WAZIRI AKUTANA NA BODI ZA USHAURI WA MAGAZETI ZANZIBAR
Na Mwanaisha Muhammed Maelezo Zanzibar 20/12/2012.
Waziri wa Habari  Utamaduni Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk amesema kuwepo kwa magazeti mengi katika nchi   kunasaidia sana kuharakisha harakati za Maendeleo . 
Aliyasema hayo huko ofisini kwake Kikwajuni  wakati alipokuwa akibadilishana mawazo na wajumbe wa Bodi ya ushauri wa   Magazeti na Vijarida  Zanzibar .
Waziri alisema kwa sasa Zanzibar magazeti yaliyopo ni machache mno  kilinganisha na nchi nyengine kama Tanzania Bara, hivyo kutokuwepo  kwa Magazeti  mengi kunadumaza maendeleo
Aliitaka
 bodi hiyo kutokuwa wakali wakati wa kusajili magazeti hayo na daima 
wawe wanawafahamisha wenye magazeti pale wanapokosea  na wasichoke ila tu wakiona muhusika  hafahamishiki ndipo  hatua za kisheria zichukuliwe.
Amesema
 kuwa jukumu kubwa kwa hivi sasa kwa bodo hiyo kihakikisha inasajili 
magazeti ya kutosha pamoja na vijarida kwa mujibu wa sheria na taratibu 
ziliopo ili Zanzibar iweze kupiga hatua za maendeleo kwa kuwa na 
magazeti mengi  kama ilivyokuwa siku za nyuma..
Hata
 hivyo Waziri alisema bodi inakazi muhimu katika nchi kwa kuhakikisha 
kwamba magazeti yatakayo ruhusiwa yawe ni yenye uhakika na sio ya 
kubahatisha na kuleta mfarakano katika jamii.  
Nae
 kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi hiyo ambae pia ni Mshauri wa Rais wa
 masuala ya Utalii Issa Ahmed Othman alisema kuwa madhumuni makubwa ya 
kuanzishwa kwa Bodi hiyo ni uangalizi wa magazeti na vijarida ili 
yasikiuke  taratibu na sheria  zilizowekwa .
 Alisema kuwa kwa upande wa Bodi hiyo huwa hawapitishi gazeti wala majarida kama vigezo husika vya kisheria  havijakidhi  haja kama sheria ilivyoelekeza ili kuepusha migogoro kutotokea katika jami
Mwenyekiti
 huyo alisema kuwa bodi inaona choyo kwa wazanzibari kutokuwa na 
magazeti mengi hivyo inakaribisha kwa watanzania kwa ujumla kuanzisha 
magazeti ili maendeleo yaweze kupatikana Zanzibar. 
 Alisema kuwa Serikali imeweka  chombo cha kushughulikia vyombo vya Habari  sio kuwabana bali ni kuweka utaratibu ambao utasaidia utendaji mzuri wa kazi za waandishi wa habari .  
IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR .20/12/2012.
No comments:
Post a Comment