TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, June 25, 2014

FASTJET YAINGIA ZIMBABWE

fastjet 2 8a847

KAMPUNI ya ndege ya Fastjet imezidi kupanua huduma zake kwa kuongeza masafa yake kwenda nchini Zimbabwe mara mbili kwa wiki ikitokea Dar es Salaam na kufikia njia ya tatu ya kimataifa baada ya zile za Zambia na Afrika Kusini.
Akizungumzia uzinduzi huo, Mwenyekiti mtendaji wa kampuni hiyo, Ed Winter, alisema wamefikia hapo baada ya kupiga hatua kimafanikio katika maeneo ya huduma zake kwenye maeneo ya awali.
"Pamoja na huduma zetu kufanikiwa, katika maeneo yetu ya huduma hapo awali, bado tunatambua mahitaji muhimu ya Watanzania na wananchi wa nchi jirani kiuchumi, kwamba wanahitaji kufika kwa wakati katika masoko yao ya kibiashara," alisema.
Waziri wa Uchukuzi na Usafirishaji wa Zimbabwe, Dk. Orbet Mpofu, alisema nchi yake imepokea kwa furaha taarifa za Fastjet kuichagua Zimbabwe kuwa sehemu yake muhimu ya kutolea huduma zake, na kwamba itakuwa faraja na mafanikio makubwa ya kibiashara.
"Itakuwa hatua moja nzuri sana ya kiuchumi baina ya wafanyabiashara wa Zimbabwe na Tanzania, kwa hiyo sisi tunawakaribisha sana Fastjet kwani tumekuwa tukisikia sifa nzuri kuhusu huduma nzuri na bei nafuu mnazotoa," alisema Dk. Mpofu.
Alisema kuwa Zimbabwe inalenga kufanya mazungumzo ya kina na Fastjet ili kuona kama itawekeza nchini humo katika nyanja ya usafirishaji na uchukuzi.
CHANZO TANZANIA DAIMA

No comments:

Post a Comment