VIKUNDI VYAKABIDHIWA MIZINGA NA MASHINE ZA KUKAMUA ASALI

Mgeni
 rasmi Jesca Msambatavangu mwenye kashda ya Tanzania shingoni akiwa na 
baadhi wa wavunaji wa asali kabla ya kwenda kuvuna asali na baadaye 
katika hafla ya kukabidhiana mashine za kukamua asali na mizinga ya 
nyuki pamoja na mavazi maalum ya uvunaji asali iliyofanyika katika 
kijiji cha Kinywang’anga hivi karibuni.

Mgeni
 rasmi Jesca Msambatavangu ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa 
Iringa akikabidhi kwa mmoja wa wenyeviti wa vikundi mashine ya kukamua 
asali wakati wa hafla ya kukabidhiana mashine za kukamua asali na mizinga ya nyuki pamoja na mavazi maalum ya uvunaji asali. (J M)

Afisa Misitu mstaafu Teresphory Kahatano akitoa maelekezo kwa walinaji wa asali kabla ya kwenda katika mizinga ya nyuki.
MFUKO wa 
Hifadhi ya Misitu Tanzania (TaFF) kwa kushirikiana na Mtandao wa Jamii 
wa Usimamizi wa Misitu Kanda ya Kitapilimwa (MJUMIKK) umewakabidhi 
mashine sita  za kukamua asali na mizinga ishirini kwa  vikundi vya 
ujasiriamali vinavyojishughulisha na ulinaji wa asali katika kata za 
Kitapilimwa na Kiwele katika jimbo la Ismani mkoani Iringa
Akizungumza
 wakati wa hafla ya makabidhiano iliyofanyika katika kijiji cha 
Kinywang’anga hivi karibuni, katibu wa mtandano wa MJUMIKK, Samson Fuko 
alisema lengo la msaada huo ni kuleta ufanisi wa kulinda, kutunza na 
kutumia kwa njia endelevu rasilimali za misitu na kuongeza kipato cha 
mwananchi mjasiriamali.
Alisema 
mashine hizo zitakuwa shamba darasa la ufugaji wa nyuki na upandaji miti
 utakaotumika kutoa mafunzo kwa vitendo kwa wanachama wake na kutoa 
elimu kwa jamii juu ya uhifadhi wa mazingira.
Fuko 
alisema mtandao huo umefanikiwa kuongeza idadi ya wanachama kutoka 50 
waliokuwa mwanzao hadi wanachama 200 walioko sasa ambao unajihusisha na 
ufugaji wa nyuki unaotekelezwa katika vijiji sita kati ya vijiji 11.
Alivitaja
 vikundi vilifaidika na msaada huo kuwa ni Kinywang’anga, Faraja group, 
Twiga group, Mshikamano. Jitegemee na kikundi cha Umoja vyote 
vikipatiwa  mizinga mashine na za kukamulia asali pamoja na mavazi 
maalumu ya kuvaa wakati wa kulina asali vyote vikiwa na thamani ya sh. 
milioni 4.5 
 Aidha 
aliwataka wadau kuvisaidia vikundi vya ufugaji nyuki mizinga ya nyuki na
 mbegu za miti kwa lengo la kuanzisha shamba darasa la ufugaji wa nyuki 
na shamba darasa la upandaji miti na mavazi ya kuvunia asali kwa vikundi
 hivyo.
Kwa 
upande wake mgeni rasmi Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Iringa
 Jesca Msambatavangu aliyekuwa mgeni rasmi katika makabidhiano ya 
mashine hizo  amewaasa wazazi na walezi kuwahamasisha vijana kujiunga 
katika shughuli za maendeleo  wasiwaache  wakilegalega kwani vijana hao 
ndio nguvu kazi ya taifa
Alisema 
maendeleo ya mtu hayaletwi kwa kukaa bila kujishughulisha na kukaa 
vijiweni na kuwataka wajasiliamali hao kutumia  fursa waliyoipata 
kuitumia katika kujiletea maendeleo yao na taifa kwa ujumla.
Aidha 
Msambatavangu aliwahidi wafugaji nyuki kuwatafutia soko la bidhaa zao 
kuweza kuwafikia watu wengi zaidi katika jamii ya mkoa wa Iringa na nje 
ya nchi.
Msambataangu
 ambae pia ni mlezi wa vikundi hvyo amewaeleza  wananchi kuwa kiongozi 
bora ni yule anaetekeleza majukumu  aliyopewa na wananchi na sio 
kuwadharau wale waliompa dhamana ya kuwa kiongozi
Msambatavangu 
 amewataka viongozi wote waliopewa dhamana na wananchi kuwatumikia na 
kuwatatulia matatizo yao mda wowote wanapowahitaji na kuwajibika  sio 
kukaa na kutoa lawama.
Aidha 
amempongeza Mkurugenzi wa Halmashauri  ya Wilaya ya Iringa  Pudensiana  
Kisaka kwa kazi anayofanya  ikiwa  ni moja  ya utekelezaji wa majukukumu
 aliyopewa na serikali  na amesema kuwa kiongozi huyo anapaswa kuigwa na
 viongozi wa halimashauri nyingine kwani amekuwa akisikiliza matatizo ya
 wananchi katika halimashauri  yake na kuyafanyia  kazi.
No comments:
Post a Comment