CFAO YAANZISHA HUDUMA MPYA KWA WAMILIKI WA MALORI YA MERCEDES BENZ NCHINI
Msimamizi
 wa ufundi wa Magari aina ya Mercedes Benz kutoka kampuni ya CFAO Motors
 Bw. Winner Mushi (wa tatu kushoto) akionyesha matumizi ya kifaa maalum 
cha ukaguzi wa Malori ya Mercedes Benz (Star Diagnosis Machine) kwa 
baadhi ya mafundi na wasimamizi wa ufundi wa magari ya kampuni ya 
Bakhresa Group.
Bakhresa 
Group ni mmoja wapo wa wateja wa CFAO Motors ambao wanamiliki malori ya 
Mercedes Benz. Bw. Heico Herzog Mtaalamu wa ufundi (Flying Doctor) 
kutoka Mercedes Benz Ujerumani,(wa tatu kulia) akisimamia shughuli hiyo 
iliyoendeshwa na Bw. Mushi. 
Wengine 
ni Key Account Manager wa Mercedes Benz, Bw. George Washington (kulia), 
Meneja wa Usafirishaji kutoka kampuni ya Bakhresa Group, Bw. Abdallah 
Seif (kushoto), Jarangi Nyabagara ambaye ni fundi wa Mercedes Benz (wa 
pili kushoto), na aliyechuchumaa ni Mohammed Shariff Meneja wa Karakana 
ya Bakhresa Group.
        
Na Mwandishi Wetu, 
KAMPUNI 
ya CFAO Motor Tanzania hivi karibuni imezindua huduma mpya ya “Service 
Camp” ambapo chini ya huduma hii wa wamiliki wa malori yanayotengenezwa 
na Mercedez Benz watapata huduma ya ukaguzi bure na mafunzo kwa madereva
 wao.
Akizungumza
 na mwandishi wetu, jijini Dar es Salaam Key Account Manager wa Mercedez
 Benz, Bw George Washington amesema kwamba wameamua kuanzisha huduma 
hiyo ili kuweza kuwahudumia wamilimi wa magari hayo kwa karibu zaidi.
“Mpango 
huu utapeleka huduma karibu na wateja na kwa kuwa hapo mwanzo wamiliki 
wa malori walikuwa hawapati huduma za matengenezo vizuri barani Afrika,”
 amesema
Amesema 
kuwa kuna upungufu katika kuwahudumia wamiliki wa malori ya Mercedez 
Benz Afrika na hivyo wameona ni busara kuja na ‘Service Camp’ ili 
kuwapeleka wateja huduma za matengenezo na mafunzo kwa madereva wao huko
 walipo.
Aliongeza
 kwamba huduma hiyo ya ‘Service Camp’ itakuwa ikitolewa kwa njia mbili 
tofauti ambazo ni kwenda kwa mteja na kukagua malori bila gharama 
yoyote.
Amesema 
kwamba vile vile chini ya huduma hiyo watakuwa wakitoa mafunzo kwa 
madereva wa malori ili waweze kujajua vizuri magari hayo pindi 
wanapopata tatizo la kiufundi.

Bw.Washighton
 aliongeza kwamba vile vile watakuwa wanawafundisha madereva jinsi 
vipuri vya Mercedez Benz vinavyopaswa kuwa ili kuweza kutambua vipuri 
bandia kwenye soko la nchini au karakana mbalimbali.
“Tunawaonesha
 vipuri halisi na vipuri bandia kwa sababu kuna madhara katika kutumia 
vipuri bandia ambapo madhara yanaweza yasionekane katika muda wa siku 
chache bali huonekana baada ya muda mrefu,”
“Ukianza 
kuangalia gharama ya kutengeneza gari baada ya madhara kutokea unakuta 
gharama yake ni kubwa kuliko ambapo ungetumia vipuri halisi,” alieleza 
Bw Washington.
Alisisitiza
 kwamba kwamba hatua ya pili ni kuweka kambi barabarani ambapo malori 
mengi ya Mercedes Benz yanapita, hivyo kila ambaye anamiliki lori aina 
ya Mercedes Benz na anataka kufanyiwa ukaguzi, hupata huduma hiyo bila 
gharama, na hatimaye taarifa kamili zake za ukaguzi kurudishwa kwa 
mmiliki wake.
Washington
 amesema kwamba kampuni ya CFAO inataka kuwa karibu zaidi na wateja 
wake, kwani inataka wateja waone kwamba kuna watu wanaowajali ili 
kudumisha na kuimarisha uhusiano kati yao na wateja wao.

