MBUNGE DODOMA KUNG'ATUKA
MBUNGE wa
 Chilonwa, Hezekiah Chibulunje (CCM), ametangaza kutogombea tena ubunge 
wa jimbo hilo mwakani baada ya kulitumikia kwa miaka 20 mfululizo.
Chibulunje
 alisema jana kuwa anastaafu ubunge ili kupisha vijana nao waongoze 
jimbo hilo alilosema limepiga hatua kubwa kimaendeleo. 
        
Alisema 
amekuwa mbunge kwa vipindi vinne mfululizo na kwamba katika miaka hiyo 
20, miaka kumi alikuwa Naibu Waziri ikiwemo katika Wizara ya Ushirika na
 Masoko mwaka 2000 hadi 2005.
Alibainisha
 kuwa, kuanzia mwaka 2006 hadi 2010, alikuwa Naibu Waziri katika wizara 
kadhaa alizozitaja kuwa ni Kilimo, Chakula na Ushirika; Viwanda na 
Biashara; Kazi; na Miundombinu.
“Katika 
nafasi zote hizi, za ubunge na unaibu waziri, sijawahi kupata 
misukosuko,” alisema Chibulunje na kutaja mafanikio katika jimbo hilo 
kuwa kupitika kwa barabara zote zikiwemo za tarafa ya Itiso, tofauti na 
alipoingia madarakani mwaka 1995
Pia, 
alisema kwa sasa asilimia 86 ya wakazi wa jimbo lake wanapata majisafi 
na kwamba, vijiji vitatu tu ambavyo vina shida ya maji, ambavyo ni 
Mlimwa kata ya Membe, Azimio kata ya Manyemba na Majengo kata ya 
Chiwondo.
Kwa 
upande wa umeme, alisema asilimia 90 ya vijiji vya jimbo hilo, vitakuwa 
na umeme ifikapo mwakani. Umeme huo unasambazwa na Wakala wa Umeme 
Vijijini (REA).
Kuhusu 
elimu ya sekondari, Chibulunje alisema alisema alipoingia madarakani 
mwaka 1995, jimbo hilo lilikuwa na sekondari moja ya Chamwino, lakini 
sasa kata zote 13 zina sekondari.
CHANZO:HABARILEO
No comments:
Post a Comment