IJUE HISTORIA YA MWANAMZIKI NICK MINAJI 
Kila mtu ambae 
amefanikiwa kwa kupanda mwenyewe kutoka chini kwenda juu lazima 
anasimulizi la maisha yake ambalo lina mabonde na milima ya kushangaza 
kidogo, lakini inavuta usikivu na hisia sana pale msichana mrembo 
aliyefanikiwa kuwa kati ya list ya juu duniani kimuziki akiwa na 
simulizi la maisha yake linalotisha ama kuogofya tena akitishwa na yule 
aliyemzaa. 
 
Jina lake la kuzaliwa ni Onika Tanya Maraj a.k.a Nicki Minaj, first lady wa Young Money mwenye umri wa miaka 30. 
 
Nicki
 Minaj ali-experience maisha ya kusikitisha hasa katika familia yake 
mwenyewe iliyomlea, lakini pia mikiki mikiki toka kwa dingi mkorofi 
ilikuwa balaaa.
 Baba yake mzazi alikuwa mtumiaji wa madawa ya kulevya 
kupitiliza, kiasi cha kuwa Teja ajabu, lakini pia alikuwa mkorofi na 
mkatili sana kitu kilichopelekea wanafamilia hao kuishi kwa uoga na 
mashaka.
 
Ilifikia
 hatua baba Nicki Minaj aliwasha moto kwenye nyumba ya familia hiyo 
akijaribu kumuua mama yake Nicki Minaj, jaribio ambalo halikufanikiwa. 
 
Lakini
 Nicki Minaj mwenyewe anasema alijaribu sana kumsaidia mama yake kadri 
anavyoweza na alitaka awe shupavu sana lakini mama yake hakuweza, Nicki 
alijiwekea malengo ya kuwa mwenye mafanikio baada ya kufanya kazi ili 
amsaidie mama yake. 
 
“Siku
 zote nilikuwa na hiki kitu cha kuwawezeshesha wanawake kwenye akili 
yangu”, aliliambia jarida la Details, “kwa sababu nilitaka mama yangu 
awe shupavu, na hakuweza. Niliwaza, kama ntakuwa mwenye mafanikio, 
Naweza kubadili maisha yake.” Huyo ni Nicki Minaj.
 
Nicki
 Minaj alianza kuandika mashairi akiwa na umri wa miaka 12 tu, na baada 
ya kumaliza La Guardia High School, ambayo inatoa elimu ya sanaa na 
Muziki aliwaza moja kwa moja kuingia kwenye biashara ya muziki. Alianzia
 chini na alianza kwa kufanya back up kwa rapperz wa jiji la New York. 
Muda
 mfupi baadae alianza kuandika mashairi yake mwenyewe, na baadae 
akakutana na Lil Wayne aliyegundua kipaji chake ni silaha ya biashara ya
 muziki na kumsaini Young Money, ambapo alimsaidia kuifanya mixtape ya 
“Playtime is Over”, baada ya hapo akaishika dunia na michano yake na 
kuchukua tuzo kibao zenye heshima duniani, na kupata heshima pia hivi 
karibuni kuwa jaji wa shindano la kuimba la American Idol wakati album 
yake ya Pink Friday Roman Reloaded; Re-Up iko sokoni. 
NB:" USITAKE MAFANIKIO PASIPO KUWEKEZA KATIKA JUHUDI" 

No comments:
Post a Comment