TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Monday, June 30, 2014

MARCIO MAXIMO AANZA KAZI YANGA

10259844_762529373768464_2298164036768070188_n
Wachezaji wa Yanga sasa kuanza mazoezi chini ya Maximo
KOCHA mpya wa Yanga sc, Mbrazil Marcio Maximo ameanza kazi leo kwa kufanya mazungumzo na baadhi ya wachezaji wa klabu hiyo .
Mkutano huo umefanyika makao makuu ya klabu ya Yanga, makutano ya Twiga na Jangwani, Kariakoo, jijini Dar es salaam.
Maximo alipata nafasi ya kuwaeleza mipango yake ya kazi na kuwataka wachezaji waelewe umuhimu wao katika kujenga mafanikio ya Yanga.
Kocha huyo aliyewahi kufanya kazi nchini kwa kuifundisha timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa stars, baada ya kukutana na wachezaji leo hii, sasa yuko tayari kuanza mazoezi ya kujiwinda na msimu mpya wa ligi kuu soka Tanzania bara unaotarajia kuanza mwezi agosti mwaka huu.

No comments:

Post a Comment