TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, June 18, 2014

KAMPUNI YALIPA MILIONI 800/= KUTAFITI GESI 

Noti10000_f133d.jpg
MOJA ya kampuni nne zilizofikia makubaliano na Mamlaka ya Ukanda Maalumu wa Uwekezaji nchini (EPZA) kutoa huduma mbalimbali kwa kampuni kubwa zinazofanya utafiti wa mafuta na gesi mkoani Mtwara, imetoa malipo ya awali kwa ajili ya kufanikisha nia hiyo.
Kampuni hiyo, Altus Oilfield Services FPZ ya Singapore imetoa hundi ya dola za Kimarekani 526, 280 sawa na Sh milioni 800 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa miundombinu ya eneo hilo.(Martha Magessa)
Mkurugenzi Mkuu wa EPZA, Dk Adelhelm Meru aliwaambia waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam wakati wa kupokea hundi hiyo kuwa fedha hizo zitatumika kuanza kujenga miundombinu ya msingi kama barabara, umeme, maji na njia ya maji taka katika eneo la kampuni hiyo.
“Uwekezaji katika eneo hilo utasaidia kukuza ajira na uchumi wa nchi kuimarika zaidi,” alisema.
EPZA inaendeleza hekta 10 za eneo huru la Bandari ya Mtwara. Mwakilishi wa Kampuni ya MAC Group Limited aliyekabidhi hundi hiyo, Nagarayan Sankaranarayanan alisema kampuni yake imejiandaa kuanza kufanya kazi ya kutoa huduma kwa kampuni za utafutaji gesi na mafuta.
Eneo hilo ni kati ya hekta 110 za eneo hilo huru la bandari ambalo limetengwa na serikali kwa ajili ya uwekezaji mbalimbali.
Hekta hizo 10 zitaendelezwa kwa kuwekewa miundombinu inayotakiwa na kisha kugawiwa kwa kampuni za kimataifa zinazofanya kazi za kutoa huduma mbalimbali kwa kampuni zinazofanya utafiti wa mafuta na gesi katika Mkoa wa Mtwara.
Imeelezwa kituo hicho cha huduma kwa kampuni zinazofanya utafiti, kitakapokamilika kitakuwa cha kipekee si kwa Tanzania pekee, bali katika ukanda mzima wa Mashariki na Kusini mwa Afrika.
Kampuni nyingine zilizoingia Mkataba na EPZA mwezi uliopita kuwekeza katika eneo hilo, ni Slumberger Seaco Inc ya Marekani, Tans Ocean Industries and Services LTD ya Dubai na Lenna ya Iran.
Kazi ya kupata wawekezaji katika eneo hilo, ilianza mwaka 2010 baada ya kampuni za utafutaji gesi na mafuta kuomba kuwepo kwa kampuni za watoa huduma.
Miongoni mwa vitu vitakavyokuwepo katika eneo hilo, ni karakana kubwa kwa ajili ya kufanyia ukarabati na matengenezo ya vifaa vya mafuta na gesi.
Karakana hizo zitajengwa kisasa na zitakuwa na uwezo pia wa kuhudumia nchi jirani kama vile Kenya, Msumbiji, na Afrika Kusini.
CHANZO:HABARILEO

No comments:

Post a Comment