DK MAGUFULI AIBUKA UPYA

Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli 
ametoa mwezi mmoja kwa watumishi wa Serikali ambao wanadaiwa mikopo ya 
nyumba kulipa madeni yao mara moja na kuonya kwamba ikiwa watashindwa 
kulipa, watanyang'anywa nyumba hizo na watakopeshwa watu wengine.
Dk Magufuli ameibuka na hoja hiyo 
mpya, zikiwa ni siku chache tangu alipopigwa 'stop' na Waziri Mkuu, 
Mizengo Pinda kutekeleza sheria ya kuondoa msamaha wa asilimia tano kwa 
mizigo inayozidi kwenye malori, hali ambayo ilizusha mvutano mkubwa 
baina ya Serikali na wasafirishaji wa mizigo nchini.
Akizungumza wakati wa kuweka jiwe la 
msingi kuzindua ujenzi wa nyumba 851 za watumishi wa Serikali eneo la 
Mabwepande jijini Dar es Salaam, Dk Magufuli alisema watumishi 2500 
hawajalipa mikopo ya nyumba walizonunua.(P.T)
Dk Magufuli alionya kuwa atafuatilia 
suala hilo na kuhakikisha madeni hayo yanalipwa mara moja, huku 
akimwomba Makamu wa Rais, Dk Mohamed Gharib Bilal kumuunga mkono kwenye 
jambo hilo, ambalo ni utekelezaji wa sheria za nchi.
"Naomba ifahamike kwamba tunapojenga 
nyumba kwa ajili ya kuwakopesha watumishi wa umma tunataka kuboresha 
makazi yao. Pia fedha tunazokusanya zinasaidia kujenga nyumba zaidi," 
alisema Dk Magufuli. Hata hivyo alisema hadi sasa watumishi wa Serikali 
4,900 ambao walikopa nyumba hizo tayari wamelipa madeni.
"Mimi nafanya kazi kwa kufuata sheria 
na kila mtumishi wa Serikali anafahamu jambo hilo, hivyo watu ambao 
wanajua tunawadai wakae kwa tahadhari, kwani ndani ya mwezi mmoja kama 
hawatalipa tutawachukulia hatua bila kupuuzia," alionya Magufuli.
Hii siyo mara ya kwanza kwa Dk 
Magufuli kutangaza kunyang'anya nyumba hizo, kwani alifanya hivyo 
mwishoni mwa Machi mwaka jana pale alipouagiza uongozi wa Wakala wa 
Majengo Tanzania (TBA), kuwapa siku saba watu wote walionunua nyumba 
hizo kulipa madeni yao.
Dk Magufuli aliwataka TBA kutoa ilani 
ya maandishi inayowataka wahusika walipe fedha hizo ndani ya wiki moja 
vinginevyo wangenyang'anywa kwa maelezo kwamba wanachelewesha malengo ya
 TBA kujenga nyumba zaidi. Hata hivyo, hakuna taarifa zozote zilizowahi 
kutolewa kuhusu kutekelezwa kwa amri hiyo iliyotolewa zaidi ya miezi 18 
iliyopita.
Jana, Makamu wa Rais, Dk Bilal 
alimuunga mkono Magufuli akisema: "Naunga mkono tamko la Waziri wa 
Ujenzi kwamba ni lazima watumishi wa Serikali ambao wanakopeshwa nyumba 
walipe haraka ili fedha hizo zisaidie kujenga nyumba nyingine."
Dk Bilal alikuwa mgeni rasmi katika 
shughuli ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa nyumba 851, kwenye eneo 
la Bunju 'B' Kinondoni, Dar es Salaam. Ofisa Mtendaji Mkuu wa TBA, Elius
 Mwakalinga, alisema ujenzi huo unafanyika kwa awamu mbili ambapo awamu 
ya kwanza iligharimu Sh2 bilioni na awamu ya pili Sh1 bilioni.
"Nyumba 851 zinazojengwa Bunju B ni 
sehemu ya ujenzi wa nyumba 4,400 katika Mkoa wa Dar es Salaam na nyumba 
10,000 kwa nchi nzima," alisema Mwakalinga.
Hafla hiyo ilisimama takriban kwa 
dakika 10 wakati Dk Bilal akitaka kuhutubia baada ya jenereta kushindwa 
kufanya kazi, hivyo kumlazimu kurudi kuketi kwenye kiti hadi umeme 
uliporejea. Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Jordan Rugimbana alilazimika 
kwenda kufuatilia suala hilo na mafundi waliokuwapo walifanikiwa 
kuunganisha mashine za kipaza sauti na umeme wa Shirika la Umeme 
Tanzania (Tanesco), hivyo Makamu wa Rais aliendelea kuhutubia.
Uuzaji wa nyumba
Nyumba nyingi za Serikali zilijengwa 
kipindi cha utawala wa ukoloni wa Wajerumani uliodumu kati ya 1885 na 
1919 na ule wa Waingereza ulioanza 1919 hadi 1961.
Taarifa zilizopo zinaonyesha kuwa 
nyumba za Serikali zilizouzwa nchi nzima tangu mwaka 2002 wakati wa 
uongozi wa awamu ya tatu chini ya Rais Benjamin Mkapa ni zaidi ya 6,000.
 Malengo ya kuuza nyumba ni kwamba, fedha zilizopatikana zingetumika 
kujenga nyumba nyingine kwa ajili ya watumishi wa Serikali katika maeneo
 mbalimbali nchini yakiwamo Dar es Salaam, Arusha, Dodoma na Mwanza.
Hata hivyo, uuzaji huo ulikuwa na 
utata hali iliyosababisha kupingwa vikali na watu wa kada mbalimbali 
wakiwamo wanasiasa na wanaharakati, kwa maelezo kwamba uliwanufaisha 
vigogo.
Malalamiko pia yalijengwa kwenye hoja 
kwamba nyumba hizo ziliuzwa kwa bei ndogo ambayo haikuzingatia thamani 
ya ardhi husika, huku wengine wakisema hakukuwa na umakini kwani 
viongozi wengi walikosa makazi na hasa wale walioteuliwa baada ya Rais 
Jakaya Kikwete kuingia madarakani.
Miongoni mwa walionunua nyumba hizo ni
 mawaziri wengi, kama si wote, wakati wa Serikali ya Awamu ya Tatu, hasa
 katika mikoa ya Dar es Salaam na Dodoma, kwa kuwa walikuwa wakiishi 
katika nyumba hizo.
Hali hiyo ilisababisha viongozi 
mbalimbali wakiwamo mawaziri, majaji, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, 
wakurugenzi wa ngazi mbalimbali na viongozi wengine kukaa hotelini na 
kuisababishia Serikali gharama kubwa.
Tatizo lingine lililoibuka ni kuwa 
baadhi ya nyumba zilizouzwa zilikuwa ndani ya maeneo ya jeshi na hasa 
Polisi, hivyo kuilazimisha Serikali ya awamu ya nne ilipoingia 
madarakani kulazimisha kurejesha baadhi ya nyumba hizo.
Hata hivyo, kulikuwa na ugumu katika 
urejeshaji kwani baadhi ya waliouziwa tayari walikuwa wamezibomoa na 
kuanza upya ujenzi wake na wengine walikuwa tayari wamezipangisha kwa 
mabalozi, kampuni binafsi, mashirika yasiyokuwa ya kiserikali (NGOs) na 
nyingine kujengewa maduka ya biashar
No comments:
Post a Comment