TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Monday, June 23, 2014

GHANA YAKANA KUPANGA MECHI BRAZIL


Kocha wa Ghana Kwesi Nyantakyi amesema kuwa waliohusika watachukuliwa hatua za kisheria
Na Mathias Canal
Rais wa shirikisho la soka nchini Ghana , amekanusha madai kuwa shirikisho hilo lilikubali timu ya Taifa kucheza katika mechi ambazo timu nyingine zilikuwa zinajiandaa kupanga.
Shirikisho hilo, pia limewataka polisi kuchunguza madai hayo.
Madai yenyewe yalitolewa kufuatia uchunguzi uliofanywa na wandishi wa jarida la The Daily Telegraph.
"madai yaliyotolewa na gazeti hilo sio ya kweli,'' alisema Rais wa shirikisho la soka la Ghana GFA Kwesi Nyantakyi.
Shirikisho hilo limewataka maafisa wa polisi kuchunguza madai ya vyombo vya habari vya Uingereza kwamba mmoja wa maafisa wake alikubali timu ya nchi hiyo kucheza katika mechi zilizo fanyiwa ufisadi.
Mamlaka ya Soka nchini Ghana imekana madai ya jaribio lolote la kuuza mechi zake ama kuhusika kwa afisa yeyote katika ufisadi.
Madai hayo yametolewa kufuatia uchunguzi wa pamoja kati ya gazeti la Uingereza la Daily Telegraph na Runinga ya Channel Four.
Katika taarifa yake shirikisho la soka duniani FIFA limesema kuwa hakuna ushahidi kwamba uadilifu wa michuano ya kombe la dunia umeathirika.
Shirikisho hilo limesema kuwa litamuwekea vikwazo vikali afisa yeyote atakayepatikana na makosa hayo.

No comments:

Post a Comment