TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Monday, March 10, 2014

Mwandishi Uingereza aja kuona vita dhidi ya ujangili 

pembe_7b02c.jpg
Mwandishi huyo jana alitembelea ghala la meno ya tembo yaliyohifadhiwa katika Wizara ya Maliasili na Utalii kumwonyesha juhudi ambazo zimekuwa zikifanyika kupambana na ujangili nchini.
Dar es Salaam. Serikali imeanza juhudi za kujinasua kwenye lawama kwamba haifanyi juhudi za kutosha kupambana na ujangili kwa kuwaalika waandishi wa habari wa kimataifa ili kujionea kazi inayofanyika.
Tayari mwandishi wa Habari wa Uingereza aliyeandika habari katika Gazeti la Daily Mail, Martin Fletcher kuwa Tanzania haifanyi jitihada zozote kukabiliana na ujangili amewasili nchini.
Mwandishi huyo aliandika habari kwenye gazeti hilo toleo la Februari 8 na 9, mwaka huu kwamba Serikali ya Tanzania imeshindwa kutimiza wajibu wake katika kuwalinda faru na tembo ambao wako hatarini kutoweka.

Mwandishi huyo jana alitembelea ghala la meno ya tembo yaliyohifadhiwa katika Wizara ya Maliasili na Utalii kumwonyesha juhudi ambazo zimekuwa zikifanyika kupambana na ujangili nchini. Akizungumza muda mfupi baada ya kuona ghala hilo, Fletcher alisema ni jambo jema kwa kuwa ameona sehemu ya hazina hiyo.
"Nimeona kwa sehemu kubwa hifadhi iliyopo, bado ninaendelea kufuata utaratibu kwa kuwa nimealikwa, siwezi kusema lolote kwa sasa," alisema Fletcher. Kwa mujibu wa ratiba, leo atapelekwa katika Mbuga ya Selous ambako atajionea 'utajiri wa wanyama kwenye mbuga hiyo'.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu alikutana na mwandishi huyo lakini akakanusha kuwa Serikali imemwalika, akisema hiyo ilikuwa ni sehemu ya mpango wake akitaka kujionea mambo yanayotendeka nchini kuhusu suala la ujangili.
Alisema mbali na mwandishi huyo, wengine wa Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) na CNN ya Marekani nao wameomba kufanya hivyo.
Habari zilizoandikwa na mwandishi huyo ziliwapa wakati mgumu Rais Jakaya Kikwete na Waziri Nyalandu kwa kuwa zilichapishwa wakati Rais akihudhuria mkutano kuhusu ulinzi wa wanyama walio hatarini kutoweka.
Chanzo, mwananchi (R.M)

No comments:

Post a Comment