WANAFUNZI WAPAMBANA NA POLISI CAIRO

Polisi wa Misri wamefyatua moshi wa 
kutoza machozi kuvunja maandamano mjini Cairo, ya wanafunzi wanaomuunga 
mkono rais wa zamani, Mohamed Morsi.
Mawe yalirushwa na pande zote mbili 
huku wanafunzi mia kadha wakijaribu kutoka chuoni kuelekea Medani ya 
Rabaa, pahala pa kambi ya wafuasi wa Morsi ambayo ilifungwa na wakuu 
miezi miwili iliyopita.
Hii ni siku ya pili ya mapambano 
katika Chuo Kikuu cha Al-Azhar, ambako kuna wafuasi wengi wa chama cha 
Muslim Brotherhood cha Bwana Morsi.
Bwana Morsi aliondolewa madarakani na jeshi mwezi wa Julai.(P.T)
No comments:
Post a Comment