KUTOKA IKULU : MARC REVALOMANANA AMEKUBALI KURUDI NCHINI KWAKE
Na: Veronica Kazimoto – 
MAELEZO 
Dar es 
Salaam
  
Rais wa Jamuhuri ya 
Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete amefanikiwa kufanya mazungumzo na Rais 
wa zamani wa Madagaska Marc Ravalomanana ambaye amekubari kurudi nchini kwake 
baada ya kuwa uhamishoni  nchini  Afrika Kusini tangu 
mwaka 2009.
  
Akizungumza na wahariri wa 
vyombo vya habari Ikulu jijini Dar es Salaam leo,  Raisi Kikwete 
amesema Ravalomanana amekubali pia kutokugombea katika uchanguzi utakaofanyika 
nchini humo mwezi Mei 2013 ili kuleta amani na 
utulivu.
  
“Nimezungumza na Rais 
Ravalomanana na amekubali kurudi nchini kwake madagaska  na 
kukubali kutokukugombea  uchaguzi ujao kama maamuzi ya 
 Jumuiya 
ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika 
(SADC) 
yalivyofikiwa katika vikao vyake vya hivi karibuni”, amesisitiza Rais 
Kikwete.
  
Raisi 
kikwete amefafanua  kuwa Ravalomanana  anarudi nchini 
Madagaska bila masharti yoyote na atapewa ulizi na Serikali ya nchi hiyo 
ikisaidiana na Jumuiya ya SADC.
  
Kwa upande 
wake Rais Ravalomanana amemshukuru Rais kikwete kwa kufanikisha mazungumzo hayo 
 na  amesema anaheshimu maamuzi yaliyotolewa na SADC 
kwa lengo la kuisaidia Madagaska kuwa katika hali ya 
amani.
  
“Ninamshukuru Rais Kikwete kwa kufanikisha mazungumzo 
haya na niko tayari kurudi nchini kwangu kujenga, kuimarisha na kushirikiana na 
wananachi  ili kuleta amani na utulivu,” amesema  
Ravalomanana.
  
Rais 
kikwete alipewa jukumu na Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi 
za Kusini mwa Afrika 
 la kufanya mazungumzo na Marais wote wa wawili,  Rais 
wa sasa wa Madagaska Andry Rajoelina 
na Rais wa zamani Marc Ravalomanana ambapo mazungumzo bado yanaendelea kwa 
upande wa Rais Rajoelina. 
No comments:
Post a Comment