SWAHILI FASHION WEEK YAHITIMISHWA
SWAHILI FASHION WEEK 2012 YAHITIMISHWA MWISHONI MWA WIKI 
HII
GABRIEL MOLLEL ANYAKUA TUZO MBILI 
GABRIEL KUIWAKILI SWAHILI FASHION WEEK KATIKA MAONYESHO 
YA MITINDO MSUMBIJI 2012
Baada ya miezi mingi ya maandalizi, 
waandaji wa Swahili Fashion Week wamefanikia kuhitimisha onyesho kubwa la 
mitindo na mavazi katika nchi za Afrika mashariki na kati, tukio lilinaloendelea 
kuiweka tasnia ya mitindo katika ramani ya mitindo Afrika na Duniani 
kiujumla.
Ikiwa na viwango vipya na vyenye 
ubora, waandaji wamefanikiwa kuwa na tukio bora la mwaka na kuwaacha 
wahudhuriaji wakihitaji maelezo zaidi kuhusu onyesho la 2013. Kama ilivyo ada 
vitu vizuri lazima viwe na mwisho, Swahili Fashion Week 2012 ilimalizika kwa 
kutolewa tuzo siku ya Jumamosi ya tarehe 8, Desemba 2012.
Tuzo za Swahili Fashion Week 2012 zimelenga kutambua 
mchango wa wabunifu mbalimbali ambao wametoa mchango mkubwa katika maendeleo ya 
tasnia ya mitindo Afrika Mashariki. Tuzo hizo zinaongeza chachu ya uvumbuzi na 
ubunifu katika tasnia ya mitindo. Hii inaendana na kuifanya mitindo ya Kiswahili 
kujulikana duniani. Alisema Mustafa Hassanali, Mmiliki na Muandaaji wa Swahili 
Fashion Week.  
Swahili 
Fashion Week 2012, imefanyika katika Hoteli ya Golden Tulip iliyopo jijini Dar 
es salaam, kuanzia tarehe 6-8 Desemba, ikiwa tukio kubwa la Mitindo ukanda wa 
Afrika Mashariki na Kati lililokutanisha wabunifu zaidi ya 50 kutoka ndani na 
nje ya Tanzania.
Mshindi 
wa Tuzo mbili mwaka huu, Mbunifu Mvumbuzi wa mwaka na Mbunifu Bora wa Mwaka, 
Gabriel Mollel ataiwakilisha Swahili Fashion Week katika week ya mitindo 
Msumbiji inayoanza Desemba 7-15. Kwa mwaka wa tano sasa Swahili Fashion Week 
imefanikiwa kuendeleza uhusiano na Mozambique Fashion Week.
“Ni 
faraja kuiwakilisha Tanzana na Swahili Fashion Week katika maonyesho ya 
Msumbiji, kushinda tuzo mbili mwaka huu, kwangu ni matokeo ya kujituma na 
ubunifu mzuri, ninatumia muda mwingi kutengeneza kazi zangu. Hii tuzo inanipa 
nguvu kubwa lakini ni changamoto kwani kazi ngumu katika maisha ni kubaki katika 
hadhi ile ile ambayo watu walikuamini na kukupa katika shughuli unayoifanya” 
Alisema Gabriel
“Kama 
Swahili Fashion Week ni jambo la fahari na kujivunia kuwa sehemu ya Mozambique 
Fashion Week, Gabriel Mollel hataiwakilisha tu Swahili Fashion Week nchini 
Msumbiji, ila pia anaiwakilisha nchi yetu kwa kuonyesha ubunifu na mitindo 
iliyotengenezwa Tanzania” Alisema Mustafa Hassanali.
Huu ni mwaka wa Tano sasa tangu Swahili Fashion Week 
ianze kushirikiana na Mozambique Fashion Week ambapo Mustafa Hassanali 
alishiriki mwaka 2007 na 2008 huku Jamila Vera Swai akiwakilisha 2009, Manju 
Msita 2010, Robbi Morro na Ailinda Sawe wote walienda 2011.
“Swahili Fashion Week inalengo la kutangaza, kuinua na 
kutafuta masoko ya bidhaa za wabunifu wa Afrika Mashariki katika soko la Afrika 
na duniani kote. Tasnia ya Mitindo afrika inaitaji kutambiliwa na kuwekwa katika 
ramani ya dunia” Aliongeza Mustafa Hassanali.
