TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Thursday, December 20, 2012

POLISI WATUHUMIWA KUBAMBIKIZA WATU KESI ARUSHA


Mahmoud Ahmad Arusha
Jeshi la polisi mkoani hapa linatuhumiwa kwa kuwabambikia kesi wanafamilia moja jijini hapa licha ya kesi ya msingi kuwepo kwenye mahakama kuu ikiendelea.
Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi mmoja wanafamilia hiyoMgeni Ally Hatibu alisema kuwa wamekuwa wakifanyashughuli zao za kujipatia riziki kwa kufuatwa na askari wa jeshi hilo huku wakiwa teyari wamefunguliwa kesi moja mara nne ya kuvamia eneo ambalo ni nyumba ya marehemu baba yao.
Mgeni alikwenda mbali kwa kusema kuwa wao wanaendelea kufanyabiashara kwenye eneeo hilo ambalo ni nyumbani kwao licha ya kuvunjiwa nyumba hiyo na mfanyabiashara wa kampuni ya Napako Enterprises akishirikiana na jeshi la polisi mkoani hapa saa nane usiku kwa madai kuwa aliuziwa nyumba hiyo.
Alisema kuwa teyari kumekuwa na mlolongo mrefu wa wenye fedha kupewa kipaumbele kwenye haki yao huku wao wakiendelea kutaabika bila msaada wa serekali na mfanyabiashara huyo kununua askari kuwazuia kufanyashughuli za kujipaitia kipato chao cha kila siku.
Bi Mgeni alisema kuwa uonevu wanaofanyiwa na mfanyabiashara huyo mkoani hapa bila ya serekali kuchuwa hatua inaonekana kuwa wamenunuliwa kwa bei poa na mfanyabiashara huyo anayeshinda kila siku kwenye kituo kikuu cha polisi jijini hapa.
Akawataka jeshi la polisi kufanyakazi za kulinda raia na mali zao na kuacha kutumiwa na wenye fedha kuwanyima haki zao raia wenye hali za chini aidha alipotafutwa kamanda wa polisi mkoani hapa Liberatus Sabas hakupatikana kwa njia ya simu kwani ilikuwa inatumika muda mrefu.

No comments:

Post a Comment