Yusuf Manji aingilia uchaguzi Simba

MWENYEKITI wa Yanga, Yusuf Manji, ametoa ya moyoni kuhusiana na mchakato wa uchaguzi wa Simba.
Mfanyabiashara
 huyo ametoa angalizo kwamba Simba inapaswa kufanya hatua za makusudi 
kupata viongozi imara na kuachana na malumbano ambayo hayajengi.
Uchaguzi 
wa Simba umekumbwa na hali ya sintofahamu baada ya Shirikisho la Soka 
Tanzania (TFF) kutangaza kuusitisha kabla ya Mwenyekiti wa klabu hiyo, 
Ismail Aden Rage na Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi, Damas Ndumbaro 
kuibuka na kusema TFF haina mamlaka hayo.(P.T)
Awali 
kulikuwa na taarifa kuwa baadhi ya viongozi na wapenzi wa Yanga 
walifurahishwa na taarifa za kurejeshwa kwa mgombea urais, Michael 
Wambura katika mchakato wa uchaguzi kwa madai kuwa wanakubaliana na 
misimamo yake.
Akizungumza
 na Mwanaspoti ofisini kwake jijini Dar es Salaam, Manji alisema Simba 
na Yanga zinategemeana na endapo timu moja kati ya hizo itakwama ni 
dhahiri kuwa madhara yake yatauathiri upande wa pili, hivyo asingependa 
kuiona klabu hiyo ikiingia kwenye vurugu na kushindwa kufanya uchaguzi 
wake kwa amani.
"Maendeleo
 ya soka la nchi hii yanategemea Simba na Yanga, hizi ni kama mapacha 
kwani moja ikiporomoka nyingine nayo inaonja chungu ya jiwe kwani 
haiwezi kuwa na msisimko kama uliokuwa mwanzo, natamani kuona Simba 
ikifanya uchaguzi wake kwa amani na kupata viongozi imara," alisema 
Manji.
"Kukiwa 
na utulivu katika klabu hizi mbili ni dhahiri kuwa tunaweza kuujenga 
mchezo wa soka nchini, klabu hizi zitasaidia kuijenga Taifa Stars hivyo 
nisingependa kuona moja inapoteza mwelekeo."
Mbali ya 
uchaguzi huo, Mwenyekiti huyo ameitaka TFF kuzungumza na na wadhamini wa
 klabu hizo, Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kuwaongezea fedha za udhamini
 kwani kampuni hiyo inatoa fedha nyingi zaidi kwenye timu ya taifa, 
Taifa Stars wakati klabu ndiyo ngazi ya wachezaji kupanda kuchezea 
Stars.
"Nashangaa
 kuona TBL inatoa fedha nyingi zaidi Stars kuliko sisi (Yanga) na Simba,
 tunaotoa wachezaji kwenda kucheza timu hiyo ya taifa , nawaomba 
walifikirie hilo mara mbili," alisema Manji.
Chanzo:Mwanaspoti
No comments:
Post a Comment