Meli ya Korea Kaskazini yanaswa Libya

Wakuu nchini Libya, wamesema kuwa 
wameikamata meli moja iliyokuwa na bendera ya Korea Kaskazini, ikiwa na 
shehena haramu ya mafuta katika bandari inayodhibitiwa na waasi.
Msemaji wa shirika la kitaifa la 
mafuta, amesema kuwa meli hiyo ilisimamishwa ilipokuwa ikijaribu kungoa 
nanga na kwa sasa inasindikizwa katika bandari inayodhibitiwa na 
serikali ya Libya.
Maafisa
 wa serikali ya Libya waliisimamisha Meli hiyo ya Korea Kaskazini 
ilipokuwa ikiondoka kutoka bandari inayodhibitiwa na waasi siku ya 
Jumatatu ikiwa imesheheni mzigo usio rasmi wa mafuta ghafi.
Jeshi la nchi hiyo limethibitisha tukio hilo.
Waasi wa zamani wanaotaka kuitenga 
eneo la Libya Mashariki, wamekuwa wakimiliki bandari ya Al-Sidra na 
vituo vingine muhimu vya kuuzia bidhaa nje katika eneo hilo tangu Julai 
mwaka uliopita.
Mnamo siku ya Jumamosi, walianza 
kupakia shehena ya mafuta yasiyosafishwa ndani ya meli hiyo ya Korea 
Kaskazini iitwayo Morning Glory, iliyokuwa imetia nanga katika bandari 
ya Al-Sidra.
Viongozi walaani wizi wa mafuta

Kiwanda cha mafuta nchini Libya
Siku ya Jumatatu jeshi la wanamaji 
lilizuilia meli hiyo ilipokuwa ikiondoka bandarini, huku amri ikitolewa 
ielekezwe hadi katika bandari inayodhibitiwa na serikali.
Chama kikuu cha kisiasa nchini humo cha General National Congress, GNC, kimethibitisha kuzuiliwa kwa meli hiyo.
Runinga ya taifa Nchini Libya Al-Nabaa pia imeripoti tukio hilo kwa undani.
Walid al-Tarhuni, ambaye ni msemaji wa
 zamani wa kundi la waasi ambalo limekuwa likidhibiti bandari hiyo, 
ameiambia runinga ya Al-Nabaa kuwa meli hiyo ya mizigo ilikuwa ikielekea
 katika bandari ya Zawiyah, kilomita 50, Magharibi mwa mji mkuu Tripoli,
 kupakua mafuta hayo.
Utawala wa Washington umesema kuwa 
umeshangazwa na tukio hilo na kukariri kuwa mafuta inayotoka Libya ni 
mali ya raia wa nchi hiyo na wala sio ya makundi fulani.(P.T)
No comments:
Post a Comment