Nigeria yakanusha maafisa wa jeshi wameshtakiwa

Maafisa 
wa Nigeria wanakanusha ripoti kwamba maafisa wa jeshi 15 wakiwemo 
majenerali 10 wamefikishwa katika mahakama ya kijeshi kwa kushirikiana 
na wanamgambo wa kundi la Boko Haram.
Gazeti 
moja nchini humo la The Leadership liliripoti kuwa maafisa hao walikutwa
 na hatia ya kutoa taarifa na silaha kwa kundi la wanamgambo wenye 
msimamo mkali ambalo linadaiwa kusababisha maelfu ya vifo katika kipindi
 cha miaka mitano iliyopita.
Jumatano,
 maafisa wawili, msemaji wa jeshi, Meja Jenerali Chris Olukolade na 
ofisa mawasiliano wa serikali Mike Olmeri wote waliiambia Sauti ya 
Amerika-VOA kwamba taarifa hiyo sio ya kweli.
Serikali 
ya Nigeria inapambana kuweza kulidhibiti kundi la Boko Haram licha ya 
amri ya dharura iliyotangazwa huko kaskazini-mashariki na kupelekwa kwa 
maelfu ya wanajeshi katika eneo. Kundi la Boko Haram limeshambulia 
mashule, masoko, nyumba za ibada na vituo vya jeshi.(Martha Magessa)
Mashahidi
 wanasema wanamgambo wakati mwingine wanavalia sare za kijeshi na mara 
kwa mara wana nguvu zaidi kulioko wanajeshi. Kundi la Boko Haram bado 
linawashikilia zaidi ya wasichana wa shule 200 waliowateka kutoka shule 
moja katika jimbo la Borno, tukio lililotokea kati kati ya mwezi April.
CHANZO:VOA
No comments:
Post a Comment