Vikosi vya Iraq vyashindwa kuteka Tiqrit

mwanajeshi wa Isis
Ripoti 
kutoka Iraq zinaarifu kuwa vikosi vya serikali vilivyojaribu kuuteka mji
 wa Tikrit kutoka kwa wapiganaji wa kisunni vimelazimika kurejea nyuma. 
Walioshuhudia
 wanasema kuwa wanajeshi hao walilazimika kurudi katika mji wa Dijla 
,yapata kilomita 25 kusini baada ya mashambulizi yao yalioshirikisha 
mizinga,magari ya kujihami na ndege kushindwa kufua dafu.
Hatahivyo kuna ripoti ya majeruhi wengi kutoka pande zote mbili.
Duru 
zimearifu kuwa vikosi hivyo vya serikali vinajitahidi kufika Tikrit kwa 
kuwa wapiganaji wa ISIS wametega vilipuzi vingi katika barabara kuu ya 
kuingia mjini humo.
Wakati 
huohuo Iraq inasema kuwa imepokea kundi la kwanza la ndege za kijeshi 
ilizoagiza kutoka Urusi ili kuisadia kukabiiana na wapiganaji wa dhehenu
 la kisunni ISIS ambao wameyateka maeneo mengi ya taifa hilo.BBC,(A.I).
No comments:
Post a Comment