Kuhusu kamati 12 zilizoundwa na Sitta na hotuba ya JK kujadiliwa

Kufuatia
 kuwepo kwa hoja mbalimbali za wajumbe wa Bunge maalum la katiba kuhusu 
kukinzana kwa Hotuba ya Rais Jakaya Kikwete aliyoitoa wakati wa uzinduzi
 wa bunge hilo na rasimu ya katiba iliyowasilishwa na mwenyekiti wa tume
 ya mabadiliko ya katiba jaji Joseph Warioba, mwenyekiti wa bunge maalum
 Samwel Sitta ameridhia kujadiliwa kwa hotuba hizo.
Amesema baada ya kutolewa kwa hotuba hizo amekuwa akipokea maombi ya 
Wajumbe mbalimbali wakishauri kutaka zijadiliwe na kupendekeza mjadala 
huo ufanyike siku ya Jumatano wiki hii.
Kauli ya Mwenyekiti huyo imetokana na muongozo ulioombwa na mmoja wa 
wajumbe wa Bunge hilo Julius Mtatiro aliyetaka mwenyekiti wa tume ya 
mabadiliko ya katiba Jaji Joseph Warioba aitwe bungeni kujibu baadhi ya 
hoja zilizotolewa na Rais kikwete ambazo zinapingana na rasimu 
iliyowasilishwa.
Namkariri Mtatiro akiuliza ‘kwa sababu Rais alikaribishwa tu kwa 
heshima kwenye bunge hili kuja kufungua na sasa akaanza kujibu ile 
hotuba, hatuoni kama kuna haja ya kujenga utaratibu wa kumleta tena mtoa
 hoja ili na yeye aje kujenga hoja juu ya maswali aliyoeleza Rais?’
Kwenye sentensi nyingine mwenyekiti wa Bunge hili maalum la katiba 
Samwel Sitta ameunda kamati 12 zitakazokuwa zikijadiliana kuhusu ibara 
za katiba zitakazopangwa kwa ajili ya kuwasilishwa bungeni kwa mijadala 
ya jumla.
No comments:
Post a Comment