TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Sunday, June 22, 2014

IRAQ YAOMBA MSAADA WA KIJESHI KWA MAREKANI

2A1CEFA1-9ED4-452E-8DC2-9AC8ABA9EE4E w443 h249 c17b2
Mkuu wa majeshi ya Marekani anasema Iraq imeiomba Marekani kusaidia kufanya mashambulizi ya anga ili kupambana na wanamgambo wa ki-Islam wa ki- sunni ambao wamechukua udhibiti wa miji muhimu ya kaskazini na wanaitishia kuishambulia Baghdad.
Mwenyekiti wa baraza la wakuu wa majeshi, Jenerali Martin Dempesy, ali-iambia kamati ndogo ya baraza la seneti la Marekani hapo jumatano kwamba serikali ya Iraq imeshindwa kuwalinda wananchi wake na amesikitishwa sana na jambo hilo.
Naye waziri wa ulinzi wa Marekani, Chuck Hagel alisema viongozi wa kishia nchini Iraq, hawajawahi kutekeleza jukumu lao la kuunda serikali ya umoja wa kitaifa pamoja na wasunni na wakurdi.
Wakati huo huo, akisafiri kuelekea Colombia, Makamu Rais wa Marekani, Joe Biden alizungumza kwa njia ya simu na Waziri Mkuu wa Iraq, Nouri al-Maliki pamoja na viongozi wa kisuni na wa kikurdi. Alisisitiza juu ya umuhimu wa serikali ya umoja nchini Iraq ambayo itaweza kukabiliana na kitisho kinachosababishwa na wanamgambo, kwa wa-Iraq wote
CHANZO BBC

No comments:

Post a Comment