RAIS WA IRAN AANZA SAFARI YA KUTEMBELEA OMAN
raisi wa Iran, Hassan Rouhani
Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya 
Kiislamu ya Iran leo ameanza safari yake ya siku mbili ya kuitembela 
nchi ya Oman. Kabla ya kuelekea Oman Rouhani amesema kuwa, lengo la 
safari yake hiyo ni kuimarisha uhusiano wa pande mbili na kujadili 
masuala muhimu zaidi ya kieneo na kimataifa.
Dakta Rouhani ameeleza kuwa, safari 
hiyo inafanyika kwa mwaliko uliotolewa na Sultani Qaboos wa Oman na 
kwamba siku zote kuimarishwa uhusiano wa pande zote na nchi za Kiislamu 
hasa zilizo jirani ni muhimu kwa Jamhuri ya Kiislamu.
Dk. Rouhani pia amesema ana matumaini 
safari yake hiyo nchini Oman itakuwa na matokeo mazuri katika kuimarisha
 amani na usalama wa kudumu katika eneo la Ghuba ya Uajemi. Hii ni mara 
ya kwanza kwa Rais Hassan Rouhani wa Iran kuitemblea moja ya nchi za 
Kiarabu za Ghuba ya Uajemi tangu aingie madarakani mwezi Agosti mwaka 
jana.
Chanzo, tehranswahili.com (R.M)

No comments:
Post a Comment