh. Milioni 1.1. | 
No comments:
Post a Comment