Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi NSSF Watembelea Miradi Dar

Baadhi ya 
Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii 
(NSSF) pamoja na maofisa wa NSSF wakitembelea mradi wa Ujenzi wa Daraja 
la Kigamboni jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya 
Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii 
(NSSF) pamoja na maofisa wa NSSF wakitembelea mradi wa nyumba za bei 
nafuu eneo la Mtoni Kijichi.

Meneja 
Mradi wa NSSF, Mhandisi Karim Mattaka (wa kwanza kulia waliokaa mezani) 
akitoa taarifa fupi kwa Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la 
Taifa la Hifadhi ya Jamii na maofisa waandamizi wa taasisi hiyo juu ya 
maendeleo ya ujenzi wa daraja la Kigamboni.

Meneja 
Mradi wa NSSF, Mhandisi Karim Mattaka (wa kwanza kushoto) akifafanua 
jambo kwa Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Taifa la Hifadhi 
ya Jamii na maofisa waandamizi wa taasisi hiyo juu ya maendeleo ya 
ujenzi wa daraja la Kigamboni.(P.T)

Baadhi ya 
Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii 
(NSSF) pamoja na maofisa wa NSSF wakiteremka kwenye gari katika moja ya 
miradi ya taasisi hiyo walipotembelea jana.

Mmoja wa maofisa wa juu na mhandisi kutoka NSSF akifafanua jambo kwa wajumbe wa bodi.

Afisa 
Mradi msimamizi na Msanifu wa NSSF, Deogratias Mponeja (wa kwanza 
kushoto) akitoa maelezo juu ya mradi wa awamu ya tatu ya ujenzi wa 
nyumba nafuu kwa wajumbe.

Mkurugenzi
 Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Dk. Ramadhan Dau (wa pili 
kulia) akiwa na Eunice Chiume wakizungumza jambo katika ziara ya 
wajumbea wa Bodi ya NSSF kutembelea miradi jijini Dar es Salaam.

Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi NSSF Watembelea Miradi Dar

Mkurugenzi
 wa Mradi na Msanifu Majengo wa NSSF, Mkurugenzi wa Mipango, Miradi na 
Uwekezaji wa NSSF, Yacoub (aliyesimama) akitoa taarifa fupi juu ya 
maendeleo ya mradi wa ujenzi wa nyumba za bei nafuu kwa wajumbw wa bodi.
Na Joachim Mushi, Dar es Salaam
WAJUMBE wa Bodi ya Wakurugenzi ya 
Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) wamefanya ziara ya 
kutembelea baadhi ya miradi kadhaa inayotekelezwa na shirika hilo 
iliyopo jijini Dar es Salaam. Miradi iliyotembelewa katika ziara hiyo ni
 pamoja na ule wa ujenzi wa nyumba za bei nafuu uliopo eneo la Mtoni 
Kijichi na ujenzi wa Daraja la Kisasa eneo la Kigamboni.
Akitoa taarifa fupi kwa wajumbe wa 
bodi ya NSSF wakiwa eneo la ujenzi wa nyumba za bei nafuu na za kisasa 
eneo la Mtoni Kijichi, Mkurugenzi wa Mipango, Miradi na Uwekezaji wa 
NSSF, Yacoub Kidula alisema eneo hilo linatekelezwa kwa awamu mbili za 
ujenzi wa nyumba aina mbalimbali.
Alisema awamu ya pili ambayo 
iliendelea baada ya kukamilika ya kwanza ya ujenzi wa nyumba 85, 
imetekelezwa kwa ujenzi wa nyumba 215 eneo la Mtoni Kijichi mradi ambao 
tayari umekamilika na nyumba zimeanza kuuzwa kwa wanachama wa NSSF. 
Alisema nyumba 200 tayari zimekamilika huku 15 zilizosalia zikiwa katika
 hatua za mwisho kukamilika.
Alisema tayari Shirika hilo limeanza 
kutekeleza ujenzi mwingine wa awamu ya tatu utakaowezesha ujenzi wa 
nyumba za kisasa na bora zaidi zenye uwezo wa kuchukua familia 820 
zikiwa na ghorofa moja huku zikiwa zimeboreshwa zaidi kihuduma 
ukilinganisha na zilizojengwa awali.
Aidha akifafanua juu ya ujenzi wa 
nyumba za bei nafuu zinazoendelea kujengwa na NSSF, alisema mbali na 
kuwa za bei ya chini zinahuduma muhimu za kijamii kama umeme, maji, 
mfumo mzuri wa kuifadhi maji taka, eneo la nje la ziada pamoja na vifaa 
vingine zikiwemo feni vyumba vyote, mfumo wa maji ya moto kwenye mabafu 
na sakafu ya kisasa 'tiles'.
Alisema nyumba zinazojengwa zinaukubwa
 na idadi ya vyumba tofauti kulingana na maitaji ya mteja, yaani kuanzia
 vyumba viwili hadi vitatu vya kulala huku vyote vikiwa na sebule, jiko,
 choo pamoja na stoo. Aliongeza kuwa milango na madirisha yamejengwa kwa
 vioo na chuma (nondo) ili kuimarisha zaidi kiusalama huku jiko likiwa 
na kabati maalumu na za kisasa kwa ajili ya kuifadhia vitu.
Kidula alisema nyumba ya chini itauzwa
 takribani sh milioni 66 za kitanzania bei hiyo ikiwa ni pamoja na VAT. 
Wajumbe wa bodi pia walitembelea mradi mkubwa wa NSSF wa ujenzi wa 
daraja la Kigamboni ambao unafanywa na taasisi hiyo kwa kushirikiana na 
Serikali.
Akitoa taarifa za maendeleo ya ujenzi 
wa daraja hilo, Meneja Mradi huo, Mhandisi Karim Mattaka alisema licha 
ya ujenzi huo kuendelea vizuri kwa sasa zipo changamoto kadhaa za ujenzi
 ambazo zilijitokeza hivyo kushughulikiwa mara moja.
Alisema daraja hilo la kisasa 
litakalokuwa na njia (barabara sita) yaani tatu za kwenda Kigamboni na 
tatu za kurudi linatarajiwa kuunganishwa kisasa na barabara ya Mandela 
huku likiwa na njia za kutosha kuzuia msongamano wa magari.
Akizungumzia ziara hiyo ya Wajumbe wa 
Bodi, Meneja Uhusiano Kiongozi, Huduma kwa Wateja wa Shirika la Taifa la
 Hifadhi ya Jamii (NSSF), Eunice Chiume alisema ni ziara ya kawaida ya 
wajumbe hao kukagua miradi ya taasisi hiyo na huenda ziara hiyo ikawa na
 manufaa ya punguzo la riba kwa wanachama wanunuzi wa nyumba hizo.
Imeandaliwa na www.thehabari.com
No comments:
Post a Comment