Muuzaji 
wa vipuli vya magari ya Mercedes Benz nchini kutoka kampuni ya CFAO 
Motors, Emmanuel Sembua akimfafanulia jambo Meneja wa Usafirishaji 
kutoka kampuni ya Bakhresa Group, Bw. Abdallah Seif jinsi ya kutambua 
vifaa feki vya magari vya Mercedes Benz ili kujieupusha na matapeli ya 
vifaa hivyo.
“Tunataka
 wateja wetu waone kwamba iwapo magari yao yanapata matatizo, kuna watu 
ambao watawafuata na kuwahudumia kwa wakati unaofaa. Kama unavyojua haya
 ni malori kwa ajili ya transport business, hivyo hayapaswi kuwa mabovu 
kwa wakati mrefu kwa kuwa hiyo itawasababishia hasara wateja wetu. 
Wameyanunua ili wayatumie kwenye biashara na kazi zao, sasa, yakiwa out 
of service, hiyo ni hasara, na sisi hatutaki wateja wetu wapate hasara,”
 aliongeza Washington.
Alipoulizwa
 kuhusu upatikanaji wa huduma hiyo ya “Service Camp”, Washington amesema
 kwamba hii ni mara ya kwanza huduma hiyo kupatikana hapa nchini, ila 
kwa nchi jirani ya Kenya, huduma hiyo imeshapatikana mara tatu. 
Aliongeza kwamba huduma ya “Service Camp” itapatikana tena mwezi Novemba
 mwaka huu.
“Tutaitoa
 huduma hii kwa muda mfupi hapa Dar es Salaam kisha tutahamia mikoani na
 huu ni mpango endelevu, sio kitu cha mara moja,” alisisitiza.
Akizungumzia
 kuhusu huduma iliyotolewa kabla ya kuanzishwa kwa “Service Camp”, 
Washington amesema kwamba awali walikuwa na huduma inayoitwa “Technical 
Exchange”, ambayo ilikuwa na lengo ya kubadilishana uzoefu wa kiufundi 
kati ya wasimamizi wa karakana za wamiliki wa magari hayo na mafundi wa 
CFAO.

 Meneja 
wa Usafirishaji kutoka kampuni ya Bakhresa Group, Bw. Abdallah Seif na 
Meneja wa Karakana ya Bakhresa Group, Mohammed Shariff wakipewa maelezo 
na Muuzaji wa vipuli vya magari ya Mercedes Benz nchini kutoka kampuni 
ya CFAO Motors, Emmanuel Sembua (kulia) ya Battery zinazouzwa na kampuni
 ya CFAO Motors yenye garantii na uwezo mkubwa kwa malori.
“Tumegundua
 kwamba baada ya kuifanya hii technical exchange kumekuwa na mafanikio 
makubwa sana na tumeenda mbele na kuiboresha zaidi na tutafika wakati 
ambapo kutakuwa na washindi, kwani tumeona tuwashindanishe hawa mafundi 
wakuu kwa nia ya kuongeza ufanisi wao ili waweze kuyasimamia magari ya 
waajiri wao vizuri zaidi.
“Kutakuwa
 na washindi ambao tutawapeleka Ujerumani, kule kwenye kiwanda, ili 
waweze kuona jinsi ambavyo magari yanaundwa na kusimamiwa,
“kuanzia 
ubunifu hadi majaribio na mwisho kwenda kiwandani kwa ajili ya uundwaji.
 Huu ndio mpango ambao tunao hivi sasa na mpaka mwaka kesho tutakuwa 
tumempata mshindi ambaye tutampeleka Ujerumani ili atuwakilishe kule na 
kuona jinsi mambo yanavyoendesha. Kwa mantiki hii mpango huu nao pia ni 
mpango endelevu,” amesema Washington.
Washington
 alihitimisha na kusema kwamba mpango huu wa “Service Camp” unahusu 
magari ambayo ni malori pekee yaani Atos, Actros na Atego, na kwamba 
magari madogo hayatahusishwa na mpango huu.

Picha ya pamoja baada ya zoezi hilo.
Amesema 
kwamba kwa sasa huduma hii inapatikana kwenye karakana zilizopo kwenye 
ofisi za CFAO zilizopo Barabara ya Nyerere na kwa upande wa Road 
Inspection, wamiliki wa malori ya Mercedes Benz watajulishwa mapema.
Aliongeza
 kwamba kuhusu mwezi Novemba, kituo kikuu cha kwanza nje ya Dar es 
Salaam kitakuwa Kibaha kwa kuwa barabara hiyo inatumiwa na magari mengi 
yanayokwenda mikoani.
Hatimaye, vituo vingine ambavyo vimepangwa vitatangazwa mapema iwezekanavyo ili wateja wa CFAO wapate muda wa kutosha kujiandaa.

No comments:
Post a Comment