TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, December 18, 2012

MASHINDANO YA WABUNGE AFRIKA MASHARIKI
Spika wa Bunge la Afrika Mashariki Mhe. Margreth Natongo Zziwa akifungua rasmi mashindano ya mpira wa miguu na mikono kwa wabunge wa mabunge ya nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki. Mashindano haya ambayo hafanyika kila mwaka huyakutanisha mabunge ya Tanzania, Kenya, Uganda, Bunrundi, Rwanda pamoja na Bunge la Afrika Mashariki. Kwa mwaka huu Bururndi haikushiri. Mwaka huu mashindono yanafanyika katika Uwanja wa Nyayo jijini Nairobi, Kenya. Spika Natongo Zziwa amewashukuru Maspika wote ambao wameziwezesha nchi zao kushiriki mashindano haya.

 Maandamano ya uzinduzI

Kikosi cha Tanzania wakati wa uzinduzi.

Kikosi cha Uganda: Baada ya uzinduzi timu ya Bunge la Uganda na timu ya Bunge la Afrika Mashariki ndizo zilizofungua dimba ambapo zilitoka sare ya bao moja kwa moja. Mechi itakayofuata ni kati ya Tanzania na Kenya.























Kikosi chaTanzania kilichoidhibu vikali Kenya.
 
 Kikosi cha Afrika Mashariki Kikosi cha Tanzania kikiusoma mchezo kati ya Uganda na Afrika Mashariki Muamuzi wa mchezo huo Bi Damaris Kimani kutoka Kenya.

Tanzania yaiangamiza Kenya kwa 5-1
Tanzania Bunge Sports Club Football imefanya maajabu katika uwanja wa Nyayo jijini Nairobi jana kwa kuwabamizwa wenyeji wao timu ya Kenya Bunge Sports Club Football mabao 5 kwa nunge katika michezo ya mabunge ya nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki yanayoendelea jijini Nairobi. Mashindano hayo yaliyofunguliwa rasmi juzi tarehe 7 Disemba na Spika wa Bunge la Afrika Mashariki Mh. Margreth Natongo Zziwa akisisitiza "let the best team win" tayari yamezikutanisha timu ya Bunge la Uganda na timu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ambapo timu hizo zimetoka sare ya 1-1.
Wakati wa kuhitimisha karamu ya mabao kwa timu ya Kenya, Watanzania walijikuta uwanjani peke yao wakishangilia huku mashabiki-wenyeji wakiwa wameondoka uwanjani hapo. Leo Tanzania itapambana na Rwanda kwenye mpira wa miguu katika uwanja wa City Stadium, na  Wabunge wanawake watakutana na Kenya kwenye mpira wa kikapu Nyayo Stadium. Mashindano haya yanalenga kuimarisha ushirikiano na kuitangaza zaidi Jum uiya ya Afrika Mashariki.
Katika mashindano haya ambayo hufanyika kila mwaka huyakutanisha mabunge ya nchi za Tanzania, Kenya, Uganda, Burundi na Rwanda. Waratibu wa michezo hii ni Jumuiya pamoja na Bunge la Afrika Mashariki. Kwa mwaka huu Burundi haikushiriki.
Chini ya ukufunzi wa Naibu Waziri (TAMISEMI) Mhe. Kasim Majaliwa (Mb) .na uongozi wa Mhe. Idd Azzan (Mb) mabao hayo yalifungwa na Mhe Amos Makala (Mb), Yusuf Soka (2), Mark Tanda na Mhe. Joshua Nassari.
Na Mahmoud Ahmad aliyekuwa Nairobi

No comments:

Post a Comment