TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Friday, June 20, 2014

Yusuf Manji aingilia uchaguzi Simba

MWENYEKITI wa Yanga, Yusuf Manji, ametoa ya moyoni kuhusiana na mchakato wa uchaguzi wa Simba.
Mfanyabiashara huyo ametoa angalizo kwamba Simba inapaswa kufanya hatua za makusudi kupata viongozi imara na kuachana na malumbano ambayo hayajengi.
Uchaguzi wa Simba umekumbwa na hali ya sintofahamu baada ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kutangaza kuusitisha kabla ya Mwenyekiti wa klabu hiyo, Ismail Aden Rage na Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi, Damas Ndumbaro kuibuka na kusema TFF haina mamlaka hayo.(P.T)
Awali kulikuwa na taarifa kuwa baadhi ya viongozi na wapenzi wa Yanga walifurahishwa na taarifa za kurejeshwa kwa mgombea urais, Michael Wambura katika mchakato wa uchaguzi kwa madai kuwa wanakubaliana na misimamo yake.
Akizungumza na Mwanaspoti ofisini kwake jijini Dar es Salaam, Manji alisema Simba na Yanga zinategemeana na endapo timu moja kati ya hizo itakwama ni dhahiri kuwa madhara yake yatauathiri upande wa pili, hivyo asingependa kuiona klabu hiyo ikiingia kwenye vurugu na kushindwa kufanya uchaguzi wake kwa amani.
"Maendeleo ya soka la nchi hii yanategemea Simba na Yanga, hizi ni kama mapacha kwani moja ikiporomoka nyingine nayo inaonja chungu ya jiwe kwani haiwezi kuwa na msisimko kama uliokuwa mwanzo, natamani kuona Simba ikifanya uchaguzi wake kwa amani na kupata viongozi imara," alisema Manji.
"Kukiwa na utulivu katika klabu hizi mbili ni dhahiri kuwa tunaweza kuujenga mchezo wa soka nchini, klabu hizi zitasaidia kuijenga Taifa Stars hivyo nisingependa kuona moja inapoteza mwelekeo."
Mbali ya uchaguzi huo, Mwenyekiti huyo ameitaka TFF kuzungumza na na wadhamini wa klabu hizo, Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kuwaongezea fedha za udhamini kwani kampuni hiyo inatoa fedha nyingi zaidi kwenye timu ya taifa, Taifa Stars wakati klabu ndiyo ngazi ya wachezaji kupanda kuchezea Stars.
"Nashangaa kuona TBL inatoa fedha nyingi zaidi Stars kuliko sisi (Yanga) na Simba, tunaotoa wachezaji kwenda kucheza timu hiyo ya taifa , nawaomba walifikirie hilo mara mbili," alisema Manji.
Chanzo:Mwanaspoti

No comments:

Post a Comment