Seif: Hatuko tayari kujadili serikali mbili
Mapendekezo yaliyowasilishwa 
na Jaji Warioba hayakuwa maoni yake, yale ni maoni ya wananchi, 
Tanganyika imevaa koti la Muungano, ametoa ushahidi wake ili kujenga 
mwafaka katika kuendeleza Muungano wenye mfumo wa serikali tatu,"
 Zanzibar.
 Makamu wa Kwanza wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Maalim Seif Sharif 
Hamad amesema chama chake cha CUF hakiko tayari kujadili mfumo wa 
Muungano wa serikali mbili kama inavyotetewa na wabunge wa CCM na Rais 
Jakaya Kikwete.
Amesema tayari amewaandikia barua Rais Kikwete na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein kuwaeleza juu ya msimamo huo.
Maalim Seif alitoa msimamo huo jana kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Kibandamaiti mjini Unguja.(Hudugu Ng'amilo)
        
                        
        
        
        
Isitoshe,
 alisema CUF imebaini kuwa kuna njama za kufuta kipengele katika Katiba 
ya Zanzibar kinachosema; "Zanzibar ni nchi" na kwamba hiyo ni sawa na 
kutwanga maji kwenye kinu kwa kuwa Wazanzibari kamwe hawatakubali 
kufanya hivyo.
Maalim 
Seif alisema haikuwa mwafaka kwa Rais Kikwete kukosoa mapendekezo ya 
Rasimu ya Katiba yanayotaka mfumo wa Muungano kuwa wa serikali tatu.
Alisema 
Jaji Warioba aliweka kando itikadi yake ya CCM katika utendaji wake 
kwenye Tume ya Mabadiliko ya Katiba na kuja na uamuzi huo kwa vile ndiyo
 tiba ya kero za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
"Mapendekezo
 yaliyowasilishwa na Jaji Warioba hayakuwa maoni yake, yale ni maoni ya 
wananchi, Tanganyika imevaa koti la Muungano, ametoa ushahidi wake ili 
kujenga mwafaka katika kuendeleza Muungano wenye mfumo wa serikali 
tatu," alisema Maalim Seif.
Alisema 
Muungano wa serikali mbili hauvumiliki na kama kuna watu wanaendelea 
kuutetea mfumo huo, Zanzibar inaweza kutumia sheria yake ya kura ya 
maoni kuwauliza wananchi wanaotaka na wasiotaka jambo hilo.
"Nimemwandikia
 barua Rais Kikwete, nakala nimempelekea Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed
 Shein, Tanzania Bara wanataka Zanzibar iondoe kifungu cha Katiba 
kinachosema Zanzibar ni nchi, jambo hilo halitapita...tutafanya kampeni 
wananchi walikatae," alieleza Katibu Mkuu huyo wa CUF.
Alisema 
ni jambo la kusikitisha katika hotuba yake alijisahau kama ni mkuu wa 
nchi na analihutubia Bunge Maalumu badala yake akaegemea kuwa mwenyekiti
 wa CCM.
Alisema 
haikuwa sahihi kutoa vitisho na kutaja ikiwa Serikali ya Muungano chini 
ya Serikali tatu italegalega, jeshi litachukua madaraka ya nchi.
"Rafiki 
na ndugu yangu Kikwete, usifikiri huu ni wakati ule wa Julius Nyerere, 
akisema yeye hakuna wa kumpinga. Mambo yamebadilika, usijifanye ni 
Nyerere mpya, hakuna atakayekusikiliza na kubabaika," alisisitiza Maalim
 Seif.Alisema ikiwa viongozi wa Muungano wanajiandaa kutisha watu na 
kusababisha ghasia katika nchi, mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai
 ipo na watakaosababisha fujo na umwagaji wa damu watafikishwa mbele ya 
mikono ya sheria bila ya kujali nyadhifa na madaraka yao.
CHANZO MWANANCHI
No comments:
Post a Comment