BENSOUDA KUKATA RUFAA KESI YA KATANGA

Fatou Bensouda
Mwendesha
 mashtaka mkuu wa mahakama ya Kimataifa ya uhalifu ICC, Fatou Bensouda 
amesema huenda akakata rufaa hukumu iliyotolewa kwa mbabe wa zamani wa 
kivita nchini Congo Germain Katanga.
Katanga 
alipatikana na hatia nne za uhalifu wa kivita na hatia moja ya uhalifu 
dhidi ya binadamu, lakini akaondolea makosa kuhusu ubakaji.
Wapiganaji wake walishutumiwa kuwabaka wanawake na kuwateka huku wakiwatumia kama watumwa wa ngono.
Makundi 
ya wanawake nchini Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Congo yameelezea hasira na
 masikitiko yao kutokana na hatua ya mahakama hiyo ya ICC ya kumuondolea
 Bwana Gatanga makosa hayo.
Wakati wa
 ziara yake katika mji mkuu wa DRC, Kinshasa, Bensouda alisema kuwa 
huenda akakata rufaa dhidi ya uamuzi huo wa mahakama.
''Majaji 
hawakumuhumu kuhusiana na mashtaka ya unyanyazaji wa kimapenzi, mashtaka
 ambayo tulikuwa tumemshtaki nayo, pamoja na ile ya kuwasajili watoto 
jeshini'' Alisema Bensouda.
Bensouda,
 amesema kuwa wanachunguza hukumu hiyo kwa undani na kuchunguza ikiwa 
kuna dosari kadhaa za kisheria ambazo wanaweza kutumia kukata rufaa.
''Majaji 
kwa hekima zao walihisi kuwa bwana Katanga hakuhusika moja kwa moja na 
mashtaka hayo. Nadhani waadhiriwa wanafurahia kuwa ofisi yake 
inafuatilia suala hili, ili kuhakikisha kuwa mashtaka mazito kama hayo 
yanachunguzwa.'' Aliongeza Bensouda.
Kuhusiana
 na kesi inayomkabili rais wa Kenya Uhuru Kenyatta, makamu wake William 
Ruto na mwandishi wa habari Joshua arap Sang, Bensouda alisema kuwa 
''Nimeonyesha wazi kuambatana na ombi niliowasilisha mbele ya mahakama, 
kuhusiana na changa moto tunazopata, baada ya mashahidi wakuu kujiondoa 
kwa sababu kadhaa''.
Bensouda 
amesema kuwa itakuwa vigumu sana kwa ofisi yake kuendelea na kesi hizo 
kama ilvyopangwa baada ya mashahidi wakuu kujiondoa.
''Nimewafahamisha
 majaji kuwa tulikuwa na mashahidi kadhaa wakuu ambao walikuwa tayari 
kutoa ushahidi kuhusiana na matukio muhimu nchini Kenya, lakini wameomba
 kujiondoa kutoka kwa kesi hiyo.
Na kama 
unavyofahamu mashtaka haya pia ni mazito, na kabla ya kwenda mahakamani 
mtu anapaswa kuwa na uhakika wa kuwa na ushahidi ambao utakidhi mahitaji
 muhimu ili kuhakisha kuwa washukiwa wanahumiwa.'' Alisema Bensouda.(P.T)
No comments:
Post a Comment