TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, March 12, 2014

RAIS WA IRAN AANZA SAFARI YA KUTEMBELEA OMAN

 houran_821c6.jpg

raisi wa Iran, Hassan Rouhani
Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran leo ameanza safari yake ya siku mbili ya kuitembela nchi ya Oman. Kabla ya kuelekea Oman Rouhani amesema kuwa, lengo la safari yake hiyo ni kuimarisha uhusiano wa pande mbili na kujadili masuala muhimu zaidi ya kieneo na kimataifa.
Dakta Rouhani ameeleza kuwa, safari hiyo inafanyika kwa mwaliko uliotolewa na Sultani Qaboos wa Oman na kwamba siku zote kuimarishwa uhusiano wa pande zote na nchi za Kiislamu hasa zilizo jirani ni muhimu kwa Jamhuri ya Kiislamu.
Dk. Rouhani pia amesema ana matumaini safari yake hiyo nchini Oman itakuwa na matokeo mazuri katika kuimarisha amani na usalama wa kudumu katika eneo la Ghuba ya Uajemi. Hii ni mara ya kwanza kwa Rais Hassan Rouhani wa Iran kuitemblea moja ya nchi za Kiarabu za Ghuba ya Uajemi tangu aingie madarakani mwezi Agosti mwaka jana.
Chanzo, tehranswahili.com (R.M)

No comments:

Post a Comment