TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Saturday, December 22, 2012

JERRY SLAA NDANI YA HEKALU KUOMBEA AMANI
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wahindu Tanzania Bw. Ramesha Patel akimpokea na kumtambulisha mgeni rasmi Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa wakati alipowasili kwenye msikiti mkuu wa Dhehebu hilo ulioko jijini Dar es Salaam kwa shughuli maalum ya kuliombea taifa Amani.
Mstahiki Meya Jerry Silaa akilakiwa na kuvishwa shada la maua.
Ibada ikendelea kwa namna ya kipekee.
 Pichani Juu na Chini watoto kwa wakubwa wakicheza ngoma za asili ya Hindu kwenye Ibada hiyo.
 

Mstahiki Meya Jerry Silaa akioneka kufurahishwa na ngoma hizo.
 Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wahindu ya Shreen Sanatan Dharma Sabha Bw. Rajesh Mistry akimkaribisha mwenyekiti wa jumuiya hiyo kuzungumza maneno machache kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi.
 Bw. Ramesh Patel akimkaribisha mgeni rasmi kuzungumza na wanajumuiya hiyo wakati wa Ibada maalum ya kuliombea Taifa Amani.


























Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa akizungumza na wanajumuiya ya Hindu ambapo amewashukuru kwa kumkaribisha kuungana nao katika Ibada hiyo maalum na kuwataka kuendelea kuwa na mshikamano na jamii nyingine pamoja na Serikali.
Mstahiki Meya ametumia fursa hiyo kuwataka wanajamii hiyo pale wanapokwama au kukwazwa kibiashara katika manispaa ya Ilala kwa jambo wanaloona linaweza kutatuliwa wasisite kuwaona viongozi wao na kuwaambia viongozi wao wasisite kumuona yeye moja kwa moja ili watafute ufumbuzi kwa manufaa ya Manispaa na jiji kwa ujumla. Kulia ni Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Bw. Ramesh Patel

No comments:

Post a Comment