FASTJET YAINGIA ZIMBABWE

KAMPUNI 
ya ndege ya Fastjet imezidi kupanua huduma zake kwa kuongeza masafa yake
 kwenda nchini Zimbabwe mara mbili kwa wiki ikitokea Dar es Salaam na 
kufikia njia ya tatu ya kimataifa baada ya zile za Zambia na Afrika 
Kusini.
        
Akizungumzia
 uzinduzi huo, Mwenyekiti mtendaji wa kampuni hiyo, Ed Winter, alisema 
wamefikia hapo baada ya kupiga hatua kimafanikio katika maeneo ya huduma
 zake kwenye maeneo ya awali.
"Pamoja 
na huduma zetu kufanikiwa, katika maeneo yetu ya huduma hapo awali, bado
 tunatambua mahitaji muhimu ya Watanzania na wananchi wa nchi jirani 
kiuchumi, kwamba wanahitaji kufika kwa wakati katika masoko yao ya 
kibiashara," alisema.
Waziri wa
 Uchukuzi na Usafirishaji wa Zimbabwe, Dk. Orbet Mpofu, alisema nchi 
yake imepokea kwa furaha taarifa za Fastjet kuichagua Zimbabwe kuwa 
sehemu yake muhimu ya kutolea huduma zake, na kwamba itakuwa faraja na 
mafanikio makubwa ya kibiashara.
"Itakuwa 
hatua moja nzuri sana ya kiuchumi baina ya wafanyabiashara wa Zimbabwe 
na Tanzania, kwa hiyo sisi tunawakaribisha sana Fastjet kwani tumekuwa 
tukisikia sifa nzuri kuhusu huduma nzuri na bei nafuu mnazotoa," alisema
 Dk. Mpofu.
Alisema 
kuwa Zimbabwe inalenga kufanya mazungumzo ya kina na Fastjet ili kuona 
kama itawekeza nchini humo katika nyanja ya usafirishaji na uchukuzi.
CHANZO TANZANIA DAIMA
No comments:
Post a Comment