Licha 
ya kutambua mchango wa wadau mbalimbali wa tasnia ya mitindo Afrika Mashariki, 
SFW pia ilitoa nafasi kwa wabunifu vijana wanaochipukia kuonyesha kazi zao na 
mitindo yao kwa mashabiki wa mitindo waliohudhuria katika Swahili Fashion Week 
mwaka huu ambapo wabunifu mbalimbali walionyesha ubunifu wao. 
Wabunifu wa Swahili Fashion Week 
pia walipata nafasi ya kushiriki katika semina iliyoandaliwa na USAID COMPETE 
kwa kushirikiana na ORIGIN AFRIKA juu ya kutafuta masoko kwa bidhaa 
wanazozitengeza. 
Swahili Fashion Week 2012 
imedhaminiwa na Vodacom, USAID Compete, Origin Africa, EATV, East Africa Radio, 
Golden Tulip Hotel. Amarula, Precision Air, 2M Media, Global Outdoor Ltd, Vayle 
Springs Ltd, Eventlites, Ultimate Security, BASATA (Baraza La Sanaa Taifa),Strut 
It Afrika, Ndibstyles, PKF Tanzania, DARLING, PUSH Mobile, DarLife, Century 
Cinemax, Natol na 361 Degrees.
Kwa Picha zaidi za Swahili Fashion 
Week 2012: http://ramp.sdr.co.za/1212SFW/
KUHUSU SWAHILI FASHION WEEK
Swahili Fashion Week ni jukwaa kubwa la mitindo ya mavazi la kila mwaka katika ukanda wa 
Afrika mashariki na kati kwa sasa. Huu ni mwaka wa Tano sasa, ambapo Swahili Fashion Week 
imekuwa ni Jukwaa la wanamitindo na watengeneza vito vya urembo kutoka katika 
nchi zinazoongea Kiswahili na bara zima la Afrika kwa ujumla kuweza kuonesha 
vipaji, kutangaza ubunifu wao na kukuza mtandao wa mawasiliano ya kibiashara 
ndani na nje ya nchi kwa wadau wa mitindo. Hili limelenga kuhamasisha ukanda huu 
wa Afrika Mashariki na Kati kwamba ubunifu wa mavazi ni njia moja wapo ya 
kujipatia kipato na wakati huo huo kukuza bidhaa zinazotengenezwa Afrika ( Made in Africa 
concept)
Ikiwa imeanzisha uhai na jukwaa la matumaini kwa 
kilinge cha mitindo katika ukanda huu, Swahili Fashion Week Swahili Fashion week 
imelenga kuwa maonyesho ya ubunifu wa mavazi linaloonekana sana Afrika na hasa 
kwa ajili ya soko la kimataifa, lililoundwa, kutengenezwa na kujengwa mwaka 2008 
na Mustafa Hassanali.
Ifikapo mwaka 2013, Swahili Fashion Week ina lengo 
la kuwa ni tukio litakalotokea mara mbili kwa mwaka, ambapo kwa kuanza tukio la 
kwanza litafanyika nchini Kenya kama sehemu ya kwanza kisha tukio lenyewe kabisa 
kufanyika baadae nchini Tanzania kama sehemu ya pili.
KUHUSU GABRIEL MOLLEL
Gabriel Mollel ni muasisi wa  Sairiamu Community Action Foundation, 
ambayo ndio nembo yake ya ubunifu, Sairiamu inamaana “Mtu anaetoa kwa mikono 
miwili” katika lugha ya kimasai. Gabriel amekua akifanya kazi zake kwa mikono 
yake mwenyewe kwa ajili ya jamii yake kwa da mrefu kabla hajawa na jina kubwa 
katika uwanda wa sanaa ya ubunifu hapa Tanzania, ameweza kushiriki katika 
maonyesho mbalimbali ikiwemo Harusi Trade Fair, Swahili Fashion Week na mengine 
mengi ambapo pia amekua mshindi wa Swahili Fashion Week katika kipengele cha 
Mbunifu Bora 2011.
No comments:
Post a Comment