TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Monday, June 23, 2014

Divock Origi Najivuania kuwa mkenya

Origi Ni bao la kujivunia kwa kenya familia yangu na Ubeljiji.
Na Mathias Canal
Mshambuliaji wa Lille ya Ufaransa , Mkenya Divorc Origi ambaye ni raiya ya Ubelgiji aliyeifungia Ubeljiji bao la pekee na la ushindi dhidi ya Urusi katika mechi yao ya pili ya kundi H amesema kuwa anajivunia kuwa mkenya licha ya kuwa anaiwakilisha Ubeljiji.
Bao hilo la dakika za mejeruhi za mechi hiyo ndiyo iliyoiwezesha Ubeljiji kufuzu kwa mkondo wa pili wa timu kumi na sita bora.
Origi ambaye aliingia kama mchezaji wa akiba baada ya kuondoka kwa Romelu Lukaku alifuma bao hilo la kipekee kunako dakika ya 88 ya kipindi cha pili ya mechi hiyo alipopokea pasi nzuri kutoka kwa Eden Hazard .

Origi, mwanawe Mike Okoth, mchezaji wa zamani wa timu ya taifa ya Kenya, Harambee Stars atakua mchezaji wa kwanza wa Afrika Mashariki kuiwakilisha Ubeljiji, na yuko pamoja na wachezaji nyota kama vile Vincent Kompany wa Manchester City na Eden Hazard wa Chelsea.
Akizungumza na BBC Origi anasema:''aliamua kuichezea Ubeljiji baada ya kutilia maanani mambo mengi kama vile usimamizi mzuri wa kandanda nchini humo, mizizi yake ya kandanda iliyoko huko, marafiki, ushauri wa babake pamoja na Ubelgiji kufuzu kwa kombe la dunia kwani haijulikani ni mwaka upi Kenya itafuzu kwa kombe la dunia.
Origi aliiambia BBC kuwa anafurahia mizizi yake na kuwa anajivunia bao hilo na familia yake iliyokuwa uwanjani kumshabikia .
Origi alisema kuwa hii ilikuwa ni tukuio spesheli kwake kwa Kenya na Ubeljiji.

 

No comments:

Post a Comment