BALOZI WA JAPAN ARIDHISHWA NA UJENZI WA DARAJA

Balozi wa
 Japan Mheshimiwa Masaki Okada (wa kwanza kushoto) akiwa na Waziri wa 
Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli (nyuma ya Balozi) pamoja na 
Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Maendeleo ya Usafirishaji nchini Rwanda
 Bw. Guy Kalisa (mwenye tai nyekundu) wakikagua eneo la kituo cha pamoja
 cha ukusanyaji ushuru kwa upande wa Rwanda. (HD)



Balozi wa
 Japan nchini Tanzania Mheshimiwa Masaki Okada ameelezea kuridhishwa na 
utekelezaji wa mradi ujenzi wa daraja la kimataifa la Rusumo na kituo 
cha pamoja cha ukusanyaji ushuru katika eneo la Rusumo mpakani wa 
Tanzania na Rwanda. Miradi hiyo miwili mikubwa inayofadhiliwa na 
Serikali ya Japan ilianza kujengwa mwezi Machi mwaka huu wa 2013 na 
imepangwa kukamilika mwezi Novemba mwaka 2014.
"Nimeridhishwa
 na viwango na kasi ya utekelezaji wa mradi huu" alisema Balozi Okada 
wakati alipotembelea eneo hilo la mpakani mwa Tanzania na Rwanda ambapo 
alisisitiza kuwa, inatia moyo kuona fedha zilizotolewa na nchi yake 
zikitumika vizuri kwa lengo la kukamilisha miradi hiyo kwa wakati.
Naye 
Meneja wa Tanroads wa Mkoa wa Kagera Injinia John Kalupale akitoa 
taarifa kwa Balozi huyo wa Japan ambaye alifuatana na Waziri wa Ujenzi 
Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, alielezea kuwa uamuzi wa kujenga 
daraja jingine katika eneo hilo la mpakani, unatokana na mahitaji halisi
 ya wakati huu kwani daraja linalotumika hivi sasa lilijengwa miaka 40 
iliyopita likiwa na uwezo wa kubeba tani 32. Aliendelea kueleza kuwa 
ingawa miaka ishirini baada ya ujenzi wa daraja hilo kulifanyika 
ukarabati mkubwa kwa lengo la kuimarisha uwezo wake, bado kumeendelea 
kuwepo kwa ongezeko kubwa la magari hasa yanayosafirisha bidhaa kati ya 
Bandari ya Dar es Salaam na nchini jirani ya Rwanda.
Injinia 
Hitoshi Kamega ambaye ni Mhandisi Mkazi wa Kampuni mbili zilizoungana 
kuusimamia mradi huo ambazo ni Chodei Co. Ltd. na Nippon Koei Co, 
amelezea kuwa ujenzi wa daraja hilo la Rusumo lenye urefu meta 80 pamoja
 na kituo cha ushuru, unatekelezwa na Mkandarasi Daiho Co. kutoka Japan 
kwa gharama ya Shilingi bilioni 31.736.
Waziri wa
 Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli hata hivyo alibainisha 
kujitokeza kwa mapungufu katika baadhi ya maeneo ya mradi huo ambayo 
wizara yake kwa kushirikiana na Ubalozi wa Japan hapa nchini 
wanayafanyiakazi ili kuhakikisha kuwa kunakuwepo na uwiano mzuri wakati 
wa utekelezaji wa mradi huo na pale huduma zenyewe zitakapoanza 
kutolewa..
Waziri 
Magufuli aliyataja baadhi ya mapungufu hayo kuwa ni pamoja na kutotengwa
 kwa eneo la kutosha la maegesho ya magari kwa upande wa Tanzania na 
kuhitajika kwa upanuzi wa majengo ya huduma za kiutawala hasa wakati wa 
kutekeleza mipango ya baadaye kwa kuzingatia ongezeko la shughuli za 
kibiashara linavyoonekana katika eneo hilo.
No comments:
Post a Comment