TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Thursday, December 20, 2012

WAZIRI AKUTANA NA BODI ZA USHAURI WA MAGAZETI ZANZIBAR























Na Mwanaisha Muhammed Maelezo Zanzibar 20/12/2012.
Waziri wa Habari  Utamaduni Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk amesema kuwepo kwa magazeti mengi katika nchi   kunasaidia sana kuharakisha harakati za Maendeleo .
Aliyasema hayo huko ofisini kwake Kikwajuni  wakati alipokuwa akibadilishana mawazo na wajumbe wa Bodi ya ushauri wa   Magazeti na Vijarida  Zanzibar .
Waziri alisema kwa sasa Zanzibar magazeti yaliyopo ni machache mno  kilinganisha na nchi nyengine kama Tanzania Bara, hivyo kutokuwepo  kwa Magazeti  mengi kunadumaza maendeleo
Aliitaka bodi hiyo kutokuwa wakali wakati wa kusajili magazeti hayo na daima wawe wanawafahamisha wenye magazeti pale wanapokosea  na wasichoke ila tu wakiona muhusika  hafahamishiki ndipo  hatua za kisheria zichukuliwe.
Amesema kuwa jukumu kubwa kwa hivi sasa kwa bodo hiyo kihakikisha inasajili magazeti ya kutosha pamoja na vijarida kwa mujibu wa sheria na taratibu ziliopo ili Zanzibar iweze kupiga hatua za maendeleo kwa kuwa na magazeti mengi  kama ilivyokuwa siku za nyuma..
Hata hivyo Waziri alisema bodi inakazi muhimu katika nchi kwa kuhakikisha kwamba magazeti yatakayo ruhusiwa yawe ni yenye uhakika na sio ya kubahatisha na kuleta mfarakano katika jamii.  
Nae kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi hiyo ambae pia ni Mshauri wa Rais wa masuala ya Utalii Issa Ahmed Othman alisema kuwa madhumuni makubwa ya kuanzishwa kwa Bodi hiyo ni uangalizi wa magazeti na vijarida ili yasikiuke  taratibu na sheria  zilizowekwa .
 Alisema kuwa kwa upande wa Bodi hiyo huwa hawapitishi gazeti wala majarida kama vigezo husika vya kisheria  havijakidhi  haja kama sheria ilivyoelekeza ili kuepusha migogoro kutotokea katika jami
Mwenyekiti huyo alisema kuwa bodi inaona choyo kwa wazanzibari kutokuwa na magazeti mengi hivyo inakaribisha kwa watanzania kwa ujumla kuanzisha magazeti ili maendeleo yaweze kupatikana Zanzibar.
 Alisema kuwa Serikali imeweka  chombo cha kushughulikia vyombo vya Habari  sio kuwabana bali ni kuweka utaratibu ambao utasaidia utendaji mzuri wa kazi za waandishi wa habari .  
IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR .20/12/2012.

No comments:

Post a Comment