TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Friday, December 28, 2012

KINYANG'ANYIRO CHA UNIQ MODEL NI LEO






















Ile siku iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu na watanzania wengi kutaka kujua nani ataibuka mshindi wa shindano la kumsaka mwanamitindo wa mwaka mwenye sifa za pekee nchini Tanzania (Unique Model 2012) sasa imewadia.

Homa ya shindano imezidi kupanda ikiwa usiku wa leo atajulikana nani atavishwa taji la unique model of the year 2012 taji lenye heshima katika tasnia ya mitindo nchini Tanzania.

Jumla ya washiriki kumi na mbili wanapanda jukwaani kuwania taji hilo kwenye fainali zake zitakazofanyika katika ukumbi wa maraha wa New Maisha club uliopo Oysterbay jijini Dar usiku wa leo.

Washiriki wanaowania taji hilo ni Vestina Jax,Judith sangu,Amina Ayoub,Catherine Masumbigana,Elizabeth Pertty,Elizabeth Boniface,Vivian Gilbert ,Darline Mmari , Zeenath Habibb,Sandra Suleiman,Cecilia Emmanuel,Magreth Msafiri.

Mratibu wa shindano hili Bwana Methusela Magese amewaomba watanzania wajitokeze kwa wingi siku ya leo kwani kuna mambo mazuri ya kufurahisha ikiwemo burudani ya muziki wa bendi toka kwa mashujaa,ngoma za asili na bongo flava kwa kiingilio cha Tshs 15,000/= tu.


Shindano hili limedhaminiwa na Giraffe ocean view hotel,Kitwe general Traders,sophanaa investment ltd,dtv,88.4 clouds fm,Gazeti la Tanzania Daima,Gazeti la Kiu,mashujaa investment ltd,Michuzi blog,jiachie blog,Lmada Apartments & Hotel,mtaa kwa mtaa blog,Fabak fashins,Genessis health center na Yung don Records,Paka wear,Mtoko Design,Dina ismail blog na Unique Entertainment Blog.

No comments:

Post a Comment