MAGARI MAALUMU TU MECHI YA SIMBA, YANGA

Magari
 yenye shughuli maalumu tu ndiyo yatakayoruhusiwa kuingia uwanja wakati 
wa mechi ya Simba na Yanga itakayochezwa keshoku(Jumapili) kwenye Uwanja
 wa Taifa, Dar es Salaam.
Mechi itaanza saa 10 kamili jioni, na kila timu inaruhusiwa kuingia 
na magari matatu tu; gari la timu na mengine mawili ya viongozi. Ukaguzi
 wa kuingia uwanjani ni kwa watu wote, kwani utaratibu huo si wa 
kumdhalilisha mtu bali lengo lake ni kuhakikisha usalama.
Vilevile watu hawataruhusiwa kuingia uwanjani na mifuko ya aina 
yoyote ikiwemo mabegi, isipokuwa kwa waandishi wa habari wanaotumia 
mabegi hayo kwa ajili ya kubebea kamera zao. Pia hakuna wafanyabishara 
watakaoruhusiwa kufanya biashara katika maeneo yanayozunguka uwanja.
Kwa washabiki watakaokuwa katika mazingira ya kuwa kero kwa wenzao 
wakiwemo walevi hawataruhusiwa kuingia uwanjani, pamoja na wale wenye 
silaha kama bastola ambapo wakikamatwa wafikishwa polisi na baadaye 
kufunguliwa mashtaka kortini.
Barabara ya Uwanja wa Taifa itafungwa kuanzia saa 2 asubuhi upande wa
 Chang’ombe, hivyo washabiki wanatakiwa kununua tiketi zao mapema leo 
(Jumamosi) ambapo zitaanza kuuzwa katika vituo mbalimbali kuanzia saa 4 
asubuhi.
Vituo hivyo ni mgahawa wa City Sports Lounge, Shule ya Sekondari 
Benjamin Mkapa, Sokoni Kariakoo, mgahawa wa Steers ulioko mtaa wa 
Ohio/Samora, Oilcom Ubungo, Kituo cha Mafuta Buguruni, Dar Live Mbagala,
 Uwanja wa Uhuru, mgahawa wa Brake Point uliopo Kijitonyama na BMM Salon
 iliyoko Sinza Madukani.
No comments:
Post a Comment