TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, March 12, 2014

Bunge la Libya lamuondoa madarakani Waziri Mkuu 

MELI_ca093.jpg
Meli inayoidaiwa kutokomea
Bunge la Libya limemuengua madarakani Waziri Mkuu wa nchi hiyo Ali Zeidan, baada ya vikosi vya nchi hiyo kushindwa kuzuia kutoroka kwa meli iliyokuwa imebeba shehena ya mafuta huku ikipeperusha bendera ya Korea ya Kaskazini. Jumla ya wabunge 124 kati ya 194 waliohudhuria bungeni Jumanne ya jana waliidhinisha kura ya kutokuwa na imani kwa wingi wa kura zaidi ya kiwango kinachotakikana na hivyo kuweza kumuondoa madarakani Waziri Mkuu wa nchi hiyo Ali Zeidan.
Wakati huohuo bunge hilo la Libya limemteuwa Waziri wa Ulinzi Abdullah al Thani kuwa Waziri Mkuu wa Mpito, na hivyo bunge hilo kuwa na muda wa wiki mbili wa kutafuta shakhsia mwingine atakayechukua nafasi ya Zeidan. Itafahamika kuwa, wanamgambo wanaoidhibiti bandari ya Sedra huko mashariki mwa Libya, Jumamosi wiki hii walipakia mafuta kwenye meli hiyo iliyokuwa na bendera ya Korea ya Kaskazini kwa jina la "Morning Glory" ambayo ilitia nanga kwenye bandari hiyo bila ya kibali cha serikali.
Chanzo, tehranswahili.com (R.M)

No comments:

Post a Comment