TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, October 30, 2013

OMARI KIMWERI KUGOMBANIA UBINGWA WA DUNIA WA WBC 

 1236109_514193065317691_1031784424_n_8afe6.jpg

BONDIA MTANZANIA Omari Kimweri 'Lion Boy' anaefanya shughuli zake Deer Park, Victoria, nchini Australia anatarajia kuwa mtanzania wa kwanza kupanda ulingoni November 30 kugombea ubingwa wa Dunia unaotambuliwa na WBC uzito wa kg47.5 minimum weight
Mpambano huo utakaopigwa nchi ya China November 30 na bingwa wa dunia wa uzito huo nchini china
xiong zhao zhong ni bingwa wa dunia WBC minimum weight ambaye anashikilia taji hilo kwa sasa katika uzito huo.(P.T)
Kimweri anakuwa mtanzania wa kwanza kuwania taji kubwa kabisa Duniani akitokea nchini Austalia uku sapoti kubwa akitegemea kutoka Tanzani ambapo alipo zaliwa
na kigezo cha kufanya apate pambano hilo kubwa ni kutokana na rekodi yake pamoja na kutakiwa mtu ambaye anatokea bara la Afrika ambapo kula imemdondokea bondia Omari Kimweri kwa mara ya kwanza mtanzania huyo ataonekana Dunia nzima akijaribu kuwania ubingwa wa WBC
Ambapo ni kiu ya mabondia wengi duniani kumiliki mikanda mikubwa ya kimataifa Kimweri mwenye rekodi ya kucheza michezo 16 ambapo ameshinda michezo 13 na kuchezea kichapo michezo 3 na mpinzani wake
Xiong Zhao Zhong amecheza michezo 26 akishinda 21 kupigwa 4 na kutoka droo moja
Mabondia hawo wote vijana wenye umri mdogo wa miaka 31 wate wawili wakitofautiana mwezi mmoja tu katika kuzalia mpambano huo umekuwa gumzo katika nchi tatu kwa sasa kwani kila mmoja anajiandaa kivyake
Kimweri kwa sasa anaefanya mazoezi makari uku akipewa sparng na bondia Randy petalcoria wa Philippines ambaye ni bingwa wa light fly weight
Omari Kimweri kwa sasa yupo katika mazoezi mazito ya kujiandaa na mpambano huo huku akitegemea zaidi duwa za watanzania kwa kuwa ushindi wake ni ushindi wa watanzania wote Mungu Ibariki Tanzania Mungu Mbariki Bondia Omari Kimweri

No comments:

Post a Comment