TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, June 25, 2014

MAXIMO :KUJA YANGA ,APISHANA NA JUMA KASEJA

maximo 163f9

KOCHA mpya wa Yanga, Marcio Maximo amezungumza moja kwa moja na Mwanaspoti jijini hapa jana na akatamka maneno mazuri kwa mashabiki wa Yanga.
Mbrazil huyo amesema kwamba anakuja Dar es Salaam kesho Jumatano(leo) kuitengeneza Yanga imara na itakayobadili soka la Tanzania.
"Huu ndio wakati muafaka kwangu kuifundisha Yanga, nataka niitengeneze Yanga kwa masilahi ya nchi nzima, siendi Tanzania kwa ajili ya Yanga pekee naenda kwa ajili ya Taifa, nataka kufanya kitu cha kipekee kabisa.
"Yanga ni sehemu ambayo imetulia sana kwa sasa, nimekuwa nafuatilia sana. Najua. Nimepata ofa za China, Dubai na klabu moja ya madaraja ya chini Uingereza, lakini nimeamua kuziacha zote hizo niende Tanzania kwa Yanga,"alisisitiza Maximo.
Kocha huyo aliiambia Mwanaspoti jijini hapa kwamba kuna mambo machache anamalizana na Yanga kisha atazungumza kwa kina zaidi kuhusiana na kila kitu kupitia Mwanaspoti pekee.
Apishana na Kaseja
Wakati Maximo, akitua nchini kesho Jumanne, kipa wa timu hiyo Juma Kaseja yupo zake majuu anapiga dili.
Habari za uhakika ambazo Mwanaspoti imezipata kutoka wa mmoja wa marafiki wa kipa huyo, zinasema Kaseja alitimka nchini wiki mbili zilizopita ambapo alianzia Oman ambako aliongozana na Meneja wake Abdulfatah Saleh.
Baada ya kutoka Oman sasa kipa huyo yupo Marekani ambapo kwa mujibu wa Abdulfatah ambaye alizungumza na Mwanaspoti jana Jumapili, kipa huyo atakuwa huko kwa wiki nzima na atarejea Jumapili wakati ambapo tayari Maximo atakuwa ameshaanza kazi na wachezaji wengine wa Yanga kwenye Uwanja wa Bandari.
"Tupo Marekani mimi na Juma (Kaseja), kikubwa tumekuja kupumzika baada ya kumaliza majukumu yetu," alisema Abdulfatah
Yanga wanakutana rasmi leo Jumatatu kwa matayarisho ya msimu mpya wa Ligi lakini kabla ya mazoezi kutakuwa na kikao cha mabosi wa juu na mazoezi yataanza rasmi kesho.
Ingawa Ajenda za kikao hicho zikiwa siri Mwanaspoti linafahamu kuwa mambo matatu yatazungumzwa ambayo ni nidhamu, mikakati mipya ya uongozi huo pamoja na taarifa za ujio wa Maximo.

No comments:

Post a Comment