TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, October 30, 2013

BARCELONA YAENDELEzA MPANGO WA KUMSAJILI KIPA WA LIVERPOOL 

 reina 0b33b

KLABU ya Barcelona imeendelea na nia yake ya kumsajili kipa wa Liverpool, Pepe Reina. (HM)

Kipa huyo wa Hispania mwenye umri wa miaka 31 amepelekwa kwa mkopo wa muda mrefu Napoli, laki Rafa Benitez bado hajaamua kumnunua jumla wakati Liverpool inataka kuachana naye moja kwa moja.
Barca imefanya mazungumzo na kipa mwenye thamani ya Pauni Milioni 8 wa Borussia Monchengladbach, Marc-Andre Ter Stegen, mwenye umri wa miaka 21, lakini bado inamsaka mbadala wa Victor Valdes.
Katibu wa Ufundi, Albert Valentin alikwedna kumuona Reina akiiongoza timu yake kushinda 2-1 dhidi ya Marseille katika mechi ya Ligi ya Mabingwa wiki iliyopita kabla hajaenda kumuona Ter Stegen akimenyana na Eintracht Frankfurt.
Lakini mabingwa hao wa La Liga pia wanamfuatilia Fraser Forster baada ya Xavi kusema kipa huyo wa Celtic ni wa kiwango cha dunia.
Valdes atakamilisha miaka yake 11 ya kuishi Nou Camp mwishoni mwa msimu huku Forster akipewa nafasi kubwa ya kurithi mikoba yake.

No comments:

Post a Comment